< Yohana 18 >

1 Yesu alipomaliza kuomba, akaondoka na wanafunzi wake wakavuka Bonde la Kidroni. Upande wa pili palikuwa na bustani, yeye na wanafunzi wake wakaingia humo.
Се промовивши Ісус, вийшов з учениками своїми за потік Кедрон, де був сад, у котрий ввійшов Він і ученики Його.
2 Basi Yuda, yule aliyemsaliti alipafahamu mahali hapo kwani Yesu alikuwa akikutana humo na wanafunzi wake mara kwa mara.
Знав же й Юда, що зрадив Його, се місце, бо почасту збирались там Ісус і ученики Його.
3 Hivyo Yuda akaja bustanini. Aliongoza kikosi cha askari wa Kirumi, na baadhi ya maafisa kutoka kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo. Nao walikuwa wamechukua taa, mienge na silaha.
Тодї Юда, взявши роту та архиєрейських і Фарисейських слуг, приходить туди з лихтарнями, та факлями [смолоскипами], та з зброєю.
4 Yesu akijua yale yote yatakayompata, akajitokeza mbele yao akawauliza, “Mnamtafuta nani?”
Знаючи ж Ісус усе, що настигає на Него, вийшов і рече Їм: Кого шукаєте?
5 Wao wakamjibu, “Yesu wa Nazareti.” Yesu akawajibu, “Mimi ndiye.” Yuda, yule aliyemsaliti alikuwa amesimama pamoja nao.
Відказали Йому: Ісуса Назорея. Рече їм Ісус: Се я. Стояв же й Юда зрадник Його, з ними.
6 Yesu alipowaambia, “Mimi ndiye,” walirudi nyuma na kuanguka chini!
Як же сказав їм: Що се я, відступили вони назад, та й попадали на землю.
7 Akawauliza tena, “Mnamtafuta nani?” Nao wakamjibu, “Yesu wa Nazareti.”
Знов же спитав їх: Кого шукаєте? Вони ж сказали: Ісуса Назорея.
8 Yesu akawaambia, “Nimekwisha kuwaambia kuwa, mimi ndiye; kwa hiyo kama mnanitafuta mimi, waacheni hawa watu waende zao.”
Відказав Ісус: Сказав вам, що се я. Коли ж мене шукаєте, дайте сим відійти.
9 Hii ilikuwa ili litimie lile neno alilosema, “Sikumpoteza hata mmoja miongoni mwa wale ulionipa.”
Щоб справдилось слово, що промовив: Що которих дав єси менї, не вгубив я з них нїкого.
10 Simoni Petro, aliyekuwa na upanga, akaufuta na kumkata sikio la kuume mtumishi wa kuhani mkuu. Jina la mtumishi huyo aliitwa Malko.
Тодї Симон Петр, маючи меч, вийняв його, і вдарив слугу архиєрейського, та й відтяв йому ухо праве. Було ж імя слузї Малх.
11 Yesu akamwambia Petro, “Rudisha upanga wako kwenye ala yake. Je, hainipasi kukinywea kikombe alichonipa Baba?”
Рече тодї Ісус Петрови: Вкинь меч твій у похву. Чашу, що дав менї Отець, хиба не пити її?
12 Hivyo wale askari, wakiwa pamoja na majemadari wao na maafisa wa Wayahudi, wakamkamata Yesu na kumfunga.
Тодї рота, й тисячник, і слуги Жидівські схопили Ісуса, та й звязали Його,
13 Kwanza wakampeleka kwa Anasi, mkwewe Kayafa, aliyekuwa kuhani mkuu mwaka ule.
і повели Його перш до Анни, був бо тестем Каяфі, що був архиєреем того року.
14 Kayafa ndiye alikuwa amewashauri Wayahudi kwamba imempasa mtu mmoja kufa kwa ajili ya watu.
Був же Каяфа той, що порадив Жидам, що лучче нехай один чоловік умре за людей.
15 Simoni Petro pamoja na mwanafunzi mwingine walikuwa wakimfuata Yesu. Huyu mwanafunzi mwingine alikuwa anafahamika kwa kuhani mkuu, hivyo aliingia ndani ya ukumbi pamoja na Yesu.
Пійшов же слїдом за Ісусом Симон Петр та ще другий ученик. Той же ученик був знаний архиєреві, і прийшов з Ісусом у двір архиєрейський.
