< Yohana 4 >

1 Mafarisayo wakasikia kwamba Yesu alikuwa anapata na kubatiza wanafunzi wengi zaidi kuliko Yohana,
Stále více lidí se připojovalo k Ježíšovi a jeho učedníci je křtili.
2 ingawa kwa kweli si Yesu mwenyewe aliyekuwa akibatiza, ila ni wanafunzi wake.
3 Bwana alipojua mambo haya, aliondoka Uyahudi akarudi tena Galilaya.
Aby zabránil případnému střetnutí s náboženskými vůdci, opustil Ježíš Judsko a vrátil se do Galileje.
4 Wakati huo ilimlazimu apitie Samaria.
Šel skrze Samařsko.
5 Akafika kwenye mji mmoja wa Samaria uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa mwanawe Yosefu.
Kolem poledne přišel k Jákobově studni u městečka Sychar.
6 Huko ndiko kulikokuwa na kile kisima cha Yakobo. Naye Yesu alikuwa amechoka kwa kuwa alikuwa ametoka safarini. Akaketi karibu na hicho kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
7 Mwanamke mmoja Msamaria akaja kuteka maji, Yesu akamwambia, “Naomba maji ninywe.”
Jeho učedníci odešli do města nakoupit něco k jídlu. Ježíš si chtěl u studny odpočinout. Sotva usedl, jedna z místních žen přišla pro vodu. „Prosím tě, dej mi napít, “obrátil se na ni Ježíš.
8 (Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wamekwenda mjini kununua chakula.)
9 Yule mwanamke Msamaria akamjibu, “Wewe ni Myahudi na mimi ni Msamaria. Yawezekanaje uniombe nikupe maji ya kunywa?” (Wayahudi walikuwa hawashirikiani kabisa na Wasamaria.)
„Jak to, že žádáš službu od Samařanky, když jsi Žid?“(Mezi Židy a Samařany vládlo totiž napětí.)
10 Yesu akajibu akamwambia, “Kama ungelijua karama ya Mungu, naye ni nani anayekuambia, Nipe maji ninywe, wewe ungelimwomba yeye, naye angelikupa maji yaliyo hai.”
Ježíš jí odpověděl: „Kdybys věděla, kdo jsem a co ti nabízím, prosila bys ty mne, abych ti dal napít té životodárné vody.“
11 Yule mwanamke akamjibu, “Bwana, wewe huna chombo cha kutekea maji na kisima hiki ni kirefu. Hayo maji ya uzima utayapata wapi?
„Vždyť nemáš žádnou nádobu! Jak chceš nabrat vodu z tak hluboké studny?“namítla žena.
12 Kwani wewe ni mkuu kuliko baba yetu Yakobo ambaye alitupatia kisima hiki, ambacho yeye pamoja na watoto wake na mifugo yake walikitumia?”
„Jsi snad mocnější, než byl náš praotec Jákob, který ji vyhloubil? Čerpal z ní vodu pro sebe, svou rodinu i svůj dobytek.“
13 Yesu akamjibu, “Kila mtu anayekunywa maji ya kisima hiki ataona kiu tena.
Nato jí Ježíš odpověděl:
14 Lakini yeyote anywaye maji nitakayompa hataona kiu kamwe. Maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujika uzima wa milele.” (aiōn g165, aiōnios g166)
„Voda, kterou nabízím já, uhašuje žízeň navždy a naplňuje touhu po věčnosti.“ (aiōn g165, aiōnios g166)
15 Yule mwanamke akamwambia, “Bwana, tafadhali nipe maji hayo ili nisipate kiu tena na wala nisije tena hapa kuteka maji!”
„Pane, tu vodu mi dej ať už sem nemusím chodit, “prosila ho žena.
16 Yesu akamjibu, “Nenda ukamwite mumeo, uje naye hapa.”
„Jdi a přiveď svého muže, “přikázal jí Ježíš.
17 Yule mwanamke akajibu, “Sina mume.” Yesu akamwambia, “Umesema kweli kuwa huna mume.
„Nemám muže, “odpověděla žena. „To máš pravdu, “řekl jí Ježíš.
18 Kwa maana umeshakuwa na wanaume watano na mwanaume unayeishi naye sasa si mume wako! Umesema ukweli.”
„Vystřídala jsi jich pět a ani ten, se kterým žiješ nyní, není tvůj muž.“
19 Yule mwanamke akasema, “Bwana, naona bila shaka wewe ni nabii.
„Pane, vidím, že jsi prorok, “vyhrkla s údivem.
20 Baba zetu waliabudu kwenye mlima huu, lakini ninyi Wayahudi mnasema ni lazima tukaabudu huko Yerusalemu.”
„To bys mi mohl odpovědět, proč vy Židé považujete jen Jeruzalém za místo vhodné k uctívání Boha. Naši předkové se od nepaměti modlili na této hoře.“
21 Yesu akamjibu, “Mwanamke, niamini, wakati unakuja ambapo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala huko Yerusalemu.
