< Yohana 3 >
1 Basi palikuwa na mtu mmoja Farisayo, jina lake Nikodemo, mmoja wa Baraza la Wayahudi lililotawala.
nikadimanAmA yihUdIyAnAm adhipatiH phirUzI kSaNadAyAM
2 Huyu alimjia Yesu usiku akamwambia, “Rabi, tunajua kuwa wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kufanya miujiza hii uifanyayo wewe, kama Mungu hayuko pamoja naye.”
yIzaurabhyarNam Avrajya vyAhArSIt, hE gurO bhavAn IzvarAd Agat Eka upadESTA, Etad asmAbhirjnjAyatE; yatO bhavatA yAnyAzcaryyakarmmANi kriyantE paramEzvarasya sAhAyyaM vinA kEnApi tattatkarmmANi karttuM na zakyantE|
3 Yesu akamjibu, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu anayeweza kuuona Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa mara ya pili.”
tadA yIzuruttaraM dattavAn tavAhaM yathArthataraM vyAharAmi punarjanmani na sati kOpi mAnava Izvarasya rAjyaM draSTuM na zaknOti|
4 Nikodemo akauliza, “Awezaje mtu kuzaliwa wakati akiwa mzee? Hakika hawezi kuingia mara ya pili kwenye tumbo la mama yake ili azaliwe!”
tatO nikadImaH pratyavOcat manujO vRddhO bhUtvA kathaM janiSyatE? sa kiM puna rmAtRrjaTharaM pravizya janituM zaknOti?
5 Yesu akamwambia, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu yeyote anayeweza kuingia Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa kwa maji na kwa Roho.
yIzuravAdId yathArthataram ahaM kathayAmi manujE tOyAtmabhyAM puna rna jAtE sa Izvarasya rAjyaM pravESTuM na zaknOti|
6 Mwili huzaa mwili, lakini Roho huzaa roho.
mAMsAd yat jAyatE tan mAMsamEva tathAtmanO yO jAyatE sa Atmaiva|
7 Kwa hiyo usishangae ninapokuambia huna budi ‘kuzaliwa mara ya pili.’
yuSmAbhiH puna rjanitavyaM mamaitasyAM kathAyAm AzcaryaM mA maMsthAH|
8 Upepo huvuma popote upendapo. Mvumo wake unausikia lakini huwezi ukafahamu utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo kwa kila mtu aliyezaliwa na Roho.”
sadAgatiryAM dizamicchati tasyAmEva dizi vAti, tvaM tasya svanaM zuNOSi kintu sa kuta AyAti kutra yAti vA kimapi na jAnAsi tadvAd AtmanaH sakAzAt sarvvESAM manujAnAM janma bhavati|
9 Nikodemo akamuuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”
tadA nikadImaH pRSTavAn Etat kathaM bhavituM zaknOti?
10 Yesu akamwambia, “Wewe ni mwalimu mashuhuri wa Waisraeli, nawe huelewi mambo haya?
yIzuH pratyaktavAn tvamisrAyElO gururbhUtvApi kimEtAM kathAM na vEtsi?
11 Amin, amin ninakuambia, sisi tunazungumza lile tunalolijua na tunashuhudia lile tuliloliona. Lakini ninyi watu hamkubali ushuhuda wetu.
tubhyaM yathArthaM kathayAmi, vayaM yad vidmastad vacmaH yaMcca pazyAmastasyaiva sAkSyaM dadmaH kintu yuSmAbhirasmAkaM sAkSitvaM na gRhyatE|
12 Nimewaambia mambo ya duniani, nanyi hamkuniamini, mtaniaminije basi nitakapowaambia mambo ya mbinguni?
Etasya saMsArasya kathAyAM kathitAyAM yadi yUyaM na vizvasitha tarhi svargIyAyAM kathAyAM kathaM vizvasiSyatha?
13 Hakuna mtu yeyote aliyekwenda mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu.
yaH svargE'sti yaM ca svargAd avArOhat taM mAnavatanayaM vinA kOpi svargaM nArOhat|
14 Kama vile Mose alivyomwinua yule nyoka kule jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu.
aparanjca mUsA yathA prAntarE sarpaM prOtthApitavAn manuSyaputrO'pi tathaivOtthApitavyaH;
15 Ili kila mtu amwaminiye awe na uzima wa milele. (aiōnios )
tasmAd yaH kazcit tasmin vizvasiSyati sO'vinAzyaH san anantAyuH prApsyati| (aiōnios )
16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (aiōnios )
Izvara itthaM jagadadayata yat svamadvitIyaM tanayaM prAdadAt tatO yaH kazcit tasmin vizvasiSyati sO'vinAzyaH san anantAyuH prApsyati| (aiōnios )
17 Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe kuuhukumu ulimwengu, bali kupitia kwake ulimwengu upate kuokolewa.
