< Yohana 21 >
1 Baada ya haya Yesu akawatokea tena wanafunzi wake kando ya Bahari ya Tiberia. Yeye alijionyesha kwao hivi:
इना गल्लां दे बाद यीशुऐ अपणे आपे जो तिबिरियास झिला दे बखे चेलयां जो दर्शण दिते कने इस तरीके ने दर्शण दिते।
2 Simoni Petro, Tomaso aitwaye Didimasi, yaani Pacha, Nathanaeli wa Kana ya Galilaya, wana wa Zebedayo na wanafunzi wengine wawili walikuwa pamoja.
शमौन पतरस कने थोमा जिसयो दिदुमुस बोलदे न, कने गलील प्रदेश दे काना शेहरे दा नतनएल कने जब्दी दे पुत्र, कने उदे चेलयां चे दो जणे होर गिठे होए थे।
3 Simoni Petro akawaambia wenzake, “Mimi naenda kuvua samaki.” Nao wakamwambia, “Tutakwenda pamoja nawe.” Wakatoka, wakaingia ndani ya mashua, lakini usiku ule hawakupata chochote.
शमौन पतरसे उना जो बोलया, मैं मछियां पकड़ना चलया है। उना उसला बोलया, “असां भी तेरे सोगी चलदे न।” तां सै निकली करी किस्तिया पर चढ़ी गे, पर उसा राती उना कुछ नी पकड़या।
4 Mara baada ya kupambazuka, Yesu akasimama ufuoni, lakini wanafunzi hawakumtambua kwamba alikuwa Yesu.
अगले दिने ब्याग होंदे ही यीशु कनारे पर खड़ोतया था, पर चेलयां उसयो पछेणया नी की ऐ यीशु है।
5 Yesu akawaambia, “Wanangu, je, mna samaki wowote?” Wakamjibu, “La.”
तालू यीशुऐ उना जो बोलया, हे मेरे प्यारो, क्या तुहाड़े बाल कुछ खांणे जो है? उना जबाब दिता, “नी।”
6 Akawaambia, “Shusheni nyavu upande wa kuume wa mashua yenu nanyi mtapata samaki.” Wakashusha nyavu na tazama wakapata samaki wengi mno hata wakashindwa kuvutia zile nyavu zilizojaa samaki ndani ya mashua.
यीशुऐ उना जो बोलया, “किस्तिया दे सजे पास्से जाल फेंका, तां मिलणियां।” तालू उना जाल फेंकया, कने हुण मछियां जादा होणे दिया बजा ने उना ला जाल नी खिची होया।
7 Yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akamwambia Petro, “Huyu ni Bwana!” Simoni Petro aliposikia haya, akajifunga nguo yake kwa kuwa alikuwa uchi, naye akajitosa baharini.
इस तांई उस चेले ने जिसने प्रभु प्यार रखदा था पतरसे जो बोलया, “ऐ तां प्रभु है।” जालू शमौने ऐ सुणया की प्रभु यीशु है, तां उनी अपणे सै कपड़े पाई ले जड़े उनी कम्म करदे बेले उतारी दितयो थे कने पाणिये च छाल देई दिती।
8 Wale wanafunzi wengine wakaja kwa ile mashua huku wakikokota ule wavu uliyojaa samaki, maana hawakuwa mbali na nchi kavu, ilikuwa yapata dhiraa 200
पर होर चेले डोंगिया पर मछियां ने भरूऐ जाले जो खिंज्जी लेई आऐ, क्योंकि सै कनारे ला जादा दूर नी थे, कोई सो मीटर दूर थे।
9 Walipofika ufuoni, wakaona moto wa makaa na samaki wakiokwa juu yake na mikate.
जालू सै कनारे पर पुज्जे, तां उना कोलयां दिया अग्गी पर मछियां कने उदे बखे रोटियां रखियां दिखियां।
10 Yesu akawaambia, “Leteni baadhi ya hao samaki mliovua sasa hivi.”
यीशुऐ उना जो बोलया, “जड़ियां मछियां तुसां हुण पकड़िया न, उना चे थोड़िया लेई ओआ।”
11 Simoni Petro akapanda kwenye mashua na kuukokota ule wavu pwani. Ulikuwa umejaa samaki wakubwa 153. Ingawa samaki walikuwa wengi kiasi hicho, ule wavu haukuchanika.
