< Yohana 4 >

1 Mafarisayo wakasikia kwamba Yesu alikuwa anapata na kubatiza wanafunzi wengi zaidi kuliko Yohana,
Linu aho Jesu heziva kuti Mafarisi vava zuwi kuti avali kupanga ni kukoloveza valutiwa vangi kuhita Johani
2 ingawa kwa kweli si Yesu mwenyewe aliyekuwa akibatiza, ila ni wanafunzi wake.
(nangati kuti Jesu iye mwine kena avali kukoloveza, kono ivali valutiwa vakwate),
3 Bwana alipojua mambo haya, aliondoka Uyahudi akarudi tena Galilaya.
chazwa mwa Judeya ni kuvola hape kwa Galileya.
4 Wakati huo ilimlazimu apitie Samaria.
Kono ivali iswanero kwali ku hita mwa Samariya.
5 Akafika kwenye mji mmoja wa Samaria uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa mwanawe Yosefu.
Cwale cha keza mwi toropo ya Samariya, i sumpwa Sychari, hembali ni chivaka chevu icho Jakovo ava here kumwane Josefa.
6 Huko ndiko kulikokuwa na kile kisima cha Yakobo. Naye Yesu alikuwa amechoka kwa kuwa alikuwa ametoka safarini. Akaketi karibu na hicho kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
Chisima cha Jakovo puchivena aho. Jesu avali kukatere kuzwa ku musipiri wakwe ni kwiza ha chisima. Chi ivali kuchutire kwinako ye chitengu zana.
7 Mwanamke mmoja Msamaria akaja kuteka maji, Yesu akamwambia, “Naomba maji ninywe.”
Mukulwakazi wa Musamariya ava kezi kuku teka menzi, mi Jesu cha wamba kwali, “Nihe ku menzi ni nywe.”
8 (Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
Kakuti valutwana vakwe vavali kuyendente mukati ke toropo kuku wula zilyo.
9 Yule mwanamke Msamaria akamjibu, “Wewe ni Myahudi na mimi ni Msamaria. Yawezekanaje uniombe nikupe maji ya kunywa?” (Wayahudi walikuwa hawashirikiani kabisa na Wasamaria.)
Yaho mukulwakazi wa Musamariya chata kwali, “Kuwoleka vule kuti iwe, kuva Mujunda, ukumbira ime, kuva mukulwakazi wa Musamariya, kuchimwi cho kunywa?” Kakuli Majunda kavana cho kupanga ni Masamariya.
10 Yesu akajibu akamwambia, “Kama ungelijua karama ya Mungu, naye ni nani anayekuambia, Nipe maji ninywe, wewe ungelimwomba yeye, naye angelikupa maji yaliyo hai.”
Jesu che tava ni kumuta, “Kambe we ziva impo ya Ireeza, mi jeni uzu yo wamba kwako, 'Unihe cho kunwa; ni wa wola kumu kumbira, mi na wola kukuha, menzi a hala.”
11 Yule mwanamke akamjibu, “Bwana, wewe huna chombo cha kutekea maji na kisima hiki ni kirefu. Hayo maji ya uzima utayapata wapi?
Mukulwakazi chata kwali, “Mukwame, kawina chitekiso imi isima litungite. Ena kuhi cwale kowina menzi a hala?
12 Kwani wewe ni mkuu kuliko baba yetu Yakobo ambaye alitupatia kisima hiki, ambacho yeye pamoja na watoto wake na mifugo yake walikitumia?”
Kena umu kando, iwe, kuhita ishetu Jakovo, uzo ava tuhi chisima ni kunya mwateni iye mwine, nivane vulyo ni ñombe zavo?
