< Yohana 4 >

1 Mafarisayo wakasikia kwamba Yesu alikuwa anapata na kubatiza wanafunzi wengi zaidi kuliko Yohana,
Therefore when the Lord knew that the Pharisees [Separated] had heard that Yeshua [Salvation] was making and baptizing more disciples than John [Yah is gracious]
2 ingawa kwa kweli si Yesu mwenyewe aliyekuwa akibatiza, ila ni wanafunzi wake.
(although Yeshua [Salvation] himself didn’t mikvah ·baptise·, but his disciples),
3 Bwana alipojua mambo haya, aliondoka Uyahudi akarudi tena Galilaya.
he left Judea [Praise], and departed into Galilee [District, Circuit].
4 Wakati huo ilimlazimu apitie Samaria.
He needed to pass through Samaria [Watch-mountain].
5 Akafika kwenye mji mmoja wa Samaria uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa mwanawe Yosefu.
So he came to a city of Samaria [Watch-mountain], called Sychar [Shoulder], near the parcel of ground that Jacob [Supplanter] gave to his son, Joseph [May he add].
6 Huko ndiko kulikokuwa na kile kisima cha Yakobo. Naye Yesu alikuwa amechoka kwa kuwa alikuwa ametoka safarini. Akaketi karibu na hicho kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
Jacob [Supplanter]’s well was there. Yeshua [Salvation] therefore, being tired from his journey, sat down by the well. It was about noon.
7 Mwanamke mmoja Msamaria akaja kuteka maji, Yesu akamwambia, “Naomba maji ninywe.”
A woman of Samaria [Watch-mountain] came to draw water. Yeshua [Salvation] said to her, “Give me a drink.”
8 (Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
For his disciples had gone away into the city to buy food.
9 Yule mwanamke Msamaria akamjibu, “Wewe ni Myahudi na mimi ni Msamaria. Yawezekanaje uniombe nikupe maji ya kunywa?” (Wayahudi walikuwa hawashirikiani kabisa na Wasamaria.)
The Samaritan [person from Watch-mountain] woman therefore said to him, “How is it that you, being a Jew [Praiser], ask for a drink from me, a Samaritan [person from Watch-mountain] woman?” (For Jews [Praisers] have no dealings with Samaritans [people from Watch-mountain].)
10 Yesu akajibu akamwambia, “Kama ungelijua karama ya Mungu, naye ni nani anayekuambia, Nipe maji ninywe, wewe ungelimwomba yeye, naye angelikupa maji yaliyo hai.”
Yeshua [Salvation] answered her, “If you knew the gift of God, and who it is who says to you, ‘Give me a drink,’ you would have asked him, and he would have given you living water.”
11 Yule mwanamke akamjibu, “Bwana, wewe huna chombo cha kutekea maji na kisima hiki ni kirefu. Hayo maji ya uzima utayapata wapi?
The woman said to him, “Sir, you have nothing to draw with, and the well is deep. So where do you get that living water?
12 Kwani wewe ni mkuu kuliko baba yetu Yakobo ambaye alitupatia kisima hiki, ambacho yeye pamoja na watoto wake na mifugo yake walikitumia?”
Are you greater than Avinu ·our Father·, Jacob [Supplanter], who gave us the well, and drank of it himself, as did his children, and his livestock?”
13 Yesu akamjibu, “Kila mtu anayekunywa maji ya kisima hiki ataona kiu tena.
Yeshua [Salvation] answered her, “Everyone who drinks of this water will thirst again,
14 Lakini yeyote anywaye maji nitakayompa hataona kiu kamwe. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujika uzima wa milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
but whoever drinks of the water that I will give him will never thirst again; but the water that I will give him will become in him a well of water springing up to eternal life.” (aiōn g165, aiōnios g166)
15 Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, tafadhali nipe maji hayo ili nisipate kiu tena na wala nisije tena hapa kuteka maji!”
The woman said to him, “Sir, give me this water, so that I don’t get thirsty, neither come all the way here to draw.”
16 Yesu akamjibu, “Nenda ukamwite mumeo, uje naye hapa.”
Yeshua [Salvation] said to her, “Go, call your husband, and come here.”
17 Yule mwanamke akajibu, “Sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli kuwa huna mume.
The woman answered, “I have no husband.” Yeshua [Salvation] said to her, “You said well, ‘I have no husband,’
18 Kwa maana umeshakuwa na wanaume watano na mwanaume unayeishi naye sasa si mume wako! Umesema ukweli.”
for you have had five husbands; and he whom you now have is not your husband. This you have said truly.”
