< Yohana 19 >
1 Ndipo Pilato akamtoa Yesu akaamuru apigwe mijeledi.
Linu Pilato ni cha hinda Jesu ni ku mushupa.
2 Askari wakasokota taji ya miiba, wakamvika Yesu kichwani. Wakamvalisha joho la zambarau.
Masole ni ba luka ihusi ya miya. Ni ba izwatika Jesu ku mutwi ni ku muzwatika muchizabalo cha mubala wabusimwine.
3 Wakawa wanapanda pale alipo tena na tena, wakisema, “Salamu! Mfalme wa Wayahudi!” Huku wakimpiga makofi usoni.
Ni chi beza kwali ni chi bati, “Yosho, Simwine wa Majuda!” mi ni chi ba mudama.
4 Pilato akatoka tena nje akawaambia wale waliokusanyika, “Tazameni, namkabidhi Yesu kwenu kuwajulisha kwamba mimi sikumwona ana hatia.”
Linu Pilato ni cha zwila hanze hape mi ni chati kubali, “Mubone, Ni muleta hanze kwenu chokuti mwizibe kuti ka na na wana mulandu kwakwe.”
5 Kwa hiyo Yesu akatoka nje akiwa amevaa ile taji ya miiba na lile vazi la zambarau. Pilato akawaambia, “Tazameni, huyu hapa huyo mtu!”
Chobulyo Jesu ni chazwila hanze, a ba zwete ihusi ya miya ni chizwato chamubala wa busimwine. Linu Pilato ni chawamba ku bali, “Mubone muntu!”
6 Wale viongozi wa makuhani na maafisa walipomwona, wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!” Pilato akawaambia, “Mchukueni ninyi mkamsulubishe, mimi sioni hatia juu yake.”
Linu ni hakwinabulyo bapurisita bakulwana ni basepahala chi ba bona Jesu, chi bahuweleza ni kuwamba kuti, “Mu mu kokotele, mu mu kokotele!” Pilato ni cha wamba kubali, “Mu muhinde mubene mi mu mu kokotele, mukuti ka kwina mulandu wa nawana kwali.”
7 Wayahudi wakamjibu, “Sisi tunayo sheria na kutokana na sheria hiyo, hana budi kufa kwa sababu yeye alijiita Mwana wa Mungu.”
Majuda ni chi ba mwitaba, “Twina mulao, mi chakuya cho wo mulao u swanela kufwa chokuti a ba libiki kuti Mwana we Ireeza.”
8 Pilato aliposikia haya, akaogopa zaidi.
Linu Pilato ha zuwa ao manzwi, ni chaba ni kutiya ahulu,
9 Akaingia tena ndani ya jumba la kifalme, akamuuliza Yesu, “Wewe umetoka wapi?” Lakini Yesu hakumjibu.
mi ni chenjila mu maofisi makando a mubuso hape ni chati kwa Jesu, “U zwa kuhi?” Kono Jesu kana a ba mwitabi.
10 Pilato akamwambia, “Wewe unakataa kuongea na mimi? Hujui ya kuwa nina mamlaka ya kukuachia huru au kukusulubisha?”
Linu Pilato ni chati kwali, “I we ko wambi kwangu? Kana kawizi kuti ni na ziho za ku ku lukulula, ni ziho za ku ku kokotela?”
11 Ndipo Yesu akamwambia, “Wewe hungekuwa na mamlaka yoyote juu yangu kama hungepewa kutoka juu. Kwa hiyo yeye aliyenitia mikononi mwako ana hatia ya dhambi iliyo kubwa zaidi.”
Jesu ni cha mwitaba, “Kawina ziho heulu lyangu konji zi ba hewa kwako kuzwilila kwiulu. Ni hakwina bulyo, i ye ya ba ni hi kwako wina chibi chikando.”
12 Tangu wakati huo, Pilato akajitahidi kutafuta njia ya kumfungua Yesu, lakini Wayahudi wakazidi kupiga kelele wakisema, “Ukimwachia huyu mtu, wewe si rafiki wa Kaisari. Mtu yeyote anayedai kuwa mfalme anampinga Kaisari.”
