< Yohana 20 >
1 Alfajiri na mapema siku ya kwanza ya juma, kulipokuwa kungali giza bado, Maria Magdalene alikwenda kaburini na kukuta lile jiwe limeondolewa penye ingilio.
But, on the first day of the week, Mary the Magdalene, cometh early, while it is yet, dark, unto the tomb, —and beholdeth the stone, already taken away out of the tomb.
2 Hivyo akaja akikimbia kwa Simoni Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, na kusema, “Wamemwondoa Bwana kaburini, na hatujui walikomweka!”
She runneth, therefore, and cometh unto Simon Peter, and unto the other disciple whom Jesus dearly loved, and saith unto them—They have taken away the Lord out of the tomb, and we know not where they have laid him.
3 Petro na yule mwanafunzi mwingine wakaondoka mara kuelekea kaburini.
Peter, therefore, went out, and the other disciple, —and they were going unto the tomb;
4 Wote wawili walikuwa wanakimbia, lakini yule mwanafunzi mwingine akakimbia mbio zaidi kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.
and the two were running together, and, the other disciple, outran Peter, and came first unto the tomb;
5 Alipofika, akainama na kuchungulia mle kaburini, akaona vile vitambaa vya kitani mle ndani, lakini hakuingia.
and, stooping aside, beholdeth, lying, the linen-bandages, nevertheless, he entered not.
6 Ndipo Simoni Petro akaja, akimfuata nyuma akaenda moja kwa moja hadi ndani ya kaburi. Naye akaona vile vitambaa vya ile sanda vikiwa pale chini
So Simon Peter also cometh, following him, and entered into the tomb, and vieweth the linen-bandages lying, —
7 na kile kitambaa kilichokuwa kichwani mwa Yesu. Kitambaa hicho kilikuwa kimekunjwa mahali pa peke yake, mbali na vile vitambaa vya kitani vya ile sanda.
and the napkin, which was upon his head, not, with the linen-bandages, lying, but apart, folded up into one place.
8 Kisha yule mwanafunzi aliyetangulia kufika kaburini naye akaingia ndani, akaona, akaamini,
Then, entered, therefore, the other disciple also, who had come first unto the tomb, and he saw and believed.
9 (kwa kuwa mpaka wakati huo walikuwa bado hawajaelewa kutoka Maandiko kwamba ilikuwa lazima Yesu afufuke kutoka kwa wafu).
For, not yet, knew they the Scripture, that he must needs, from among the dead, arise.
10 Kisha hao wanafunzi wakaondoka wakarudi nyumbani kwao.
The disciples, therefore, departed again, by themselves.
11 Lakini Maria Magdalene akasimama nje ya kaburi akilia. Alipokuwa akilia, akainama, kuchungulia mle kaburini,
Howbeit, Mary, remained standing against the tomb, outside, weeping. So then, as she wept, she stooped aside into the tomb,
12 naye akaona malaika wawili wamevaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa, mmoja upande wa kichwani na mwingine upande wa miguuni.
and beholdeth two messengers, in white garments, sitting, one at the head, and the other at the feet, where had been lying the body of Jesus.
13 Wakamuuliza Maria, “Mwanamke, mbona unalia?” Akawaambia, “Nalia kwa kuwa wamemchukua Bwana wangu na sijui walikomweka.”
And, they, say unto her—Woman! why weepest thou? She saith unto them—They have taken away my Lord, and I know not where they have laid him.
14 Baada ya kusema hayo, akageuka, akamwona Yesu amesimama, lakini hakumtambua.
These things saying, she turned round, and seeth Jesus standing, and knew not that it was, Jesus.
15 Yesu akamwambia, “Mwanamke, mbona unalia? Unamtafuta nani?” Maria akidhani ya kuwa aliyekuwa anaongea naye ni mtunza bustani, kwa hiyo akamwambia, “Bwana, kama ni wewe umemchukua, tafadhali nionyeshe ulikomweka, nami nitamchukua.”
Jesus saith unto her—Woman! why weepest thou? Whom seekest thou? She, supposing he was, the gardener, saith unto him—Sir! If, thou, hast borne him hence, tell me where thou hast laid him; and, I, will take him away.
16 Yesu akamwita, “Maria!” Ndipo Maria akamgeukia Yesu na kusema naye kwa Kiebrania, “Rabboni!” (maana yake Mwalimu).
Jesus saith unto her—Mary! She, turning saith unto him, in Hebrew—Rabboni! which meaneth, Teacher.
