< Yohana 6 >
1 Baada ya haya, Yesu alikwenda ngʼambo ya Bahari ya Galilaya, ambayo pia huitwa Bahari ya Tiberia.
After these things Jesus went away to the other side of the sea of Galilee, which is [the sea] of Tiberias.
2 Umati mkubwa wa watu uliendelea kumfuata, kwa sababu waliona ishara nyingi za miujiza alizofanya kwa wagonjwa.
And a great multitude followed him, because they beheld the signs which he did on them that were sick.
3 Kisha Yesu akapanda mlimani akaketi huko pamoja na wanafunzi wake.
And Jesus went up into the mountain, and there he sat with his disciples.
4 Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
Now the passover, the feast of the Jews, was at hand.
5 Yesu alipotazama na kuuona ule umati mkubwa wa watu ukimjia, akamwambia Filipo, “Tutanunua wapi mikate ili watu hawa wale?”
Jesus therefore lifting up his eyes, and seeing that a great multitude cometh unto him, saith unto Philip, Whence are we to buy bread, that these may eat?
6 Aliuliza swali hili kumpima, kwa maana alishajua la kufanya.
And this he said to prove him: for he himself knew what he would do.
7 Filipo akamjibu, “Hata fedha kiasi cha dinari mia mbili, hazitoshi kununua mikate ya kuwapa watu hawa ili kila mtu apate kidogo.”
Philip answered him, Two hundred pennyworth of bread is not sufficient for them, that every one may take a little.
8 Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, ndugu yake Simoni Petro, akamwambia,
One of his disciples, Andrew, Simon Peter’s brother, saith unto him,
9 “Hapa kuna mvulana mmoja mwenye mikate mitano ya shayiri na samaki wawili wadogo. Lakini hivi vitatosha nini kwa umati huu wote?”
There is a lad here, which hath five barley loaves, and two fishes: but what are these among so many?
10 Yesu akasema, “Waketisheni watu chini.” Palikuwa na majani mengi katika eneo lile, nao watu wakaketi. Palikuwa na wanaume wapatao 5,000.
Jesus said, Make the people sit down. Now there was much grass in the place. So the men sat down, in number about five thousand.
11 Ndipo Yesu akachukua ile mikate, akamshukuru Mungu na kuwagawia wale watu waliokuwa wameketi. Akafanya vivyo hivyo na wale samaki. Kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
Jesus therefore took the loaves; and having given thanks, he distributed to them that were set down; likewise also of the fishes as much as they would.
12 Watu wote walipokwisha kula na kushiba, akawaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vilivyobaki vya ile mikate, kisipotee chochote.”
And when they were filled, he saith unto his disciples, Gather up the broken pieces which remain over, that nothing be lost.
13 Hivyo wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vya ile mikate mitano ya shayiri na samaki wale wawili wadogo vilivyobakishwa na waliokula.
So they gathered them up, and filled twelve baskets with broken pieces from the five barley loaves, which remained over unto them that had eaten.
14 Baada ya watu kuona muujiza ule Yesu aliofanya, walianza kusema, “Hakika huyu ndiye Nabii ajaye ulimwenguni!”
When therefore the people saw the sign which he did, they said, This is of a truth the prophet that cometh into the world.
15 Yesu akijua kwamba walitaka kuja kumfanya awe mfalme wao, kwa nguvu, akajitenga nao akaenda milimani peke yake.
Jesus therefore perceiving that they were about to come and take him by force, to make him king, withdrew again into the mountain himself alone.
16 Ilipofika jioni, wanafunzi wake waliteremka kwenda baharini.
And when evening came, his disciples went down unto the sea;
17 Wakaingia kwenye mashua, wakaanza kuvuka bahari kwenda Kapernaumu. Wakati huu kulikuwa tayari giza na Yesu alikuwa hajajumuika nao.
and they entered into a boat, and were going over the sea unto Capernaum. And it was now dark, and Jesus had not yet come to them.