13 Yesu akamjibu, “Kila mtu anayekunywa maji ya kisima hiki ataona kiu tena.
Jesu che tava ni kumu ta, “Yense yo nwa kwaya menzi mwa fwe inyota hape,
14 Lakini yeyote anywaye maji nitakayompa hataona kiu kamwe. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujika uzima wa milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
kono yense yo nwa kumenzi awo ite ni muhe kate na fwe inyota hape. Nihakuli, menzi ete ni muhe muave chisima chamezi mwali, kuvuvira ku vuhalo vusa mani.” (aiōn g165, aiōnios g166)
15 Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, tafadhali nipe maji hayo ili nisipate kiu tena na wala nisije tena hapa kuteka maji!”
Mukulwakazi chati kwali, “Mukwame, unihe aya menzi iri kuli nisiye ni kufwanga inyonta mi nisiye niku kezanga kunu kuku teka menzi.”
16 Yesu akamjibu, “Nenda ukamwite mumeo, uje naye hapa.”
Jesu chata kwali, “Yende, kasupe mwihyenu, mi ukavole kunu.”
17 Yule mwanamke akajibu, “Sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli kuwa huna mume.
Mukulwakazi chetava ni kumuti, “Kanina mukwame.”Jesu chetava, “Wina hande mukuwamba,”Kanina mwihyetu;
18 Kwa maana umeshakuwa na wanaume watano na mwanaume unayeishi naye sasa si mume wako! Umesema ukweli.”
kakuti uva vire ni vakwame vakuma ha minwe ye yanza, mi nozu yo wina naye hanu kanji mwihyenu. Chiwa wamba che niti.”
19 Yule mwanamke akasema, “Bwana, naona bila shaka wewe ni nabii.
Mukulwakazi cha wamba kwali, “Mukwame, Ni vona kuti umu porofita.
20 Baba zetu waliabudu kwenye mlima huu, lakini ninyi Wayahudi mnasema ni lazima tukaabudu huko Yerusalemu.”
Veshetu vavali kulaperera heli irundu, kono inwe muwamba kuti Jerusalema je chivaka uko vantu vaswanera ku laperela.”
21 Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala huko Yerusalemu.
Jesu chata kwali, “Uni zumine, mwanakazi, kuti i hola i kezite aho kamulapere Tayo kamba heli rundu kamba mwa Jerusalema.
22 Ninyi Wasamaria mnaabudu msichokijua. Sisi Wayahudi tunamwabudu Mungu tunayemjua kwa sababu wokovu unatoka kwa Wayahudi.
Inwe mulapera icho chimusezi. I swe tulapera chi twizi, kakuti ipuluso i zwirira kuMajuda.
23 Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta.
Niha kuva vulyo, I hola ikezite, imi ina hanu, aho valaperi ve niti kava lapere Tayo muluhuho ni mwi niti, kakuli Tayo u kwete kulola vantu vaswana vulyo kuva valaperi vakwe.
24 Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”
Ireeza luhuho, mi vantu vamulapera vaswanera kumu lapera muluhuho ni mwi niti.”
25 Yule mwanamke akamwambia, “Ninafahamu kwamba Masiya (aitwaye Kristo) anakuja. Yeye akija, atatueleza mambo yote.”
Mukulwakazi chati kwali, “Ni izi kuti Mesiya ukezite (uzo usupiwa Keresite). A ho hasana kakeze, keze a tutoloke zintu zonse kwetu.”
26 Yesu akamwambia, “Mimi ninayezungumza nawe, ndiye.”
Jesu chamuta, “Jeme uzu, yo kwete kuwamba kwako.”
27 Wakati huo wanafunzi wake wakarudi, wakashangaa sana kumwona akizungumza na mwanamke. Lakini hakuna aliyemuuliza, “Unataka nini kwake?” Au “Kwa nini unazungumza naye?”
Heyo inako valutwana vakwe chivaka vola. Hanu vavali ku komoketwe chinzi havali kuwamba ni mwanakazi, kono kakwina ava wambi, “Usaka nzi?”kamba “Chinzi hau wamba naye?”
