< Yohana 20 >

1 Alfajiri na mapema siku ya kwanza ya juma, kulipokuwa kungali giza bado, Maria Magdalene alikwenda kaburini na kukuta lile jiwe limeondolewa penye ingilio.
Now on the first day of the week Mary Magdalene comes to the tomb early, while it is still dark, and sees that the stone has been removed from the tomb.
2 Hivyo akaja akikimbia kwa Simoni Petro pamoja na yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, na kusema, “Wamemwondoa Bwana kaburini, na hatujui walikomweka!”
So she runs and comes to Simon Peter, and to the other disciple, whom Jesus loved, and says to them, “They have taken the Lord out of the tomb, and we don't know where they put Him!”
3 Petro na yule mwanafunzi mwingine wakaondoka mara kuelekea kaburini.
So Peter and the other disciple took off, heading for the tomb.
4 Wote wawili walikuwa wanakimbia, lakini yule mwanafunzi mwingine akakimbia mbio zaidi kuliko Petro, akatangulia kufika kaburini.
Well the two started running together, and the other disciple outran Peter and got to the tomb first.
5 Alipofika, akainama na kuchungulia mle kaburini, akaona vile vitambaa vya kitani mle ndani, lakini hakuingia.
And stooping to look he sees the linen strips lying there; however he did not go in.
6 Ndipo Simoni Petro akaja, akimfuata nyuma akaenda moja kwa moja hadi ndani ya kaburi. Naye akaona vile vitambaa vya ile sanda vikiwa pale chini
Then following him comes Simon Peter and went into the tomb; and he sees the linen strips lying there,
7 na kile kitambaa kilichokuwa kichwani mwa Yesu. Kitambaa hicho kilikuwa kimekunjwa mahali pa peke yake, mbali na vile vitambaa vya kitani vya ile sanda.
and the facecloth that had been on His head not lying with the linen strips, but folded up in a separate place.
8 Kisha yule mwanafunzi aliyetangulia kufika kaburini naye akaingia ndani, akaona, akaamini,
So then the other disciple went in too, the one who got to the tomb first; and he saw and believed.
9 (kwa kuwa mpaka wakati huo walikuwa bado hawajaelewa kutoka Maandiko kwamba ilikuwa lazima Yesu afufuke kutoka kwa wafu).
(For they did not yet know the Scripture, that He had to rise from among the dead.)
10 Kisha hao wanafunzi wakaondoka wakarudi nyumbani kwao.
Then the disciples went back home.
11 Lakini Maria Magdalene akasimama nje ya kaburi akilia. Alipokuwa akilia, akainama, kuchungulia mle kaburini,
Well Mary stood outside at the tomb, crying. Then, while she was crying, she stooped to look into the tomb.
12 naye akaona malaika wawili wamevaa mavazi meupe, wameketi pale mwili wa Yesu ulipokuwa umelazwa, mmoja upande wa kichwani na mwingine upande wa miguuni.
And she sees two angels in white, sitting one at the head and one at the feet of where the body of Jesus had lain.
13 Wakamuuliza Maria, “Mwanamke, mbona unalia?” Akawaambia, “Nalia kwa kuwa wamemchukua Bwana wangu na sijui walikomweka.”
And they say to her, “Woman, why are you crying?” She says to them, “Because they removed my Lord, and I don't know where they put Him.”
14 Baada ya kusema hayo, akageuka, akamwona Yesu amesimama, lakini hakumtambua.
And upon saying this she turned around and saw Jesus standing there, yet did not know that it was Jesus.
15 Yesu akamwambia, “Mwanamke, mbona unalia? Unamtafuta nani?” Maria akidhani ya kuwa aliyekuwa anaongea naye ni mtunza bustani, kwa hiyo akamwambia, “Bwana, kama ni wewe umemchukua, tafadhali nionyeshe ulikomweka, nami nitamchukua.”
Jesus says to her: “Woman, why are you crying? Whom are you seeking?” She, supposing that He was the gardener, says to Him, “Sir, if you carried Him away, tell me where you put Him, and I will remove Him.”
16 Yesu akamwita, “Maria!” Ndipo Maria akamgeukia Yesu na kusema naye kwa Kiebrania, “Rabboni!” (maana yake Mwalimu).
Jesus says to her, “Mary!” Turning she says to Him, “Raboni!” (which means ‘Teacher’).