19 Yule mwanamke akasema, “Bwana, naona bila shaka wewe ni nabii.
The woman said to him, “Sir, I perceive that you are a prophet.
20 Baba zetu waliabudu kwenye mlima huu, lakini ninyi Wayahudi mnasema ni lazima tukaabudu huko Yerusalemu.”
Our fathers worshiped in this mountain, and you Jews [Praisers] say that in Jerusalem [City of peace] is the place where people ought to worship.”
21 Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala huko Yerusalemu.
Yeshua [Salvation] said to her, “Woman, trust me, the time will come, when neither in this mountain, nor in Jerusalem [City of peace], will you worship Abba Father.
22 Ninyi Wasamaria mnaabudu msichokijua. Sisi Wayahudi tunamwabudu Mungu tunayemjua kwa sababu wokovu unatoka kwa Wayahudi.
You worship that which you don’t know. We worship that which we know; for yishu'ah ·salvation· is from the Jews [Praisers].
23 Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta.
But the time will come, and now is, when the true worshipers will worship Abba Father in spirit and truth, for Abba Father seeks such to be his worshipers.
24 Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”
God is spirit, and those who worship him must worship in spirit and truth.”
25 Yule mwanamke akamwambia, “Ninafahamu kwamba Masiya (aitwaye Kristo) anakuja. Yeye akija, atatueleza mambo yote.”
The woman said to him, “I know that Messiah [Anointed one] comes, he who is called Messiah [Anointed one]. When he has come, he will declare to us all things.”
26 Yesu akamwambia, “Mimi ninayezungumza nawe, ndiye.”
Yeshua [Salvation] said to her, “Ena Na [I AM (the Living God)], I who is speaking to you.”
27 Wakati huo wanafunzi wake wakarudi, wakashangaa sana kumwona akizungumza na mwanamke. Lakini hakuna aliyemuuliza, “Unataka nini kwake?” Au “Kwa nini unazungumza naye?”
At this, his disciples came. They marveled that he was speaking with a woman; yet no one said, “What are you looking for?” or, “Why do you speak with her?”
28 Yule mwanamke akaacha mtungi wake, akarudi mjini akawaambia watu,
So the woman left her water pot, and went away into the city, and said to the people,
29 “Njooni mkamwone mtu aliyeniambia kila kitu nilichotenda! Je, yawezekana huyu ndiye Kristo?”
“Come, see a man who told me everything that I did. Can this be the Messiah [Anointed one]?”
30 Basi wakamiminika watu kutoka mjini wakamwendea Yesu.
They went out of the city, and were coming to him.
31 Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wakimsihi, “Rabi, kula angalau chochote.”
In the meanwhile, the disciples urged him, saying, “Rabbi ·Teacher·, eat.”
32 Lakini yeye akawajibu, “Mimi ninacho chakula ambacho ninyi hamkifahamu.”
But he said to them, “I have food to eat that you don’t know about.”
33 Basi wanafunzi wakaanza kuulizana, “Kuna mtu ambaye amemletea chakula?”
The disciples therefore said to one another, “Has anyone brought him something to eat?”
34 Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma na kuikamilisha kazi yake.
Yeshua [Salvation] said to them, “My food is to do the will of him who sent me, and to accomplish his work.
35 Je, ninyi hamsemi, ‘Bado miezi minne tuvune?’ Inueni macho yenu myaangalie mashamba jinsi mazao yalivyo tayari kuvunwa!
Don’t you say, ‘There are yet four months until the harvest?’ Behold, I tell you, lift up your eyes, and look at the fields, that they are white for harvest already.
36 Mvunaji tayari anapokea mshahara wake, naye anakusanya mazao kwa ajili ya uzima wa milele. Ili yeye apandaye na yeye avunaye wafurahi pamoja. (aiōnios g166)
He who reaps receives wages, and gathers fruit to eternal life; that both he who sows and he who reaps may rejoice together. (aiōnios g166)
37 Hivyo kule kusema, ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna,’ ni kweli kabisa.
For in this the saying is true, ‘One sows, and another reaps.’
38 Niliwatuma mkavune mazao ambayo hamkupanda, wengine walifanya kazi ngumu, nanyi mmevuna faida ya taabu yao.”
I sent you to reap that for which you haven’t labored. Others have labored, and you have entered into their labor.”