Che yi inkalabo, Pilato ni cha lika ku mulukulula, kono Majuda ni chi ba huweleza ni chi bati, “Heba ne u lukulula u zu muntu, kahena u mulikani wa Sesare: Zumwi ni zumwi u li bika busimwine u wamba cha kulwisa Sesare.”
13 Pilato aliposikia maneno haya akamtoa Yesu nje tena akaketi katika kiti chake cha hukumu, mahali palipoitwa Sakafu ya Jiwe, kwa Kiebrania paliitwa Gabatha
Linu Pilato ha zuwa ao manzwi, ni chaleta Jesu hanze mi ni chekala muchipula cha buatuli muchibaka chi sumpwa, “Chibaka chi Bumwinwe,” Kono mu chi Heberu, “Gabati.”
14 Basi ilikuwa siku ya Maandalio ya Pasaka, yapata kama saa sita hivi. Pilato akawaambia Wayahudi, “Huyu hapa mfalme wenu!”
Linu chi bali izuba lye ntukiso ye Impaseka, chi i bakusaka ku ba inako i kwana i yanza ni konke. Pilato ni chati ku Majuda, “Mubone, u zu simwine wenu!”
15 Wao wakapiga kelele, “Mwondoe! Mwondoe! Msulubishe!” Pilato akawauliza, “Je, nimsulubishe mfalme wenu?” Wale viongozi wa makuhani wakamjibu, “Sisi hatuna mfalme mwingine ila Kaisari.”
Ni chi bahuwa kuti, “Muzwise, muzwise; u mukokotele!” Pilato ni cha ti kubali, “ni kokotele Simwine wenu?” Ba purisita ba kulwana ni chi betaba, “Katwina Simwine esi bulyo Sesare,”
16 Ndipo Pilato akamkabidhi Yesu kwao ili wamsulubishe. Kwa hiyo askari wakamchukua Yesu.
Linu Pilato na ba ha Jesu kuti a kokotelwe.
17 Yesu, akiwa ameubeba msalaba wake, akatoka kuelekea mahali palipoitwa Fuvu la Kichwa (kwa Kiebrania ni Golgotha).
Cwale ni bahinda Jesu, mi ni cha ya hanze, kulihindila chifapano i ye mwine, ku chibaka chi sumpwa “Chibaka cha Katendele,” I cho mu chi Heberu chi sumpwa, “Kologota.”
18 Hapo ndipo walipomsulubisha. Pamoja naye walisulubisha watu wengine wawili, mmoja kila upande wake, naye Yesu katikati.
Ba ba kokoteli Jesu u mo. Mi ne na ni bantu bamwi bo bele, yenke kwi neku ni neku lyakwe, ni Jesu ne na hakati.
19 Pilato akaamuru tangazo liandikwe na liwekwe juu kwenye msalaba wa Yesu, likasema: “Yesu wa Nazareti, Mfalme wa Wayahudi.”
Pilato hape na ñola chisupo mi na chibika ha chifapano. Haho ha bañoletwe: JESU WA NAZARETA, SIMWINE WA MAJUDA.
20 Kwa kuwa mahali hapo Yesu aliposulubiwa palikuwa karibu na mjini, Wayahudi wengi walisoma maandishi haya yaliyokuwa yameandikwa kwa lugha za Kiebrania, Kiyunani na Kilatini.
Bungi bwa Majuda ni chi ba bala i cho chisupo chokuti chibaka cha ba kokotelwa Jesu chi bena hafuhi ni tolopo. Chisupo chi bañoletwe mu chi Heberu, mu chi Latini, ni mu chi Gerike.
21 Viongozi wa makuhani wa Wayahudi wakapinga, wakamwambia Pilato, “Usiandike ‘Mfalme wa Wayahudi,’ bali andika kwamba mtu huyu alisema yeye ni mfalme wa Wayahudi.”
Linu mupurisita mukulwana wa Majuda ni cha wamba kwa Pilato, “Kanji u ñoli, “Simwine wa Majuda; kono u ti, I ye mwine a ba wambi, “Njime ni Simwine wa Majuda.”
22 Pilato akawajibu, “Nilichokwisha kuandika, nimeandika!”
Pilato ne taba, “Chi ni ba ñoli ni ba ñoli.”