शमौन पतरसे डोंगिया पर चढ़ी करी इकसो त्रियूँजा मछियां ने भरया जाल कनारे पर खिचया, कने इतणियां मछियां होंणे ने भी जाल नी फटया।
12 Yesu akawaambia, “Njooni mpate kifungua kinywa.” Hakuna hata mmoja wa wanafunzi aliyethubutu kumuuliza, “Wewe ni nani?” Kwa sababu walijua ya kuwa ni Bwana.
यीशुऐ उना जो बोलया, “ओआ रोटी खाई लिया।” कने चेलयां चे कुसयो भी होंसला नी होया, की उसला पूछन, तू कुण है? “क्योंकि सै जाणदे थे की ऐ प्रभु ही है।”
13 Yesu akaja, akachukua ule mkate, akawapa na vivyo hivyo akawagawia pia wale samaki.
यीशुऐ रोटी लेईकरी उना जो दिती, कने तियां ही मच्छी भी दिती।
14 Hii ilikuwa mara ya tatu Yesu kuwatokea wanafunzi wake baada yake kufufuliwa kutoka kwa wafu.
ऐ तिजी बरी है की यीशुऐ मरी करी जिंदा होणे बाद चेलयां जो दर्शण दिते न।
15 Walipokwisha kula, Yesu akamuuliza Simoni Petro, “Je, Simoni mwana wa Yohana, unanipenda kweli kuliko hawa?” Yeye akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha wana-kondoo wangu.”
रोटी खाणे बाद यीशुऐ शमौन पतरसे जो पुछया, हे यूहन्ना दे पुत्र शमौन, क्या तू सच्ची इना बाकियां ला जादा मिंजो ने प्यार करदा है? उनी यीशुऐ जो बोलया, हां प्रभु; तू तां जाणदा है, की मैं तिजो पर भरोसा रखदा है, उनी उना जो बोलया, “मेरे छेलुआं दी रखबाली कर।”
16 Yesu akamwambia tena, “Simoni, mwana wa Yohana, wanipenda?” Petro akamjibu, “Ndiyo Bwana, wewe unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Chunga kondoo zangu.”
यीशुऐ फिरी दूजी बरी उसयो पुछया, “हे यूहन्ना दे पुत्र शमौन, क्या तू मिंजो ने प्यार रखदा है?” उनी उसयो बोलया, “हाँ, प्रभु तू तां जाणदा हे की मैं तिजो ने प्यार करदा है?” उनी उसयो बोलया, “मेरियां भेडां दा पुआल बण।”
17 Kwa mara ya tatu Yesu akamuuliza Petro, “Simoni mwana wa Yohana, unanipenda?” Petro akahuzunika sana kwa kuwa Yesu alimuuliza mara ya tatu, “Unanipenda?” Akamjibu, “Bwana, wewe unajua yote, unajua ya kuwa ninakupenda.” Yesu akamwambia, “Lisha kondoo wangu.
यीशुऐ तीजी बरी उसयो पुछया, “यूहन्ना दे पुत्र शमौन, क्या तू मिंजो ने प्यार करदा है?” पतरस उदास होई गिया, की उनी उसयो तीजी बरी ऐसा बोलया, “क्या तू मिंजो ने प्यार करदा है।” कने उनी बोलया, “प्रभु जी, तू तां सब कुछ जाणदा है की मैं तिजो ने प्यार करदा है।” यीशुऐ उसला बोलया, “मेरियां भेडां जो चुगा।”
18 Amin, amin nakuambia, ulipokuwa kijana ulivaa na kwenda unakotaka, lakini utakapokuwa mzee utanyoosha mikono yako na mtu mwingine atakuvika na kukupeleka usipotaka kwenda.”
