< Yohana 19 >

1 Ndipo Pilato akamtoa Yesu akaamuru apigwe mijeledi.
O Pilato amwejile oYesu na hushete.
2 Askari wakasokota taji ya miiba, wakamvika Yesu kichwani. Wakamvalisha joho la zambarau.
Bhala asikari bhapotile aminvwa nalenganye taji. Bhaibheha pitwe lya Yesu na hukwatizye amenda ge rangi ye nshamwamu nshamwamu.
3 Wakawa wanapanda pale alipo tena na tena, wakisema, “Salamu! Mfalme wa Wayahudi!” Huku wakimpiga makofi usoni.
Bhamwenzela na aje, “Awe mwene wa Yahudi! na hukhome hu makhono gabho.
4 Pilato akatoka tena nje akawaambia wale waliokusanyika, “Tazameni, namkabidhi Yesu kwenu kuwajulisha kwamba mimi sikumwona ana hatia.”
O Pilato afumile honze na bhabhozye abhantu, “Enyaji embaletela ono omuntu hulimwe aje mumanye ane senalilolile ibhibhi lyalyonti muhati yabho.”
5 Kwa hiyo Yesu akatoka nje akiwa amevaa ile taji ya miiba na lile vazi la zambarau. Pilato akawaambia, “Tazameni, huyu hapa huyo mtu!”
Eshi oYesu afumile honze; ali akwete etaji ye minvwa na menda amashamwamu. O Pilato ayanga, “Enyaji abhozya mwenyi omuntu ono epa!”
6 Wale viongozi wa makuhani na maafisa walipomwona, wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!” Pilato akawaambia, “Mchukueni ninyi mkamsulubishe, mimi sioni hatia juu yake.”
Omuda ochungaji ogosi wa gosi nabhahalola oYesu, bhakhoma ekelele bhaga, “Yenvyaji, yenvyaji.” O Pilato abhabhozya, “Mwenji amwe mwemwe muyenvyaje, afuatanaje ane sendilola akosa muhati yakwe.”
7 Wayahudi wakamjibu, “Sisi tunayo sheria na kutokana na sheria hiyo, hana budi kufa kwa sababu yeye alijiita Mwana wa Mungu.”
Ayahudi bhabhozya oPilato, “Ate tili ne ndajizyo, na hundajizyo yeeyo ehwanziwa afwe afuatanaje omwene ahwilola aje mwana wa Ngolobhe.”
8 Pilato aliposikia haya, akaogopa zaidi.
O Pilato nahonvwa enongwa ezyo azidile ahwogope,
9 Akaingia tena ndani ya jumba la kifalme, akamuuliza Yesu, “Wewe umetoka wapi?” Lakini Yesu hakumjibu.
ahinjila Mpraitorio nantele na hubhozye oYesu, “Awe ofuma hwii? Ata sheshi, oYesu sagayanjile.
10 Pilato akamwambia, “Wewe unakataa kuongea na mimi? Hujui ya kuwa nina mamlaka ya kukuachia huru au kukusulubisha?”
Nantele iPilato abhozya, “Aje, awe soyanga nane? Aje, awe somenye aje ane endi nouwezo wa humwigugulile no uwezo wa huyemvye?”
11 Ndipo Yesu akamwambia, “Wewe hungekuwa na mamlaka yoyote juu yangu kama hungepewa kutoka juu. Kwa hiyo yeye aliyenitia mikononi mwako ana hatia ya dhambi iliyo kubwa zaidi.”
O Yesu ajile, “Ogali ne nguvu ashile ane ogalisopewilwe afume amwanya. Eshi, omuntu wanefwizye huliwe ali ne mbibhi engosi.”
12 Tangu wakati huo, Pilato akajitahidi kutafuta njia ya kumfungua Yesu, lakini Wayahudi wakazidi kupiga kelele wakisema, “Ukimwachia huyu mtu, wewe si rafiki wa Kaisari. Mtu yeyote anayedai kuwa mfalme anampinga Kaisari.”