23 Askari walipokwisha kumsulubisha Yesu, walichukua nguo zake wakazigawa mafungu manne, kila askari fungu lake. Ila walikubaliana wasilichane lile vazi lake kwa maana lilikuwa halina mshono bali limefumwa tangu juu hadi chini.
Ha bamana masole ku kokotela Jesu, ni chi bahinda zi zwato zakwe ni ku li abela che inkalulo zone; inkabelo ku isole ni isole, ni chizwato cha hewulu. Kono chizwato che hewulu ke na chibena mapeka, chi ba ku lukililwe hamwina ku zwililila kwiwulu.
24 Wakaambiana, “Tusilichane ila tulipigie kura ili kuamua ni nani atalichukua.” Hili lilitukia ili Maandiko yapate kutimizwa yale yaliyosema, “Wanagawana nguo zangu, na vazi langu wanalipigia kura.” Hayo ndiyo waliyoyafanya wale askari.
Linu ni chi ba li wambila a bo beene, “Kanji tu chi ñatuli hakati, kono ni hakwina bulyo tulaule che loto i yo italuhanye kuti ka chi be chani,” I chi chiba chitahali chokuti iñolo li zuzilizwe li wamba kuti, “Ba ba lyiabili zizwato zangu mukati kabo; ba ba lauli che loto chizwato changu.”
25 Wakati huo huo karibu na msalaba wa Yesu walikuwa wamesimama mama yake, na dada wa mamaye, na Maria mke wa Klopa, na Maria Magdalene.
Masole ba ba chiti izi zintu. Banyina wa Jesu, mwanche u banyina, Maria mwihabwe wa Kulopa, ni Maria Magadalena. A ba banakazi ba bazimene ku chifapano cha Jesu.
26 Yesu alipomwona mama yake mahali pale pamoja na yule mwanafunzi aliyempenda wamesimama karibu, akamwambia mama yake, “Mwanamke, huyo hapo ndiye mwanao,”
Jesu ha bona banyina ni mulutwana ya ba kusuna ni bazimine hembali, na ti ku banyina, “Mwanakazi, bone, mwanako!”
27 kisha akamwambia yule mwanafunzi, “Nawe huyo hapo ndiye mama yako.” Tangu wakati huo yule mwanafunzi akamchukua mama yake Yesu nyumbani kwake.
Linu nchati ku mulutwana, “Bone, banyoko!” Kuzwililila he nako yo mulutwana na muhinda ku mutwala kumunzi wa kwe.
28 Baada ya haya, Yesu hali akijua kuwa mambo yote yamemalizika, alisema ili kutimiza Maandiko, “Naona kiu.”
Ha kumana ichi Jesu, mukuti a bakwizi kuti zintu zonse linu chi zamana, kuti kwi zuzilizwe mañolo, ati, “Ni fwile inyotwa,”
29 Hapo palikuwa na bakuli lililojaa siki. Kwa hiyo wakachovya sifongo kwenye hiyo siki, wakaiweka kwenye ufito wa mti wa hisopo, wakampelekea mdomoni.
Chibikilo chi bezwile i waine i canchumuka chi ba bikitwe aho, linu chi ba bika chiponji chi zwile i waine i chanchumuka ku mutabi we haisopu ni ku inyamwina ku kaholo ka kwe.
30 Baada ya kuionja hiyo siki, Yesu akasema, “Imekwisha.” Akainamisha kichwa chake, akaitoa roho yake.
Mi Jesu a cha nywine ku i waine i chanchumuka, chati, “Çhi kwamana.” Ni cha kotamisa mutwi wa kwe ni kuha luhuho lwakwe.
31 Kwa kuwa ilikuwa siku ya Maandalio ya Pasaka, Wayahudi hawakutaka miili ibaki msalabani siku ya Sabato, hasa kwa kuwa hiyo Sabato ingekuwa Sikukuu. Wakamwomba Pilato aamuru miguu ya wale waliosulubiwa ivunjwe ili wafe haraka miili iondolewe kwenye misalaba.