18 Bahari ikachafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
And the sea was rising by reason of a great wind that blew.
19 Wanafunzi walipokuwa wamekwenda mwendo wa karibu maili tatu au nne, walimwona Yesu akitembea juu ya maji akikaribia mashua, nao wakaogopa sana.
When therefore they had rowed about five and twenty or thirty furlongs, they behold Jesus walking on the sea, and drawing nigh unto the boat: and they were afraid.
20 Lakini Yesu akawaambia, “Ni mimi. Msiogope.”
But he saith unto them, It is I; be not afraid.
21 Ndipo wakamkaribisha kwa furaha ndani ya mashua, na mara wakafika ufuoni walikokuwa wakienda.
They were willing therefore to receive him into the boat: and straightway the boat was at the land whither they were going.
22 Siku iliyofuata, wale watu waliokuwa wamebaki ngʼambo waliona kwamba palikuwepo na mashua moja tu na kwamba Yesu hakuwa ameondoka pamoja na wanafunzi wake, ila walikuwa wameondoka peke yao.
On the morrow the multitude which stood on the other side of the sea saw that there was none other boat there, save one, and that Jesus entered not with his disciples into the boat, but [that] his disciples went away alone
23 Lakini zikaja mashua nyingine kutoka Tiberia zikafika karibu na mahali pale walipokula mikate baada ya Bwana kumshukuru Mungu.
(howbeit there came boats from Tiberias nigh unto the place where they ate the bread after the Lord had given thanks):
24 Mara wale watu wakatambua kwamba Yesu hakuwepo hapo, wala wanafunzi wake. Wakaingia kwenye mashua hizo, wakaenda Kapernaumu ili kumtafuta Yesu.
when the multitude therefore saw that Jesus was not there, neither his disciples, they themselves got into the boats, and came to Capernaum, seeking Jesus.
25 Walipomkuta Yesu ngʼambo ya bahari wakamuuliza, “Rabi, umefika lini huku?”
And when they found him on the other side of the sea, they said unto him, Rabbi, when camest thou hither?
26 Yesu akawajibu, “Amin, amin nawaambia, ninyi hamnitafuti kwa kuwa mliona ishara na miujiza, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
Jesus answered them and said, Verily, verily, I say unto you, Ye seek me, not because ye saw signs, but because ye ate of the loaves, and were filled.
27 Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba amemtia muhuri.” (aiōnios )
Work not for the meat which perisheth, but for the meat which abideth unto eternal life, which the Son of man shall give unto you: for him the Father, [even] God, hath sealed. (aiōnios )
28 Ndipo wakamuuliza, “Tufanye nini ili tupate kuitenda kazi ya Mungu?”
They said therefore unto him, What must we do, that we may work the works of God?
29 Yesu akawajibu, “Kazi ya Mungu ndiyo hii: Mwaminini yeye aliyetumwa naye.”
Jesus answered and said unto them, This is the work of God, that ye believe on him whom he hath sent.
30 Hivyo wakamuuliza, “Utafanya ishara gani ya muujiza, ili tuione tukuamini? Utafanya jambo gani?
They said therefore unto him, What then doest thou for a sign, that we may see, and believe thee? what workest thou?
31 Baba zetu walikula mana jangwani, kama ilivyoandikwa, ‘Aliwapa mikate kutoka mbinguni ili wale.’”
Our fathers ate the manna in the wilderness; as it is written, He gave them bread out of heaven to eat.
32 Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, si Mose aliyewapa mikate kutoka mbinguni, bali Baba yangu ndiye anawapa mkate wa kweli kutoka mbinguni.
Jesus therefore said unto them, Verily, verily, I say unto you, It was not Moses that gave you the bread out of heaven; but my Father giveth you the true bread out of heaven.
33 Kwa maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.”
For the bread of God is that which cometh down out of heaven, and giveth life unto the world.
