< Yohana 20 >
1 Alfajiri na mapema siku ya kwanza ya juma, kulipokuwa kungali giza bado, Maria Magdalene alikwenda kaburini na kukuta lile jiwe limeondolewa penye ingilio.
The first [day] of the week cometh Mary Magdalene early, when it was yet dark, to the sepulcher, and seeth the stone taken away from the sepulcher.
2 Hivyo akaja akikimbia kwa Simoni Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, na kusema, “Wamemwondoa Bwana kaburini, na hatujui walikomweka!”
Then she runneth, and cometh to Simon Peter, and to the other disciple whom Jesus loved, and saith to them, They have taken away the Lord out of the sepulcher, and we know not where they have laid him.
3 Petro na yule mwanafunzi mwingine wakaondoka mara kuelekea kaburini.
Peter therefore went forth, and that other disciple, and came to the sepulcher.
4 Wote wawili walikuwa wanakimbia, lakini yule mwanafunzi mwingine akakimbia mbio zaidi kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.
So they ran both together: and the other disciple outran Peter, and came first to the sepulcher.
5 Alipofika, akainama na kuchungulia mle kaburini, akaona vile vitambaa vya kitani mle ndani, lakini hakuingia.
And he stooping down, saw the linen cloths lying; yet he went not in.
6 Ndipo Simoni Petro akaja, akimfuata nyuma akaenda moja kwa moja hadi ndani ya kaburi. Naye akaona vile vitambaa vya ile sanda vikiwa pale chini
Then cometh Simon Peter following him, and went into the sepulcher, and seeth the linen cloths lying;
7 na kile kitambaa kilichokuwa kichwani mwa Yesu. Kitambaa hicho kilikuwa kimekunjwa mahali pa peke yake, mbali na vile vitambaa vya kitani vya ile sanda.
And the napkin that was about his head, not lying with the linen cloths, but wrapped together in a place by itself.
8 Kisha yule mwanafunzi aliyetangulia kufika kaburini naye akaingia ndani, akaona, akaamini,
Then went in also that other disciple who came first to the sepulcher, and he saw, and believed.
9 (kwa kuwa mpaka wakati huo walikuwa bado hawajaelewa kutoka Maandiko kwamba ilikuwa lazima Yesu afufuke kutoka kwa wafu).
For as yet they knew not the scripture, that he must rise again from the dead.
10 Kisha hao wanafunzi wakaondoka wakarudi nyumbani kwao.
Then the disciples went away again to their own home.
11 Lakini Maria Magdalene akasimama nje ya kaburi akilia. Alipokuwa akilia, akainama, kuchungulia mle kaburini,
But Mary stood without at the sepulcher weeping: and as she wept she stooped down [to look] into the sepulcher,
12 naye akaona malaika wawili wamevaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa, mmoja upande wa kichwani na mwingine upande wa miguuni.
And seeth two angels in white, sitting, the one at the head, and the other at the feet, where the body of Jesus had lain.
13 Wakamuuliza Maria, “Mwanamke, mbona unalia?” Akawaambia, “Nalia kwa kuwa wamemchukua Bwana wangu na sijui walikomweka.”
And they say to her, Woman, why weepest thou? she saith to them, Because they have taken away my Lord, and I know not where they have laid him.
14 Baada ya kusema hayo, akageuka, akamwona Yesu amesimama, lakini hakumtambua.
And when she had thus said, she turned herself about, and saw Jesus standing, and knew not that it was Jesus.
15 Yesu akamwambia, “Mwanamke, mbona unalia? Unamtafuta nani?” Maria akidhani ya kuwa aliyekuwa anaongea naye ni mtunza bustani, kwa hiyo akamwambia, “Bwana, kama ni wewe umemchukua, tafadhali nionyeshe ulikomweka, nami nitamchukua.”
Jesus saith to her, Woman, why weepest thou? whom seekest thou? She, supposing him to be the gardener, saith to him, Sir, if thou hast borne him hence, tell me where thou hast laid him, and I will take him away.
16 Yesu akamwita, “Maria!” Ndipo Maria akamgeukia Yesu na kusema naye kwa Kiebrania, “Rabboni!” (maana yake Mwalimu).
Jesus saith to her, Mary. She turned herself, and saith to him, Rabboni, which is to say, Master.
