< Yohana 4 >
1 Mafarisayo wakasikia kwamba Yesu alikuwa anapata na kubatiza wanafunzi wengi zaidi kuliko Yohana,
Now when the Lord learned that the Pharisees heard he was making and baptizing more disciples than John
2 ingawa kwa kweli si Yesu mwenyewe aliyekuwa akibatiza, ila ni wanafunzi wake.
(although it was not Jesus himself who baptized them, but his disciples),
3 Bwana alipojua mambo haya, aliondoka Uyahudi akarudi tena Galilaya.
he left Judea and went away to Galilee.
4 Wakati huo ilimlazimu apitie Samaria.
But he had to pass through Samaria.
5 Akafika kwenye mji mmoja wa Samaria uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa mwanawe Yosefu.
So he came to a town of Samaria called Sychar, near the plot of land that Jacob had given to his son Joseph.
6 Huko ndiko kulikokuwa na kile kisima cha Yakobo. Naye Yesu alikuwa amechoka kwa kuwa alikuwa ametoka safarini. Akaketi karibu na hicho kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
Jacob's well was there, so Jesus, wearied as he was from the journey, sat by the well. It was about the sixth hour.
7 Mwanamke mmoja Msamaria akaja kuteka maji, Yesu akamwambia, “Naomba maji ninywe.”
When a woman from Samaria came to draw water, Jesus said to her, “Give me some water to drink.”
8 (Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
(For his disciples had gone into the city to buy food.)
9 Yule mwanamke Msamaria akamjibu, “Wewe ni Myahudi na mimi ni Msamaria. Yawezekanaje uniombe nikupe maji ya kunywa?” (Wayahudi walikuwa hawashirikiani kabisa na Wasamaria.)
So the Samaritan woman said to him, “How is it that yoʋ, a Jew, ask for water to drink from me, a Samaritan woman?” (For Jews have no dealings with Samaritans.)
10 Yesu akajibu akamwambia, “Kama ungelijua karama ya Mungu, naye ni nani anayekuambia, Nipe maji ninywe, wewe ungelimwomba yeye, naye angelikupa maji yaliyo hai.”
Jesus answered her, “If yoʋ knew the gift of God and who it is that is saying to yoʋ, ‘Give me some water to drink,’ yoʋ would have asked him, and he would have given yoʋ living water.”
11 Yule mwanamke akamjibu, “Bwana, wewe huna chombo cha kutekea maji na kisima hiki ni kirefu. Hayo maji ya uzima utayapata wapi?
The woman said to him, “Sir, yoʋ do not even have a bucket to draw with, and the well is deep. Where then can yoʋ get this living water?
12 Kwani wewe ni mkuu kuliko baba yetu Yakobo ambaye alitupatia kisima hiki, ambacho yeye pamoja na watoto wake na mifugo yake walikitumia?”
Are yoʋ greater than our father Jacob, who gave us this well and drank from it himself, as did his sons and livestock?”
13 Yesu akamjibu, “Kila mtu anayekunywa maji ya kisima hiki ataona kiu tena.
Jesus answered her, “Everyone who drinks this water will thirst again,
14 Lakini yeyote anywaye maji nitakayompa hataona kiu kamwe. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujika uzima wa milele.” (aiōn , aiōnios )
but whoever drinks the water I give him will certainly never thirst again. On the contrary, the water I give him will become in him a spring of water welling up to eternal life.” (aiōn , aiōnios )
15 Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, tafadhali nipe maji hayo ili nisipate kiu tena na wala nisije tena hapa kuteka maji!”
The woman said to him, “Sir, give me this water so that I will not get thirsty again and have to come here to draw water.”
16 Yesu akamjibu, “Nenda ukamwite mumeo, uje naye hapa.”
Jesus said to her, “Go call yoʋr husband and come back here.”
17 Yule mwanamke akajibu, “Sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli kuwa huna mume.
The woman said in response, “I have no husband.” Jesus said to her, “Yoʋ have rightly said, ‘I have no husband,’
18 Kwa maana umeshakuwa na wanaume watano na mwanaume unayeishi naye sasa si mume wako! Umesema ukweli.”
for yoʋ have had five husbands, and the man yoʋ now have is not yoʋr husband; what yoʋ have said is true.”