IzvarO jagatO lOkAn daNPayituM svaputraM na prESya tAn paritrAtuM prESitavAn|
18 Yeyote amwaminiye hahukumiwi, lakini asiyeamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
ataEva yaH kazcit tasmin vizvasiti sa daNPArhO na bhavati kintu yaH kazcit tasmin na vizvasiti sa idAnImEva daNPArhO bhavati, yataH sa IzvarasyAdvitIyaputrasya nAmani pratyayaM na karOti|
19 Hii ndiyo hukumu kwamba: Nuru imekuja ulimwenguni, nao watu wakapenda giza kuliko nuru kwa sababu matendo yao ni maovu.
jagatO madhyE jyOtiH prAkAzata kintu manuSyANAM karmmaNAM dRSTatvAt tE jyOtiSOpi timirE prIyantE EtadEva daNPasya kAraNAM bhavati|
20 Kwa kuwa kila atendaye maovu huchukia nuru, wala haji kwenye nuru ili matendo yake maovu yasifichuliwe.
yaH kukarmma karOti tasyAcArasya dRSTatvAt sa jyOtirRRtIyitvA tannikaTaM nAyAti;
21 Lakini yule aishiye kwa ukweli huja kwenye nuru, ili ionekane wazi kwamba matendo yake yametendeka katika Mungu.”
kintu yaH satkarmma karOti tasya sarvvANi karmmANIzvarENa kRtAnIti sathA prakAzatE tadabhiprAyENa sa jyOtiSaH sannidhim AyAti|
22 Baada ya haya, Yesu na wanafunzi wake walikwenda katika nchi ya Uyahudi, nao wakakaa huko kwa muda na kubatiza.
tataH param yIzuH ziSyaiH sArddhaM yihUdIyadEzaM gatvA tatra sthitvA majjayitum Arabhata|
23 Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni karibu na Salimu kwa sababu huko kulikuwa na maji tele. Watu wazima wakamjia huko ili kubatizwa.
tadA zAlam nagarasya samIpasthAyini ainan grAmE bahutaratOyasthitEstatra yOhan amajjayat tathA ca lOkA Agatya tEna majjitA abhavan|
24 (Hii ilikuwa kabla Yohana hajatiwa gerezani).
tadA yOhan kArAyAM na baddhaH|
25 Mashindano yakazuka kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi mmoja kuhusu suala la desturi ya kunawa kwa utakaso.
aparanjca zAcakarmmaNi yOhAnaH ziSyaiH saha yihUdIyalOkAnAM vivAdE jAtE, tE yOhanaH saMnnidhiM gatvAkathayan,
26 Wakamwendea Yohana wakamwambia, “Rabi, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ngʼambo ya Mto Yordani, yule uliyeshuhudia habari zake, sasa anabatiza na kila mtu anamwendea!”
hE gurO yarddananadyAH pArE bhavatA sArddhaM ya AsIt yasmiMzca bhavAn sAkSyaM pradadAt pazyatu sOpi majjayati sarvvE tasya samIpaM yAnti ca|
27 Yohana akawajibu, “Hakuna mtu yeyote awezaye kupata kitu chochote isipokuwa kile tu alichopewa kutoka mbinguni.
tadA yOhan pratyavOcad IzvarENa na dattE kOpi manujaH kimapi prAptuM na zaknOti|
28 Ninyi wenyewe ni mashahidi wangu kwamba nilisema, ‘Mimi si Kristo, ila nimetumwa nimtangulie.’
ahaM abhiSiktO na bhavAmi kintu tadagrE prESitOsmi yAmimAM kathAM kathitavAnAhaM tatra yUyaM sarvvE sAkSiNaH stha|
29 Bibi arusi ni wa bwana arusi. Lakini rafiki yake bwana arusi anayesimama karibu naye na kusikiliza kutoka kwake, hufurahi sana aisikiapo sauti ya bwana arusi. Kwa sababu hii furaha yangu imekamilika.
yO janaH kanyAM labhatE sa Eva varaH kintu varasya sannidhau daNPAyamAnaM tasya yanmitraM tEna varasya zabdE zrutE'tIvAhlAdyatE mamApi tadvad AnandasiddhirjAtA|
30 Yeye hana budi kuwa mkuu zaidi na mimi nizidi kuwa mdogo.”
tEna kramazO varddhitavyaM kintu mayA hsitavyaM|
31 “Yeye ajaye kutoka juu yu juu ya yote, yeye aliye wa duniani ni wa dunia, naye huzungumza mambo ya duniani. Yeye aliyekuja kutoka mbinguni, yu juu ya yote.
ya UrdhvAdAgacchat sa sarvvESAM mukhyO yazca saMsArAd udapadyata sa sAMsArikaH saMsArIyAM kathAnjca kathayati yastu svargAdAgacchat sa sarvvESAM mukhyaH|
32 Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna yeyote anayekubali ushuhuda wake.
sa yadapazyadazRNOcca tasminnEva sAkSyaM dadAti tathApi prAyazaH kazcit tasya sAkSyaM na gRhlAti;
33 Lakini yeyote anayekubali huo ushuhuda anathibitisha kwamba, Mungu ni kweli.
kintu yO gRhlAti sa Izvarasya satyavAditvaM mudrAggitaM karOti|
34 Yeye aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, kwa kuwa Mungu humtoa Roho pasipo kipimo.
IzvarENa yaH prEritaH saEva IzvarIyakathAM kathayati yata Izvara AtmAnaM tasmai aparimitam adadAt|
35 Baba anampenda Mwana, naye ametia vitu vyote mikononi mwake.
pitA putrE snEhaM kRtvA tasya hastE sarvvANi samarpitavAn|
36 Yeyote anayemwamini Mwana ana uzima wa milele, lakini yeye asiyemwamini Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu itakuwa juu yake.” (aiōnios )
yaH kazcit putrE vizvasiti sa EvAnantam paramAyuH prApnOti kintu yaH kazcit putrE na vizvasiti sa paramAyuSO darzanaM na prApnOti kintvIzvarasya kOpabhAjanaM bhUtvA tiSThati| (aiōnios )