Afumilane ni jibu eli, oPilato ahanzaga ahuleshe weene, ila Aayahudi wahakhoma ekelele bhaga, “Nkashe obhahuleshe wene awe soli wamwabho oKaisari: Shila wahwibheha aje mwene ayanga shingunga sha Kaisari.”
13 Pilato aliposikia maneno haya akamtoa Yesu nje tena akaketi katika kiti chake cha hukumu, mahali palipoitwa Sakafu ya Jiwe, kwa Kiebrania paliitwa Gabatha
O Pilato na honvwa enongwa aleta oYesu honze nantele ahakhala pitengo lye lonzi pala papamanyi she aje sakafu, ila hushiEbrania, Gabhatha.
14 Basi ilikuwa siku ya Maandalio ya Pasaka, yapata kama saa sita hivi. Pilato akawaambia Wayahudi, “Huyu hapa mfalme wenu!”
Isiku lye maandalizi ge pasaka nalyafishile, omuda gwe saa tanda. O Pilato abhozya Ayahudi, “Enyaaji omwene wenyu ono epa!”
15 Wao wakapiga kelele, “Mwondoe! Mwondoe! Msulubishe!” Pilato akawauliza, “Je, nimsulubishe mfalme wenu?” Wale viongozi wa makuhani wakamjibu, “Sisi hatuna mfalme mwingine ila Kaisari.”
Bhakhoma ekelele, “Sogozi, sogozi, muyenvye!” O Pilato abhabhozya, “Aje eyenvye omwene wenyu?” Wope Ochungaji ogosi ajile, “Ate setili no mwene ila o Kaisari.”
16 Ndipo Pilato akamkabidhi Yesu kwao ili wamsulubishe. Kwa hiyo askari wakamchukua Yesu.
O Pilato nkafumya oYesu hwabhene aje ayenvewe.
17 Yesu, akiwa ameubeba msalaba wake, akatoka kuelekea mahali palipoitwa Fuvu la Kichwa (kwa Kiebrania ni Golgotha).
Wope bhamwega oYesu, wope wafuma, ohu anyemuye eshikhobhe hanyo shakwe yoyo paka hula hufuvu litwe, hu Shiebrania bhaiga hu Golgota.
18 Hapo ndipo walipomsulubisha. Pamoja naye walisulubisha watu wengine wawili, mmoja kila upande wake, naye Yesu katikati.
Nkabhayenvya oYesu na bhala alume bhabhele, omo oupande ou owamwabho oupande ou, no Yesu pahati yabho.
19 Pilato akaamuru tangazo liandikwe na liwekwe juu kwenye msalaba wa Yesu, likasema: “Yesu wa Nazareti, Mfalme wa Wayahudi.”
O Pilato ahandiha eshimanyilo na bheshe pamwanya pashi khobhehanyo. Epo pahandihwe: YESU WENAZALETI, OMWENE WA YAHUDI.
20 Kwa kuwa mahali hapo Yesu aliposulubiwa palikuwa karibu na mjini, Wayahudi wengi walisoma maandishi haya yaliyokuwa yameandikwa kwa lugha za Kiebrania, Kiyunani na Kilatini.
Abhinji bha Yahudi bhabhazya eshimanyilo esho pantu pala pabhayenvezye oYesu pali pepe ne khaaya. Eshi manyilo esho shahandihwe hushi Ebrania, hushi Rumi na hushi Yunani.
21 Viongozi wa makuhani wa Wayahudi wakapinga, wakamwambia Pilato, “Usiandike ‘Mfalme wa Wayahudi,’ bali andika kwamba mtu huyu alisema yeye ni mfalme wa Wayahudi.”
Ogosi bha dimi bha Yahudi bhabhozya oPilato, “Sio hwandishe, 'Omwene wa Yahudi; ila omwene ajile ane endi mwene Wayahudi.”
22 Pilato akawajibu, “Nilichokwisha kuandika, nimeandika!”
Wope oPilato ajile, “Genandishe enandishe.”
