< Yohana 21 >
1 Baada ya haya Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kando ya Bahari ya Tiberia. Yeye alijionyesha kwao hivi:
After these things Jesus showed himself again to the disciples at the sea of Tiberias: and in this manner did he show [himself].
2 Simoni Petro, Tomaso aitwaye Didimasi, yaani Pacha, Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili walikuwa pamoja.
There were together Simon Peter, and Thomas called Didymus, and Nathanael of Cana in Galilee, and the [sons] of Zebedee, and two others of his disciples.
3 Simoni Petro akawaambia wenzake, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Tutakwenda pamoja nawe.” Wakatoka, wakaingia ndani ya mashua, lakini usiku ule hawakupata chochote.
Simon Peter saith to them, I go a fishing. They say to him, We also go with thee. They went forth, and entered into a boat immediately; and that night they caught nothing.
4 Mara baada ya kupambazuka, Yesu akasimama ufuoni, lakini wanafunzi hawakumtambua kwamba alikuwa Yesu.
But when the morning had now come, Jesus stood on the shore: but the disciples knew not that it was Jesus.
5 Yesu akawaambia, “Wanangu, je, mna samaki wowote?” Wakamjibu, “La.”
Then Jesus saith to them, Children, have ye any victuals? They answered him, No.
6 Akawaambia, “Shusheni nyavu upande wa kuume wa mashua yenu nanyi mtapata samaki.” Wakashusha nyavu na tazama wakapata samaki wengi mno hata wakashindwa kuvutia zile nyavu zilizojaa samaki ndani ya mashua.
And he said to them, Cast the net on the right side of the boat, and ye shall find. They cast therefore, and now they were not able to draw it for the multitude of fishes.
7 Yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, “Huyu ni Bwana!” Simoni Petro aliposikia haya, akajifunga nguo yake kwa kuwa alikuwa uchi, naye akajitosa baharini.
Therefore that disciple whom Jesus loved saith to Peter, It is the Lord. Now when Simon Peter heard that it was the Lord, he girt [on] his fisher's coat, (for he was naked) and cast himself into the sea.
8 Wale wanafunzi wengine wakaja kwa ile mashua huku wakikokota ule wavu uliyojaa samaki, maana hawakuwa mbali na nchi kavu, ilikuwa yapata dhiraa 200
And the other disciples came in a little boat (for they were not far from land, but as it were two hundred cubits) dragging the net with fishes.
9 Walipofika ufuoni, wakaona moto wa makaa na samaki wakiokwa juu yake na mikate.
As soon then as they had come to land, they saw a fire of coals there, and fish laid upon them, and bread.
10 Yesu akawaambia, “Leteni baadhi ya hao samaki mliovua sasa hivi.”
Jesus saith to them, Bring of the fish which ye have now caught.
11 Simoni Petro akapanda kwenye mashua na kuukokota ule wavu pwani. Ulikuwa umejaa samaki wakubwa 153. Ingawa samaki walikuwa wengi kiasi hicho, ule wavu haukuchanika.
Simon Peter went up, and drew the net to land full of great fishes, a hundred and fifty and three: and notwithstanding there were so many, yet the net was not broken.
12 Yesu akawaambia, “Njooni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyethubutu kumuuliza, “Wewe ni nani?” Kwa sababu walijua ya kuwa ni Bwana.
Jesus saith to them, Come [and] dine. And none of the disciples durst ask him, Who art thou? knowing that it was the Lord.
13 Yesu akaja, akachukua ule mkate, akawapa na vivyo hivyo akawagawia pia wale samaki.
Jesus then cometh, and taketh bread, and giveth them, and fish likewise.
14 Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada yake kufufuliwa kutoka kwa wafu.
This is now the third time that Jesus showed himself to his disciples, after he had risen from the dead.
15 Walipokwisha kula, Yesu akamuuliza Simoni Petro, “Je, Simoni mwana wa Yohana, unanipenda kweli kuliko hawa?” Yeye akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wana-kondoo wangu.”
So when they had dined, Jesus saith to Simon Peter, Simon [son] of Jonas, lovest thou me more than these? He saith to him, Yes, Lord: thou knowest that I love thee. He saith to him, Feed my lambs.
16 Yesu akamwambia tena, “Simoni, mwana wa Yohana, wanipenda?” Petro akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Chunga kondoo zangu.”
He saith to him again the second time, Simon [son] of Jonas, lovest thou me? He saith to him, Yes, Lord: thou knowest that I love thee. He saith to him, Feed my sheep.
17 Kwa mara ya tatu Yesu akamuuliza Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akahuzunika sana kwa kuwa Yesu alimuuliza mara ya tatu, “Unanipenda?” Akamjibu, “Bwana, wewe unajua yote, unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha kondoo wangu.
He saith to him the third time, Simon [son] of Jonas, lovest thou me? Peter was grieved, because he said to him the third time, Lovest thou me? And he said to him, Lord, thou knowest all things; thou knowest that I love thee. Jesus saith to him, Feed my sheep.
18 Amin, amin nakuambia, ulipokuwa kijana ulivaa na kwenda unakotaka, lakini utakapokuwa mzee utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvika na kukupeleka usipotaka kwenda.”
Verily, verily, I say to thee, When thou wast young, thou didst gird thyself and walk whither thou wouldest: but when thou shalt be old, thou shalt stretch forth thy hands, and another shall gird thee, and carry [thee] whither thou wouldst not.
19 Yesu alisema haya ili kuashiria ni kifo cha aina gani Petro atakachomtukuza nacho Mungu. Kisha Yesu akamwambia Petro, “Nifuate!”
This he spoke, signifying by what death he should glorify God. And when he had spoken this, he saith to him, Follow me.
20 Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akiwafuata. (Huyu ndiye yule mwanafunzi aliyeegama kifuani mwa Yesu walipokula naye chakula cha mwisho na kuuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”)
Then Peter turning about, seeth the disciple whom Jesus loved, following; (who also leaned on his breast at supper, and said, Lord, who is he that betrayeth thee?)
21 Petro alipomwona huyo mwanafunzi, akamuuliza Yesu, “Bwana na huyu je?”
Peter seeing him, saith to Jesus, Lord, and what [shall] this man [do]?
22 Yesu akamjibu, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini? Wewe inakupasa unifuate!”
Jesus saith to him, If I will that he shall tarry till I come, what [is that] to thee? Follow thou me.
23 Kwa sababu ya maneno haya ya Yesu, uvumi ukaenea miongoni mwa ndugu kwamba huyu mwanafunzi hangekufa. Lakini Yesu hakusema kuwa hangekufa. Yeye alisema tu kwamba, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini?”
Then this saying went abroad among the brethren, that that disciple should not die: yet Jesus said not to him, He shall not die; but, if I will that he shall tarry till I come, what [is that] to thee?
24 Huyu ndiye yule mwanafunzi anayeshuhudia mambo haya na ndiye ambaye ameandika habari hizi. Nasi tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
This is the disciple who testifieth of these things, and wrote these things: and we know that his testimony is true.
25 Lakini kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya. Kama yote yangeliandikwa, nadhani hata ulimwengu wote usingekuwa na nafasi ya kutosha kuweka vitabu vyote ambavyo vingeandikwa. Amen.
And there are also many other things which Jesus did, which, if they should be written every one, I suppose that even the world itself could not contain the books that would be written. Amen.