17 Yesu akamwambia, “Usinishike, kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu ukawaambie, ‘Ninapaa kwenda kwa Baba yangu ambaye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu ambaye ni Mungu wenu.’”
Jesus saith to her, Touch me not: for I have not yet ascended to my Father: but go to my brethren, and say to them, I ascend to my Father and your Father, and [to] my God and your God.
18 Kwa hiyo Maria Magdalene akaenda kuwatangazia wanafunzi wa Yesu, akisema, “Nimemwona Bwana!” Naye akawaambia kwamba Yesu alikuwa amemweleza mambo hayo yote.
Mary Magdalene came and told the disciples that she had seen the Lord, and [that] he had spoken these things to her.
19 Ikawa jioni ya ile siku ya kwanza ya juma, wanafunzi wake walikuwa pamoja, milango ikiwa imefungwa kwa kuwaogopa Wayahudi. Naye Yesu aliwatokea, akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”
Then the same day at evening, being the first [day] of the week, when the doors were shut where the disciples were assembled for fear of the Jews, Jesus came and stood in the midst, and saith to them, Peace [be] to you.
20 Baada ya kusema haya, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Wanafunzi wake wakafurahi sana walipomwona Bwana.
And when he had so said, he showed to them [his] hands and his side. Then were the disciples glad when they saw the Lord.
21 Yesu akawaambia tena, “Amani iwe nanyi! Kama vile Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawatuma ninyi.”
Then said Jesus to them again, Peace [be] to you: as [my] Father hath sent me, even so I send you.
22 Naye alipokwisha kusema haya, akawavuvia, akawaambia, “Pokeeni Roho Mtakatifu.
And when he had said this, he breathed on [them], and saith to them, Receive ye the Holy Spirit.
23 Mkimwondolea mtu yeyote dhambi zake, zitaondolewa, na yeyote msiyemwondolea dhambi zake, hazitaondolewa.”
Whose soever sins ye remit, they are remitted to them; [and] whose soever [sins] ye retain, they are retained.
24 Lakini Tomaso, aliyeitwa Didimasi, yaani Pacha, mmoja wa wale kumi na wawili, hakuwa pamoja nao Yesu alipokuja.
But Thomas, one of the twelve, called Didymus, was not with them when Jesus came.
25 Hivyo wale wanafunzi wengine wakamwambia, “Tumemwona Bwana.” Lakini yeye akawaambia, “Nisipoona zile alama za misumari mikononi mwake, na kuweka kidole changu kwenye hizo alama za misumari na mkono wangu ubavuni mwake, sitaamini.”
The other disciples therefore said to him, We have seen the Lord. But he said to them, Except I shall see in his hands the print of the nails, and put my finger into the print of the nails, and thrust my hand into his side, I will not believe.
26 Baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwa tena pamoja ndani ya nyumba, naye Tomaso alikuwa pamoja nao. Ndipo Yesu akaja milango ikiwa imefungwa na kusimama katikati yao akasema, “Amani iwe nanyi.”
And after eight days again his disciples were within, and Thomas with them: [then] came Jesus, the doors being shut, and stood in the midst, and said, Peace [be] to you.
27 Kisha akamwambia Tomaso, “Weka kidole chako hapa na uone mikono yangu, nyoosha mkono wako uguse ubavuni mwangu. Usiwe na shaka, bali uamini tu.”
Then saith he to Thomas, Reach hither thy finger, and behold my hands; and reach hither thy hand, and thrust [it] into my side; and be not faithless, but believing.
28 Tomaso akamwambia, “Bwana wangu na Mungu wangu!”
And Thomas answered and said to him, My Lord and my God.
29 Yesu akamwambia, “Umeamini kwa kuwa umeniona? Wamebarikiwa wale ambao hawajaona lakini wameamini.”
Jesus saith to him, Thomas, because thou hast seen me, thou hast believed: blessed [are] they that have not seen, and [yet] have believed.
30 Yesu alifanya miujiza mingine mingi mbele za wanafunzi wake, ambayo haikuandikwa katika kitabu hiki.
And many other signs truly did Jesus in the presence of his disciples, which are not written in this book.
31 Lakini haya yameandikwa ili mweze kuamini ya kuwa Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mpate uzima katika jina lake.
But these are written, that ye may believe that Jesus is the Christ, the Son of God, and that believing ye may have life through his name.