< Yohana 6 >

1 Baada ya haya, Yesu alikwenda ngʼambo ya Bahari ya Galilaya, ambayo pia huitwa Bahari ya Tiberia.
Potem odszedł Jezus za morze Galilejskie, które jest Tyberyjadzkie;
2 Umati mkubwa wa watu uliendelea kumfuata, kwa sababu waliona ishara nyingi za miujiza alizofanya kwa wagonjwa.
I szedł za nim lud wielki, iż widzieli cuda jego, które czynił nad chorymi.
3 Kisha Yesu akapanda mlimani akaketi huko pamoja na wanafunzi wake.
I wszedł Jezus na górę, i siedział tam z uczniami swoimi;
4 Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
A była blisko wielkanoc, święto żydowskie.
5 Yesu alipotazama na kuuona ule umati mkubwa wa watu ukimjia, akamwambia Filipo, “Tutanunua wapi mikate ili watu hawa wale?”
Tedy podniósł Jezus oczy i ujrzawszy, iż wielki lud idzie do niego, rzekł do Filipa: Skąd kupimy chleba, aby ci jedli?
6 Aliuliza swali hili kumpima, kwa maana alishajua la kufanya.
(Ale to mówił, kusząc go; bo on wiedział, co miał czynić.)
7 Filipo akamjibu, “Hata fedha kiasi cha dinari mia mbili, hazitoshi kununua mikate ya kuwapa watu hawa ili kila mtu apate kidogo.”
Odpowiedział mu Filip: Za dwieście groszy chleba nie dosyć im będzie, choćby każdy z nich mało co wziął.
8 Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, ndugu yake Simoni Petro, akamwambia,
Rzekł mu jeden z uczniów jego, Andrzej, brat Szymona Piotra:
9 “Hapa kuna mvulana mmoja mwenye mikate mitano ya shayiri na samaki wawili wadogo. Lakini hivi vitatosha nini kwa umati huu wote?”
Jest tu jedno pacholę, co ma pięcioro chleba jęczmiennego i dwie rybki; ale cóż to jest na tak wielu?
10 Yesu akasema, “Waketisheni watu chini.” Palikuwa na majani mengi katika eneo lile, nao watu wakaketi. Palikuwa na wanaume wapatao 5,000.
Tedy rzekł Jezus: Każcie ludowi usiąść. A było trawy dość na onemże miejscu, i usiadło mężów w liczbie około pięciu tysięcy.
11 Ndipo Yesu akachukua ile mikate, akamshukuru Mungu na kuwagawia wale watu waliokuwa wameketi. Akafanya vivyo hivyo na wale samaki. Kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
Wziął tedy Jezus one chleby, a podziękowawszy rozdał uczniom, a uczniowie siedzącym; także i z onych rybek, ile jedno chcieli.
12 Watu wote walipokwisha kula na kushiba, akawaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vilivyobaki vya ile mikate, kisipotee chochote.”
A gdy byli nasyceni, rzekł uczniom swoim: Zbierzcie te ułomki, które zbywają, żeby nic nie zginęło.
13 Hivyo wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vya ile mikate mitano ya shayiri na samaki wale wawili wadogo vilivyobakishwa na waliokula.
I zebrali i napełnili dwanaście koszów ułomków z onego pięciorga chleba jęczmiennego, które zbywały tym, co jedli.
14 Baada ya watu kuona muujiza ule Yesu aliofanya, walianza kusema, “Hakika huyu ndiye Nabii ajaye ulimwenguni!”
A oni ludzie, ujrzawszy cud, który uczynił Jezus, mówili: Tenci jest zaprawdę on prorok, który miał przyjść na świat.
15 Yesu akijua kwamba walitaka kuja kumfanya awe mfalme wao, kwa nguvu, akajitenga nao akaenda milimani peke yake.
Tedy Jezus poznawszy, iż mieli przyjść i porwać go, aby go uczynili królem, uszedł zasię sam tylko na górę.
16 Ilipofika jioni, wanafunzi wake waliteremka kwenda baharini.
A gdy był wieczór, zstąpili uczniowie jego do morza.
17 Wakaingia kwenye mashua, wakaanza kuvuka bahari kwenda Kapernaumu. Wakati huu kulikuwa tayari giza na Yesu alikuwa hajajumuika nao.
A wstąpiwszy w łódź, jechali za morze do Kapernaum, a już było ciemno, a Jezus nie przyszedł był do nich.
18 Bahari ikachafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
A morze, gdy powstał wielki wiatr, burzyć się poczynało.
