< Yohana 3 >
1 Basi palikuwa na mtu mmoja Farisayo, jina lake Nikodemo, mmoja wa Baraza la Wayahudi lililotawala.
E havia entre os phariseos um homem, chamado Nicodemos, principe dos judeos.
2 Huyu alimjia Yesu usiku akamwambia, “Rabi, tunajua kuwa wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kufanya miujiza hii uifanyayo wewe, kama Mungu hayuko pamoja naye.”
Este foi ter de noite com Jesus, e disse-lhe: Rabbi, bem sabemos que és Mestre, vindo de Deus: porque ninguem pode fazer estes signaes que tu fazes, se Deus não fôr com elle.
3 Yesu akamjibu, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu anayeweza kuuona Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa mara ya pili.”
Jesus respondeu, e disse-lhe: Na verdade, na verdade te digo que aquelle que não nascer de novo, não pode vêr o reino de Deus.
4 Nikodemo akauliza, “Awezaje mtu kuzaliwa wakati akiwa mzee? Hakika hawezi kuingia mara ya pili kwenye tumbo la mama yake ili azaliwe!”
Disse-lhe Nicodemos: Como pode um homem nascer, sendo velho? porventura pode tornar a entrar no ventre de sua mãe, e nascer?
5 Yesu akamwambia, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu yeyote anayeweza kuingia Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa kwa maji na kwa Roho.
Jesus respondeu: Na verdade, na verdade, te digo que aquelle que não nascer da agua e do Espirito não pode entrar no reino de Deus,
6 Mwili huzaa mwili, lakini Roho huzaa roho.
O que é nascido da carne é carne, e o que é nascido do Espirito é espirito.
7 Kwa hiyo usishangae ninapokuambia huna budi ‘kuzaliwa mara ya pili.’
Não te maravilhes de te ter dito: Necessario vos é nascer de novo.
8 Upepo huvuma popote upendapo. Mvumo wake unausikia lakini huwezi ukafahamu utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo kwa kila mtu aliyezaliwa na Roho.”
O vento assopra onde quer, e ouves a sua voz; porém não sabes d'onde vem, nem para onde vae; assim é todo aquelle que é nascido do Espirito.
9 Nikodemo akamuuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”
Nicodemos respondeu, e disse-lhe: Como se pode fazer isto?
10 Yesu akamwambia, “Wewe ni mwalimu mashuhuri wa Waisraeli, nawe huelewi mambo haya?
Jesus respondeu, e disse-lhe: Tu és mestre de Israel, e não sabes isto?
11 Amin, amin ninakuambia, sisi tunazungumza lile tunalolijua na tunashuhudia lile tuliloliona. Lakini ninyi watu hamkubali ushuhuda wetu.
Na verdade, na verdade te digo que dizemos o que sabemos e testificamos o que vimos; e não acceitaes o nosso testemunho.
12 Nimewaambia mambo ya duniani, nanyi hamkuniamini, mtaniaminije basi nitakapowaambia mambo ya mbinguni?
Se vos fallei de coisas terrestres, e não crestes, como crereis, se vos fallar das celestiaes?
13 Hakuna mtu yeyote aliyekwenda mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu.
E ninguem subiu ao céu, senão o que desceu do céu, a saber, o Filho do homem, que está no céu
14 Kama vile Mose alivyomwinua yule nyoka kule jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu.
E, como Moysés levantou a serpente no deserto, assim importa que o Filho do homem seja levantado;
15 Ili kila mtu amwaminiye awe na uzima wa milele. (aiōnios )
Para que todo aquelle que n'elle crê não pereça, mas tenha a vida eterna. (aiōnios )
16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (aiōnios )
Porque Deus amou o mundo de tal maneira, que deu o seu Filho unigenito, para que todo aquelle que n'elle crê não pereça, mas tenha a vida eterna. (aiōnios )
17 Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe kuuhukumu ulimwengu, bali kupitia kwake ulimwengu upate kuokolewa.
Porque Deus enviou o seu Filho ao mundo, não para que condemnasse o mundo, mas para que o mundo fosse salvo por elle.
18 Yeyote amwaminiye hahukumiwi, lakini asiyeamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
Quem crê n'elle não é condemnado; mas quem não crê já está condemnado; porquanto não crê no nome do Unigenito Filho de Deus.
19 Hii ndiyo hukumu kwamba: Nuru imekuja ulimwenguni, nao watu wakapenda giza kuliko nuru kwa sababu matendo yao ni maovu.
