< Yohana 4 >
1 Mafarisayo wakasikia kwamba Yesu alikuwa anapata na kubatiza wanafunzi wengi zaidi kuliko Yohana,
Therefore when the Lord knew, the pharisees had heard that Jesus made and baptized more disciples than John,
2 ingawa kwa kweli si Yesu mwenyewe aliyekuwa akibatiza, ila ni wanafunzi wake.
(though Jesus Himself did not baptize, but his disciples, )
3 Bwana alipojua mambo haya, aliondoka Uyahudi akarudi tena Galilaya.
He left Judea, and departed again into Galilee.
4 Wakati huo ilimlazimu apitie Samaria.
And as He must pass through the country of Samaria, He came to a Samaritan city called Sichar,
5 Akafika kwenye mji mmoja wa Samaria uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa mwanawe Yosefu.
near the piece of ground which Jacob gave to his son Joseph.
6 Huko ndiko kulikokuwa na kile kisima cha Yakobo. Naye Yesu alikuwa amechoka kwa kuwa alikuwa ametoka safarini. Akaketi karibu na hicho kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
And Jacob's well was there. Now Jesus was tired with his journey, and sat down at the well: and it was about the sixth hour of the day,
7 Mwanamke mmoja Msamaria akaja kuteka maji, Yesu akamwambia, “Naomba maji ninywe.”
when a woman of Samaria coming to draw water, Jesus saith unto her, Give me to drink.
8 (Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
(For his disciples were gone away to the city to buy food.)
9 Yule mwanamke Msamaria akamjibu, “Wewe ni Myahudi na mimi ni Msamaria. Yawezekanaje uniombe nikupe maji ya kunywa?” (Wayahudi walikuwa hawashirikiani kabisa na Wasamaria.)
But the Samaritan saith unto Him, How is it that thou who art a Jew askest drink of me, who am a Samaritan? for the Jews have no friendly intercourse with the Samaritans.
10 Yesu akajibu akamwambia, “Kama ungelijua karama ya Mungu, naye ni nani anayekuambia, Nipe maji ninywe, wewe ungelimwomba yeye, naye angelikupa maji yaliyo hai.”
Jesus answered and said unto her, If thou knewest the gift of God, and who it is that saith unto thee, Give me to drink; thou wouldst have asked of Him, and He would have given thee living water.
11 Yule mwanamke akamjibu, “Bwana, wewe huna chombo cha kutekea maji na kisima hiki ni kirefu. Hayo maji ya uzima utayapata wapi?
The woman saith unto Him, Sir, thou hast nothing to draw with, and the well is deep: whence then hast thou the living water?
12 Kwani wewe ni mkuu kuliko baba yetu Yakobo ambaye alitupatia kisima hiki, ambacho yeye pamoja na watoto wake na mifugo yake walikitumia?”
Art thou greater than our father Jacob, who gave us the well, and drank of it himself, and his children, and his cattle?
13 Yesu akamjibu, “Kila mtu anayekunywa maji ya kisima hiki ataona kiu tena.
Jesus answered and said unto her, Whosoever drinketh of this water, will thirst again;
14 Lakini yeyote anywaye maji nitakayompa hataona kiu kamwe. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujika uzima wa milele.” (aiōn , aiōnios )
but he that drinketh of the water which I shall give him, shall never thirst: but the water, which I shall give him, will be in him a fountain of water springing up unto eternal life. (aiōn , aiōnios )
15 Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, tafadhali nipe maji hayo ili nisipate kiu tena na wala nisije tena hapa kuteka maji!”
The woman saith unto Him, Sir, give me this water, that I may not thirst, nor come hither to draw.
16 Yesu akamjibu, “Nenda ukamwite mumeo, uje naye hapa.”
Jesus saith unto her, Go call thine husband, and come hither.
17 Yule mwanamke akajibu, “Sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli kuwa huna mume.
The woman answered, I have no husband. Jesus saith unto her, Thou hast said right, I have no husband:
18 Kwa maana umeshakuwa na wanaume watano na mwanaume unayeishi naye sasa si mume wako! Umesema ukweli.”
for thou hast had five husbands; and he, whom thou now hast, is not thy husband: this thou hast said true.