19 Wanafunzi walipokuwa wamekwenda mwendo wa karibu maili tatu au nne, walimwona Yesu akitembea juu ya maji akikaribia mashua, nao wakaogopa sana.
Gdy tedy odpłynęli jakoby na dwadzieścia i pięć lub trzydzieści stajan, ujrzeli Jezusa chodzącego po morzu, przybliżającego się ku łodzi, i ulękli się.
20 Lakini Yesu akawaambia, “Ni mimi. Msiogope.”
A on im rzekł: Jamci jest, nie bójcie się.
21 Ndipo wakamkaribisha kwa furaha ndani ya mashua, na mara wakafika ufuoni walikokuwa wakienda.
I wzięli go ochotnie do łodzi, a zarazem łódź przypłynęła do ziemi, do której jechali.
22 Siku iliyofuata, wale watu waliokuwa wamebaki ngʼambo waliona kwamba palikuwepo na mashua moja tu na kwamba Yesu hakuwa ameondoka pamoja na wanafunzi wake, ila walikuwa wameondoka peke yao.
Nazajutrz lud, który był za morzem, widząc, że tam nie było drugiej łodzi, tylko ona jedna, w którą byli wstąpili uczniowie jego, a iż Jezus nie wszedł był w łódź z uczniami swoimi, ale sami uczniowie jego ujechali;
23 Lakini zikaja mashua nyingine kutoka Tiberia zikafika karibu na mahali pale walipokula mikate baada ya Bwana kumshukuru Mungu.
(Przyszły też były drugie łodzie z Tyberyjady, blisko do onego miejsca, gdzie jedli chleb, gdy był Pan dzięki uczynił.)
24 Mara wale watu wakatambua kwamba Yesu hakuwepo hapo, wala wanafunzi wake. Wakaingia kwenye mashua hizo, wakaenda Kapernaumu ili kumtafuta Yesu.
To gdy obaczył lud, iż tam nie było Jezusa, ani uczniów jego, wstąpili i oni w łodzie i przeprawili się do Kapernaum, szukając Jezusa;
25 Walipomkuta Yesu ngʼambo ya bahari wakamuuliza, “Rabi, umefika lini huku?”
A znalazłszy go za morzem, rzekli mu: Mistrzu! kiedyś tu przybył?
26 Yesu akawajibu, “Amin, amin nawaambia, ninyi hamnitafuti kwa kuwa mliona ishara na miujiza, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
Odpowiedział im Jezus i rzekł: Zaprawdę, zaprawdę powiadam wam: Szukacie mię nie przeto, iżeście widzieli cuda, ale iżeście jedli chleb, i byliście nasyceni.
27 Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba amemtia muhuri.” (aiōnios g166)
Sprawujcież nie pokarm, który ginie, ale pokarm, który trwa ku żywotowi wiecznemu, który wam da Syn człowieczy; albowiem tego zapieczętował Bóg Ojciec. (aiōnios g166)
28 Ndipo wakamuuliza, “Tufanye nini ili tupate kuitenda kazi ya Mungu?”
Rzekli tedy do niego: Cóż będziemy czynili, abyśmy sprawowali sprawy Boże?
29 Yesu akawajibu, “Kazi ya Mungu ndiyo hii: Mwaminini yeye aliyetumwa naye.”
Odpowiedział Jezus i rzekł im: Toć jest sprawa Boża, abyście wierzyli w tego, którego on posłał.
30 Hivyo wakamuuliza, “Utafanya ishara gani ya muujiza, ili tuione tukuamini? Utafanya jambo gani?
Rzekli mu tedy: Cóż wżdy ty za znak czynisz, abyśmy widzieli i wierzyli tobie? Cóż czynisz?
31 Baba zetu walikula mana jangwani, kama ilivyoandikwa, ‘Aliwapa mikate kutoka mbinguni ili wale.’”
Ojcowie nasi jedli mannę na puszczy, jako jest napisano: Chleb z nieba dał im ku jedzeniu.
32 Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, si Mose aliyewapa mikate kutoka mbinguni, bali Baba yangu ndiye anawapa mkate wa kweli kutoka mbinguni.
Rzekł im tedy Jezus: Zaprawdę, zaprawdę powiadam wam: Nie Mojżesz wam dał chleb z nieba, ale Ojciec mój daje wam chleb on prawdziwy z nieba.
33 Kwa maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.”
Albowiem chleb Boży ten jest, który zstępuje z nieba i żywot daje światu.
34 Wakamwambia, “Bwana, kuanzia sasa tupatie huo mkate siku zote.”
Tedy mu rzekli: Panie! daj nam zawsze tego chleba.
