< Yohana 2 >

1 Siku ya tatu kulikuwa na arusi katika mji wa Kana ya Galilaya, naye mama yake Yesu alikuwepo pale.
Třetího pak dne stala se svadba v Káni Galilejské, a byla matka Ježíšova tam.
2 Yesu pamoja na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa arusini pia.
A pozván jest také Ježíš i učedlníci jeho na tu svadbu.
3 Divai ilipokwisha, mama yake Yesu akamwambia, “Wameishiwa na divai.”
Když se pak nedostalo vína, řekla matka Ježíšova jemu: Vína nemají.
4 Yesu akamwambia, “Mwanamke, nina nini nawe? Saa yangu haijawadia.”
Dí jí Ježíš: Co mně a tobě ženo? Ještě nepřišla hodina má.
5 Mama yake akawaambia wale watumishi, “Lolote atakalowaambia, fanyeni.”
Dí matka jeho služebníkům: Což by koli vám řekl, učiňte.
6 Basi ilikuwepo mitungi sita ya kuhifadhia maji iliyotengenezwa kwa mawe kwa ajili ya kujitakasa kwa desturi ya Kiyahudi; kila mtungi ungeweza kuchukua vipipa viwili au vitatu.
I bylo tu kamenných stoudví šest postaveno, podlé očišťování Židovského, beroucí v sebe jedna každá dvě neb tři míry.
7 Yesu akawaambia wale watumishi, “Ijazeni hiyo mitungi maji.” Nao wakaijaza ile mitungi mpaka juu.
Řekl jim Ježíš: Naplňte ty stoudve vodou. I naplnili je až do vrchu.
8 Kisha akawaambia, “Sasa choteni hayo maji kidogo, mpelekeeni mkuu wa meza.” Hivyo wakachota, wakampelekea.
I dí jim: Nalévejtež již, a neste vrchnímu správci svadby. I nesli.
9 Yule mkuu wa meza akayaonja yale maji ambayo yalikuwa yamebadilika kuwa divai. Hakujua divai hiyo ilikotoka ingawa wale watumishi waliochota yale maji wao walifahamu. Basi akamwita bwana arusi kando
A jakž okusil vrchní správce svadby té vody, vínem učiněné, (nevěděl pak, odkud by bylo, ale služebníci věděli, kteříž vážili vodu, ) povolal ženicha ten vrchní správce,
10 akamwambia, “Watu wote hutoa kwanza divai nzuri, kisha huleta ile divai hafifu wageni wakisha kunywa vya kutosha, lakini wewe umeiweka ile nzuri kupita zote mpaka sasa.”
A řekl mu: Každý člověk nejprvé dobré víno dává, a když by se hojně napili, tedy to, kteréž horší. Ty zachoval jsi víno dobré až dosavad.
11 Huu, ndio uliokuwa muujiza wa kwanza Yesu aliofanya Kana ya Galilaya. Hivyo Yesu alidhihirisha utukufu wake, nao wanafunzi wake wakamwamini.
To učinil Ježíš počátek divů v Káni Galilejské, a zjevil slávu svou. I uvěřili v něho učedlníci jeho.
12 Baada ya hayo, Yesu pamoja na mama yake, ndugu zake na wanafunzi wake, walishuka mpaka Kapernaumu, wakakaa huko siku chache.
Potom sstoupil do Kafarnaum, on i matka jeho, i bratří jeho, i učedlníci jeho, a pobyli tam nemnoho dní;
13 Ilipokaribia wakati wa Pasaka ya Wayahudi, Yesu alipanda kwenda Yerusalemu.
Nebo blízko byla velikanoc Židovská. I vstoupil Ježíš do Jeruzaléma.
14 Huko Hekaluni aliwakuta watu wakiuza ngʼombe, kondoo na njiwa, nao wengine walikuwa wameketi mezani wakibadili fedha.
A nalezl v chrámě prodavače volů a ovec i holubic, a penězoměnce sedící.
15 Akatengeneza mjeledi kutokana na kamba, akawafukuza wote kutoka kwenye eneo la Hekalu, pamoja na kondoo na ngʼombe. Akazipindua meza za wale wabadili fedha na kuzimwaga fedha zao.
A udělav bič z provázků, všecky vyhnal z chrámu, i ovce i voly, a penězoměncům rozsypal peníze, a stoly zpřevracel.
16 Akawaambia wale waliokuwa wakiuza njiwa, “Waondoeni hapa! Mnathubutuje kuifanya nyumba ya Baba yangu kuwa mahali pa biashara?”
A těm, kteříž holuby prodávali, řekl: Odneste tyto věci odsud, a nečiňte domu Otce mého domem kupeckým.
17 Wanafunzi wake wakakumbuka kuwa imeandikwa: “Wivu wa nyumba yako utanila.”
I rozpomenuli se učedlníci jeho, že psáno jest: Horlivost domu tvého snědla mne.
18 Ndipo Wayahudi wakamuuliza, “Unaweza kutuonyesha ishara gani ili kuthibitisha mamlaka uliyo nayo ya kufanya mambo haya?”
Tedy odpověděli Židé a řekli jemu: Jaké znamení nám ukážeš, že tyto věci činíš?
19 Yesu akawajibu, “Libomoeni hili Hekalu, nami nitalijenga tena kwa siku tatu!”
Odpověděl Ježíš a řekl jim: Zrušte chrám tento, a ve třech dnech zase vzdělám jej.
20 Wale Wayahudi wakamjibu, “Hekalu hili lilijengwa kwa muda wa miaka arobaini na sita, nawe wasema utalijenga kwa siku tatu?”
I řekli Židé: Čtyřidceti a šest let dělán jest chrám tento, a ty ve třech dnech vzděláš jej?
21 Lakini yeye Hekalu alilozungumzia ni mwili wake.
Ale on mluvil o chrámu těla svého.
22 Baada ya kufufuliwa kutoka kwa wafu, wanafunzi wake wakakumbuka yale aliyokuwa amesema. Ndipo wakayaamini Maandiko na yale maneno Yesu aliyokuwa amesema.
A protož když z mrtvých vstal, rozpomenuli se učedlníci jeho, že jim to byl pověděl. I uvěřili písmu a slovu, kteréž pověděl Ježíš.
23 Ikawa Yesu alipokuwa Yerusalemu kwenye Sikukuu ya Pasaka, watu wengi waliona ishara na miujiza aliyokuwa akifanya, wakaamini katika jina lake.
A když byl v Jeruzalémě na velikunoc v den sváteční, mnozí uvěřili ve jméno jeho, vidouce divy jeho, kteréž činil.
24 Lakini Yesu hakujiaminisha kwao kwa sababu aliwajua wanadamu wote.
Ale Ježíš nesvěřil sebe samého jim, proto že on znal všecky.
25 Hakuhitaji ushuhuda wa mtu yeyote kuhusu mtu, kwa kuwa alijua yote yaliyokuwa moyoni mwa mtu.
Aniž potřeboval, aby kdo svědectví vydával o člověku; nebo on věděl, co by bylo v člověku.

< Yohana 2 >