< Yohana 19 >

1 Ndipo Pilato akamtoa Yesu akaamuru apigwe mijeledi.
Acunüng, Pilat naw Jesuh cehpüi lü a kpaih.
2 Askari wakasokota taji ya miiba, wakamvika Yesu kichwani. Wakamvalisha joho la zambarau.
Yekape naw nghling lukhüm pyang u lü ami ngbüngsak. Acun käna, jih sennu ngvüihsak u lü,
3 Wakawa wanapanda pale alipo tena na tena, wakisema, “Salamu! Mfalme wa Wayahudi!” Huku wakimpiga makofi usoni.
a peia law u lü, “Judahea Sangpuxang, xüng soa” ti lü a hmai ami kbeih.
4 Pilato akatoka tena nje akawaambia wale waliokusanyika, “Tazameni, namkabidhi Yesu kwenu kuwajulisha kwamba mimi sikumwona ana hatia.”
Pilat naw lut law betü lü, “Teng u, thih vai awnga mkhyenak i pi am hmu nawng ti nami ksing vaia, nami veia ka lawpüi beki” a ti.
5 Kwa hiyo Yesu akatoka nje akiwa amevaa ile taji ya miiba na lile vazi la zambarau. Pilato akawaambia, “Tazameni, huyu hapa huyo mtu!”
Jesuh cun nghling lukhüm ngbüng lü jih sennu pi ngvaih lü kpunga lut lawki. Pilat naw, “Teng u, hina khyang” a ti.
6 Wale viongozi wa makuhani na maafisa walipomwona, wakapiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!” Pilato akawaambia, “Mchukueni ninyi mkamsulubishe, mimi sioni hatia juu yake.”
Ktaiyü ngvaie ja Temple ngänge naw ami hmu ja, “Kutlamktung üng taiha, kutlamktung üng taiha” ti lü ngpyangkie. Pilat naw, “Nangmi naw cehpüi u lü, kutlamktung üng taih ua; kei naw ta thih awng vai a mkhyenak am hmu veng” a ti.
7 Wayahudi wakamjibu, “Sisi tunayo sheria na kutokana na sheria hiyo, hana budi kufa kwa sababu yeye alijiita Mwana wa Mungu.”
Judahe naw, “Pamhnama Capaa mhnüneikia kyase, kami thuma tia kba, thi khaia nglawi ve” ti lü ami msang.
8 Pilato aliposikia haya, akaogopa zaidi.
Pilat naw acun a ngjak ja kyühei law dämdäm lü,
9 Akaingia tena ndani ya jumba la kifalme, akamuuliza Yesu, “Wewe umetoka wapi?” Lakini Yesu hakumjibu.
a Bawingawhnaka cit be lü, “Nang hawia ka naw na lawki ni?” a ti. Jesuh naw mkhap mat am pi am msang be.
10 Pilato akamwambia, “Wewe unakataa kuongea na mimi? Hujui ya kuwa nina mamlaka ya kukuachia huru au kukusulubisha?”
Pilat naw, “Am na na msang hlüki aw? Ning khyah be vai ja kutlamktung üng ning taih vai hin keia mkhyaha kya khai, ti cun ksinga” a ti.
11 Ndipo Yesu akamwambia, “Wewe hungekuwa na mamlaka yoyote juu yangu kama hungepewa kutoka juu. Kwa hiyo yeye aliyenitia mikononi mwako ana hatia ya dhambi iliyo kubwa zaidi.”
Jesuh naw, “Pamhnam naw a ning pet pänga phäh däk ni, ka khana khyaibahnak na tak ve. Acunakyase, kei hin na veia ning msum lawki cen mkhyekatnak akdäm bawk pawhki ni” a ti.
12 Tangu wakati huo, Pilato akajitahidi kutafuta njia ya kumfungua Yesu, lakini Wayahudi wakazidi kupiga kelele wakisema, “Ukimwachia huyu mtu, wewe si rafiki wa Kaisari. Mtu yeyote anayedai kuwa mfalme anampinga Kaisari.”