“मैं तुसां ने सच्च-सच्च बोलदा है, जालू तू जवान था, तां अपणे लक्के जो बन्नी करी जिथू चांदा था, ओथु गुमदा था; पर जालू तू बुडा होइ जाणा, तां तू अपणे हथां जो फेलांगा, कने कोई तिजो बन्नी लेंगा कने तिजो ओथु लेई जाणा जिथू तू जाणा नी चांदा।”
19 Yesu alisema haya ili kuashiria ni kifo cha aina gani Petro atakachomtukuza nacho Mungu. Kisha Yesu akamwambia Petro, “Nifuate!”
यीशुऐ ऐसा ऐ दसणे तांई बोलया की पतरसे कियां मरणा कने परमेश्वरे दी महिमा करणी है; ऐ बोली करी, उसयो बोलया, “मेरा चेला बणी रे।”
20 Petro akageuka, akamwona yule mwanafunzi aliyependwa na Yesu akiwafuata. (Huyu ndiye yule mwanafunzi aliyeegama kifuani mwa Yesu walipokula naye chakula cha mwisho na kuuliza, “Bwana, ni nani atakayekusaliti?”)
पतरसे मुड़ी करी उस चेले जो पिच्छे ओंदे दिखया जिसने यीशु प्यार रखदा था। ऐ सै ही है जिनी फसह दी रोटी खाणे बेले यीशुऐ बखे बेईकरी पुछया था, “प्रभु जी, तिजो पकड़ाणे बाला कुण है?”
21 Petro alipomwona huyo mwanafunzi, akamuuliza Yesu, “Bwana na huyu je?”
उसयो दिखीकरी पतरसे यीशुऐ जो बोलया, “प्रभु जी, इदे सोगी क्या होणा है?”
22 Yesu akamjibu, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini? Wewe inakupasa unifuate!”
यीशुऐ उसयो बोलया, “अगर मैं चां की सै मेरे ओंणे दीकर जिन्दा रे, तां तिजो क्या? तू मेरा चेला बणी रे।”
23 Kwa sababu ya maneno haya ya Yesu, uvumi ukaenea miongoni mwa ndugu kwamba huyu mwanafunzi hangekufa. Lakini Yesu hakusema kuwa hangekufa. Yeye alisema tu kwamba, “Ikiwa nataka aishi mpaka nitakaporudi, inakuhusu nini?”
तांई तां भाईयां च ऐ गल्ल फेली गेई की उनी दुज्जे चेले नी मरणा है; तमी यीशुऐ उसयो ऐ नी बोलया, की इनी नी मरणा है, पर ऐ की “अगर मैं चां की ऐ मेरे ओणे दीकर जिन्दा रे, तां तिजो इसला क्या?”
24 Huyu ndiye yule mwanafunzi anayeshuhudia mambo haya na ndiye ambaye ameandika habari hizi. Nasi tunajua ya kuwa ushuhuda wake ni kweli.
जिनी माणुऐ ऐ सब कुछ दिखया, उनी ऐ गबाई दिती है, ताकि तुसां भी यीशु पर भरोसा करी सकन। कने उदी गबाई सच्ची है। कने असां जाणदे न की सै सच्चाईया ने बोलदा है।
25 Lakini kuna mambo mengine mengi ambayo Yesu alifanya. Kama yote yangeliandikwa, nadhani hata ulimwengu wote usingekuwa na nafasi ya kutosha kuweka vitabu vyote ambavyo vingeandikwa. Amen.
यीशुऐ होर भी मते कम्म किते, अगर उना सारे कम्मा जो लिखया जांदा, तां मिंजो लगदा की सारे संसार च इतणी भी जगा नी होणी थी की उना सारियां कताबां जो रखी सके।