19 Yule mwanamke akasema, “Bwana, naona bila shaka wewe ni nabii.
The woman saith unto Him, Sir, I perceive that thou art a prophet.
20 Baba zetu waliabudu kwenye mlima huu, lakini ninyi Wayahudi mnasema ni lazima tukaabudu huko Yerusalemu.”
Our fathers worshipped on this mountain, and ye say that in Jerusalem is the place where men ought to worship.
21 Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala huko Yerusalemu.
Jesus saith unto her, Woman, believe me, the time is coming, when ye shall worship the Father neither on this mountain nor in Jerusalem.
22 Ninyi Wasamaria mnaabudu msichokijua. Sisi Wayahudi tunamwabudu Mungu tunayemjua kwa sababu wokovu unatoka kwa Wayahudi.
Ye worship ye know not what; but we worship what we know: for salvation is from the Jews.
23 Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta.
But the time is coming, and now is, when the true worshippers shall worship the Father in spirit and truth: for the Father requireth such worshippers of Him.
24 Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”
God is a spirit, and they that worship Him, must worship in spirit and truth.
25 Yule mwanamke akamwambia, “Ninafahamu kwamba Masiya (aitwaye Kristo) anakuja. Yeye akija, atatueleza mambo yote.”
Then saith the woman unto Him, I know that the Messiah, that is to say the Christ, is coming; and when He comes, He will tell us all things.
26 Yesu akamwambia, “Mimi ninayezungumza nawe, ndiye.”
Jesus saith unto her, I, who am talking to thee, am He.
27 Wakati huo wanafunzi wake wakarudi, wakashangaa sana kumwona akizungumza na mwanamke. Lakini hakuna aliyemuuliza, “Unataka nini kwake?” Au “Kwa nini unazungumza naye?”
And upon this came his disciples and wondered that He talked with the woman: (though none of them said, What dost thou seek? or, Why dost thou talk with her?)
28 Yule mwanamke akaacha mtungi wake, akarudi mjini akawaambia watu,
therefore the woman left her water-pot, and went away into the city,
29 “Njooni mkamwone mtu aliyeniambia kila kitu nilichotenda! Je, yawezekana huyu ndiye Kristo?”
and saith to the people, Come, see a man who hath told me all that ever I did; is not this the Christ?
30 Basi wakamiminika watu kutoka mjini wakamwendea Yesu.
They therefore went out of the city, and came to Him.
31 Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wakimsihi, “Rabi, kula angalau chochote.”
In the mean time his disciples addressed Him, saying, Master, eat.
32 Lakini yeye akawajibu, “Mimi ninacho chakula ambacho ninyi hamkifahamu.”
But He said unto them, I have food to eat, which ye know not of.
33 Basi wanafunzi wakaanza kuulizana, “Kuna mtu ambaye amemletea chakula?”
Therefore the disciples said one to another, Hath any one brought Him aught to eat?
34 Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma na kuikamilisha kazi yake.
Jesus saith unto them, My food is to do the will of Him that sent me, and to finish his work.
35 Je, ninyi hamsemi, ‘Bado miezi minne tuvune?’ Inueni macho yenu myaangalie mashamba jinsi mazao yalivyo tayari kuvunwa!
Do not ye say, it is yet four months, and then cometh harvest? Behold, lift up your eyes, and see the fields, they are already white for harvest.
36 Mvunaji tayari anapokea mshahara wake, naye anakusanya mazao kwa ajili ya uzima wa milele. Ili yeye apandaye na yeye avunaye wafurahi pamoja. (aiōnios )
And he that reapeth receiveth wages, and gathereth the fruit together unto life eternal: that both he that soweth and he that reapeth may rejoice together; (aiōnios )
37 Hivyo kule kusema, ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna,’ ni kweli kabisa.
for herein the saying is verified, that one soweth, and another reapeth,
38 Niliwatuma mkavune mazao ambayo hamkupanda, wengine walifanya kazi ngumu, nanyi mmevuna faida ya taabu yao.”
in as much as I have sent you to reap that on which ye have not laboured: others have laboured, and ye are entered into their labors.