16 Lakini Petro alisimama nje karibu na lango, ndipo yule mwanafunzi mwingine, aliyejulikana na kuhani mkuu, akazungumza na msichana aliyekuwa analinda lango, akamruhusu Petro aingie ndani.
Петр же стояв перед дверми знадвору. Вийшов тодї другий ученик, що був знаний архиєреві, і сказав дверницї, і ввела Петра.
17 Yule msichana akamuuliza Petro, “Je, wewe pia si mmoja wa wanafunzi wa mtu huyu?” Petro akajibu, “Sio mimi.”
Каже тодї слуга двернипя Петрові: Чи й ти єси з учеників чоловіка сього? Каже той: Нї.
18 Wale watumishi na askari walikuwa wamesimama wakiota moto wa makaa kwa sababu palikuwa na baridi, Petro naye alikuwa amesimama pamoja nao akiota moto.
Стояли ж раби й слуги, що розложили огонь; холодно бо було, та й грілись. Стояв з ними й Петр, і грів ся.
19 Wakati huo kuhani mkuu akawa anamuuliza Yesu kuhusu wanafunzi wake na mafundisho yake.
Тодї архиєрей спитав Ісуса про учеників Його й про науку Його.
20 Yesu akamjibu, “Nimekuwa nikizungumza waziwazi mbele ya watu wote. Siku zote nimefundisha katika masinagogi na Hekaluni, mahali ambapo Wayahudi wote hukusanyika. Sikusema jambo lolote kwa siri.
Відказав йому Ісус: Я глаголав ясно сьвітові; я завсїди учив у школї і в церкві, куди Жиди завсїди сходять ся, і потай не глаголав нїчого.
21 Mbona unaniuliza mimi maswali? Waulize wale walionisikia yale niliyowaambia. Wao wanajua niliyosema.”
Чого мене питаєш? Спитай тих, Що слухали, що я глаголав їм; ось вони знають, що я казав
22 Alipomaliza kusema hayo, mmoja wa askari aliyekuwa amesimama karibu naye, akampiga Yesu kofi usoni, kisha akasema, “Je, hivyo ndivyo unavyomjibu kuhani mkuu?”
Як же Він де промовив, один із слуг, стоячи тут, ударив у лице Ісуса, кажучи: Так відказуєш архиєреві?
23 Yesu akamjibu akasema, “Kama nimesema jambo baya, shuhudia huo ubaya niliousema. Lakini kama nimesema yaliyo kweli, mbona umenipiga?”
Відказав йому Ісус: Коли недобре сказав я, сьвідкуй про недобре; коли добре, за що мене бєш?
24 Ndipo Anasi akampeleka Yesu kwa kuhani mkuu Kayafa, akiwa bado amefungwa.
Післав Його Анна звязаного до Каяфи архиєрея.
25 Wakati huo Simoni Petro alikuwa amesimama akiota moto. Baadhi ya wale waliokuwepo wakamuuliza, “Je, wewe si mmoja wa wanafunzi wake?” Petro akakana, akasema, “Sio mimi.”
Симон же Петр стояв та грів ся. Кажуть тодї йому: Чи й ти з Його учеників? Він же відрік ся і сказав: Нї.
26 Mmoja wa watumishi wa kuhani mkuu, ndugu yake yule mtu ambaye Petro alikuwa amemkata sikio, akamuuliza, “Je, mimi sikukuona kule bustanini ukiwa na Yesu?”
Каже один із слуг архиєрейських, свояк того, котрому відтяв Петр ухо: Чи ж не бачив я тебе в саду з Ним?
27 Kwa mara nyingine tena Petro akakana, naye jogoo akawika wakati huo huo.
Знов тодї відрік ся Петр, і зараз пївень запіяв.
28 Ndipo Wayahudi wakamchukua Yesu kutoka kwa Kayafa na kumpeleka kwenye jumba la kifalme la mtawala wa Kirumi. Wakati huo ilikuwa ni alfajiri, ili kuepuka kuwa najisi kwa taratibu za ibada, Wayahudi hawakuingia ndani kwa sababu ya sheria za Kiyahudi. Wangehesabiwa kuwa najisi kama wangeingia nyumbani mwa mtu asiye Myahudi na wasingeruhusiwa kushiriki katika Sikukuu ya Pasaka.
