< Yohana 6 >

1 Baada ya haya, Yesu alikwenda ngʼambo ya Bahari ya Galilaya, ambayo pia huitwa Bahari ya Tiberia.
After these thinges, Iesus went his way ouer the sea of Galile, which is Tiberias.
2 Umati mkubwa wa watu uliendelea kumfuata, kwa sababu waliona ishara nyingi za miujiza alizofanya kwa wagonjwa.
And a great multitude followed him, because they sawe his miracles, which hee did on them that were diseased.
3 Kisha Yesu akapanda mlimani akaketi huko pamoja na wanafunzi wake.
Then Iesus went vp into a mountaine, and there he sate with his disciples.
4 Pasaka ya Wayahudi ilikuwa imekaribia.
Now the Passeouer, a feast of the Iewes, was neere.
5 Yesu alipotazama na kuuona ule umati mkubwa wa watu ukimjia, akamwambia Filipo, “Tutanunua wapi mikate ili watu hawa wale?”
Then Iesus lift vp his eyes, and seeing that a great multitude came vnto him, hee sayde vnto Philippe, Whence shall we buy breade, that these might eate?
6 Aliuliza swali hili kumpima, kwa maana alishajua la kufanya.
(And this he sayde to prooue him: for hee himselfe knewe what he would doe.)
7 Filipo akamjibu, “Hata fedha kiasi cha dinari mia mbili, hazitoshi kununua mikate ya kuwapa watu hawa ili kila mtu apate kidogo.”
Philippe answered him, Two hundreth penie worth of bread is not sufficient for them, that euery one of them may take a litle.
8 Mmoja wa wanafunzi wake aitwaye Andrea, ndugu yake Simoni Petro, akamwambia,
Then saide vnto him one of his disciples, Andrew, Simon Peters brother,
9 “Hapa kuna mvulana mmoja mwenye mikate mitano ya shayiri na samaki wawili wadogo. Lakini hivi vitatosha nini kwa umati huu wote?”
There is a little boy heere, which hath fiue barlie loaues, and two fishes: but what are they among so many?
10 Yesu akasema, “Waketisheni watu chini.” Palikuwa na majani mengi katika eneo lile, nao watu wakaketi. Palikuwa na wanaume wapatao 5,000.
And Iesus saide, Make ye people sit downe. (Nowe there was much grasse in that place.) Then the men sate downe in nomber, about fiue thousande.
11 Ndipo Yesu akachukua ile mikate, akamshukuru Mungu na kuwagawia wale watu waliokuwa wameketi. Akafanya vivyo hivyo na wale samaki. Kila mtu akapata kadiri alivyotaka.
And Iesus tooke the bread, and gaue thanks, and gaue to the disciples, and the disciples, to them that were set downe: and likewise of the fishes as much as they would.
12 Watu wote walipokwisha kula na kushiba, akawaambia wanafunzi wake, “Kusanyeni vipande vilivyobaki vya ile mikate, kisipotee chochote.”
And when they were satisfied, he said vnto his disciples, Gather vp the broken meat which remaineth, that nothing be lost.
13 Hivyo wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili kwa vipande vya ile mikate mitano ya shayiri na samaki wale wawili wadogo vilivyobakishwa na waliokula.
Then they gathered it together, and filled twelue baskets with the broken meat of the fiue barly loaues, which remained vnto them that had eaten.
14 Baada ya watu kuona muujiza ule Yesu aliofanya, walianza kusema, “Hakika huyu ndiye Nabii ajaye ulimwenguni!”
Then the men, when they had seene the miracle that Iesus did, saide, This is of a trueth that Prophet that should come into the world.
15 Yesu akijua kwamba walitaka kuja kumfanya awe mfalme wao, kwa nguvu, akajitenga nao akaenda milimani peke yake.
When Iesus therfore perceiued that they would come, and take him to make him a King, hee departed againe into a mountaine himselfe alone.
16 Ilipofika jioni, wanafunzi wake waliteremka kwenda baharini.
When euen was nowe come, his disciples went downe vnto the sea,
17 Wakaingia kwenye mashua, wakaanza kuvuka bahari kwenda Kapernaumu. Wakati huu kulikuwa tayari giza na Yesu alikuwa hajajumuika nao.
And entred into a shippe, and went ouer the sea, towardes Capernaum: and nowe it was darke, and Iesus was not come to them.
18 Bahari ikachafuka kwa sababu upepo mkali ulikuwa unavuma.
And the Sea arose with a great winde that blewe.
