< Yohana 4 >

1 Mafarisayo wakasikia kwamba Yesu alikuwa anapata na kubatiza wanafunzi wengi zaidi kuliko Yohana,
Accordingly when the Lord knew that the Pharisees had heard it said, "Jesus is making and baptizing more disciples than John,"
2 ingawa kwa kweli si Yesu mwenyewe aliyekuwa akibatiza, ila ni wanafunzi wake.
(though Jesus himself was not accustomed to baptize, but his disciples),
3 Bwana alipojua mambo haya, aliondoka Uyahudi akarudi tena Galilaya.
he left Judea and returned to Galilee.
4 Wakati huo ilimlazimu apitie Samaria.
Now he had to pass through Samaria;
5 Akafika kwenye mji mmoja wa Samaria uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa mwanawe Yosefu.
so he came to a city of Samaria called Sychar, near the piece of ground that Jacob gave to his son Joseph.
6 Huko ndiko kulikokuwa na kile kisima cha Yakobo. Naye Yesu alikuwa amechoka kwa kuwa alikuwa ametoka safarini. Akaketi karibu na hicho kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
Jacob’s Spring was there. So Jesus, tired out with his journey, was sitting thus by the spring.
7 Mwanamke mmoja Msamaria akaja kuteka maji, Yesu akamwambia, “Naomba maji ninywe.”
It was about noon, and a woman of Samaria came to draw water.
8 (Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
Jesus said to her, "Give me a drink" (for his disciples were gone away into the city to buy food.)
9 Yule mwanamke Msamaria akamjibu, “Wewe ni Myahudi na mimi ni Msamaria. Yawezekanaje uniombe nikupe maji ya kunywa?” (Wayahudi walikuwa hawashirikiani kabisa na Wasamaria.)
"How is it," answered the Samaritan woman, "that you who are a Jew ask a drink from me, a woman, and a Samaritan?" (For Jews have no dealings with Samaritans.)
10 Yesu akajibu akamwambia, “Kama ungelijua karama ya Mungu, naye ni nani anayekuambia, Nipe maji ninywe, wewe ungelimwomba yeye, naye angelikupa maji yaliyo hai.”
"If you had known the free gift of God," Jesus answered, "and who it is that says to you, ‘Give me a drink,’ you would have asked of him, and he would have given you living water."
11 Yule mwanamke akamjibu, “Bwana, wewe huna chombo cha kutekea maji na kisima hiki ni kirefu. Hayo maji ya uzima utayapata wapi?
"Sir," said the woman, "you have nothing to draw with, and the well is deep; whence have you that living water?
12 Kwani wewe ni mkuu kuliko baba yetu Yakobo ambaye alitupatia kisima hiki, ambacho yeye pamoja na watoto wake na mifugo yake walikitumia?”
Surely you are not greater than our Father Jacob, who gave us the well, and used to drink from it himself, and his sons, and his cattle, too?"
13 Yesu akamjibu, “Kila mtu anayekunywa maji ya kisima hiki ataona kiu tena.
"All who drink of this water," Jesus answered, "will thirst again;
14 Lakini yeyote anywaye maji nitakayompa hataona kiu kamwe. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujika uzima wa milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
but whoever once drinks of the water that I will give him, shall never thirst any more, but the water that I will give him shall become a living spring of water within him, welling up into eternal life." (aiōn g165, aiōnios g166)
15 Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, tafadhali nipe maji hayo ili nisipate kiu tena na wala nisije tena hapa kuteka maji!”
"Sir!" exclaimed the woman, "give me this water, so that I may not be thirsty, nor come all this way to draw water."
16 Yesu akamjibu, “Nenda ukamwite mumeo, uje naye hapa.”
Jesus said to her, "Go, call your husband, and then come here."
17 Yule mwanamke akajibu, “Sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli kuwa huna mume.
"I have no husband," answered the woman. "You are right in saying ‘I have no husband,’"Jesus said to her,
18 Kwa maana umeshakuwa na wanaume watano na mwanaume unayeishi naye sasa si mume wako! Umesema ukweli.”
"for you have had five husbands, and the man you now have is not your husband; in this you have spoken truly."