17 Yesu akamwambia, “Usinishike, kwa maana sijapaa kwenda kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu ukawaambie, ‘Ninapaa kwenda kwa Baba yangu ambaye ni Baba yenu, kwa Mungu wangu ambaye ni Mungu wenu.’”
Jesus says to her: “Stop clinging to me, for I have not yet ascended to my Father; but go to my brothers and say to them, ‘I am ascending to my Father and your Father—my God and your God.’”
18 Kwa hiyo Maria Magdalene akaenda kuwatangazia wanafunzi wa Yesu, akisema, “Nimemwona Bwana!” Naye akawaambia kwamba Yesu alikuwa amemweleza mambo hayo yote.
Mary Magdalene goes to the disciples, reporting that she had seen the Lord and He had said these things to her.
19 Ikawa jioni ya ile siku ya kwanza ya juma, wanafunzi wake walikuwa pamoja, milango ikiwa imefungwa kwa kuwaogopa Wayahudi. Naye Yesu aliwatokea, akasimama katikati yao, akasema, “Amani iwe nanyi!”
Then at evening on that first day of the week, the doors being locked where the disciples were assembled, for fear of the Jews, Jesus came and stood in the middle, and He says to them, “Peace to you!”
20 Baada ya kusema haya, akawaonyesha mikono yake na ubavu wake. Wanafunzi wake wakafurahi sana walipomwona Bwana.
And upon saying this He showed them His hands and His side. Well, the disciples were overjoyed when they saw the Lord!
21 Yesu akawaambia tena, “Amani iwe nanyi! Kama vile Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawatuma ninyi.”
So Jesus said to them again: “Peace to you! Just as the Father sent me, I also send you.”
22 Naye alipokwisha kusema haya, akawavuvia, akawaambia, “Pokeeni Roho Mtakatifu.
Upon saying this He breathed on them and said: “Receive Holy Spirit!
23 Mkimwondolea mtu yeyote dhambi zake, zitaondolewa, na yeyote msiyemwondolea dhambi zake, hazitaondolewa.”
To whomever you forgive the sins, they are forgiven to them; to whomever you retain, they have been retained.”
24 Lakini Tomaso, aliyeitwa Didimasi, yaani Pacha, mmoja wa wale kumi na wawili, hakuwa pamoja nao Yesu alipokuja.
Now one of the twelve, Thomas (called Twin), was not with them when Jesus came.
25 Hivyo wale wanafunzi wengine wakamwambia, “Tumemwona Bwana.” Lakini yeye akawaambia, “Nisipoona zile alama za misumari mikononi mwake, na kuweka kidole changu kwenye hizo alama za misumari na mkono wangu ubavuni mwake, sitaamini.”
So the other disciples said to him, “We have seen the Lord!” But he said to them, “If I do not see the nail prints in His hands and put my finger into the nail prints, and put my hand into His side, I will not believe!”
26 Baada ya siku nane, wanafunzi wake walikuwa tena pamoja ndani ya nyumba, naye Tomaso alikuwa pamoja nao. Ndipo Yesu akaja milango ikiwa imefungwa na kusimama katikati yao akasema, “Amani iwe nanyi.”
Well after eight days His disciples were inside again, and Thomas with them. The doors were locked [again]; Jesus came and stood in the middle, and said, “Peace to you!”
27 Kisha akamwambia Tomaso, “Weka kidole chako hapa na uone mikono yangu, nyoosha mkono wako uguse ubavuni mwangu. Usiwe na shaka, bali uamini tu.”
Then He says to Thomas: “Bring your finger here and perceive my hands; bring your hand and put it into my side; do not be unbelieving but believing!”
28 Tomaso akamwambia, “Bwana wangu na Mungu wangu!”
Thomas answered and said to Him, “My Lord and my God!”
29 Yesu akamwambia, “Umeamini kwa kuwa umeniona? Wamebarikiwa wale ambao hawajaona lakini wameamini.”
Jesus says to him: “Because you have observed me, you have believed. Blessed are those who believe without seeing!”
30 Yesu alifanya miujiza mingine mingi mbele za wanafunzi wake, ambayo haikuandikwa katika kitabu hiki.
Now then, Jesus actually performed many other miraculous signs in the presence of His disciples, that are not written in this book;
31 Lakini haya yameandikwa ili mweze kuamini ya kuwa Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mpate uzima katika jina lake.
but these have been written so that you may believe that Jesus is the Christ, the Son of God, and that believing you may have Life through His Name.

< Yohana 20 >