23 Askari walipokwisha kumsulubisha Yesu, walichukua nguo zake wakazigawa mafungu manne, kila askari fungu lake. Ila walikubaliana wasilichane lile vazi lake kwa maana lilikuwa halina mshono bali limefumwa tangu juu hadi chini.
Askari nabhayenvya oYesu, bhahega amenda gakwe na gagabhanye vilondo viine, shila sikari ilondo limo, Shesho inkanzu, lila selyalilisonilwe ila lyali litabhilwe lyonti afumile pamwanya.
24 Wakaambiana, “Tusilichane ila tulipigie kura ili kuamua ni nani atalichukua.” Hili lilitukia ili Maandiko yapate kutimizwa yale yaliyosema, “Wanagawana nguo zangu, na vazi langu wanalipigia kura.” Hayo ndiyo waliyoyafanya wale askari.
Bhakwepelana bhebho hu bhebho, “Tinganje alipasule ila tikhome yekola aje libhe lyananu.” Eli lyafumiye aje lila izu likamilishe, lila lyalyajile bhagabhenye amenda gane, no ninkanza lyane bhakhomeye ekola.”
25 Wakati huo huo karibu na msalaba wa Yesu walikuwa wamesimama mama yake, na dada wa mamaye, na Maria mke wa Klopa, na Maria Magdalene.
Asikari bhabhombile embombo ezi. Onyina wakwe oYesu, no dada wa nyina wakwe, oMariamu oshe wa Kleopa no Mariamu Magedelena - abhashe ebha bhali bhemeleye pepe neshi khobhehanyo sha Yesu.
26 Yesu alipomwona mama yake mahali pale pamoja na yule mwanafunzi aliyempenda wamesimama karibu, akamwambia mama yake, “Mwanamke, huyo hapo ndiye mwanao,”
O Yesu nalolile onyina wakwe pamonola omwanafunzi wagene bhemeleye peepe, abhozye onyina wakwe, “Wee shee, enya, lola omwana waho ono epa!”
27 kisha akamwambia yule mwanafunzi, “Nawe huyo hapo ndiye mama yako.” Tangu wakati huo yule mwanafunzi akamchukua mama yake Yesu nyumbani kwake.
Abhozya omwanafunzi, “Enya, ono epa onyina waho. “Afume esala eyo ola omwanafunzi amwega abhale akhaya yakwe.
28 Baada ya haya, Yesu hali akijua kuwa mambo yote yamemalizika, alisema ili kutimiza Maandiko, “Naona kiu.”
Baada yelyo, o Yesu amenye aje gonti gamalishe gamalishiye aje akamilisye amaazu, ajile, “Elola eshomelwa.”
29 Hapo palikuwa na bakuli lililojaa siki. Kwa hiyo wakachovya sifongo kwenye hiyo siki, wakaiweka kwenye ufito wa mti wa hisopo, wakampelekea mdomoni.
Eshelelo shashilimemile shali shibhehwelwe pala, bhabheha esifongo yememile Isiki pamwanya ye ufito we hisopo, bhabheshela mwilomu lyakwe.
30 Baada ya kuionja hiyo siki, Yesu akasema, “Imekwisha.” Akainamisha kichwa chake, akaitoa roho yake.
Wope oYesu naibhonga ezyo, ajile, “Emalishe.” Pamande aundamiha itwe lyakwe, aibheha eroho yakwe.
31 Kwa kuwa ilikuwa siku ya Maandalio ya Pasaka, Wayahudi hawakutaka miili ibaki msalabani siku ya Sabato, hasa kwa kuwa hiyo Sabato ingekuwa Sikukuu. Wakamwomba Pilato aamuru miguu ya wale waliosulubiwa ivunjwe ili wafe haraka miili iondolewe kwenye misalaba.