Pilat naw acun a ngjak üngkhyüh Jesuh a mhlät vaia lam suiki. Acunsepi Judahe naw ngpyang u lü, “Hina khyang na mhlät üng Emperoa püia käh na kya khai. Sangpuxanga mhnüneiki naküt cun Emperoa yee ni” ami ti.
13 Pilato aliposikia maneno haya akamtoa Yesu nje tena akaketi katika kiti chake cha hukumu, mahali palipoitwa Sakafu ya Jiwe, kwa Kiebrania paliitwa Gabatha
Pilat naw acun a ngjak ja Jesuh luh lawpüi lü, Hebru läk am Kabbata ami ti Ngthumkhyahnak Lungsüma khana ngawki.
14 Basi ilikuwa siku ya Maandalio ya Pasaka, yapata kama saa sita hivi. Pilato akawaambia Wayahudi, “Huyu hapa mfalme wenu!”
Acuna mhnüp cun Lätnak Pawi am a pha ham mhnüp mat a hlüa mhnüpa; mhnüp ngsunga kyase, Pilat naw Judahea veia, “Teng u, nami sangpuxang” a ti.
15 Wao wakapiga kelele, “Mwondoe! Mwondoe! Msulubishe!” Pilato akawauliza, “Je, nimsulubishe mfalme wenu?” Wale viongozi wa makuhani wakamjibu, “Sisi hatuna mfalme mwingine ila Kaisari.”
Amimi naw ngpyang u lü, “Hnima, hnima, mkhyüha, kutlamktung üng taiha” ami ti. Pilat naw, “Nami sangpuxang, kutlamktung üng ka taih vai nami hlüeiki aw?” a ti. Ktaiyü ngvaie naw, “Emperoa thea sangpuxang akce am ta u nawng” ti lü, ami msang.
16 Ndipo Pilato akamkabidhi Yesu kwao ili wamsulubishe. Kwa hiyo askari wakamchukua Yesu.
Acunüng, Pilat naw Jesuh cun kutlamktung üng taih vaia a jah msum. Jesuh cun ami cehpüi.
17 Yesu, akiwa ameubeba msalaba wake, akatoka kuelekea mahali palipoitwa Fuvu la Kichwa (kwa Kiebrania ni Golgotha).
Jesuh naw amäta phäha kutlamktung kawt lü ‘Luyuh Hnün’ ami ti, Hebru läk am Kolkothaa citki.
18 Hapo ndipo walipomsulubisha. Pamoja naye walisulubisha watu wengine wawili, mmoja kila upande wake, naye Yesu katikati.
Acuia kutlamktung üng khyang nghngih am ami jah taih yüm. A peia mat cim jah taih u lü Jesuh anglung üng ami taih.
19 Pilato akaamuru tangazo liandikwe na liwekwe juu kwenye msalaba wa Yesu, likasema: “Yesu wa Nazareti, Mfalme wa Wayahudi.”
Pilat naw, “Nazaret Jesuh, Judahea Sangpuxang” ti lü kca yuk lü kutlamktung khana a taih.
20 Kwa kuwa mahali hapo Yesu aliposulubiwa palikuwa karibu na mjini, Wayahudi wengi walisoma maandishi haya yaliyokuwa yameandikwa kwa lugha za Kiebrania, Kiyunani na Kilatini.
Jesuh kutlamktung üng ami taihnaka hnün cun Jerusalem mlüha peia kyaki. Acuna kca cun Hebru, Latin ja Krik läke üng ami yuka kyase Judah khyang khawhah naw khekie.
21 Viongozi wa makuhani wa Wayahudi wakapinga, wakamwambia Pilato, “Usiandike ‘Mfalme wa Wayahudi,’ bali andika kwamba mtu huyu alisema yeye ni mfalme wa Wayahudi.”
Ktaiyü ngvaie naw Pilat aw, “Judahea Sangpuxang” ti lü käh yuka, “Kei, Judahea Sangpuxang ni, ti ve” ti lü yuka’” ami ti.
