< Yohana 2 >

1 Siku ya tatu kulikuwa na arusi katika mji wa Kana ya Galilaya, naye mama yake Yesu alikuwepo pale.
And the third day, there was a marriage in Cana of Galilee: and the mother of Jesus was there.
2 Yesu pamoja na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa arusini pia.
And Jesus also was invited, and his disciples, to the marriage.
3 Divai ilipokwisha, mama yake Yesu akamwambia, “Wameishiwa na divai.”
And the wine failing, the mother of Jesus saith to him: They have no wine.
4 Yesu akamwambia, “Mwanamke, nina nini nawe? Saa yangu haijawadia.”
And Jesus saith to her: Woman, what is that to me and to thee? my hour is not yet come.
5 Mama yake akawaambia wale watumishi, “Lolote atakalowaambia, fanyeni.”
His mother saith to the waiters: Whatsoever he shall say to you, do ye.
6 Basi ilikuwepo mitungi sita ya kuhifadhia maji iliyotengenezwa kwa mawe kwa ajili ya kujitakasa kwa desturi ya Kiyahudi; kila mtungi ungeweza kuchukua vipipa viwili au vitatu.
Now there were set there six waterpots of stone, according to the manner of the purifying of the Jews, containing two or three measures apiece.
7 Yesu akawaambia wale watumishi, “Ijazeni hiyo mitungi maji.” Nao wakaijaza ile mitungi mpaka juu.
Jesus saith to them: Fill the waterpots with water. And they filled them up to the brim.
8 Kisha akawaambia, “Sasa choteni hayo maji kidogo, mpelekeeni mkuu wa meza.” Hivyo wakachota, wakampelekea.
And Jesus saith to them: Draw out now, and carry to the chief steward of the feast. And they carried it.
9 Yule mkuu wa meza akayaonja yale maji ambayo yalikuwa yamebadilika kuwa divai. Hakujua divai hiyo ilikotoka ingawa wale watumishi waliochota yale maji wao walifahamu. Basi akamwita bwana arusi kando
And when the chief steward had tasted the water made wine, and knew not whence it was, but the waiters knew who had drawn the water; the chief steward calleth the bridegroom,
10 akamwambia, “Watu wote hutoa kwanza divai nzuri, kisha huleta ile divai hafifu wageni wakisha kunywa vya kutosha, lakini wewe umeiweka ile nzuri kupita zote mpaka sasa.”
And saith to him: Every man at first setteth forth good wine, and when men have well drunk, then that which is worse. But thou hast kept the good wine until now.
11 Huu, ndio uliokuwa muujiza wa kwanza Yesu aliofanya Kana ya Galilaya. Hivyo Yesu alidhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini.
This beginning of miracles did Jesus in Cana of Galilee; and manifested his glory, and his disciples believed in him.
12 Baada ya hayo, Yesu pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, walishuka mpaka Kapernaumu, wakakaa huko siku chache.
After this he went down to Capharnaum, he and his mother, and his brethren, and his disciples: and they remained there not many days.
13 Ilipokaribia wakati wa Pasaka ya Wayahudi, Yesu alipanda kwenda Yerusalemu.
And the pasch of the Jews was at hand, and Jesus went up to Jerusalem.
14 Huko Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ngʼombe, kondoo na njiwa, nao wengine walikuwa wameketi mezani wakibadili fedha.
And he found in the temple them that sold oxen and sheep and doves, and the changers of money sitting.
15 Akatengeneza mjeledi kutokana na kamba, akawafukuza wote kutoka kwenye eneo la Hekalu, pamoja na kondoo na ngʼombe. Akazipindua meza za wale wabadili fedha na kuzimwaga fedha zao.
And when he had made, as it were, a scourge of little cords, he drove them all out of the temple, the sheep also and the oxen, and the money of the changers he poured out, and the tables he overthrew.
16 Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, “Waondoeni hapa! Mnathubutuje kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa biashara?”
And to them that sold doves he said: Take these things hence, and make not the house of my Father a house of traffic.
17 Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa imeandikwa: “Wivu wa nyumba yako utanila.”
And his disciples remembered, that it was written: The zeal of thy house hath eaten me up.
18 Ndipo Wayahudi wakamuuliza, “Unaweza kutuonyesha ishara gani ili kuthibitisha mamlaka uliyo nayo ya kufanya mambo haya?”
The Jews, therefore, answered, and said to him: What sign dost thou shew unto us, seeing thou dost these things?
19 Yesu akawajibu, “Libomoeni hili Hekalu, nami nitalijenga tena kwa siku tatu!”
Jesus answered, and said to them: Destroy this temple, and in three days I will raise it up.
20 Wale Wayahudi wakamjibu, “Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita, nawe wasema utalijenga kwa siku tatu?”
The Jews then said: Six and forty years was this temple in building; and wilt thou raise it up in three days?
21 Lakini yeye Hekalu alilozungumzia ni mwili wake.
But he spoke of the temple of his body.
22 Baada ya kufufuliwa kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka yale aliyokuwa amesema. Ndipo wakayaamini Maandiko na yale maneno Yesu aliyokuwa amesema.
When therefore he was risen again from the dead, his disciples remembered, that he had said this, and they believed the scripture, and the word that Jesus had said.
23 Ikawa Yesu alipokuwa Yerusalemu kwenye Sikukuu ya Pasaka, watu wengi waliona ishara na miujiza aliyokuwa akifanya, wakaamini katika jina lake.
Now when he was at Jerusalem, at the pasch, upon the festival day, many believed in his name, seeing his signs which he did.
24 Lakini Yesu hakujiaminisha kwao kwa sababu aliwajua wanadamu wote.
But Jesus did not trust himself unto them, for that he knew all men,
25 Hakuhitaji ushuhuda wa mtu yeyote kuhusu mtu, kwa kuwa alijua yote yaliyokuwa moyoni mwa mtu.
And because he needed not that any should give testimony of man: for he knew what was in man.

< Yohana 2 >