Afwatanaje waali wakati wahwiyandaale, afuatanaje amabele segahanziwaga asagale pashikhobhehanyo owakati we Sabato (afuatanaje eSabato yaali ye muhimu), ayahudi bhalabhile oPilato aje amagaga gabho bhala bhabhali bhayenvezewa gabudulwe, naje na mabeele gabho bhagisye.
32 Kwa hiyo askari wakaenda wakavunja miguu ya mtu wa kwanza aliyesulubiwa pamoja na Yesu na yule mwingine pia.
Osikari ahenza abudule amagaga gamuntu owa kwanza no wa bhele ali ayonvewa pandwemo no Yesu.
33 Lakini walipomkaribia Yesu, wakaona ya kuwa amekwisha kufa, hivyo hawakuvunja miguu yake.
Nabhafishila oYesu, bhamweje afwiye eshieshi sebhabudula amagaga gakwe.
34 Badala yake mmoja wa wale askari akamchoma mkuki ubavuni na mara pakatoka damu na maji.
Ata sheshi omo wa sikari alese oYesu hu mbazu ne mpalala, gahafuma amenze gidanda.
35 Mtu aliyeona mambo hayo ndiye alitoa ushuhuda, nao ushuhuda wake ni kweli. Anajua kuwa anasema kweli, naye anashuhudia ili pia nanyi mpate kuamini.
Wope walolile eli afumwizye olweteho no lweteho lwakwe lwe lyoli. Omwene amenye hayanjile he lyoli aje namwe mweteshele.
36 Kwa maana mambo haya yalitukia ili Maandiko yapate kutimia, yale yasemayo, “Hakuna hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa.”
Enongwa ezi zyahali aje lila izu lyalya ya ngwilwe nkalifishile, “Nomo hata omo wamwene waibudulwa.”
37 Tena Andiko lingine lasema, “Watamtazama yeye waliyemchoma.”
Nantele izu lyamwabho liyiga, “Bhahumwenya omwene wabhalese”
38 Baada ya mambo haya, Yosefu wa Arimathaya, aliyekuwa mfuasi wa Yesu, ingawa kwa siri kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi, alimwomba Pilato ruhusa ili kuuchukua mwili wa Yesu. Pilato alimruhusu, hivyo akaja, akauchukua.
Baadaye nongo ezi oYusufu we Arimathaya, afuatanaje ali mwanafunzi wa Yesu, ila shi siri abhogope Ayahudi, alabhile oPilato aje agweje obele gwa Yesu. Wope oPilato apiye oluhusa. O Yusufu ahenza agwefwe obele gwa Yesu.
39 Naye Nikodemo, yule ambaye kwanza alimwendea Yesu usiku, akaja, akaleta mchanganyiko wa manemane na manukato, yenye uzito wa zaidi ya kilo thelathini
Wope o Nikodemo ola olwahwande wafwatile oYesu no siku wope ahenzele. Omwene aletile osangano manemane no udi, oumwamuwe latili mia e yeeka.
40 Wakauchukua mwili wa Yesu, wakaufunga katika sanda ya kitani safi pamoja na yale manukato, kama ilivyokuwa desturi ya Wayahudi.
Bhahega obele gwa Yesu bhagupinya mumpongoso ye shitani pandwemo na gala amafuta, nanshi shahali ekawaida ya Yahudi omuda gwa syele.
41 Basi palikuwa na bustani karibu na mahali pale aliposulubiwa, na pale ndani ya ile bustani palikuwa na kaburi jipya, ambalo halikuwa limezikiwa mtu bado.
Apantu oYesu pabhayenvezye pali nee bustani; muhati yela ebustani mwali ni kaburi ipya sayahali omuntu wawaile asyelwe omwo.
42 Kwa hiyo, kwa kuwa ilikuwa siku ya Wayahudi ya Maandalio, nalo kaburi hilo lilikuwa karibu, wakamzika Yesu humo.
Afuatanaje lyali lisiku lye maandalizi hwa Yahudi, na afuatanaje lila ikaburi lyali peepe, bhahagoni oYesu muhati yakwe.

< Yohana 19 >