E a condemnação é esta: Que a luz veiu ao mundo, e os homens amaram mais as trevas do que a luz, porque as suas obras eram más.
20 Kwa kuwa kila atendaye maovu huchukia nuru, wala haji kwenye nuru ili matendo yake maovu yasifichuliwe.
Porque todo aquelle que faz o mal aborrece a luz, e não vem para a luz, para que as suas obras não sejam arguidas.
21 Lakini yule aishiye kwa ukweli huja kwenye nuru, ili ionekane wazi kwamba matendo yake yametendeka katika Mungu.”
Mas quem obra a verdade vem para a luz, afim de que as suas obras sejam manifestas, porque são feitas em Deus.
22 Baada ya haya, Yesu na wanafunzi wake walikwenda katika nchi ya Uyahudi, nao wakakaa huko kwa muda na kubatiza.
Depois d'isto foi Jesus com os seus discipulos para a terra da Judea; e estava ali com elles, e baptizava.
23 Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni karibu na Salimu kwa sababu huko kulikuwa na maji tele. Watu wazima wakamjia huko ili kubatizwa.
Ora João baptizava tambem em Enon, junto a Salim, porquanto havia ali muitas aguas; e vinham ali, e eram baptizados.
24 (Hii ilikuwa kabla Yohana hajatiwa gerezani).
Porque ainda João não tinha sido lançado na prisão.
25 Mashindano yakazuka kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi mmoja kuhusu suala la desturi ya kunawa kwa utakaso.
Houve pois uma questão entre os discipulos de João e os judeos, ácerca da purificação.
26 Wakamwendea Yohana wakamwambia, “Rabi, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ngʼambo ya Mto Yordani, yule uliyeshuhudia habari zake, sasa anabatiza na kila mtu anamwendea!”
E foram ter com João, e disseram-lhe: Rabbi, aquelle que estava comtigo além do Jordão, do qual tu déste testemunho, eis que baptiza, e todos vão ter com elle
27 Yohana akawajibu, “Hakuna mtu yeyote awezaye kupata kitu chochote isipokuwa kile tu alichopewa kutoka mbinguni.
João respondeu, e disse: O homem não pode receber coisa alguma, se lhe não fôr dada do céu
28 Ninyi wenyewe ni mashahidi wangu kwamba nilisema, ‘Mimi si Kristo, ila nimetumwa nimtangulie.’
Vós mesmos me sois testemunhas de que disse: Eu não sou o Christo, mas sou enviado adiante d'elle.
29 Bibi arusi ni wa bwana arusi. Lakini rafiki yake bwana arusi anayesimama karibu naye na kusikiliza kutoka kwake, hufurahi sana aisikiapo sauti ya bwana arusi. Kwa sababu hii furaha yangu imekamilika.
Aquelle que tem a esposa é o esposo; mas o amigo do esposo, que lhe assiste e o ouve, alegra-se muito com a voz do esposo. Assim pois já este meu gozo está cumprido.
30 Yeye hana budi kuwa mkuu zaidi na mimi nizidi kuwa mdogo.”
A elle convem crescer, porém a mim diminuir.
31 “Yeye ajaye kutoka juu yu juu ya yote, yeye aliye wa duniani ni wa dunia, naye huzungumza mambo ya duniani. Yeye aliyekuja kutoka mbinguni, yu juu ya yote.
Aquelle que vem de cima é sobre todos: aquelle que vem da terra é da terra e falla da terra. Aquelle que vem do céu é sobre todos.
32 Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna yeyote anayekubali ushuhuda wake.
E aquillo que viu e ouviu isso testifica; e ninguem acceita o seu testemunho.
33 Lakini yeyote anayekubali huo ushuhuda anathibitisha kwamba, Mungu ni kweli.
Aquelle que acceitou o seu testemunho, esse sellou que Deus é verdadeiro.
34 Yeye aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, kwa kuwa Mungu humtoa Roho pasipo kipimo.
Porque aquelle que Deus enviou falla as palavras de Deus; porque não lhe dá Deus o Espirito por medida.
35 Baba anampenda Mwana, naye ametia vitu vyote mikononi mwake.
O Pae ama o Filho, e todas as coisas entregou nas suas mãos.
36 Yeyote anayemwamini Mwana ana uzima wa milele, lakini yeye asiyemwamini Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu itakuwa juu yake.” (aiōnios )
Aquelle que crê no Filho tem a vida eterna; porém aquelle que não crê no Filho não verá a vida; mas a ira de Deus sobre elle permanece. (aiōnios )