< Yohana 3 >

1 Basi palikuwa na mtu mmoja Farisayo, jina lake Nikodemo, mmoja wa Baraza la Wayahudi lililotawala.
Now there was a man among the Pharisees whose name was Nicodemus, a ruler of the Jews.
2 Huyu alimjia Yesu usiku akamwambia, “Rabi, tunajua kuwa wewe ni mwalimu uliyetumwa na Mungu, kwa maana hakuna mtu awezaye kufanya miujiza hii uifanyayo wewe, kama Mungu hayuko pamoja naye.”
The same went to Jesus at night and said to Him, “Rabbi, we know that you have come as a teacher from God, because no one can do these signs that you do unless God is with him.”
3 Yesu akamjibu, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu anayeweza kuuona Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa mara ya pili.”
Jesus answered and said to him, “Most assuredly I say to you, unless someone is begotten from Above, he is not able to see the kingdom of God.”
4 Nikodemo akauliza, “Awezaje mtu kuzaliwa wakati akiwa mzee? Hakika hawezi kuingia mara ya pili kwenye tumbo la mama yake ili azaliwe!”
Nicodemus says to Him: “How can a man be begotten, being old? He can't enter his mother's womb a second time and be born, can he?”
5 Yesu akamwambia, “Amin, amin nakuambia, hakuna mtu yeyote anayeweza kuingia Ufalme wa Mungu kama hajazaliwa kwa maji na kwa Roho.
Jesus answered: “Most assuredly I say to you, unless someone is begotten by water and Spirit he is not able to enter the kingdom of God.
6 Mwili huzaa mwili, lakini Roho huzaa roho.
That which has been begotten by the flesh is flesh, and that which has been begotten by the Spirit is spirit.
7 Kwa hiyo usishangae ninapokuambia huna budi ‘kuzaliwa mara ya pili.’
Do not be perplexed that I said to you, ‘You (pl) need to be begotten from Above.’
8 Upepo huvuma popote upendapo. Mvumo wake unausikia lakini huwezi ukafahamu utokako wala uendako. Ndivyo ilivyo kwa kila mtu aliyezaliwa na Roho.”
The wind blows where it wishes, and you (sg) hear its sound, but you do not know where it comes from or where it goes. So it is with everyone who has been begotten by the Spirit.”
9 Nikodemo akamuuliza, “Mambo haya yanawezekanaje?”
Nicodemus answered and said to Him, “How can these things be?”
10 Yesu akamwambia, “Wewe ni mwalimu mashuhuri wa Waisraeli, nawe huelewi mambo haya?
Jesus answered and said to Him: “You are the teacher of Israel, yet you do not understand these things?
11 Amin, amin ninakuambia, sisi tunazungumza lile tunalolijua na tunashuhudia lile tuliloliona. Lakini ninyi watu hamkubali ushuhuda wetu.
Most assuredly I say to you, we speak what we know and testify to what we have seen, but you (pl) do not receive our testimony.
12 Nimewaambia mambo ya duniani, nanyi hamkuniamini, mtaniaminije basi nitakapowaambia mambo ya mbinguni?
If I have told you earthly things and you do not believe, how will you believe if I should tell you the heavenly?
13 Hakuna mtu yeyote aliyekwenda mbinguni isipokuwa yeye aliyeshuka kutoka mbinguni, yaani, Mwana wa Adamu.
No one has gone up into Heaven except the One who came down out of Heaven —the Son of the Man, who is in Heaven.
14 Kama vile Mose alivyomwinua yule nyoka kule jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu.
Also, just as Moses lifted up the snake in the wilderness, just so the Son of the Man must be lifted up,
15 Ili kila mtu amwaminiye awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
so that everyone who believes into Him should not be wasted, but should have eternal life. (aiōnios g166)
16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. (aiōnios g166)
Because God loved the world so much that He gave His only begotten Son, so that everyone who believes into Him should not be wasted, but should have eternal life. (aiōnios g166)
17 Kwa maana Mungu hakumtuma Mwanawe kuuhukumu ulimwengu, bali kupitia kwake ulimwengu upate kuokolewa.
For God did not send His Son into the world in order to condemn the world, but so that the world might be saved through Him.
18 Yeyote amwaminiye hahukumiwi, lakini asiyeamini amekwisha kuhukumiwa, kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.
The one believing into Him is not condemned, but the one not believing has already been condemned, because he has not believed into the name of the only begotten Son of God.