Ведуть тодї Ісуса від Каяфи у претор; був же ранок; і не ввійшли вони в претор, щоб не опоганитись та щоб їсти їм пасху.
29 Hivyo Pilato akatoka nje walikokuwa akawauliza, “Mmeleta mashtaka gani kumhusu mtu huyu?”
Вийшов тодї Пилат до них, і каже: Яку вину приносите на чоловіка сього?
30 Wao wakamjibu, “Kama huyu mtu hakuwa mhalifu tusingemleta kwako.”
Озвались і казали йому: Коли б Він не був лиходій, не віддавали б ми Його тобі.
31 Pilato akawaambia, “Basi mchukueni ninyi mkamhukumu kwa kufuata sheria zenu.” Wayahudi wakamjibu, “Sisi haturuhusiwi kutoa hukumu ya kifo kwa mtu yeyote.”
Каже тодї їм Пилат: Візьміть ви Його й по закону вашому осудїть Його. Сказали тодї йому Жиди: Нам не годить ся вбивати нїкого.
32 Walisema hivyo ili yale maneno aliyosema Yesu kuhusu kifo atakachokufa yapate kutimia.
Щоб Ісусове слово справдилось, що промовив, означуючи, якою смертю має вмерти.
33 Kwa hiyo Pilato akaingia ndani ya jumba la kifalme, akamwita Yesu, akamuuliza, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?”
Увійшов тодї знов Пилат у претор, і покликав Ісуса, і каже Йому: Ти єси цар Жидівський?
34 Yesu akamjibu, “Je, unauliza swali hili kutokana na mawazo yako mwenyewe, au uliambiwa na watu kunihusu mimi?”
Відказав йому Ісус: Від себе ти се говориш, чи инші тобі сказали про мене?
35 Pilato akamjibu, “Mimi si Myahudi, ama sivyo? Taifa lako mwenyewe na viongozi wa makuhani wamekukabidhi kwangu. Umefanya kosa gani?”
Озвавсь Пилат: Хиба я Жид? Нарід Твій і архиєреї видали менї Тебе. Що зробив єси?
36 Yesu akajibu, “Ufalme wangu si wa ulimwengu huu. Ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, wafuasi wangu wangenipigania ili nisitiwe mikononi mwa Wayahudi. Lakini kama ilivyo, ufalme wangu hautoki hapa ulimwenguni.”
Відказав Ісус: Царство моє не од сьвіта сього. Коли б од cьвіта сього було царство моє, слуги мої воювали б, щоб не видано мене Жидам; тільки ж царство моє не звідсїля.
37 Pilato akamuuliza, “Kwa hiyo wewe ni mfalme?” Yesu akajibu, “Wewe wasema kwamba mimi ni mfalme. Kwa kusudi hili nilizaliwa, na kwa ajili ya hili nilikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Mtu yeyote aliye wa kweli husikia sauti yangu.”
Рече тоді Йому Пилат: Так Ти цар? Відказав Ісус: Ти кажеш, що цар я. Я на се родивсь і на се прийшов у сьвіт, щоб сьвідкувати правдї. Кожен, хто від правди, слухає мого голосу.
38 Pilato akamuuliza Yesu, “Kweli ni nini?” Baada ya kusema haya Pilato akaenda nje tena akawaambia wale viongozi wa Wayahudi waliomshtaki Yesu, “Sioni kosa lolote alilotenda mtu huyu.
Каже Йому Пилат: Що таке правда? І, се сказавши, знов вийшов до Жидів, і каже їм: Нїякої вини не знаходжу я в Йому.
39 Lakini ninyi mna desturi yenu kwamba wakati wa Pasaka nimwachie huru mfungwa mmoja mnayemtaka. Je, mnataka niwafungulie huyu ‘Mfalme wa Wayahudi’?”
Єсть же звичай у вас, щоб одного вам відпускав я на пасху. Хочете ж, щоб випустив вам царя Жидівського.
40 Wao wakapiga kelele wakisema, “Si huyu mtu, bali tufungulie Baraba!” Yule Baraba alikuwa mnyangʼanyi.
Закричали тоді вони всї знов, кажучи: Не Сього, а Вараву. Був же Варава розбійник.

< Yohana 18 >