Ježíš jí odpověděl: „Věř mi, blíží se doba, kdy lidé nebudou uctívat Boha ani v Jeruzalémě, ani na této hoře.
22 Ninyi Wasamaria mnaabudu msichokijua. Sisi Wayahudi tunamwabudu Mungu tunayemjua kwa sababu wokovu unatoka kwa Wayahudi.
My známe smysl naší bohoslužby, ale vy ho neznáte, protože Mesiáš vyjde ze Židů.
23 Lakini saa yaja, tena ipo, ambapo wale waabuduo halisi, watamwabudu Baba katika roho na kweli. Watu wanaoabudu namna hii, ndio Baba anawatafuta.
Nastává však doba, kdy nebude záležet na tom, kde se kdo modlí, ale jak se modlí. Skuteční vyznavači budou ctít Otce upřímně a neformálně. O takové vyznavače Otci jde.
24 Mungu ni Roho na wote wanaomwabudu imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.”
Bůh je duchovní bytost a ti, kdo ho vzývají, mají tak činit opravdově a pod vedením Ducha svatého.“
25 Yule mwanamke akamwambia, “Ninafahamu kwamba Masiya (aitwaye Kristo) anakuja. Yeye akija, atatueleza mambo yote.”
„Vím, že přijde Mesiáš, “pravila žena, „ten nám všechno vysvětlí.“
26 Yesu akamwambia, “Mimi ninayezungumza nawe, ndiye.”
„Ten Mesiáš jsem já, “řekl jí nato Ježíš.
27 Wakati huo wanafunzi wake wakarudi, wakashangaa sana kumwona akizungumza na mwanamke. Lakini hakuna aliyemuuliza, “Unataka nini kwake?” Au “Kwa nini unazungumza naye?”
V té chvíli se učedníci vrátili z města a byli překvapeni, když Ježíše zastihli v rozhovoru se ženou. Neodvážili se však zeptat, proč s ní mluví.
28 Yule mwanamke akaacha mtungi wake, akarudi mjini akawaambia watu,
Žena nechala své vědro ležet u studny a spěchala do města, kde řekla lidem:
29 “Njooni mkamwone mtu aliyeniambia kila kitu nilichotenda! Je, yawezekana huyu ndiye Kristo?”
„Pojďte se podívat na člověka, s nímž jsem se dosud nesetkala, a přesto o mně všechno ví. Není to snad Mesiáš?“
30 Basi wakamiminika watu kutoka mjini wakamwendea Yesu.
Lidé z města se tedy vydali za Ježíšem.
31 Wakati huo wanafunzi wake walikuwa wakimsihi, “Rabi, kula angalau chochote.”
Učedníci ho zatím pobízeli, aby se najedl.
32 Lakini yeye akawajibu, “Mimi ninacho chakula ambacho ninyi hamkifahamu.”
On však odmítl: „Nebudu jíst. Mám jiný pokrm, který neznáte.“
33 Basi wanafunzi wakaanza kuulizana, “Kuna mtu ambaye amemletea chakula?”
„Kdo mu přinesl jídlo?“říkali si.
34 Lakini Yesu akawajibu, “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya Mungu ambaye amenituma na kuikamilisha kazi yake.
Ježíš je hned vyvedl z nejistoty: „Sytím se tím, že konám Boží vůli. Dokončit jeho dílo – to je můj pokrm.
35 Je, ninyi hamsemi, ‘Bado miezi minne tuvune?’ Inueni macho yenu myaangalie mashamba jinsi mazao yalivyo tayari kuvunwa!
Obilí bude zralé za čtyři měsíce, ale lidé jsou již zralí ke žni.
36 Mvunaji tayari anapokea mshahara wake, naye anakusanya mazao kwa ajili ya uzima wa milele. Ili yeye apandaye na yeye avunaye wafurahi pamoja. (aiōnios g166)
Ten, kdo bude sklízet a shromažďovat tuto úrodu pro věčnost, dostane za svou práci odměnu. A ten, kdo rozséval, bude se radovat spolu s ním. (aiōnios g166)
37 Hivyo kule kusema, ‘Mmoja hupanda na mwingine huvuna,’ ni kweli kabisa.
Neříká se nadarmo, že jeden zasévá a druhý žne.
38 Niliwatuma mkavune mazao ambayo hamkupanda, wengine walifanya kazi ngumu, nanyi mmevuna faida ya taabu yao.”
Já vás posílám sklízet pole, které jste neosévali. Jiní se před vámi lopotili a vy sbíráte výsledky jejich práce.“
39 Wasamaria wengi katika mji ule wakamwamini Yesu kwa sababu ya ushuhuda wa yule mwanamke alipowaambia kwamba, “Ameniambia kila kitu nilichotenda.”
