< Yohana 2 >

1 Siku ya tatu kulikuwa na arusi katika mji wa Kana ya Galilaya, naye mama yake Yesu alikuwepo pale.
The third day, there was a wedding in Cana of Galilee. Jesus’ mother was there.
2 Yesu pamoja na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa arusini pia.
Jesus also was invited, with his disciples, to the wedding.
3 Divai ilipokwisha, mama yake Yesu akamwambia, “Wameishiwa na divai.”
When the wine ran out, Jesus’ mother said to him, “They have no wine.”
4 Yesu akamwambia, “Mwanamke, nina nini nawe? Saa yangu haijawadia.”
Jesus said to her, “Woman, what does that have to do with you and me? My hour has not yet come.”
5 Mama yake akawaambia wale watumishi, “Lolote atakalowaambia, fanyeni.”
His mother said to the servants, “Whatever he says to you, do it.”
6 Basi ilikuwepo mitungi sita ya kuhifadhia maji iliyotengenezwa kwa mawe kwa ajili ya kujitakasa kwa desturi ya Kiyahudi; kila mtungi ungeweza kuchukua vipipa viwili au vitatu.
Now there were six water pots of stone set there after the Jews’ way of purifying, containing two or three metretes apiece.
7 Yesu akawaambia wale watumishi, “Ijazeni hiyo mitungi maji.” Nao wakaijaza ile mitungi mpaka juu.
Jesus said to them, “Fill the water pots with water.” So they filled them up to the brim.
8 Kisha akawaambia, “Sasa choteni hayo maji kidogo, mpelekeeni mkuu wa meza.” Hivyo wakachota, wakampelekea.
He said to them, “Now draw some out, and take it to the ruler of the feast.” So they took it.
9 Yule mkuu wa meza akayaonja yale maji ambayo yalikuwa yamebadilika kuwa divai. Hakujua divai hiyo ilikotoka ingawa wale watumishi waliochota yale maji wao walifahamu. Basi akamwita bwana arusi kando
When the ruler of the feast tasted the water now become wine, and did not know where it came from (but the servants who had drawn the water knew), the ruler of the feast called the bridegroom
10 akamwambia, “Watu wote hutoa kwanza divai nzuri, kisha huleta ile divai hafifu wageni wakisha kunywa vya kutosha, lakini wewe umeiweka ile nzuri kupita zote mpaka sasa.”
and said to him, “Everyone serves the good wine first, and when the guests have drunk freely, then that which is worse. You have kept the good wine until now!”
11 Huu, ndio uliokuwa muujiza wa kwanza Yesu aliofanya Kana ya Galilaya. Hivyo Yesu alidhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini.
This beginning of his signs Jesus did in Cana of Galilee, and revealed his glory; and his disciples believed in him.
12 Baada ya hayo, Yesu pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, walishuka mpaka Kapernaumu, wakakaa huko siku chache.
After this, he went down to Capernaum, he, and his mother, his brothers, and his disciples; and they stayed there a few days.
13 Ilipokaribia wakati wa Pasaka ya Wayahudi, Yesu alipanda kwenda Yerusalemu.
The Passover of the Jews was at hand, and Jesus went up to Jerusalem.
14 Huko Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ngʼombe, kondoo na njiwa, nao wengine walikuwa wameketi mezani wakibadili fedha.
He found in the temple those who sold oxen, sheep, and doves, and the changers of money sitting.
15 Akatengeneza mjeledi kutokana na kamba, akawafukuza wote kutoka kwenye eneo la Hekalu, pamoja na kondoo na ngʼombe. Akazipindua meza za wale wabadili fedha na kuzimwaga fedha zao.
He made a whip of cords and drove all out of the temple, both the sheep and the oxen; and he poured out the changers’ money and overthrew their tables.
16 Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, “Waondoeni hapa! Mnathubutuje kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa biashara?”
To those who sold the doves, he said, “Take these things out of here! Do not make my Father’s house a marketplace!”
17 Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa imeandikwa: “Wivu wa nyumba yako utanila.”
His disciples remembered that it was written, “Zeal for your house will eat me up.”
18 Ndipo Wayahudi wakamuuliza, “Unaweza kutuonyesha ishara gani ili kuthibitisha mamlaka uliyo nayo ya kufanya mambo haya?”
The Jews therefore answered him, “What sign do you show us, seeing that you do these things?”
19 Yesu akawajibu, “Libomoeni hili Hekalu, nami nitalijenga tena kwa siku tatu!”
Jesus answered them, “Destroy this temple, and in three days I will raise it up.”
20 Wale Wayahudi wakamjibu, “Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita, nawe wasema utalijenga kwa siku tatu?”
The Jews therefore said, “It took forty-six years to build this temple! Will you raise it up in three days?”
21 Lakini yeye Hekalu alilozungumzia ni mwili wake.
But he spoke of the temple of his body.
22 Baada ya kufufuliwa kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka yale aliyokuwa amesema. Ndipo wakayaamini Maandiko na yale maneno Yesu aliyokuwa amesema.
When therefore he was raised from the dead, his disciples remembered that he said this, and they believed the Scripture and the word which Jesus had said.
23 Ikawa Yesu alipokuwa Yerusalemu kwenye Sikukuu ya Pasaka, watu wengi waliona ishara na miujiza aliyokuwa akifanya, wakaamini katika jina lake.
Now when he was in Jerusalem at the Passover, during the feast, many believed in his name, observing his signs which he did.
24 Lakini Yesu hakujiaminisha kwao kwa sababu aliwajua wanadamu wote.
But Jesus did not entrust himself to them, because he knew everyone,
25 Hakuhitaji ushuhuda wa mtu yeyote kuhusu mtu, kwa kuwa alijua yote yaliyokuwa moyoni mwa mtu.
and because he did not need for anyone to testify concerning man; for he himself knew what was in man.

< Yohana 2 >