19 Yule mwanamke akasema, “Bwana, naona bila shaka wewe ni nabii.
"I see, Sir, that you are a prophet," replied the woman.
20 Baba zetu waliabudu kwenye mlima huu, lakini ninyi Wayahudi mnasema ni lazima tukaabudu huko Yerusalemu.”
"Our forefathers worshiped in this mountain, yet you Jews say that in Jerusalem is the place where one must worship."
21 Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala huko Yerusalemu.
"Woman, believe me," said Jesus, "that the hour is coming when neither in this mountain nor in Jerusalem will you worship the Father.
22 Ninyi Wasamaria mnaabudu msichokijua. Sisi Wayahudi tunamwabudu Mungu tunayemjua kwa sababu wokovu unatoka kwa Wayahudi.
You are worshiping something you do not know. we know what we worship, for salvation comes from the Jews.
23 Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta.
But an hour is coming, and is now here, when the true worshipers will worship the Father in spirit and in truth. For the Father is seeking such as his worshipers.
24 Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”
God is spirit, and those who worship him must worship him in spirit and in truth."
25 Yule mwanamke akamwambia, “Ninafahamu kwamba Masiya (aitwaye Kristo) anakuja. Yeye akija, atatueleza mambo yote.”
"I know," said the woman, "that Messiah is coming, who is called the Christ; when he has come he will tell us everything."
26 Yesu akamwambia, “Mimi ninayezungumza nawe, ndiye.”
Jesus said to her, "I who am now talking to you, am he."
27 Wakati huo wanafunzi wake wakarudi, wakashangaa sana kumwona akizungumza na mwanamke. Lakini hakuna aliyemuuliza, “Unataka nini kwake?” Au “Kwa nini unazungumza naye?”
Just then his disciples came up, and were astonished that he was talking with a woman; yet not one of them asked him, "What do you want?" or "Why are you talking with her?"
28 Yule mwanamke akaacha mtungi wake, akarudi mjini akawaambia watu,
Then the woman left her water-jar, and went away into the city and began saying to the people.
29 “Njooni mkamwone mtu aliyeniambia kila kitu nilichotenda! Je, yawezekana huyu ndiye Kristo?”
"Come! see a man who has told me everything that I ever did. He can’t be the Christ, can he?"
30 Basi wakamiminika watu kutoka mjini wakamwendea Yesu.
They left the city and set out to go to him.
31 Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wakimsihi, “Rabi, kula angalau chochote.”
Meanwhile the disciples kept urging him.
32 Lakini yeye akawajibu, “Mimi ninacho chakula ambacho ninyi hamkifahamu.”
"Rabbi," they said, "eat something." But he answered, "I have food to eat of which you know nothing."
33 Basi wanafunzi wakaanza kuulizana, “Kuna mtu ambaye amemletea chakula?”
So the disciples began to say to one another, "Can any one have brought him something to eat?"
34 Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma na kuikamilisha kazi yake.
Jesus said to them. "My food is to do the will of Him who sent me, and to accomplish his work.
35 Je, ninyi hamsemi, ‘Bado miezi minne tuvune?’ Inueni macho yenu myaangalie mashamba jinsi mazao yalivyo tayari kuvunwa!
Do you not say, ‘It wants yet four months, and then comes the harvest’? Look, I tell you! Lift up your eyes and behold the fields, that they are already white for harvest.
36 Mvunaji tayari anapokea mshahara wake, naye anakusanya mazao kwa ajili ya uzima wa milele. Ili yeye apandaye na yeye avunaye wafurahi pamoja. (aiōnios g166)
The reaper is already receiving wages and gathering a crop for eternal life, so that the sower and the reaper may rejoice together. (aiōnios g166)
37 Hivyo kule kusema, ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna,’ ni kweli kabisa.
For in this respect the saying is true, ‘One sows, another reaps.’
38 Niliwatuma mkavune mazao ambayo hamkupanda, wengine walifanya kazi ngumu, nanyi mmevuna faida ya taabu yao.”
I sent you to reap a crop on which you have not toiled. Others have toiled, and you have reaped the benefit of their toil."