19 Yule mwanamke akasema, “Bwana, naona bila shaka wewe ni nabii.
The woman said to him, “Sir, I see that yoʋ are a prophet.
20 Baba zetu waliabudu kwenye mlima huu, lakini ninyi Wayahudi mnasema ni lazima tukaabudu huko Yerusalemu.”
Our fathers worshiped on this mountain, but you say that the place where people must worship is in Jerusalem.”
21 Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala huko Yerusalemu.
Jesus said to her, “Woman, believe me, an hour is coming when neither on this mountain nor in Jerusalem will you worship the Father.
22 Ninyi Wasamaria mnaabudu msichokijua. Sisi Wayahudi tunamwabudu Mungu tunayemjua kwa sababu wokovu unatoka kwa Wayahudi.
You worship what you do not know; we worship what we know, because salvation is from the Jews.
23 Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta.
But an hour is coming, and is now here, when the true worshipers will worship the Father in spirit and truth, for the Father seeks such people to worship him.
24 Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”
God is spirit, and those who worship him must worship in spirit and truth.”
25 Yule mwanamke akamwambia, “Ninafahamu kwamba Masiya (aitwaye Kristo) anakuja. Yeye akija, atatueleza mambo yote.”
The woman said to him, “I know that Messiah is coming” (who is called Christ). “When he comes, he will explain everything to us.”
26 Yesu akamwambia, “Mimi ninayezungumza nawe, ndiye.”
Jesus said to her, “I who speak to yoʋ am he.”
27 Wakati huo wanafunzi wake wakarudi, wakashangaa sana kumwona akizungumza na mwanamke. Lakini hakuna aliyemuuliza, “Unataka nini kwake?” Au “Kwa nini unazungumza naye?”
Just then his disciples came back, and they were amazed that he was speaking with a woman. However, no one said, “What do yoʋ want?” or, “Why are yoʋ speaking with her?”
28 Yule mwanamke akaacha mtungi wake, akarudi mjini akawaambia watu,
Then the woman left her water jar, went into the town, and said to the people,
29 “Njooni mkamwone mtu aliyeniambia kila kitu nilichotenda! Je, yawezekana huyu ndiye Kristo?”
“Come see a man who told me everything I have ever done. Could this be the Christ?”
30 Basi wakamiminika watu kutoka mjini wakamwendea Yesu.
So they left the town and began coming to him.
31 Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wakimsihi, “Rabi, kula angalau chochote.”
In the meantime the disciples were urging him, “Rabbi, eat.”
32 Lakini yeye akawajibu, “Mimi ninacho chakula ambacho ninyi hamkifahamu.”
But he said to them, “I have food to eat that you do not know about.”
33 Basi wanafunzi wakaanza kuulizana, “Kuna mtu ambaye amemletea chakula?”
So the disciples said to one another, “Could someone have brought him something to eat?”
34 Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma na kuikamilisha kazi yake.
Jesus said to them, “My food is to do the will of him who sent me and to complete his work.
35 Je, ninyi hamsemi, ‘Bado miezi minne tuvune?’ Inueni macho yenu myaangalie mashamba jinsi mazao yalivyo tayari kuvunwa!
Do you not say, ‘There are still four months and then comes the harvest’? I tell you, lift up your eyes and see that the fields are already ripe for harvest.
36 Mvunaji tayari anapokea mshahara wake, naye anakusanya mazao kwa ajili ya uzima wa milele. Ili yeye apandaye na yeye avunaye wafurahi pamoja. (aiōnios )
He who reaps receives wages and gathers fruit for eternal life, so that both he who sows and he who reaps may rejoice together. (aiōnios )
37 Hivyo kule kusema, ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna,’ ni kweli kabisa.
For in this the true saying is verified: ‘One sows and another reaps.’
38 Niliwatuma mkavune mazao ambayo hamkupanda, wengine walifanya kazi ngumu, nanyi mmevuna faida ya taabu yao.”
I sent you to reap what you have not labored for; others have labored, and you have entered into their labor.”
