< Yohana 21 >
1 Baada ya haya Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kando ya Bahari ya Tiberia. Yeye alijionyesha kwao hivi:
Після сього явив ся знов Ісус ученикам на морі Тивериядському; явив ся ж так.
2 Simoni Petro, Tomaso aitwaye Didimasi, yaani Pacha, Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili walikuwa pamoja.
Були в купі Симон Петр та Тома, на прізвище Близняк, та Натанаїл із Кани Галилейської, та сини Зеведеєві, та инших учеників Його двоє.
3 Simoni Petro akawaambia wenzake, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Tutakwenda pamoja nawe.” Wakatoka, wakaingia ndani ya mashua, lakini usiku ule hawakupata chochote.
Каже їм Симон Петр: Пійду рибиловити. Кажуть вони йому: Пійдемо й ми з тобою. Вийшли та й улїзли зараз у човен; та не піймали тієї ночі нїчого.
4 Mara baada ya kupambazuka, Yesu akasimama ufuoni, lakini wanafunzi hawakumtambua kwamba alikuwa Yesu.
Як же настав уже ранок, стояв Ісус на березї; та не знали ученики що се був Ісус.
5 Yesu akawaambia, “Wanangu, je, mna samaki wowote?” Wakamjibu, “La.”
Рече тоді їм Ісус: Дїти; чи маєте що їсти? Відказали Йому: Нї.
6 Akawaambia, “Shusheni nyavu upande wa kuume wa mashua yenu nanyi mtapata samaki.” Wakashusha nyavu na tazama wakapata samaki wengi mno hata wakashindwa kuvutia zile nyavu zilizojaa samaki ndani ya mashua.
Він же рече їм: Закиньте невода з правого боку човна, то й знайдете. Закинули ж, і вже не здолїли його витягти задля множества риби.
7 Yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, “Huyu ni Bwana!” Simoni Petro aliposikia haya, akajifunga nguo yake kwa kuwa alikuwa uchi, naye akajitosa baharini.
Каже тоді ученик той, котрого любив Ісус, Петрові: Се Господь. Симон же Петр, почувши, що се Господь, підперезавсь (був бо нагий), та й кинувсь у море.
8 Wale wanafunzi wengine wakaja kwa ile mashua huku wakikokota ule wavu uliyojaa samaki, maana hawakuwa mbali na nchi kavu, ilikuwa yapata dhiraa 200
Инші ж ученики човником приплили (бо недалеко були від землі, а локот на двісті), тягнучи невода з рибою.
9 Walipofika ufuoni, wakaona moto wa makaa na samaki wakiokwa juu yake na mikate.
Скоро вийшли на землю, бачять розложений жар, а на йому рибу і хліб.
10 Yesu akawaambia, “Leteni baadhi ya hao samaki mliovua sasa hivi.”
Рече їм Ісус: Принесіть риби, що вловили тепер.
11 Simoni Petro akapanda kwenye mashua na kuukokota ule wavu pwani. Ulikuwa umejaa samaki wakubwa 153. Ingawa samaki walikuwa wengi kiasi hicho, ule wavu haukuchanika.
Уліз же Симон Петр, та й витяг невід на землю повен риби великої, сто й пятьдесять і три; і хоч стільки її було, не порвав ся невід.
12 Yesu akawaambia, “Njooni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyethubutu kumuuliza, “Wewe ni nani?” Kwa sababu walijua ya kuwa ni Bwana.
рече їм Ісус: Ідіть обідайте. Ніхто ж не важив ся з учеників спитати Його: Хто Ти єси? знаючи, що се Господь.
13 Yesu akaja, akachukua ule mkate, akawapa na vivyo hivyo akawagawia pia wale samaki.
Приходить тоді Ісус і бере хліб, та й дає їм, і риби так само.
14 Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada yake kufufuliwa kutoka kwa wafu.
Се вже втретє явивсь Ісус ученикам своїм, уставши з мертвих.