Linu Majuda, chokuti i ba li izuba lya kuli bakanya, ni kuti mibili kanji i shali ha chifapano mu lye Insabata (Mukuti Insabata i bali ya butokwa ahulu), ni chi bakumbila Pilato kucholola matende a bo ni ku bahangula.
32 Kwa hiyo askari wakaenda wakavunja miguu ya mtu wa kwanza aliyesulubiwa pamoja na Yesu na yule mwingine pia.
Lunu masole chibeza ni kucholola matende a mukwame wa matangilo ni a mukwame wa bubeli ya ba kokotelwe ni Jesu.
33 Lakini walipomkaribia Yesu, wakaona ya kuwa amekwisha kufa, hivyo hawakuvunja miguu yake.
Linu ha be za kwa Jesu, chi ba bona kuti cha bafwile kale, chobulyo ka na ba ba muchololi matende.
34 Badala yake mmoja wa wale askari akamchoma mkuki ubavuni na mara pakatoka damu na maji.
Ni hakubabulyo, zumwi wa masole cha muhweza mumpati yakwe ni mulinga, mi hohwaho malaha ni menzi ni za zwa.
35 Mtu aliyeona mambo hayo ndiye alitoa ushuhuda, nao ushuhuda wake ni kweli. Anajua kuwa anasema kweli, naye anashuhudia ili pia nanyi mpate kuamini.
I ye ya ba boni izi nja bapaki, imi bupaki bwakwe bwe niti. Wizi kuti cha ba wambi i niti njo kuti nanwe bulyo chi muzumina.
36 Kwa maana mambo haya yalitukia ili Maandiko yapate kutimia, yale yasemayo, “Hakuna hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa.”
Chokuti izi zintu zi ba chitahali cha kwi zuziliza iñolo, “Kakwina nanta chimwina ku zifuha za kwe chete chi cholwe.”
37 Tena Andiko lingine lasema, “Watamtazama yeye waliyemchoma.”
Hape, limwi iñolo liti, “Ka ba lole kwali iye u ba bahwezi.”
38 Baada ya mambo haya, Yosefu wa Arimathaya, aliyekuwa mfuasi wa Yesu, ingawa kwa siri kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi, alimwomba Pilato ruhusa ili kuuchukua mwili wa Yesu. Pilato alimruhusu, hivyo akaja, akauchukua.
Ha kumana izi zintu Josefa wa Arimatea, sina ha ba li mulutwana wa Jesu (kono cha kuliungula ka lyowa ku Majuda) cha kumbila Pilato heba u wola kuhinda mubili wa Jesu. Pilato cha muha chibaka. Linu Josefa ni cheza ni kuhinda mubili wakwe.
39 Naye Nikodemo, yule ambaye kwanza alimwendea Yesu usiku, akaja, akaleta mchanganyiko wa manemane na manukato, yenye uzito wa zaidi ya kilo thelathini
Nekudema na ye cheza, u zo kumatangilo ya bezite kwa Jesu masiku. A baleti i maire i kopenywe ni incenka, cha buima busika ha mwanda wonke.
40 Wakauchukua mwili wa Yesu, wakaufunga katika sanda ya kitani safi pamoja na yale manukato, kama ilivyokuwa desturi ya Wayahudi.
Linu chi bahinda mubili wa Jesu ni ku u zingelela mu majira a zi zabalo ni mi nunkiso, si na haibali chizo cha Majuda cha kuzika zitupu.
41 Basi palikuwa na bustani karibu na mahali pale aliposulubiwa, na pale ndani ya ile bustani palikuwa na kaburi jipya, ambalo halikuwa limezikiwa mtu bado.
Linu muchibaka umo mwa ba kankamizwe, kubena luwa lwa zibyalantu; mi mwelyo iwa lya zi byalantu ku bena ikumbu ihya umo musena mu beni ku ungwa muntu kale.
42 Kwa hiyo, kwa kuwa ilikuwa siku ya Wayahudi ya Maandalio, nalo kaburi hilo lilikuwa karibu, wakamzika Yesu humo.
Kakuti i ba li izuba lye intukiso za Majuda mi ni kuti ikumbu li bena hafuhi, ni ba lazika Jesu mwa teni.