< Yohana 21 >
1 Baada ya haya Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kando ya Bahari ya Tiberia. Yeye alijionyesha kwao hivi:
After these things Jesus showed himself again to the disciples at the Sea of Tiberias. This is how he showed himself:
2 Simoni Petro, Tomaso aitwaye Didimasi, yaani Pacha, Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili walikuwa pamoja.
Simon Peter was together with Thomas called Didymus, Nathaniel from Cana in Galilee, the sons of Zebedee, and two other disciples of Jesus.
3 Simoni Petro akawaambia wenzake, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Tutakwenda pamoja nawe.” Wakatoka, wakaingia ndani ya mashua, lakini usiku ule hawakupata chochote.
Simon Peter said to them, “I am going fishing.” They said to him, “We, too, will come with you.” They went and got into a boat, but they caught nothing during the whole night.
4 Mara baada ya kupambazuka, Yesu akasimama ufuoni, lakini wanafunzi hawakumtambua kwamba alikuwa Yesu.
Now, when it was already early in the morning, Jesus stood on the beach, but the disciples did not know it was Jesus.
5 Yesu akawaambia, “Wanangu, je, mna samaki wowote?” Wakamjibu, “La.”
So Jesus said to them, “Young men, do you have anything to eat?” They answered him, “No.”
6 Akawaambia, “Shusheni nyavu upande wa kuume wa mashua yenu nanyi mtapata samaki.” Wakashusha nyavu na tazama wakapata samaki wengi mno hata wakashindwa kuvutia zile nyavu zilizojaa samaki ndani ya mashua.
He said to them, “Throw your net on the right side of the boat, and you will find some.” So they threw their net and were not able to draw it in because of the large number of fish.
7 Yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, “Huyu ni Bwana!” Simoni Petro aliposikia haya, akajifunga nguo yake kwa kuwa alikuwa uchi, naye akajitosa baharini.
Then the disciple whom Jesus loved said to Peter, “It is the Lord.” When Simon Peter heard that it was the Lord, he tied up his outer garment (for he was undressed), and threw himself into the sea.
8 Wale wanafunzi wengine wakaja kwa ile mashua huku wakikokota ule wavu uliyojaa samaki, maana hawakuwa mbali na nchi kavu, ilikuwa yapata dhiraa 200
The other disciples came in the boat (for they were not far from the land, about two hundred cubits off), and they were pulling the net full of fish.
9 Walipofika ufuoni, wakaona moto wa makaa na samaki wakiokwa juu yake na mikate.
When they got out upon the land, they saw a charcoal fire there and fish laid on it, with bread.
10 Yesu akawaambia, “Leteni baadhi ya hao samaki mliovua sasa hivi.”
Jesus said to them, “Bring some of the fish that you have just caught.”
11 Simoni Petro akapanda kwenye mashua na kuukokota ule wavu pwani. Ulikuwa umejaa samaki wakubwa 153. Ingawa samaki walikuwa wengi kiasi hicho, ule wavu haukuchanika.
Simon Peter then went up and drew the net to land, full of large fish; 153. There were so many, but the net was not torn.
12 Yesu akawaambia, “Njooni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyethubutu kumuuliza, “Wewe ni nani?” Kwa sababu walijua ya kuwa ni Bwana.
Jesus said to them, “Come and eat breakfast.” None of the disciples dared ask him, “Who are you?” They knew it was the Lord.
13 Yesu akaja, akachukua ule mkate, akawapa na vivyo hivyo akawagawia pia wale samaki.
Jesus came, took the bread, and gave it to them, and the fish also.
14 Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada yake kufufuliwa kutoka kwa wafu.
This was the third time that Jesus showed himself to the disciples after he had risen from the dead.
15 Walipokwisha kula, Yesu akamuuliza Simoni Petro, “Je, Simoni mwana wa Yohana, unanipenda kweli kuliko hawa?” Yeye akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wana-kondoo wangu.”
After they ate breakfast, Jesus said to Simon Peter, “Simon son of John, do you love me more than these?” Peter said to him, “Yes Lord, you know that I love you.” Jesus said to him, “Feed my lambs.”
16 Yesu akamwambia tena, “Simoni, mwana wa Yohana, wanipenda?” Petro akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Chunga kondoo zangu.”
He said to him again a second time, “Simon son of John, do you love me?” Peter said to him, “Yes Lord, you know that I love you.” Jesus said to him, “Take care of my sheep.”
17 Kwa mara ya tatu Yesu akamuuliza Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akahuzunika sana kwa kuwa Yesu alimuuliza mara ya tatu, “Unanipenda?” Akamjibu, “Bwana, wewe unajua yote, unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha kondoo wangu.
He said to him a third time, “Simon son of John, do you love me?” Peter was sad because Jesus had said to him a third time, “Do you love me?” He said to him, “Lord, you know all things, you know that I love you.” Jesus said to him, “Feed my sheep.
18 Amin, amin nakuambia, ulipokuwa kijana ulivaa na kwenda unakotaka, lakini utakapokuwa mzee utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvika na kukupeleka usipotaka kwenda.”
Truly, truly, I say to you, when you were young, you used to clothe yourself and walk wherever you wanted, but when you become old, you will stretch out your hands, and someone else will clothe you and carry you where you will not want to go.”
19 Yesu alisema haya ili kuashiria ni kifo cha aina gani Petro atakachomtukuza nacho Mungu. Kisha Yesu akamwambia Petro, “Nifuate!”
Now Jesus said this in order to indicate with what kind of death Peter would glorify God. After he had said this, he said to Peter, “Follow me.”
20 Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akiwafuata. (Huyu ndiye yule mwanafunzi aliyeegama kifuani mwa Yesu walipokula naye chakula cha mwisho na kuuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”)
Peter turned around and saw the disciple whom Jesus loved following them, the one who had also leaned back against the side of Jesus at the dinner and who had said, “Lord, who is the one who will betray you?”
21 Petro alipomwona huyo mwanafunzi, akamuuliza Yesu, “Bwana na huyu je?”
Peter saw him and then said to Jesus, “Lord, what will this man do?”
22 Yesu akamjibu, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini? Wewe inakupasa unifuate!”
Jesus said to him, “If I want him to stay until I come, what is that to you? Follow me.”
23 Kwa sababu ya maneno haya ya Yesu, uvumi ukaenea miongoni mwa ndugu kwamba huyu mwanafunzi hangekufa. Lakini Yesu hakusema kuwa hangekufa. Yeye alisema tu kwamba, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini?”
So this statement spread among the brothers, that that disciple would not die. Yet Jesus did not say to Peter that the other disciple would not die, but, “If I want him to stay until I come, what is that to you?”
24 Huyu ndiye yule mwanafunzi anayeshuhudia mambo haya na ndiye ambaye ameandika habari hizi. Nasi tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
This is the disciple who testifies about these things, and who wrote these things, and we know that his testimony is true.
25 Lakini kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya. Kama yote yangeliandikwa, nadhani hata ulimwengu wote usingekuwa na nafasi ya kutosha kuweka vitabu vyote ambavyo vingeandikwa. Amen.
There are also many other things that Jesus did. If each one were written down, I suppose that even the world itself could not contain the books that would be written.