< Yohana 21 >

1 Baada ya haya Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kando ya Bahari ya Tiberia. Yeye alijionyesha kwao hivi:
After these things Jesus, risen from the dead, revealed Himself to His disciples at the Sea of Tiberias, and He did it like this:
2 Simoni Petro, Tomaso aitwaye Didimasi, yaani Pacha, Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili walikuwa pamoja.
Simon Peter, Thomas (called Twin), Nathanael (from Cana of Galilee), Zebedee's sons and two others of His disciples were together.
3 Simoni Petro akawaambia wenzake, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Tutakwenda pamoja nawe.” Wakatoka, wakaingia ndani ya mashua, lakini usiku ule hawakupata chochote.
Simon Peter says to them, “I'm going fishing.” They say to him, “We're coming with you.” Off they went and got right into the boat, and that whole night they caught nothing.
4 Mara baada ya kupambazuka, Yesu akasimama ufuoni, lakini wanafunzi hawakumtambua kwamba alikuwa Yesu.
Well when daybreak had now come Jesus stood on the beach; however the disciples did not know that it was Jesus.
5 Yesu akawaambia, “Wanangu, je, mna samaki wowote?” Wakamjibu, “La.”
Then Jesus says to them, “Boys, you don't have any food, do you?” They answered Him, “No.”
6 Akawaambia, “Shusheni nyavu upande wa kuume wa mashua yenu nanyi mtapata samaki.” Wakashusha nyavu na tazama wakapata samaki wengi mno hata wakashindwa kuvutia zile nyavu zilizojaa samaki ndani ya mashua.
So He said to them, “Cast the net on the right side of the boat and you will find.” So they did, and now they were unable to haul it in because of the multitude of fish!
7 Yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, “Huyu ni Bwana!” Simoni Petro aliposikia haya, akajifunga nguo yake kwa kuwa alikuwa uchi, naye akajitosa baharini.
Then that disciple whom Jesus loved says to Peter, “It's the Lord!” Upon hearing that it was the Lord, Simon Peter tied on his outer garment (for he was stripped) and plunged into the sea.
8 Wale wanafunzi wengine wakaja kwa ile mashua huku wakikokota ule wavu uliyojaa samaki, maana hawakuwa mbali na nchi kavu, ilikuwa yapata dhiraa 200
But the other disciples came in the little boat dragging the net with the fish (for they were not far from the land, but about 100 yards).
9 Walipofika ufuoni, wakaona moto wa makaa na samaki wakiokwa juu yake na mikate.
Then, as they stepped onto the land they saw a charcoal fire in place with fish lying on it, and bread.
10 Yesu akawaambia, “Leteni baadhi ya hao samaki mliovua sasa hivi.”
Jesus says to them, “Bring some of the fish that you have just caught.”
11 Simoni Petro akapanda kwenye mashua na kuukokota ule wavu pwani. Ulikuwa umejaa samaki wakubwa 153. Ingawa samaki walikuwa wengi kiasi hicho, ule wavu haukuchanika.
Simon Peter got up and dragged the net onto the land, full of one hundred and fifty-three large fish; and although being so many, the net was not torn.
12 Yesu akawaambia, “Njooni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyethubutu kumuuliza, “Wewe ni nani?” Kwa sababu walijua ya kuwa ni Bwana.
Jesus says to them, “Come have breakfast!” Well not one of the disciples dared to ask Him, “Who are you?”—knowing that it was the Lord.
13 Yesu akaja, akachukua ule mkate, akawapa na vivyo hivyo akawagawia pia wale samaki.
Then Jesus comes and takes the bread and gives it to them, as also the fish.
14 Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada yake kufufuliwa kutoka kwa wafu.
This was already a third time that Jesus appeared to His disciples after He was raised from among the dead.
15 Walipokwisha kula, Yesu akamuuliza Simoni Petro, “Je, Simoni mwana wa Yohana, unanipenda kweli kuliko hawa?” Yeye akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wana-kondoo wangu.”
So, when they had eaten breakfast, Jesus says to Simon Peter, “Simon, son of Jonah, do you love me more than these?” He says to Him, “Yes, Lord, you know that I'm fond of you.” He says to him, “Feed my lambs.”
16 Yesu akamwambia tena, “Simoni, mwana wa Yohana, wanipenda?” Petro akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Chunga kondoo zangu.”
He says to him again, a second time, “Simon, son of Jonah, do you love me?” He says to Him, “Yes, Lord, you know that I'm fond of you.” He says to him, “Shepherd my sheep.”
17 Kwa mara ya tatu Yesu akamuuliza Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akahuzunika sana kwa kuwa Yesu alimuuliza mara ya tatu, “Unanipenda?” Akamjibu, “Bwana, wewe unajua yote, unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha kondoo wangu.
The third time He says to him, “Simon, son of Jonah, are you fond of me?” Peter was grieved in that the third time He said to him, “Are you fond of me?” and said to Him: “Lord, you know all things. You know that I'm fond of you!” Jesus says to him: “Feed my sheep.
18 Amin, amin nakuambia, ulipokuwa kijana ulivaa na kwenda unakotaka, lakini utakapokuwa mzee utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvika na kukupeleka usipotaka kwenda.”
Most assuredly I say to you, when you were younger you used to get dressed and walk where you wished; but when you are old you will stretch out your hands and another will dress you and carry you where you do not wish.”
19 Yesu alisema haya ili kuashiria ni kifo cha aina gani Petro atakachomtukuza nacho Mungu. Kisha Yesu akamwambia Petro, “Nifuate!”
(He said this to indicate the kind of death by which he would glorify God.) And upon saying that He says to him, “Follow me!”
20 Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akiwafuata. (Huyu ndiye yule mwanafunzi aliyeegama kifuani mwa Yesu walipokula naye chakula cha mwisho na kuuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”)
But turning around Peter sees the disciple whom Jesus loved following (that is the one who reclined on His chest at the supper and said, “Lord, who is the one who is betraying you?”).
21 Petro alipomwona huyo mwanafunzi, akamuuliza Yesu, “Bwana na huyu je?”
Seeing him, Peter says to Jesus, “Lord, what about him?”
22 Yesu akamjibu, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini? Wewe inakupasa unifuate!”
Jesus says to him: “If I want him to remain until I come, what is that to you? You follow me.”
23 Kwa sababu ya maneno haya ya Yesu, uvumi ukaenea miongoni mwa ndugu kwamba huyu mwanafunzi hangekufa. Lakini Yesu hakusema kuwa hangekufa. Yeye alisema tu kwamba, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini?”
So this saying spread among the brothers, that this disciple would not die. Yet Jesus did not say to him [Peter] that he [John] would not die, but, “If I want him to remain until I come, what is that to you?”
24 Huyu ndiye yule mwanafunzi anayeshuhudia mambo haya na ndiye ambaye ameandika habari hizi. Nasi tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
This is the disciple who is testifying to these things, and who wrote them; and we know that his testimony is true.
25 Lakini kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya. Kama yote yangeliandikwa, nadhani hata ulimwengu wote usingekuwa na nafasi ya kutosha kuweka vitabu vyote ambavyo vingeandikwa. Amen.
Indeed, there are also many other things that Jesus did, which if they were written one by one, I suppose that not even the whole world could contain the books that would be written! Amen.

< Yohana 21 >