19 Wanafunzi walipokuwa wamekwenda mwendo wa karibu maili tatu au nne, walimwona Yesu akitembea juu ya maji akikaribia mashua, nao wakaogopa sana.
And when they had rowed about fiue and twentie, or thirtie furlongs, they sawe Iesus walking on the sea, and drawing neere vnto the ship: so they were afraide.
20 Lakini Yesu akawaambia, “Ni mimi. Msiogope.”
But he said vnto them, It is I: be not afraid.
21 Ndipo wakamkaribisha kwa furaha ndani ya mashua, na mara wakafika ufuoni walikokuwa wakienda.
Then willingly they receiued him into the ship, and the ship was by and by at the lande, whither they went.
22 Siku iliyofuata, wale watu waliokuwa wamebaki ngʼambo waliona kwamba palikuwepo na mashua moja tu na kwamba Yesu hakuwa ameondoka pamoja na wanafunzi wake, ila walikuwa wameondoka peke yao.
The day following, the people which stoode on the other side of the sea, saw that there was none other ship there, saue that one, whereinto his disciples were entred, and that Iesus went not with his disciples in the ship, but that his disciples were gone alone,
23 Lakini zikaja mashua nyingine kutoka Tiberia zikafika karibu na mahali pale walipokula mikate baada ya Bwana kumshukuru Mungu.
And that there came other ships from Tiberias neere vnto the place where they ate the bread, after the Lord had giuen thankes.
24 Mara wale watu wakatambua kwamba Yesu hakuwepo hapo, wala wanafunzi wake. Wakaingia kwenye mashua hizo, wakaenda Kapernaumu ili kumtafuta Yesu.
Nowe when the people sawe that Iesus was not there, neither his disciples, they also tooke shipping, and came to Capernaum, seeking for Iesus.
25 Walipomkuta Yesu ngʼambo ya bahari wakamuuliza, “Rabi, umefika lini huku?”
And when they had founde him on the other side of the sea, they sayde vnto him, Rabbi, when camest thou hither?
26 Yesu akawajibu, “Amin, amin nawaambia, ninyi hamnitafuti kwa kuwa mliona ishara na miujiza, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
Iesus answered them; and sayde, Verely, verely I say vnto you, ye seeke me not because ye sawe the miracles, but because yee ate of ye loaues, and were filled.
27 Msishughulikie chakula kiharibikacho, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele, ambacho Mwana wa Adamu atawapa. Yeye ndiye ambaye Mungu Baba amemtia muhuri.” (aiōnios g166)
Labour not for ye meate which perisheth, but for the meate that endureth vnto euerlasting life, which the Sonne of man shall giue vnto you: for him hath God the Father sealed. (aiōnios g166)
28 Ndipo wakamuuliza, “Tufanye nini ili tupate kuitenda kazi ya Mungu?”
Then sayde they vnto him, What shall we doe, that we might worke the workes of God?
29 Yesu akawajibu, “Kazi ya Mungu ndiyo hii: Mwaminini yeye aliyetumwa naye.”
Iesus answered, and sayde vnto them, This is the woorke of God, that yee beleeue in him, whome he hath sent.
30 Hivyo wakamuuliza, “Utafanya ishara gani ya muujiza, ili tuione tukuamini? Utafanya jambo gani?
They sayde therefore vnto him, What signe shewest thou then, that we may see it, and beleeue thee? what doest thou woorke?
31 Baba zetu walikula mana jangwani, kama ilivyoandikwa, ‘Aliwapa mikate kutoka mbinguni ili wale.’”
Our fathers did eate Manna in the desart, as it is written, Hee gaue them bread from heauen to eate.
32 Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, si Mose aliyewapa mikate kutoka mbinguni, bali Baba yangu ndiye anawapa mkate wa kweli kutoka mbinguni.
Then Iesus said vnto them, Verely, verely I say vnto you, Moses gaue you not that bread from heauen, but my Father giueth you that true bread from heauen.
33 Kwa maana mkate wa Mungu ni yule ashukaye kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.”
For the breade of God is hee which commeth downe from heauen, and giueth life vnto the world.
34 Wakamwambia, “Bwana, kuanzia sasa tupatie huo mkate siku zote.”
Then they said vnto him, Lord, euermore giue vs this bread.
35 Yesu akawaambia, “Mimi ndimi mkate wa uzima. Yeye ajaye kwangu, hataona njaa kamwe na yeye aniaminiye, hataona kiu kamwe.