17 Yesu akamwambia, “Usinishike, kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu ukawaambie, ‘Ninapaa kwenda kwa Baba yangu ambaye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu ambaye ni Mungu wenu.’”
Jesus saith unto her—Be not detaining me, for, not yet, have I ascended unto the Father; but be going unto my disciples, and say unto them—I am ascending unto my Father and your Father, and my God and your God.
18 Kwa hiyo Maria Magdalene akaenda kuwatangazia wanafunzi wa Yesu, akisema, “Nimemwona Bwana!” Naye akawaambia kwamba Yesu alikuwa amemweleza mambo hayo yote.
Mary the Magdalene cometh, bringing tidings unto the disciples—I have seen the Lord! and that these things he had said unto her.
19 Ikawa jioni ya ile siku ya kwanza ya juma, wanafunzi wake walikuwa pamoja, milango ikiwa imefungwa kwa kuwaogopa Wayahudi. Naye Yesu aliwatokea, akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”
It being late, therefore, on that day, the first of the week, —and, the doors, having been made fast where the disciples were, for fear of the Jews, Jesus came, and stood in the midst, and saith unto them—Peace be unto you!
20 Baada ya kusema haya, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Wanafunzi wake wakafurahi sana walipomwona Bwana.
and, this, saying he pointed out both his hands and his side unto them. The disciples, therefore, rejoiced, seeing the Lord.
21 Yesu akawaambia tena, “Amani iwe nanyi! Kama vile Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawatuma ninyi.”
Jesus, therefore, said unto them, again, —Peace be unto you! Just as, my Father, sent me forth, I, also, send you.
22 Naye alipokwisha kusema haya, akawavuvia, akawaambia, “Pokeeni Roho Mtakatifu.
And, this, saying, he breathed strongly, and saith unto them—Receive ye Holy Spirit: —
23 Mkimwondolea mtu yeyote dhambi zake, zitaondolewa, na yeyote msiyemwondolea dhambi zake, hazitaondolewa.”
Whosesoever sins ye shall remit, they are remitted unto them, whosesoever ye shall retain, they are retained.
24 Lakini Tomaso, aliyeitwa Didimasi, yaani Pacha, mmoja wa wale kumi na wawili, hakuwa pamoja nao Yesu alipokuja.
But, Thomas, one of the twelve, the one called Didymus, was not with them when Jesus came.
25 Hivyo wale wanafunzi wengine wakamwambia, “Tumemwona Bwana.” Lakini yeye akawaambia, “Nisipoona zile alama za misumari mikononi mwake, na kuweka kidole changu kwenye hizo alama za misumari na mkono wangu ubavuni mwake, sitaamini.”
The other disciples, therefore, were saying unto him—We have seen the Lord! But, he, said unto them—Except I see, in his hands, the print of the nails, and press my finger into the print of the nails, and press my hand into his side, in nowise will I believe.
26 Baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwa tena pamoja ndani ya nyumba, naye Tomaso alikuwa pamoja nao. Ndipo Yesu akaja milango ikiwa imefungwa na kusimama katikati yao akasema, “Amani iwe nanyi.”
And, eight days after, his disciples again were within, and Thomas with them. Jesus cometh—the doors having been made fast—and stood in the midst, and said—Peace be unto you!
27 Kisha akamwambia Tomaso, “Weka kidole chako hapa na uone mikono yangu, nyoosha mkono wako uguse ubavuni mwangu. Usiwe na shaka, bali uamini tu.”
Then, saith he unto Thomas—Reach thy finger hither, and see my hands, and reach thy hand, and press into my side, —and become not disbelieving, but believing.
28 Tomaso akamwambia, “Bwana wangu na Mungu wangu!”
Thomas answered, and said unto him—My Lord, and my God!
29 Yesu akamwambia, “Umeamini kwa kuwa umeniona? Wamebarikiwa wale ambao hawajaona lakini wameamini.”
Jesus saith unto him—Because thou hast seen me, hast thou believed? Happy, they who have not seen, and yet have believed!
30 Yesu alifanya miujiza mingine mingi mbele za wanafunzi wake, ambayo haikuandikwa katika kitabu hiki.
Many other signs, doubtless, did Jesus, in presence of the disciples, which are not written in this book;
31 Lakini haya yameandikwa ili mweze kuamini ya kuwa Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mpate uzima katika jina lake.
but, these, are written, that ye may believe that, Jesus, is, the Christ, the Son of God; and that, believing, ye may have life in his name.