< Yohana 2 >
1 Siku ya tatu kulikuwa na arusi katika mji wa Kana ya Galilaya, naye mama yake Yesu alikuwepo pale.
And the thirde day, was there a mariage in Cana a towne of Galile, and the mother of Iesus was there.
2 Yesu pamoja na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa arusini pia.
And Iesus was called also, and his disciples vnto the mariage.
3 Divai ilipokwisha, mama yake Yesu akamwambia, “Wameishiwa na divai.”
Nowe when the wine failed, the mother of Iesus saide vnto him, They haue no wine.
4 Yesu akamwambia, “Mwanamke, nina nini nawe? Saa yangu haijawadia.”
Iesus saide vnto her, Woman, what haue I to doe with thee? mine houre is not yet come.
5 Mama yake akawaambia wale watumishi, “Lolote atakalowaambia, fanyeni.”
His mother saide vnto the seruants, Whatsoeuer he sayeth vnto you, doe it.
6 Basi ilikuwepo mitungi sita ya kuhifadhia maji iliyotengenezwa kwa mawe kwa ajili ya kujitakasa kwa desturi ya Kiyahudi; kila mtungi ungeweza kuchukua vipipa viwili au vitatu.
And there were set there, sixe waterpots of stone, after the maner of the purifying of the Iewes, conteining two or three firkins a piece.
7 Yesu akawaambia wale watumishi, “Ijazeni hiyo mitungi maji.” Nao wakaijaza ile mitungi mpaka juu.
And Iesus sayde vnto them, Fill the waterpots with water. Then they filled them vp to the brim.
8 Kisha akawaambia, “Sasa choteni hayo maji kidogo, mpelekeeni mkuu wa meza.” Hivyo wakachota, wakampelekea.
Then he sayde vnto them, Draw out nowe and beare vnto the gouernour of the feast. So they bare it.
9 Yule mkuu wa meza akayaonja yale maji ambayo yalikuwa yamebadilika kuwa divai. Hakujua divai hiyo ilikotoka ingawa wale watumishi waliochota yale maji wao walifahamu. Basi akamwita bwana arusi kando
Nowe when the gouernour of the feast had tasted the water that was made wine, (for he knewe not whence it was: but the seruants, which drewe the water, knewe) the gouernour of ye feast called the bridegrome,
10 akamwambia, “Watu wote hutoa kwanza divai nzuri, kisha huleta ile divai hafifu wageni wakisha kunywa vya kutosha, lakini wewe umeiweka ile nzuri kupita zote mpaka sasa.”
And saide vnto him, All men at the beginning set foorth good wine, and when men haue well drunke, then that which is worse: but thou hast kept backe the good wine vntill nowe.
11 Huu, ndio uliokuwa muujiza wa kwanza Yesu aliofanya Kana ya Galilaya. Hivyo Yesu alidhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini.
This beginning of miracles did Iesus in Cana a towne of Galile, and shewed forth his glorie: and his disciples beleeued on him.
12 Baada ya hayo, Yesu pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, walishuka mpaka Kapernaumu, wakakaa huko siku chache.
After that, he went downe into Capernaum, he and his mother, and his brethren, and his disciples: but they continued not many daies there.
13 Ilipokaribia wakati wa Pasaka ya Wayahudi, Yesu alipanda kwenda Yerusalemu.
For the Iewes Passeouer was at hande. Therefore Iesus went vp to Hierusalem.
14 Huko Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ngʼombe, kondoo na njiwa, nao wengine walikuwa wameketi mezani wakibadili fedha.
And he found in the Temple those that sold oxen, and sheepe, and doues, and changers of money, sitting there.
15 Akatengeneza mjeledi kutokana na kamba, akawafukuza wote kutoka kwenye eneo la Hekalu, pamoja na kondoo na ngʼombe. Akazipindua meza za wale wabadili fedha na kuzimwaga fedha zao.
Then hee made a scourge of small cordes, and draue them all out of the Temple with the sheepe and oxen, and powred out the changers money, and ouerthrewe the tables,
16 Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, “Waondoeni hapa! Mnathubutuje kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa biashara?”
And said vnto them that solde doues, Take these things hence: make not my fathers house, an house of marchandise.
17 Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa imeandikwa: “Wivu wa nyumba yako utanila.”
And his disciples remembred, that it was written, The zeale of thine house hath eaten me vp.
18 Ndipo Wayahudi wakamuuliza, “Unaweza kutuonyesha ishara gani ili kuthibitisha mamlaka uliyo nayo ya kufanya mambo haya?”
Then answered the Iewes, and saide vnto him, What signe shewest thou vnto vs, that thou doest these things?
19 Yesu akawajibu, “Libomoeni hili Hekalu, nami nitalijenga tena kwa siku tatu!”
Iesus answered, and said vnto them, Destroy this Temple, and in three daies I will raise it vp againe.
20 Wale Wayahudi wakamjibu, “Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita, nawe wasema utalijenga kwa siku tatu?”
Then said the Iewes, Fourtie and sixe yeeres was this Temple a building, and wilt thou reare it vp in three daies?
21 Lakini yeye Hekalu alilozungumzia ni mwili wake.
But he spake of the temple of his bodie.
22 Baada ya kufufuliwa kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka yale aliyokuwa amesema. Ndipo wakayaamini Maandiko na yale maneno Yesu aliyokuwa amesema.
Assoone therefore as he was risen from the dead, his disciples remembred that hee thus sayde vnto them: and they beleeued the Scripture, and the worde which Iesus had saide.
23 Ikawa Yesu alipokuwa Yerusalemu kwenye Sikukuu ya Pasaka, watu wengi waliona ishara na miujiza aliyokuwa akifanya, wakaamini katika jina lake.
Nowe when hee was at Hierusalem at the Passeouer in the feast, many beleeued in his Name, when they sawe his miracles which he did.
24 Lakini Yesu hakujiaminisha kwao kwa sababu aliwajua wanadamu wote.
But Iesus did not commit him selfe vnto them, because he knewe them all,
25 Hakuhitaji ushuhuda wa mtu yeyote kuhusu mtu, kwa kuwa alijua yote yaliyokuwa moyoni mwa mtu.
And had no neede that any should testifie of man: for he knewe what was in man.