22 Pilato akawajibu, “Nilichokwisha kuandika, nimeandika!”
Pilat naw, “Ka yuk päng cen ka yuka kba ve se” ti lü a jah msang.
23 Askari walipokwisha kumsulubisha Yesu, walichukua nguo zake wakazigawa mafungu manne, kila askari fungu lake. Ila walikubaliana wasilichane lile vazi lake kwa maana lilikuwa halina mshono bali limefumwa tangu juu hadi chini.
Yekape naw kutlamktung khana Jesuh ami taih päng üng a suisake jah lo u lü, kphyüa ktek u lü mat cima ami ng’yatei. Ak’uma a phyang jih cun am xüi u, alu üngka naw ale cäpa taha kyaki.
24 Wakaambiana, “Tusilichane ila tulipigie kura ili kuamua ni nani atalichukua.” Hili lilitukia ili Maandiko yapate kutimizwa yale yaliyosema, “Wanagawana nguo zangu, na vazi langu wanalipigia kura.” Hayo ndiyo waliyoyafanya wale askari.
Yekape naw, “Käh mi ktek vai, u naw a bi vai cungkek mi kphawng vai u” ami ti. Acun cun Pamhnama cangcim üng, “Ka suisake jah ng’yetei u lü, ka kcu nglünglawknak khaie ni” ti a küm lawnak vaia kyaki. Acun cun yekape naw ami pawha kyaki.
25 Wakati huo huo karibu na msalaba wa Yesu walikuwa wamesimama mama yake, na dada wa mamaye, na Maria mke wa Klopa, na Maria Magdalene.
Jesuha kutlamktung peia, Jesuha nu ja Kalawphaa a khyu Marih ja Marih Makdalin ngdüikie.
26 Yesu alipomwona mama yake mahali pale pamoja na yule mwanafunzi aliyempenda wamesimama karibu, akamwambia mama yake, “Mwanamke, huyo hapo ndiye mwanao,”
Jesuh naw a nu ja a kphyanak axüisaw a peia ngdüi ni se jah hmu lü, a nu üng, “Na capa ta ani ni” a ti.
27 kisha akamwambia yule mwanafunzi, “Nawe huyo hapo ndiye mama yako.” Tangu wakati huo yule mwanafunzi akamchukua mama yake Yesu nyumbani kwake.
Axüisaw üng, “Ani ni na nu” a ti. Acunüng tün lü, acuna axüisaw naw Jesuha nu cun a ima a cehpüi.
28 Baada ya haya, Yesu hali akijua kuwa mambo yote yamemalizika, alisema ili kutimiza Maandiko, “Naona kiu.”
Acunkäna, atuh ta ahmäi naküt kümcei pängki ti Jesuh naw ksing lü, cangcima kümnak vaia, “Tui cawi veng” a ti.
29 Hapo palikuwa na bakuli lililojaa siki. Kwa hiyo wakachovya sifongo kwenye hiyo siki, wakaiweka kwenye ufito wa mti wa hisopo, wakampelekea mdomoni.
Acuia Capyitui kpaih k’am mat ami tak. Hisop Capyitui k'am üng kphum lü cung üng taihkie naw a mpyawng üng ami jeng sun.
30 Baada ya kuionja hiyo siki, Yesu akasema, “Imekwisha.” Akainamisha kichwa chake, akaitoa roho yake.
Jesuh naw Capyitui kpaih a awk päng ja “Ngpäng ve” a ti. Acunüng, a ngmüm üng a sak päihki.
31 Kwa kuwa ilikuwa siku ya Maandalio ya Pasaka, Wayahudi hawakutaka miili ibaki msalabani siku ya Sabato, hasa kwa kuwa hiyo Sabato ingekuwa Sikukuu. Wakamwomba Pilato aamuru miguu ya wale waliosulubiwa ivunjwe ili wafe haraka miili iondolewe kwenye misalaba.