39 Wasamaria wengi katika mji ule wakamwamini Yesu kwa sababu ya ushuhuda wa yule mwanamke alipowaambia kwamba, “Ameniambia kila kitu nilichotenda.”
Many of the Samaritans of that city believed on him because of the word of the woman when she declared, "He told me everything that I ever did."
40 Hivyo wale Wasamaria walipomjia, wakamsihi akae kwao. Naye akakaa huko siku mbili.
So when the Samaritans arrived, they began asking him to remain with them; and he stayed there two days.
41 Kwa sababu ya neno lake, watu wengi wakaamini.
Then many more believed because of what he said, himself; and they told the woman.
42 Wakamwambia yule mwanamke, “Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu, bali kwa kuwa tumemsikia sisi wenyewe. Tumejua hakika kweli ya kwamba huyu ndiye Kristo, Mwokozi wa ulimwengu.”
"We no longer believe because of what you said. for we ourselves have heard him, and we know that this is certainly the Saviour of the world."
43 Baada ya zile siku mbili, Yesu aliondoka kwenda Galilaya.
After these two days Jesus went away from there into Galilee.
44 (Basi Yesu mwenyewe alikuwa amesema kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.)
For Jesus himself testified that a prophet has no honor in his own country.
45 Alipofika Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha, kwani walikuwa wameona yale aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa Sikukuu ya Pasaka. Kwa maana wao pia walikuwa wamehudhuria hiyo Sikukuu.
When he reached Galilee, however, the Galileans welcomed him, for they had seen all that he did in Jerusalem at the feast; for they, too, had been at the feast.
46 Hivyo Yesu akaja tena mpaka Kana ya Galilaya, kule alikokuwa amebadili maji kuwa divai. Huko kulikuwepo na afisa mmoja wa mfalme, ambaye mwanawe alikuwa mgonjwa huko Kapernaumu.
So he came back again to Cana of Galilee, where he made the water wine. Now there was one of the king’s officers whose son was lying ill at Capernaum.
47 Huyo mtu aliposikia kwamba Yesu alikuwa amewasili Galilaya kutoka Uyahudi, alimwendea na kumwomba ili aje kumponya mwanawe, aliyekuwa mgonjwa karibu ya kufa.
When he heard that Jesus had come from Judea into Galilee, he went to him, and begged him to come down and heal his son who was lying at the point of death.
48 Yesu akamwambia, “Ninyi watu msipoona ishara na miujiza kamwe hamtaamini.”
Then Jesus said to him, "Unless you all see signs and wonders, you will not believe."
49 Yule afisa wa mfalme akamwambia, “Bwana, tafadhali shuka kabla mwanangu hajafa.”
"Sir," said the king’s officer, "come down before my little boy dies."
50 Yesu akamjibu, “Enenda zako, mwanao yu hai.” Yule afisa akaamini yale maneno Yesu aliyomwambia, akaondoka akaenda zake.
Jesus answered. "Go your way. Your son lives." And the man believed the word which Jesus spoke to him, and started to go home.
51 Alipokuwa bado yuko njiani, akakutana na watumishi wake wakamwambia kwamba mwanawe yu mzima.
And when he was already on his way down, his slaves met him, saying that his boy was living.
52 Akawauliza saa ambayo alianza kupata nafuu. Wakamwambia, “Jana yapata saa saba, homa ilimwacha.”
So he asked them at what hour he had begun mend. They answered, "Yesterday, about one o’clock, the fever left him."
53 Ndipo baba wa huyo mtoto akakumbuka kuwa huo ndio wakati ambapo Yesu alikuwa amemwambia, “Mwanao yu hai.” Kwa hiyo yeye pamoja na wote wa nyumbani mwake wakamwamini Yesu.
Then the father realized that it had left him at the very hour when Jesus had said to him, "Your son lives," and he himself believed, and his whole household.
54 Hii ilikuwa ishara ya pili ambayo Yesu alifanya aliporudi Galilaya kutoka Uyahudi.
This is the second sign which Jesus performed, on returning from Judea to Galilee.

< Yohana 4 >