34 Wakamwambia, “Bwana, kuanzia sasa tupatie huo mkate siku zote.”
They said therefore unto him, Lord, evermore give us this bread.
35 Yesu akawaambia, “Mimi ndimi mkate wa uzima. Yeye ajaye kwangu, hataona njaa kamwe na yeye aniaminiye, hataona kiu kamwe.
Jesus said unto them, I am the bread of life: he that cometh to me shall not hunger, and he that believeth on me shall never thirst.
36 Lakini kama nilivyowaambia, mmeniona lakini bado hamwamini.
But I said unto you, that ye have seen me, and yet believe not.
37 Wale wote anipao Baba watakuja kwangu na yeyote ajaye kwangu, sitamfukuzia nje kamwe.
All that which the Father giveth me shall come unto me; and him that cometh to me I will in no wise cast out.
38 Kwa kuwa nimeshuka kutoka mbinguni si ili kufanya mapenzi yangu, bali mapenzi yake yeye aliyenituma.
For I am come down from heaven, not to do mine own will, but the will of him that sent me.
39 Haya ndiyo mapenzi yake yeye aliyenituma, kwamba, nisimpoteze hata mmoja wa wale alionipa, bali niwafufue siku ya mwisho.
And this is the will of him that sent me, that of all that which he hath given me I should lose nothing, but should raise it up at the last day.
40 Kwa maana mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mmoja amtazamaye, Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele, nami nitawafufua siku ya mwisho.” (aiōnios )
For this is the will of my Father, that every one that beholdeth the Son, and believeth on him, should have eternal life; and I will raise him up at the last day. (aiōnios )
41 Wayahudi wakaanza kunungʼunika kwa kuwa alisema, “Mimi ndimi mkate ulioshuka kutoka mbinguni.”
The Jews therefore murmured concerning him, because he said, I am the bread which came down out of heaven.
42 Wakasema, “Huyu si Yesu, mwana wa Yosefu, ambaye baba yake na mama yake tunawajua? Anawezaje basi sasa kusema, ‘Nimeshuka kutoka mbinguni’?”
And they said, Is not this Jesus, the son of Joseph, whose father and mother we know? how doth he now say, I am come down out of heaven?
43 Hivyo Yesu akawaambia, “Acheni kunungʼunikiana ninyi kwa ninyi.
Jesus answered and said unto them, Murmur not among yourselves.
44 Hakuna mtu awezaye kuja kwangu kama asipovutwa na Baba aliyenituma, nami nitamfufua siku ya mwisho.
No man can come to me, except the Father which sent me draw him: and I will raise him up in the last day.
45 Imeandikwa katika Manabii, ‘Wote watafundishwa na Mungu.’ Yeyote amsikilizaye Baba na kujifunza kutoka kwake, huyo huja kwangu.
It is written in the prophets, And they shall all be taught of God. Every one that hath heard from the Father, and hath learned, cometh unto me.
46 Hakuna mtu yeyote aliyemwona Baba isipokuwa yeye atokaye kwa Mungu, yeye ndiye peke yake aliyemwona Baba.
Not that any man hath seen the Father, save he which is from God, he hath seen the Father.
47 Amin, amin nawaambia, yeye anayeamini anao uzima wa milele. (aiōnios )
Verily, verily, I say unto you, He that believeth hath eternal life. (aiōnios )
48 Mimi ni mkate wa uzima.
I am the bread of life.
49 Baba zenu walikula mana jangwani, lakini wakafa.
Your fathers did eat the manna in the wilderness, and they died.
50 Lakini hapa kuna mkate utokao mbinguni, ambao mtu yeyote akiula, hatakufa.
This is the bread which cometh down out of heaven, that a man may eat thereof, and not die.
51 Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu yeyote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.” (aiōn )
I am the living bread which came down out of heaven: if any man eat of this bread, he shall live for ever: yea and the bread which I will give is my flesh, for the life of the world. (aiōn )
52 Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?”