And Iesus saide vnto them, I am that bread of life: he that commeth to me, shall not hunger, and he that beleeueth in me, shall neuer thirst.
36 Lakini kama nilivyowaambia, mmeniona lakini bado hamwamini.
But I said vnto you, that ye also haue seene me, and beleeue not.
37 Wale wote anipao Baba watakuja kwangu na yeyote ajaye kwangu, sitamfukuzia nje kamwe.
All that the Father giueth me, shall come to mee: and him that commeth to me, I cast not away.
38 Kwa kuwa nimeshuka kutoka mbinguni si ili kufanya mapenzi yangu, bali mapenzi yake yeye aliyenituma.
For I came downe from heauen, not to do mine owne wil, but his wil which hath sent me.
39 Haya ndiyo mapenzi yake yeye aliyenituma, kwamba, nisimpoteze hata mmoja wa wale alionipa, bali niwafufue siku ya mwisho.
And this is the Fathers will which hath sent mee, that of all which hee hath giuen mee, I should lose nothing, but shoulde raise it vp againe at the last day.
40 Kwa maana mapenzi ya Baba yangu ni kwamba kila mmoja amtazamaye, Mwana na kumwamini awe na uzima wa milele, nami nitawafufua siku ya mwisho.” (aiōnios g166)
And this is the will of him that sent mee, that euery man which seeth the Sonne, and beleeueth in him, should haue euerlasting life: and I will raise him vp at the last day. (aiōnios g166)
41 Wayahudi wakaanza kunungʼunika kwa kuwa alisema, “Mimi ndimi mkate ulioshuka kutoka mbinguni.”
The Iewes then murmured at him because hee sayde, I am that bread, which is come downe from heauen.
42 Wakasema, “Huyu si Yesu, mwana wa Yosefu, ambaye baba yake na mama yake tunawajua? Anawezaje basi sasa kusema, ‘Nimeshuka kutoka mbinguni’?”
And they said, Is not this Iesus that sonne of Ioseph, whose father and mother wee knowe? howe then sayth he, I came downe from heauen?
43 Hivyo Yesu akawaambia, “Acheni kunungʼunikiana ninyi kwa ninyi.
Iesus then answered, and saide vnto them, Murmure not among your selues.
44 Hakuna mtu awezaye kuja kwangu kama asipovutwa na Baba aliyenituma, nami nitamfufua siku ya mwisho.
No man can come to mee, except the Father, which hath sent mee, drawe him: and I will raise him vp at the last day.
45 Imeandikwa katika Manabii, ‘Wote watafundishwa na Mungu.’ Yeyote amsikilizaye Baba na kujifunza kutoka kwake, huyo huja kwangu.
It is written in the Prophetes, And they shalbe al taught of God. Euery man therefore that hath heard, and hath learned of the Father, commeth vnto me:
46 Hakuna mtu yeyote aliyemwona Baba isipokuwa yeye atokaye kwa Mungu, yeye ndiye peke yake aliyemwona Baba.
Not that any man hath seene the Father, saue hee which is of God, hee hath seene the Father.
47 Amin, amin nawaambia, yeye anayeamini anao uzima wa milele. (aiōnios g166)
Verely, verely I say vnto you, hee that beleeueth in me, hath euerlasting life. (aiōnios g166)
48 Mimi ni mkate wa uzima.
I am that bread of life.
49 Baba zenu walikula mana jangwani, lakini wakafa.
Your fathers did eate Manna in the wildernesse, and are dead.
50 Lakini hapa kuna mkate utokao mbinguni, ambao mtu yeyote akiula, hatakufa.
This is that breade, which commeth downe from heauen, that hee which eateth of it, shoulde not die.
51 Mimi ni mkate wa uzima ule uliotoka mbinguni. Mtu yeyote akiula mkate huu, ataishi milele. Mkate huu ni mwili wangu, ambao nitautoa kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.” (aiōn g165)
I am that liuing breade, which came downe from heauen: if any man eate of this breade, hee shall liue for euer: and the bread that I will giue, is my flesh, which I will giue for the life of the world. (aiōn g165)
52 Ndipo Wayahudi wakaanza kuhojiana vikali wao kwa wao wakisema, “Mtu huyu awezaje kutupatia mwili wake tuule?”
Then the Iewes stroue among themselues, saying, Howe can this man giue vs his flesh to eate?