19 Hii ndiyo hukumu kwamba: Nuru imekuja ulimwenguni, nao watu wakapenda giza kuliko nuru kwa sababu matendo yao ni maovu.
“Now this is the basis for the condemning, that the Light has come into the world, but the people loved the darkness rather than the Light, because their deeds were malignant.
20 Kwa kuwa kila atendaye maovu huchukia nuru, wala haji kwenye nuru ili matendo yake maovu yasifichuliwe.
For whoever practices evil hates the Light and does not come to the Light, so that his deeds may not be exposed.
21 Lakini yule aishiye kwa ukweli huja kwenye nuru, ili ionekane wazi kwamba matendo yake yametendeka katika Mungu.”
But whoever does the truth comes to the Light so that his deeds may be clearly seen, that they are done in God.”
22 Baada ya haya, Yesu na wanafunzi wake walikwenda katika nchi ya Uyahudi, nao wakakaa huko kwa muda na kubatiza.
After these things Jesus, with His disciples, went into the Judean countryside, and there He spent time with them and baptized.
23 Yohana naye alikuwa akibatiza huko Ainoni karibu na Salimu kwa sababu huko kulikuwa na maji tele. Watu wazima wakamjia huko ili kubatizwa.
Now John also was baptizing in Aenon, near Salem, because there was plenty of water there. And people were coming and being baptized;
24 (Hii ilikuwa kabla Yohana hajatiwa gerezani).
for John had not yet been thrown into prison.
25 Mashindano yakazuka kati ya baadhi ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi mmoja kuhusu suala la desturi ya kunawa kwa utakaso.
Then some of John's disciples had an argument with a Judean about purification.
26 Wakamwendea Yohana wakamwambia, “Rabi, yule mtu aliyekuwa pamoja nawe ngʼambo ya Mto Yordani, yule uliyeshuhudia habari zake, sasa anabatiza na kila mtu anamwendea!”
So they came to John and said to him, “Rabbi, the One who was with you across the Jordan, about whom you have testified—well, here He is baptizing, and everyone is flocking to Him!”
27 Yohana akawajibu, “Hakuna mtu yeyote awezaye kupata kitu chochote isipokuwa kile tu alichopewa kutoka mbinguni.
John answered and said: “A person can receive nothing unless it has been given to him from Heaven.
28 Ninyi wenyewe ni mashahidi wangu kwamba nilisema, ‘Mimi si Kristo, ila nimetumwa nimtangulie.’
You yourselves can testify that I said, ‘I am not the Christ, but I have been sent ahead of Him.’
29 Bibi arusi ni wa bwana arusi. Lakini rafiki yake bwana arusi anayesimama karibu naye na kusikiliza kutoka kwake, hufurahi sana aisikiapo sauti ya bwana arusi. Kwa sababu hii furaha yangu imekamilika.
He who has the bride is the bridegroom, but the friend of the bridegroom, who stands by and hears him, has great joy at the bridegroom's voice. So this my joy has been fulfilled.
30 Yeye hana budi kuwa mkuu zaidi na mimi nizidi kuwa mdogo.”
He must increase, but I must decrease.
31 “Yeye ajaye kutoka juu yu juu ya yote, yeye aliye wa duniani ni wa dunia, naye huzungumza mambo ya duniani. Yeye aliyekuja kutoka mbinguni, yu juu ya yote.
“He who comes from Above is above all; he who is from the earth is earthly, and speaks of the earth. He who comes from Heaven is above all.
32 Yeye hushuhudia yale aliyoyaona na kuyasikia, lakini hakuna yeyote anayekubali ushuhuda wake.
And to what He has seen and heard He testifies, yet no one receives His testimony.
33 Lakini yeyote anayekubali huo ushuhuda anathibitisha kwamba, Mungu ni kweli.
The one who receives His testimony certifies that God is true.
34 Yeye aliyetumwa na Mungu husema maneno ya Mungu, kwa kuwa Mungu humtoa Roho pasipo kipimo.
For He whom God sent speaks God's words, because God does not give the Spirit by measure.
35 Baba anampenda Mwana, naye ametia vitu vyote mikononi mwake.
The Father loves the Son and has given all things into His hand.
36 Yeyote anayemwamini Mwana ana uzima wa milele, lakini yeye asiyemwamini Mwana hatauona uzima, bali ghadhabu ya Mungu itakuwa juu yake.” (aiōnios g166)
The one believing into the Son has eternal life, but the one disobeying the Son will not see the Life, but the wrath of God will remain upon him.” (aiōnios g166)

< Yohana 3 >