Na základě svědectví té ženy uvěřilo v Ježíše mnoho Samařanů ze Sychar.
40 Hivyo wale Wasamaria walipomjia, wakamsihi akae kwao. Naye akakaa huko siku mbili.
Prosili ho, aby u nich zůstal. Zdržel se tam dva dny, mluvil k nim a jejich víra rostla.
41 Kwa sababu ya neno lake, watu wengi wakaamini.
42 Wakamwambia yule mwanamke, “Sasa tunaamini, wala si kwa sababu ya maneno yako tu, bali kwa kuwa tumemsikia sisi wenyewe. Tumejua hakika kweli ya kwamba huyu ndiye Kristo, Mwokozi wa ulimwengu.”
Ženě řekli: „Teď už věříme ne pro to, co jsi o něm pověděla, ale slyšeli jsme ho a víme, že je opravdu Spasitel světa.“
43 Baada ya zile siku mbili, Yesu aliondoka kwenda Galilaya.
Po dvou dnech pokračoval Ježíš v cestě do Galileje.
44 (Basi Yesu mwenyewe alikuwa amesema kwamba nabii hapati heshima katika nchi yake mwenyewe.)
I když doma nebývá nikdo ve vážnosti, přijali ho Galilejští velmi srdečně. I oni byli totiž o Velikonocích v Jeruzalémě a stali se tam svědky některých jeho zázraků.
45 Alipofika Galilaya, Wagalilaya walimkaribisha, kwani walikuwa wameona yale aliyoyatenda huko Yerusalemu wakati wa Sikukuu ya Pasaka. Kwa maana wao pia walikuwa wamehudhuria hiyo Sikukuu.
46 Hivyo Yesu akaja tena mpaka Kana ya Galilaya, kule alikokuwa amebadili maji kuwa divai. Huko kulikuwepo na afisa mmoja wa mfalme, ambaye mwanawe alikuwa mgonjwa huko Kapernaumu.
Když Ježíš procházel Galileou, zastavil se také v Káni, kde před nedávnem při svatbě proměnil vodu ve víno. Nedaleko odtud leželo město Kafarnaum. Zde žil jeden královský úředník, jehož syn těžce onemocněl.
47 Huyo mtu aliposikia kwamba Yesu alikuwa amewasili Galilaya kutoka Uyahudi, alimwendea na kumwomba ili aje kumponya mwanawe, aliyekuwa mgonjwa karibu ya kufa.
Jakmile se dověděl o Ježíšově návratu, hned ho vyhledal a prosil o pomoc. Žádal ho, aby s ním šel domů a vrátil zdraví umírajícímu synovi.
48 Yesu akamwambia, “Ninyi watu msipoona ishara na miujiza kamwe hamtaamini.”
Ježíš mu odpověděl: „Cožpak mi neuvěříte, pokud neuvidíte zázraky?“
49 Yule afisa wa mfalme akamwambia, “Bwana, tafadhali shuka kabla mwanangu hajafa.”
Královský úředník úpěnlivě prosil: „Pane, pojď hned se mnou, vždyť mi doma umírá syn.“
50 Yesu akamjibu, “Enenda zako, mwanao yu hai.” Yule afisa akaamini yale maneno Yesu aliyomwambia, akaondoka akaenda zake.
Ježíš mu však jen krátce řekl: „Vrať se domů. Tvůj syn je zdráv.“Úředník jeho slovům uvěřil a rychle spěchal domů.
51 Alipokuwa bado yuko njiani, akakutana na watumishi wake wakamwambia kwamba mwanawe yu mzima.
Již cestou potkal své sluhy, kteří mu běželi naproti se zprávou o synově uzdravení.
52 Akawauliza saa ambayo alianza kupata nafuu. Wakamwambia, “Jana yapata saa saba, homa ilimwacha.”
Ten se jich dychtivě zeptal, v kterou dobu se jeho syn uzdravil. „Včera v jednu hodinu odpoledne mu přestala horečka, “odpověděli.
53 Ndipo baba wa huyo mtoto akakumbuka kuwa huo ndio wakati ambapo Yesu alikuwa amemwambia, “Mwanao yu hai.” Kwa hiyo yeye pamoja na wote wa nyumbani mwake wakamwamini Yesu.
Radostí naplněný otec si uvědomil, že právě v tu chvíli mu Ježíš řekl: „Tvůj syn je zdráv.“Po této události královský úředník uvěřil, že Ježíš je pravý Mesiáš. A uvěřila tomu i jeho rodina a všechno služebnictvo.
54 Hii ilikuwa ishara ya pili ambayo Yesu alifanya aliporudi Galilaya kutoka Uyahudi.
Tak Ježíš učinil druhý zázrak v Galileji po svém návratu z Judska.

< Yohana 4 >