35 Yesu akawaambia, “Mimi ndimi mkate wa uzima. Yeye ajaye kwangu, hataona njaa kamwe na yeye aniaminiye, hataona kiu kamwe.
I rzekł im Jezus: Jamci jest on chleb żywota; kto do mnie przychodzi, łaknąć nie będzie, a kto wierzy w mię, nigdy pragnąć nie będzie.
36 Lakini kama nilivyowaambia, mmeniona lakini bado hamwamini.
Alem wam powiedział: Owszem, widzieliście mię, a nie wierzycie.
37 Wale wote anipao Baba watakuja kwangu na yeyote ajaye kwangu, sitamfukuzia nje kamwe.
Wszystko, co mi daje Ojciec, do mnie przyjdzie, a tego, co do mnie przyjdzie, nie wyrzucę precz.
38 Kwa kuwa nimeshuka kutoka mbinguni si ili kufanya mapenzi yangu, bali mapenzi yake yeye aliyenituma.
Bom zstąpił z nieba, nie iżbym czynił wolę moję, ale wolę onego, który mię posłał.
39 Haya ndiyo mapenzi yake yeye aliyenituma, kwamba, nisimpoteze hata mmoja wa wale alionipa, bali niwafufue siku ya mwisho.
A tać jest wola onego, który mię posłał, Ojca, abym z tego wszystkiego, co mi dał, nic nie stracił, ale abym to wzbudził w on ostateczny dzień.
40 Kwa maana mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mmoja amtazamaye, Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele, nami nitawafufua siku ya mwisho.” (aiōnios g166)
A tać jest wola onego, który mię posłał, aby każdy, kto widzi Syna, a wierzy weń, miał żywot wieczny; a ja go wzbudzę w on ostateczny dzień. (aiōnios g166)
41 Wayahudi wakaanza kunungʼunika kwa kuwa alisema, “Mimi ndimi mkate ulioshuka kutoka mbinguni.”
I szemrali Żydowie o nim, iż rzekł: Jam jest on chleb, który z nieba zstąpił.
42 Wakasema, “Huyu si Yesu, mwana wa Yosefu, ambaye baba yake na mama yake tunawajua? Anawezaje basi sasa kusema, ‘Nimeshuka kutoka mbinguni’?”
I mówili: Izaż ten nie jest Jezus, syn Józefa, którego my ojca i matkę znamy; jakoż teraz tedy ten powiada: Żem z nieba zstąpił?
43 Hivyo Yesu akawaambia, “Acheni kunungʼunikiana ninyi kwa ninyi.
Tedy odpowiedział Jezus i rzekł im: Nie szemrzyjcie między sobą.
44 Hakuna mtu awezaye kuja kwangu kama asipovutwa na Baba aliyenituma, nami nitamfufua siku ya mwisho.
Żaden do mnie przyjść nie może, jeźli go Ojciec mój, który mię posłał, nie pociągnie; a ja go wzbudzę w ostateczny dzień.
45 Imeandikwa katika Manabii, ‘Wote watafundishwa na Mungu.’ Yeyote amsikilizaye Baba na kujifunza kutoka kwake, huyo huja kwangu.
Napisano w prorokach: I będą wszyscy wyuczeni od Boga; przetoż każdy, kto słyszał od Ojca, a nauczył się, przychodzi do mnie.
46 Hakuna mtu yeyote aliyemwona Baba isipokuwa yeye atokaye kwa Mungu, yeye ndiye peke yake aliyemwona Baba.
Nie iżby kto widział Ojca, oprócz tego, który jest od Boga; ten widział Ojca.
47 Amin, amin nawaambia, yeye anayeamini anao uzima wa milele. (aiōnios g166)
Zaprawdę, zaprawdę powiadam wam: Kto w mię wierzy, ma żywot wieczny. (aiōnios g166)
48 Mimi ni mkate wa uzima.
Jam jest on chleb żywota.
49 Baba zenu walikula mana jangwani, lakini wakafa.
Ojcowie wasi jedli mannę na puszczy, a pomarli.
50 Lakini hapa kuna mkate utokao mbinguni, ambao mtu yeyote akiula, hatakufa.
Ten jest on chleb, który z nieba zstępuje; jeźliby go kto jadł, nie umrze.
51 Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu yeyote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.” (aiōn g165)
Jamci jest chleb on żywy, którym z nieba zstąpił: jeźliby kto jadł z tego chleba, żyć będzie na wieki; a chleb, który ja dam, jest ciało moje, które ja dam za żywot świata. (aiōn g165)
52 Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?”
Wadzili się tedy Żydowie między sobą, mówiąc: Jakoż ten może nam dać ciało swoje ku jedzeniu?