15 Walipokwisha kula, Yesu akamuuliza Simoni Petro, “Je, Simoni mwana wa Yohana, unanipenda kweli kuliko hawa?” Yeye akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wana-kondoo wangu.”
Як же обідали, рече Ісус Симонові Петру: Симоне Ионин, чи любиш мене більш, нїж сі: Каже Йому: Так, Господи; Ти знаєш, що я люблю Тебе. Рече йому: Паси ягнята мої.
16 Yesu akamwambia tena, “Simoni, mwana wa Yohana, wanipenda?” Petro akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Chunga kondoo zangu.”
Рече йому знов удруге: Симоне Йонин, чи любиш мене? Каже Йому: Так, Господи, Ти знаєш, що я люблю Тебе. Рече йому: Паси вівці мої.
17 Kwa mara ya tatu Yesu akamuuliza Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akahuzunika sana kwa kuwa Yesu alimuuliza mara ya tatu, “Unanipenda?” Akamjibu, “Bwana, wewe unajua yote, unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha kondoo wangu.
Рече йому втретє: Симоне Йонин, чи любиш мене? Засмутив ся Петр, що сказав йому втретє: Чи любиш мене? й каже Йому: Господи, Ти все знаєш; Ти знаєш, що люблю Тебе. Рече йому Ісус: Паси вівці мої.
18 Amin, amin nakuambia, ulipokuwa kijana ulivaa na kwenda unakotaka, lakini utakapokuwa mzee utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvika na kukupeleka usipotaka kwenda.”
Істино, істино глаголю тобі: Як був єси молодий, то підперізував ся сам, і ходив єси куди хотїв; як же зістарієш ся, то простягнеш руки твої, і инший тебе підпереже, й поведе, куди не схочеш.
19 Yesu alisema haya ili kuashiria ni kifo cha aina gani Petro atakachomtukuza nacho Mungu. Kisha Yesu akamwambia Petro, “Nifuate!”
Се ж промовив, означуючи, якою смертю прославить Бога. І, сказавши се, рече йому: Йди слідом за мною.
20 Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akiwafuata. (Huyu ndiye yule mwanafunzi aliyeegama kifuani mwa Yesu walipokula naye chakula cha mwisho na kuuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”)
І обернувшись Петр, бачить ученика, котрого любив Ісус, слідом ідучого, що й на вечері пригорнувсь до грудей Його, і питав: Господи, хто се, що зрадить Тебе?
21 Petro alipomwona huyo mwanafunzi, akamuuliza Yesu, “Bwana na huyu je?”
Сього побачивши Петр, каже Ісусові: Господи, сей же що?
22 Yesu akamjibu, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini? Wewe inakupasa unifuate!”
Рече йому Ісус: Коли схочу, щоб він пробував, доки прийду, що тобі до того? ти йди за мною.
23 Kwa sababu ya maneno haya ya Yesu, uvumi ukaenea miongoni mwa ndugu kwamba huyu mwanafunzi hangekufa. Lakini Yesu hakusema kuwa hangekufa. Yeye alisema tu kwamba, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini?”
І пійшло слово се між братів, що ученик той не вмре, та не сказав йому Ісус, що не вмре; а: Коли схочу, щоб він пробував, доки прийду, що тобі до того?
24 Huyu ndiye yule mwanafunzi anayeshuhudia mambo haya na ndiye ambaye ameandika habari hizi. Nasi tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
Се той ученик, що сьвідкує про се, і писав се; і знаємо, що правдиве сьвідкуваннє його.
25 Lakini kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya. Kama yote yangeliandikwa, nadhani hata ulimwengu wote usingekuwa na nafasi ya kutosha kuweka vitabu vyote ambavyo vingeandikwa. Amen.
Єсть же й иншого багато, що зробив Ісус, що, коли б писати з'осїбна, то думаю, що й сам сьвіт не помістив би писаних книг. Амінь.