< Yohana 21 >
1 Baada ya haya Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kando ya Bahari ya Tiberia. Yeye alijionyesha kwao hivi:
After these things he manifested himself again to the disciples at the lake of Tiberias. And he manifested himself in this manner.
2 Simoni Petro, Tomaso aitwaye Didimasi, yaani Pacha, Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili walikuwa pamoja.
There were together Simon Peter, and Thomas called Didymus, and Nathanael of Cana of Galilee, and the sons of Zebedee, and two others of his disciples.
3 Simoni Petro akawaambia wenzake, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Tutakwenda pamoja nawe.” Wakatoka, wakaingia ndani ya mashua, lakini usiku ule hawakupata chochote.
Simon Peter saith to them, I am going a fishing. They say to him, We also will go with thee. They set out and went into the boat, and on that night caught nothing.
4 Mara baada ya kupambazuka, Yesu akasimama ufuoni, lakini wanafunzi hawakumtambua kwamba alikuwa Yesu.
But when the morning was coming on, Jesus stood on the shore; but the disciples did not know that it was Jesus.
5 Yesu akawaambia, “Wanangu, je, mna samaki wowote?” Wakamjibu, “La.”
Then Jesus saith to them, Children, have ye any fish? They answered him, No.
6 Akawaambia, “Shusheni nyavu upande wa kuume wa mashua yenu nanyi mtapata samaki.” Wakashusha nyavu na tazama wakapata samaki wengi mno hata wakashindwa kuvutia zile nyavu zilizojaa samaki ndani ya mashua.
And he said to them, Cast the net on the right side of the boat, and ye will find. And they cast it, and now they were not able to draw it for the multitude of the fishes.
7 Yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, “Huyu ni Bwana!” Simoni Petro aliposikia haya, akajifunga nguo yake kwa kuwa alikuwa uchi, naye akajitosa baharini.
Therefore that disciple whom Jesus loved saith to Peter, It is the Lord. Simon Peter therefore, hearing that it was the Lord, girded on his outer garment, for he had on nothing but his under one, and threw himself into the lake.
8 Wale wanafunzi wengine wakaja kwa ile mashua huku wakikokota ule wavu uliyojaa samaki, maana hawakuwa mbali na nchi kavu, ilikuwa yapata dhiraa 200
And the other disciples came in the boat, (for they were not far from land, only about two hundred cubits, ) dragging the net with the fishes.
9 Walipofika ufuoni, wakaona moto wa makaa na samaki wakiokwa juu yake na mikate.
When therefore they had come to land, they see a fire of coals there, and a fish lying thereon, and bread.
10 Yesu akawaambia, “Leteni baadhi ya hao samaki mliovua sasa hivi.”
Jesus saith to them, Bring of the fish which ye have now caught.
11 Simoni Petro akapanda kwenye mashua na kuukokota ule wavu pwani. Ulikuwa umejaa samaki wakubwa 153. Ingawa samaki walikuwa wengi kiasi hicho, ule wavu haukuchanika.
Simon Peter therefore went on board, and drew the net to land full of great fishes, a hundred and fifty three; and though there were so many, the net was not broken.
12 Yesu akawaambia, “Njooni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyethubutu kumuuliza, “Wewe ni nani?” Kwa sababu walijua ya kuwa ni Bwana.
Jesus saith to them, Come and breakfast. But no one of the disciples durst ask him, Who art thou? knowing that it was the Lord.
13 Yesu akaja, akachukua ule mkate, akawapa na vivyo hivyo akawagawia pia wale samaki.
Jesus cometh and taketh the bread, and giveth them, and the fish likewise.
14 Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada yake kufufuliwa kutoka kwa wafu.
This is now the third time that Jesus manifested himself to his disciples, after he had risen from the dead.
15 Walipokwisha kula, Yesu akamuuliza Simoni Petro, “Je, Simoni mwana wa Yohana, unanipenda kweli kuliko hawa?” Yeye akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wana-kondoo wangu.”
So when they had breakfasted, Jesus saith to Simon Peter, Simon, son of John, lovest thou me more than these? He saith to him, Yea, Lord, thou knowest that I love thee. He saith to him, Feed my lambs.
16 Yesu akamwambia tena, “Simoni, mwana wa Yohana, wanipenda?” Petro akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Chunga kondoo zangu.”
He saith to him again a second time, Simon, son of John, lovest thou me? He saith to him, Yea, Lord, thou knowest that I love thee. He saith to him, Tend my sheep.
17 Kwa mara ya tatu Yesu akamuuliza Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akahuzunika sana kwa kuwa Yesu alimuuliza mara ya tatu, “Unanipenda?” Akamjibu, “Bwana, wewe unajua yote, unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha kondoo wangu.
He saith to him the third time, Simon, son of John, lovest thou me? Peter was grieved because he said to him the third time, Lovest thou me? And he said to him, Lord, thou knowest all things; thou knowest that I love thee. He saith to him, Feed my sheep.
18 Amin, amin nakuambia, ulipokuwa kijana ulivaa na kwenda unakotaka, lakini utakapokuwa mzee utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvika na kukupeleka usipotaka kwenda.”
Truly, truly do I say to thee, when thou wast young, thou didst gird thyself, and walk whither thou wouldst; but when thou hast grown old, thou wilt stretch forth thy hands, and another will gird thee, and carry thee whither thou wouldst not.
19 Yesu alisema haya ili kuashiria ni kifo cha aina gani Petro atakachomtukuza nacho Mungu. Kisha Yesu akamwambia Petro, “Nifuate!”
This he said, signifying by what manner of death he was to glorify God. And having thus spoken, he saith to him, Follow me.
20 Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akiwafuata. (Huyu ndiye yule mwanafunzi aliyeegama kifuani mwa Yesu walipokula naye chakula cha mwisho na kuuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”)
Peter, turning round, seeth the disciple whom Jesus loved following, —who also at supper leaned back on his breast, and said, Lord, who is he that betrayeth thee?—
21 Petro alipomwona huyo mwanafunzi, akamuuliza Yesu, “Bwana na huyu je?”
Peter, seeing him, saith to Jesus, Lord, and how will it be with him?
22 Yesu akamjibu, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini? Wewe inakupasa unifuate!”
Jesus saith to him, If it be my will that he remain till I come, what is it to thee? Follow thou me.
23 Kwa sababu ya maneno haya ya Yesu, uvumi ukaenea miongoni mwa ndugu kwamba huyu mwanafunzi hangekufa. Lakini Yesu hakusema kuwa hangekufa. Yeye alisema tu kwamba, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini?”
This report therefore went abroad among the brethren, that this disciple was not to die. And yet Jesus did not say to him, He will not die; but, If it be my will that he remain till I come, what is it to thee?
24 Huyu ndiye yule mwanafunzi anayeshuhudia mambo haya na ndiye ambaye ameandika habari hizi. Nasi tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
This is the disciple who testifieth of these things, and hath written these things; and we know that his testimony is true.
25 Lakini kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya. Kama yote yangeliandikwa, nadhani hata ulimwengu wote usingekuwa na nafasi ya kutosha kuweka vitabu vyote ambavyo vingeandikwa. Amen.