The Jews therefore strove one with another, saying, How can this man give us his flesh to eat?
53 Hivyo Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.
Jesus therefore said unto them, Verily, verily, I say unto you, Except ye eat the flesh of the Son of man and drink his blood, ye have not life in yourselves.
54 Mtu yeyote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho. (aiōnios )
He that eateth my flesh and drinketh my blood hath eternal life; and I will raise him up at the last day. (aiōnios )
55 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
For my flesh is meat indeed, and my blood is drink indeed.
56 Yeyote alaye mwili wangu na kunywa damu yangu, atakaa ndani yangu nami nitakaa ndani yake.
He that eateth my flesh and drinketh my blood abideth in me, and I in him.
57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, na kama nami ninavyoishi kwa sababu ya Baba, hivyo anilaye mimi ataishi kwa sababu yangu.
As the living Father sent me, and I live because of the Father; so he that eateth me, he also shall live because of me.
58 Huu ndio mkate ushukao kutoka mbinguni, si kama ule mkate baba zenu waliokula nao wakafa. Lakini yeye aulaye mkate huu ataishi milele.” (aiōn )
This is the bread which came down out of heaven: not as the fathers did eat, and died: he that eateth this bread shall live for ever. (aiōn )
59 Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika sinagogi huko Kapernaumu.
These things said he in the synagogue, as he taught in Capernaum.
60 Wengi wa wafuasi wake waliposikia jambo hili wakasema, “Mafundisho haya ni magumu. Ni nani awezaye kuyapokea?”
Many therefore of his disciples, when they heard [this], said, This is a hard saying; who can hear it?
61 Yesu alipojua kwamba wafuasi wake wananungʼunika kuhusu mafundisho yake, akawaambia, “Je, jambo hili limewaudhi?
But Jesus knowing in himself that his disciples murmured at this, said unto them, Doth this cause you to stumble?
62 Ingekuwaje basi kama mngemwona Mwana wa Adamu akipaa kwenda zake huko alipokuwa kwanza?
[What] then if ye should behold the Son of man ascending where he was before?
63 Roho ndiye atiaye uzima, mwili haufai kitu. Maneno haya niliyowaambia ni Roho tena ni uzima.
It is the spirit that quickeneth; the flesh profiteth nothing: the words that I have spoken unto you are spirit, and are life.
64 Lakini baadhi yenu hamwamini.” Kwa maana Yesu alifahamu tangu mwanzo wale ambao hawangemwamini miongoni mwao na yule ambaye angemsaliti.
But there are some of you that believe not. For Jesus knew from the beginning who they were that believed not, and who it was that should betray him.
65 Akaendelea kusema, “Hii ndiyo sababu niliwaambia kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.”
And he said, For this cause have I said unto you, that no man can come unto me, except it be given unto him of the Father.
66 Tangu wakati huo wafuasi wake wengi wakarejea nyuma wakaacha kumfuata.
Upon this many of his disciples went back, and walked no more with him.
67 Hivyo Yesu akawauliza wale wanafunzi wake kumi na wawili, “Je, ninyi pia mnataka kuondoka?”
Jesus said therefore unto the twelve, Would ye also go away?
68 Simoni Petro akamjibu, “Bwana, tuondoke twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. (aiōnios )
Simon Peter answered him, Lord, to whom shall we go? thou hast the words of eternal life. (aiōnios )
69 Tunaamini na kujua kuwa wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu.”
And we have believed and know that thou art the Holy One of God.
70 Ndipo Yesu akajibu, “Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Lakini mmoja wenu ni ibilisi.”
Jesus answered them, Did not I choose you the twelve, and one of you is a devil?
71 (Hapa alikuwa anasema juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskariote. Ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili, ndiye ambaye baadaye angemsaliti Yesu.)
Now he spake of Judas [the son] of Simon Iscariot, for he it was that should betray him, [being] one of the twelve.