53 Hivyo Yesu akawaambia, “Amin, amin nawaambia, msipoula mwili wa Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.
Then Iesus saide vnto them, Verely, verely I say vnto you, Except yee eate the flesh of the Sonne of man, and drinke his blood, yee haue no life in you.
54 Mtu yeyote aulaye mwili wangu na kunywa damu yangu, anao uzima wa milele. Nami nitamfufua siku ya mwisho. (aiōnios g166)
Whosoeuer eateth my flesh, and drinketh my blood, hath eternall life, and I will raise him vp at the last day. (aiōnios g166)
55 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
For my flesh is meat in deede, and my blood is drinke in deede.
56 Yeyote alaye mwili wangu na kunywa damu yangu, atakaa ndani yangu nami nitakaa ndani yake.
Hee that eateth my flesh, and drinketh my blood, dwelleth in me, and I in him.
57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, na kama nami ninavyoishi kwa sababu ya Baba, hivyo anilaye mimi ataishi kwa sababu yangu.
As that liuing Father hath sent me, so liue I by the Father, and he that eateth me, euen he shall liue by me.
58 Huu ndio mkate ushukao kutoka mbinguni, si kama ule mkate baba zenu waliokula nao wakafa. Lakini yeye aulaye mkate huu ataishi milele.” (aiōn g165)
This is that bread which came downe from heauen: not as your fathers haue eaten Manna, and are deade. Hee that eateth of this bread, shall liue for euer. (aiōn g165)
59 Yesu alisema maneno haya alipokuwa akifundisha katika sinagogi huko Kapernaumu.
These things spake he in the Synagogue, as he taught in Capernaum.
60 Wengi wa wafuasi wake waliposikia jambo hili wakasema, “Mafundisho haya ni magumu. Ni nani awezaye kuyapokea?”
Many therefore of his disciples (when they heard this) sayde, This is an hard saying: who can heare it?
61 Yesu alipojua kwamba wafuasi wake wananungʼunika kuhusu mafundisho yake, akawaambia, “Je, jambo hili limewaudhi?
But Iesus knowing in himselfe, that his disciples murmured at this, saide vnto them, Doeth this offend you?
62 Ingekuwaje basi kama mngemwona Mwana wa Adamu akipaa kwenda zake huko alipokuwa kwanza?
What then if yee should see that Sonne of man ascend vp where he was before?
63 Roho ndiye atiaye uzima, mwili haufai kitu. Maneno haya niliyowaambia ni Roho tena ni uzima.
It is the spirite that quickeneth: the flesh profiteth nothing: the woordes that I speake vnto you, are spirite and life.
64 Lakini baadhi yenu hamwamini.” Kwa maana Yesu alifahamu tangu mwanzo wale ambao hawangemwamini miongoni mwao na yule ambaye angemsaliti.
But there are some of you that beleeue not: for Iesus knewe from the beginning, which they were that beleeued not, and who shoulde betray him.
65 Akaendelea kusema, “Hii ndiyo sababu niliwaambia kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.”
And hee saide, Therefore saide I vnto you, that no man can come vnto mee, except it be giuen vnto him of my Father.
66 Tangu wakati huo wafuasi wake wengi wakarejea nyuma wakaacha kumfuata.
From that time, many of his disciples went backe, and walked no more with him.
67 Hivyo Yesu akawauliza wale wanafunzi wake kumi na wawili, “Je, ninyi pia mnataka kuondoka?”
Then sayde Iesus to the twelue, Will yee also goe away?
68 Simoni Petro akamjibu, “Bwana, tuondoke twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele. (aiōnios g166)
Then Simon Peter answered him, Master, to whome shall we goe? thou hast the wordes of eternall life: (aiōnios g166)
69 Tunaamini na kujua kuwa wewe ndiwe Aliye Mtakatifu wa Mungu.”
And we beleeue and knowe that thou art that Christ that Sonne of the liuing God.
70 Ndipo Yesu akajibu, “Je, sikuwachagua ninyi kumi na wawili? Lakini mmoja wenu ni ibilisi.”
Iesus answered them, Haue not I chosen you twelue, and one of you is a deuill?
71 (Hapa alikuwa anasema juu ya Yuda, mwana wa Simoni Iskariote. Ingawa alikuwa mmoja wa wale kumi na wawili, ndiye ambaye baadaye angemsaliti Yesu.)
Now he spake it of Iudas Iscariot the sonne of Simon: for hee it was that shoulde betraie him, though he was one of the twelue.

< Yohana 6 >