Judah ngvaie naw kutlamktung üng ami taiha khaw jah k'ek lü, ami yawke ami jah khyak vaia Pilat ami kthäh. Isenitiüng, acuna mhnüp cun Amhma mhnüpa kyaki. Angawi Sabbath mhnüp (Lawkia Sabbath mhnüp cun Judahea thuma aktäa ngcingcaihkia mhnüpa kyaki) üng ami yawke kutlamktung üng a ngtaihei vai am jum u.
32 Kwa hiyo askari wakaenda wakavunja miguu ya mtu wa kwanza aliyesulubiwa pamoja na Yesu na yule mwingine pia.
Yekape law u lü Jesuh am atänga ami jah taih yüm xawia ani khawe cun ami jah k’ek.
33 Lakini walipomkaribia Yesu, wakaona ya kuwa amekwisha kufa, hivyo hawakuvunja miguu yake.
Acunsepi, Jesuha veia ami law üng, Jesuh thi pängki ti ksing u lü a khawe am jah k’ek u.
34 Badala yake mmoja wa wale askari akamchoma mkuki ubavuni na mara pakatoka damu na maji.
Acunsepi yekape üngka mat naw Jesuha kpem kcei am a sun. Acunüng thi ja tui ngsawi law yümki xawi. (
35 Mtu aliyeona mambo hayo ndiye alitoa ushuhuda, nao ushuhuda wake ni kweli. Anajua kuwa anasema kweli, naye anashuhudia ili pia nanyi mpate kuamini.
Hmuki mat naw pyen lü ngsingsak pängki. A ngsingsak pi cangki. Nami jum vaia a ngthu pyen cangki ti pi ani naw ksing lawki.)
36 Kwa maana mambo haya yalitukia ili Maandiko yapate kutimia, yale yasemayo, “Hakuna hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa.”
Acun cun, “A yuh mat pi käh ek khai” ti lü, Cangcima a küm lawnak vaia kyaki.
37 Tena Andiko lingine lasema, “Watamtazama yeye waliyemchoma.”
Acuna thea cangcim naw, “Khyange naw kcei am a kpem ami sun cun hmu khaie” pi Cangcim naw ti hamki.
38 Baada ya mambo haya, Yosefu wa Arimathaya, aliyekuwa mfuasi wa Yesu, ingawa kwa siri kwa sababu ya kuwaogopa Wayahudi, alimwomba Pilato ruhusa ili kuuchukua mwili wa Yesu. Pilato alimruhusu, hivyo akaja, akauchukua.
Acunkäna Arimahte mlüha ka Josep, Jesuha axüisaw, acunsepi Judah ngvaie a jah kyüha phäh, ampyua veki. Ani naw Jesuha yawk a cehpüi vaia Pilat kthäh se, Pilat naw a khyah. Josep naw law lü Jesuha a yawk cun a cehpüi.
39 Naye Nikodemo, yule ambaye kwanza alimwendea Yesu usiku, akaja, akaleta mchanganyiko wa manemane na manukato, yenye uzito wa zaidi ya kilo thelathini
Ahlana mthana Jesuha veia lawkia Nikawdim naw mura ng'ui ja aloe jah kcaw, khin mku bang cehpüi lü Josep am citki xawi.
40 Wakauchukua mwili wa Yesu, wakaufunga katika sanda ya kitani safi pamoja na yale manukato, kama ilivyokuwa desturi ya Wayahudi.
Jesuha yawk cun lo ni lü Judahea ami ng’utei khawia thuma, mura ng’ui ja jih am ani hlawp.
41 Basi palikuwa na bustani karibu na mahali pale aliposulubiwa, na pale ndani ya ile bustani palikuwa na kaburi jipya, ambalo halikuwa limezikiwa mtu bado.
Kutlamktung üng ami taihnaka peia ngvawng mat veki. Acuna ngvawng üng u pi am ami k’utnak khawia lungdü kthai mat veki.
42 Kwa hiyo, kwa kuwa ilikuwa siku ya Wayahudi ya Maandalio, nalo kaburi hilo lilikuwa karibu, wakamzika Yesu humo.
Angawi cun Judahea Sabbath mhnüpa kya lü, lungdü ng'etkia kyase, acun üng Jesuh ami k’ut.

< Yohana 19 >