53 Hivyo Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.
I rzekł im Jezus: Zaprawdę, zaprawdę powiadam wam: Jeźli nie będziecie jedli ciała Syna człowieczego, i pili krwi jego, nie macie żywota w sobie.
54 Mtu yeyote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho. (aiōnios g166)
Kto je ciało moje, a pije krew moję, ma żywot wieczny, a ja go wzbudzę w on ostateczny dzień. (aiōnios g166)
55 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
Albowiem ciało moje prawdziwie jest pokarm, a krew moja prawdziwie jest napój.
56 Yeyote alaye mwili wangu na kunywa damu yangu, atakaa ndani yangu nami nitakaa ndani yake.
Kto je ciało moje i pije krew moję, we mnie mieszka, a ja w nim.
57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, na kama nami ninavyoishi kwa sababu ya Baba, hivyo anilaye mimi ataishi kwa sababu yangu.
Jako mię posłał żyjący Ojciec, i ja żyję przez Ojca; tak kto mnie pożywa, i on żyć będzie przez mię.
58 Huu ndio mkate ushukao kutoka mbinguni, si kama ule mkate baba zenu waliokula nao wakafa. Lakini yeye aulaye mkate huu ataishi milele.” (aiōn g165)
Tenci jest chleb on, który z nieba zstąpił, nie jako ojcowie wasi jedli mannę, a pomarli; kto je ten chleb, żyć będzie na wieki. (aiōn g165)
59 Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika sinagogi huko Kapernaumu.
To mówił w bóżnicy, ucząc w Kapernaum.
60 Wengi wa wafuasi wake waliposikia jambo hili wakasema, “Mafundisho haya ni magumu. Ni nani awezaye kuyapokea?”
Wiele ich tedy z uczniów jego słysząc to, mówili: Twardać to jest mowa, któż jej słuchać może?
61 Yesu alipojua kwamba wafuasi wake wananungʼunika kuhusu mafundisho yake, akawaambia, “Je, jambo hili limewaudhi?
Ale wiedząc Jezus sam w sobie, iż o tem szemrali uczniowie jego, rzekł im: Toż was obraża?
62 Ingekuwaje basi kama mngemwona Mwana wa Adamu akipaa kwenda zake huko alipokuwa kwanza?
Cóż, gdybyście ujrzeli Syna człowieczego wstępującego, gdzie był pierwej?
63 Roho ndiye atiaye uzima, mwili haufai kitu. Maneno haya niliyowaambia ni Roho tena ni uzima.
Duchci jest, który ożywia, ciało nic nie pomaga; słowa, które ja wam mówię, duch są i żywot są.
64 Lakini baadhi yenu hamwamini.” Kwa maana Yesu alifahamu tangu mwanzo wale ambao hawangemwamini miongoni mwao na yule ambaye angemsaliti.
Ale są niektórzy z was, co nie wierzą; albowiem wiedział od początku Jezus, którzy byli, co nie wierzyli, i kto jest, co go miał wydać;
65 Akaendelea kusema, “Hii ndiyo sababu niliwaambia kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.”
I mówił: Dlategomci wam powiedział: Iż żaden nie może przyjść do mnie, jeźliby mu nie było dane od Ojca mojego.
66 Tangu wakati huo wafuasi wake wengi wakarejea nyuma wakaacha kumfuata.
Od tego czasu wiele uczniów jego odeszło nazad, a więcej z nim nie chodzili.
67 Hivyo Yesu akawauliza wale wanafunzi wake kumi na wawili, “Je, ninyi pia mnataka kuondoka?”
Tedy rzekł Jezus do onych dwunastu: Izali i wy chcecie odejść?
68 Simoni Petro akamjibu, “Bwana, tuondoke twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. (aiōnios g166)
I odpowiedział mu Szymon Piotr: Panie! do kogóż pójdziemy? Ty masz słowa żywota wiecznego; (aiōnios g166)
69 Tunaamini na kujua kuwa wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu.”
A myśmy uwierzyli i poznali, żeś ty jest Chrystus, on Syn Boga żywego.
70 Ndipo Yesu akajibu, “Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Lakini mmoja wenu ni ibilisi.”
Odpowiedział im Jezus: Izalim ja nie dwunastu was obrał? a jeden z was jest dyjabeł.
71 (Hapa alikuwa anasema juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskariote. Ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili, ndiye ambaye baadaye angemsaliti Yesu.)
A to mówił o Judaszu, synu Szymona, Iszkaryjocie; bo go ten wydać miał, będąc jednym z onych dwunastu.

< Yohana 6 >