39 Wasamaria wengi katika mji ule wakamwamini Yesu kwa sababu ya ushuhuda wa yule mwanamke alipowaambia kwamba, “Ameniambia kila kitu nilichotenda.”
From that city many of the Samaritans [people from Watch-mountain] trusted in him because of the word of the woman, who testified, “He told me everything that I did.”
40 Hivyo wale Wasamaria walipomjia, wakamsihi akae kwao. Naye akakaa huko siku mbili.
So when the Samaritans [people from Watch-mountain] came to him, they begged him to stay with them. He stayed there two days.
41 Kwa sababu ya neno lake, watu wengi wakaamini.
Many more trusted because of his word.
42 Wakamwambia yule mwanamke, “Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu, bali kwa kuwa tumemsikia sisi wenyewe. Tumejua hakika kweli ya kwamba huyu ndiye Kristo, Mwokozi wa ulimwengu.”
They said to the woman, “Now we trust, not because of your speaking; for we have heard for ourselves, and know that this is indeed the Messiah [Anointed one], the Savior of the world.”
43 Baada ya zile siku mbili, Yesu aliondoka kwenda Galilaya.
After the two days he went out from there and went into Galilee [District, Circuit].
44 (Basi Yesu mwenyewe alikuwa amesema kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.)
For Yeshua [Salvation] himself testified that a prophet has no honor in his own country.
45 Alipofika Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha, kwani walikuwa wameona yale aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa Sikukuu ya Pasaka. Kwa maana wao pia walikuwa wamehudhuria hiyo Sikukuu.
So when he came into Galilee [District, Circuit], the Galileans received him, having seen all the things that he did in Jerusalem [City of peace] at the feast, for they also went to the feast.
46 Hivyo Yesu akaja tena mpaka Kana ya Galilaya, kule alikokuwa amebadili maji kuwa divai. Huko kulikuwepo na afisa mmoja wa mfalme, ambaye mwanawe alikuwa mgonjwa huko Kapernaumu.
Yeshua [Salvation] came therefore again to Cana of Galilee [District, Circuit], where he made the water into wine. There was a certain nobleman whose son was sick at Capernaum [Village-Comfort, Village-Compassion].
47 Huyo mtu aliposikia kwamba Yesu alikuwa amewasili Galilaya kutoka Uyahudi, alimwendea na kumwomba ili aje kumponya mwanawe, aliyekuwa mgonjwa karibu ya kufa.
When he heard that Yeshua [Salvation] had come out of Judea [Praise] into Galilee [District, Circuit], he went to him, and begged him that he would come down and heal his son, for he was at the point of death.
48 Yesu akamwambia, “Ninyi watu msipoona ishara na miujiza kamwe hamtaamini.”
Yeshua [Salvation] therefore said to him, “Unless you see signs and wonders, you will in no way trust.”
49 Yule afisa wa mfalme akamwambia, “Bwana, tafadhali shuka kabla mwanangu hajafa.”
The nobleman said to him, “Sir, come down before my child dies.”
50 Yesu akamjibu, “Enenda zako, mwanao yu hai.” Yule afisa akaamini yale maneno Yesu aliyomwambia, akaondoka akaenda zake.
Yeshua [Salvation] said to him, “Go your way. Your son lives.” The man trusted the word that Yeshua [Salvation] spoke to him, and he went his way.
51 Alipokuwa bado yuko njiani, akakutana na watumishi wake wakamwambia kwamba mwanawe yu mzima.
As he was now going down, his servants met him and reported, saying “Your child lives!”
52 Akawauliza saa ambayo alianza kupata nafuu. Wakamwambia, “Jana yapata saa saba, homa ilimwacha.”
So he inquired of them the hour when he began to get better. They said therefore to him, “Yesterday at one o'clock in the afternoon, the fever left him.”
53 Ndipo baba wa huyo mtoto akakumbuka kuwa huo ndio wakati ambapo Yesu alikuwa amemwambia, “Mwanao yu hai.” Kwa hiyo yeye pamoja na wote wa nyumbani mwake wakamwamini Yesu.
So the Abba Father knew that it was at that hour in which Yeshua [Salvation] said to him, “Your son lives.” He trusted, as did his whole house.
54 Hii ilikuwa ishara ya pili ambayo Yesu alifanya aliporudi Galilaya kutoka Uyahudi.
This is again the second sign that Yeshua [Salvation] did, having come out of Judea [Praise] into Galilee [District, Circuit].

< Yohana 4 >