28 Yule mwanamke akaacha mtungi wake, akarudi mjini akawaambia watu,
Cwale mukulwakazi chasiya i hemere lyakwe, ni kuvola mwi toropo, ni kuwamba kuvantu,
29 “Njooni mkamwone mtu aliyeniambia kila kitu nilichotenda! Je, yawezekana huyu ndiye Kristo?”
“Mwize, muvone mukwame wani wambira zintu zonse ziniva pangi. Uzu uswanera kuva iye Keresite, iwola kuva?”
30 Basi wakamiminika watu kutoka mjini wakamwendea Yesu.
Chiva siya itoporopo ni kukeza kwali.
31 Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wakimsihi, “Rabi, kula angalau chochote.”
Mwinako zana, varutwana vavali kumukumbira, nivati, “Rabbi, Lye.”
32 Lakini yeye akawajibu, “Mimi ninacho chakula ambacho ninyi hamkifahamu.”
Kono cha wamba kuvali, “Nina zilyo zo kulya inzo zimusezi chazo.”
33 Basi wanafunzi wakaanza kuulizana, “Kuna mtu ambaye amemletea chakula?”
Cwale varutwana chiva wambolisana kuvali vene, “Kakwina zumwi wa muletera zokulya, vamu letera?”
34 Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma na kuikamilisha kazi yake.
Jesu cha wamba kuvali, “Zilyo zangu ku panga itato yakwe uzo yava kani tumi ni kumana musevezi wa kwe.
35 Je, ninyi hamsemi, ‘Bado miezi minne tuvune?’ Inueni macho yenu myaangalie mashamba jinsi mazao yalivyo tayari kuvunwa!
Kamu wambi kuti, 'Kwina myezi imwi yone mi ikutulo jese ikeze'? Ni wamba kwenu, mulole kwi wulu ni kuvone mawa, kakuli chi alitukiseze kusizwa!
36 Mvunaji tayari anapokea mshahara wake, naye anakusanya mazao kwa ajili ya uzima wa milele. Ili yeye apandaye na yeye avunaye wafurahi pamoja. (aiōnios g166)
Uzo yo kwete kusiza u tambula i tuwero ni kukunganya misero yo vuhalo vusa mani, iri kuti uzo yo vyala nozo yo sinza va sangwe hamwina. (aiōnios g166)
37 Hivyo kule kusema, ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna,’ ni kweli kabisa.
Mowu muwambiro, 'Yenke ubyala, mi zumwi usinza; vuniti.
38 Niliwatuma mkavune mazao ambayo hamkupanda, wengine walifanya kazi ngumu, nanyi mmevuna faida ya taabu yao.”
Ni va mitumi kuku sinza inzo zisina muva severezi. Vamwi vava sevezi, mi muvengiri mumi sevezi yavo.”
39 Wasamaria wengi katika mji ule wakamwamini Yesu kwa sababu ya ushuhuda wa yule mwanamke alipowaambia kwamba, “Ameniambia kila kitu nilichotenda.”
Vungi bwa Masamariya mowuna muleneñi chiva zumina kwali vakeñi che vaka lyue ñusa lyo mukulwakazi lya paka, “Wani wambira zintu zonse izo zini vapangi.”
40 Hivyo wale Wasamaria walipomjia, wakamsihi akae kwao. Naye akakaa huko siku mbili.
Cwale Masamariya hava keza kwali, chiva muvuza kwikala navo, mi ave kali kwateni mazuva overe.
41 Kwa sababu ya neno lake, watu wengi wakaamini.
Mi vungi vomwi vuva zumini chevaka lya manzwi akwe.
42 Wakamwambia yule mwanamke, “Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu, bali kwa kuwa tumemsikia sisi wenyewe. Tumejua hakika kweli ya kwamba huyu ndiye Kristo, Mwokozi wa ulimwengu.”
Chiva wamba ku mwanakazi, “Katusizumini chevaka lyezo ziwawamba, kakuti iswe tuvene chitwa muzuwa, mi twizi kuti uzu luli chovuniti jo muhazi we kanda.”