39 Wasamaria wengi katika mji ule wakamwamini Yesu kwa sababu ya ushuhuda wa yule mwanamke alipowaambia kwamba, “Ameniambia kila kitu nilichotenda.”
Many of the Samaritans from that town believed in Jesus because of the woman's testimony: “He told me everything I have ever done.”
40 Hivyo wale Wasamaria walipomjia, wakamsihi akae kwao. Naye akakaa huko siku mbili.
So when the Samaritans came to him, they asked him to stay with them, and he stayed there for two days.
41 Kwa sababu ya neno lake, watu wengi wakaamini.
And many more believed because of his word.
42 Wakamwambia yule mwanamke, “Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu, bali kwa kuwa tumemsikia sisi wenyewe. Tumejua hakika kweli ya kwamba huyu ndiye Kristo, Mwokozi wa ulimwengu.”
So they said to the woman, “It is no longer because of yoʋr report that we believe, for we ourselves have heard, and we know that this is truly the Christ, the Savior of the world.”
43 Baada ya zile siku mbili, Yesu aliondoka kwenda Galilaya.
After two days, he departed from there and went to Galilee.
44 (Basi Yesu mwenyewe alikuwa amesema kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.)
(For Jesus himself had testified that a prophet has no honor in his own hometown.)
45 Alipofika Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha, kwani walikuwa wameona yale aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa Sikukuu ya Pasaka. Kwa maana wao pia walikuwa wamehudhuria hiyo Sikukuu.
When he came to Galilee, the Galileans received him because they had seen all that he had done in Jerusalem at the feast, for they also had gone to the feast.
46 Hivyo Yesu akaja tena mpaka Kana ya Galilaya, kule alikokuwa amebadili maji kuwa divai. Huko kulikuwepo na afisa mmoja wa mfalme, ambaye mwanawe alikuwa mgonjwa huko Kapernaumu.
Once more Jesus went to Cana of Galilee, where he had turned the water into wine. Now there was a certain royal official whose son was sick in Capernaum.
47 Huyo mtu aliposikia kwamba Yesu alikuwa amewasili Galilaya kutoka Uyahudi, alimwendea na kumwomba ili aje kumponya mwanawe, aliyekuwa mgonjwa karibu ya kufa.
When he heard that Jesus had come from Judea to Galilee, he went to him and asked him to come down and heal his son, for his son was about to die.
48 Yesu akamwambia, “Ninyi watu msipoona ishara na miujiza kamwe hamtaamini.”
Then Jesus said to him, “Unless you see signs and wonders, you will certainly not believe.”
49 Yule afisa wa mfalme akamwambia, “Bwana, tafadhali shuka kabla mwanangu hajafa.”
The royal official said to him, “Sir, come down before my boy dies.”
50 Yesu akamjibu, “Enenda zako, mwanao yu hai.” Yule afisa akaamini yale maneno Yesu aliyomwambia, akaondoka akaenda zake.
Jesus said to him, “Go; yoʋr son will live.” And the man believed what Jesus said to him and went on his way.
51 Alipokuwa bado yuko njiani, akakutana na watumishi wake wakamwambia kwamba mwanawe yu mzima.
As he was going back down to his house, his servants met him and told him, “Yoʋr son is alive.”
52 Akawauliza saa ambayo alianza kupata nafuu. Wakamwambia, “Jana yapata saa saba, homa ilimwacha.”
So he asked them the hour when he began to get better. They said to him, “Yesterday at the seventh hour the fever left him.”
53 Ndipo baba wa huyo mtoto akakumbuka kuwa huo ndio wakati ambapo Yesu alikuwa amemwambia, “Mwanao yu hai.” Kwa hiyo yeye pamoja na wote wa nyumbani mwake wakamwamini Yesu.
Then the father realized that this was the hour when Jesus had said to him, “Yoʋr son will live.” So he believed, along with his entire household.
54 Hii ilikuwa ishara ya pili ambayo Yesu alifanya aliporudi Galilaya kutoka Uyahudi.
This was the second sign that Jesus did after coming from Judea to Galilee.