39 Wasamaria wengi katika mji ule wakamwamini Yesu kwa sababu ya ushuhuda wa yule mwanamke alipowaambia kwamba, “Ameniambia kila kitu nilichotenda.”
And many of the Samaritans of that city believed on Him, because of what the woman said, testifying, He told me all that ever I did.
40 Hivyo wale Wasamaria walipomjia, wakamsihi akae kwao. Naye akakaa huko siku mbili.
Therefore when the Samaritans came to Him, they desired Him to stay with them: and He staid there two days.
41 Kwa sababu ya neno lake, watu wengi wakaamini.
And many more believed on account of his own discourse:
42 Wakamwambia yule mwanamke, “Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu, bali kwa kuwa tumemsikia sisi wenyewe. Tumejua hakika kweli ya kwamba huyu ndiye Kristo, Mwokozi wa ulimwengu.”
and said to the woman, Now we believe, not because of what thou hast spoken; for we ourselves have heard Him, and know that this is indeed the Christ, the Saviour of the world.
43 Baada ya zile siku mbili, Yesu aliondoka kwenda Galilaya.
And after two days he departed thence, and went into Cana of Galilee.
44 (Basi Yesu mwenyewe alikuwa amesema kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.)
For Jesus himself had testified that a prophet hath no honor in his own country.
45 Alipofika Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha, kwani walikuwa wameona yale aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa Sikukuu ya Pasaka. Kwa maana wao pia walikuwa wamehudhuria hiyo Sikukuu.
And when He was come into Galilee, the Galileans received Him, having seen all that he did in Jerusalem at the feast: for they also went to the feast.
46 Hivyo Yesu akaja tena mpaka Kana ya Galilaya, kule alikokuwa amebadili maji kuwa divai. Huko kulikuwepo na afisa mmoja wa mfalme, ambaye mwanawe alikuwa mgonjwa huko Kapernaumu.
Therefore Jesus came again into Cana of Galilee, where He had made the water wine.
47 Huyo mtu aliposikia kwamba Yesu alikuwa amewasili Galilaya kutoka Uyahudi, alimwendea na kumwomba ili aje kumponya mwanawe, aliyekuwa mgonjwa karibu ya kufa.
And there was a certain nobleman, whose son was sick at Capernaum: who, when he heard that Jesus was come out of Judea into Galilee, went to Him, and intreated Him, that he would come down and heal his son; for he was at the point of death.
48 Yesu akamwambia, “Ninyi watu msipoona ishara na miujiza kamwe hamtaamini.”
Jesus therefore said unto him, Except ye see signs and wonders ye will not believe.
49 Yule afisa wa mfalme akamwambia, “Bwana, tafadhali shuka kabla mwanangu hajafa.”
The nobleman saith unto Him, Lord, come down before my child die.
50 Yesu akamjibu, “Enenda zako, mwanao yu hai.” Yule afisa akaamini yale maneno Yesu aliyomwambia, akaondoka akaenda zake.
Jesus saith unto him, Go, thy son is well. And the man believed what Jesus said unto him, and went his way.
51 Alipokuwa bado yuko njiani, akakutana na watumishi wake wakamwambia kwamba mwanawe yu mzima.
And as he was now going down, his servants met him and told him, saying, Thy son is well.
52 Akawauliza saa ambayo alianza kupata nafuu. Wakamwambia, “Jana yapata saa saba, homa ilimwacha.”
He inquired therefore of them the hour in which he grew better: and they said unto him, Yesterday at the seventh hour the fever left him.
53 Ndipo baba wa huyo mtoto akakumbuka kuwa huo ndio wakati ambapo Yesu alikuwa amemwambia, “Mwanao yu hai.” Kwa hiyo yeye pamoja na wote wa nyumbani mwake wakamwamini Yesu.
So the father knew that it was in that same hour, in which Jesus said to him, Thy son is well. And he and his whole family believed.
54 Hii ilikuwa ishara ya pili ambayo Yesu alifanya aliporudi Galilaya kutoka Uyahudi.
This is the second miracle that Jesus wrought, upon coming out of Judea into Galilee.