43 Baada ya zile siku mbili, Yesu aliondoka kwenda Galilaya.
Hakumana awo mazuva o vere, Chazwa kwatenio ni kuya kwa Ngalileya.
44 (Basi Yesu mwenyewe alikuwa amesema kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.)
Kakuli Jesu iye mwina ava wambi kuti muporofita mwi kanda yakwe kakutekiwa.
45 Alipofika Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha, kwani walikuwa wameona yale aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa Sikukuu ya Pasaka. Kwa maana wao pia walikuwa wamehudhuria hiyo Sikukuu.
Hacha keza mwa Galileya, Mangalileya chi vamu tambula. Vava voni zintu zonse zava pangi mwa Jerusalema ha mukiti, kakuti navo vavali kuyendete kwateni.
46 Hivyo Yesu akaja tena mpaka Kana ya Galilaya, kule alikokuwa amebadili maji kuwa divai. Huko kulikuwepo na afisa mmoja wa mfalme, ambaye mwanawe alikuwa mgonjwa huko Kapernaumu.
Hanu chakeza hape mwa Kana mwa Ngalileya, umo mwava sanduli menzi i waine. Kuvena zumwi induna ili uzo mwane we chiswisu mwa Capenaume yavali kulwala.
47 Huyo mtu aliposikia kwamba Yesu alikuwa amewasili Galilaya kutoka Uyahudi, alimwendea na kumwomba ili aje kumponya mwanawe, aliyekuwa mgonjwa karibu ya kufa.
Aho heza kuzuwa kuti Jesu ava kezi kukazwa kwa Judeya kwiza kwa Galileya, Cha yenda kwa Jesu ni kuka mukumbira kuti akeze ni kuhoza mwane we chiswisu, ya chavali kwina hafuhi ni kutokwala.
48 Yesu akamwambia, “Ninyi watu msipoona ishara na miujiza kamwe hamtaamini.”
Jesu cwale cha wamba kwali, “Mbwita chi mwavona isupo ni makazo, kate muzumine.”
49 Yule afisa wa mfalme akamwambia, “Bwana, tafadhali shuka kabla mwanangu hajafa.”
Induna chati kwali, “Mukwame, wize kunu mwanangu naseni kufwa.”
50 Yesu akamjibu, “Enenda zako, mwanao yu hai.” Yule afisa akaamini yale maneno Yesu aliyomwambia, akaondoka akaenda zake.
Jesu chawamba kwali, “Yende. Mwanako we chiswisu uhala.”Mukwame ava zumini manzwi awo Jesu ava wambi kwali, mi chayenda kuzwa hateni.
51 Alipokuwa bado yuko njiani, akakutana na watumishi wake wakamwambia kwamba mwanawe yu mzima.
Havali kushetumuka, muhikana wakwe chamu katana, nawamba kuti mwanakwe we chiswisu avali kuhala.
52 Akawauliza saa ambayo alianza kupata nafuu. Wakamwambia, “Jana yapata saa saba, homa ilimwacha.”
Cwale chava vunza inako hatangira kuli zuwa hande. Chiva mwitava, Inzona mwinako ya musihali i fivere chiya musiya.”
53 Ndipo baba wa huyo mtoto akakumbuka kuwa huo ndio wakati ambapo Yesu alikuwa amemwambia, “Mwanao yu hai.” Kwa hiyo yeye pamoja na wote wa nyumbani mwake wakamwamini Yesu.
Cwale vensi chiva lemuha kuti ivali jiyona inako ina Jesu yava wambi kwali, “Mwanako we chiswisu uhala.”Cwale iye mwine niver zuvo yakwe yonse chiva zumina.
54 Hii ilikuwa ishara ya pili ambayo Yesu alifanya aliporudi Galilaya kutoka Uyahudi.
Iyi ivali ivali je makazo yo vuveri yava pangi Jesu hakazwa kwa Judeya kuya kwa Ngalileya.

< Yohana 4 >