< Yohana 18 >
1 Yesu alipomaliza kuomba, akaondoka na wanafunzi wake wakavuka Bonde la Kidroni. Upande wa pili palikuwa na bustani, yeye na wanafunzi wake wakaingia humo.
tAH kathAH kathayitvA yIshuH shiShyAnAdAya kidronnAmakaM srota uttIryya shiShyaiH saha tatratyodyAnaM prAvishat|
2 Basi Yuda, yule aliyemsaliti alipafahamu mahali hapo kwani Yesu alikuwa akikutana humo na wanafunzi wake mara kwa mara.
kintu vishvAsaghAtiyihUdAstat sthAnaM parichIyate yato yIshuH shiShyaiH sArddhaM kadAchit tat sthAnam agachChat|
3 Hivyo Yuda akaja bustanini. Aliongoza kikosi cha askari wa Kirumi, na baadhi ya maafisa kutoka kwa viongozi wa makuhani na Mafarisayo. Nao walikuwa wamechukua taa, mienge na silaha.
tadA sa yihUdAH sainyagaNaM pradhAnayAjakAnAM phirUshinA ncha padAtigaNa ncha gR^ihItvA pradIpAn ulkAn astrANi chAdAya tasmin sthAna upasthitavAn|
4 Yesu akijua yale yote yatakayompata, akajitokeza mbele yao akawauliza, “Mnamtafuta nani?”
svaM prati yad ghaTiShyate taj j nAtvA yIshuragresaraH san tAnapR^ichChat kaM gaveShayatha?
5 Wao wakamjibu, “Yesu wa Nazareti.” Yesu akawajibu, “Mimi ndiye.” Yuda, yule aliyemsaliti alikuwa amesimama pamoja nao.
te pratyavadan, nAsaratIyaM yIshuM; tato yIshuravAdId ahameva saH; taiH saha vishvAsaghAtI yihUdAshchAtiShThat|
6 Yesu alipowaambia, “Mimi ndiye,” walirudi nyuma na kuanguka chini!
tadAhameva sa tasyaitAM kathAM shrutvaiva te pashchAdetya bhUmau patitAH|
7 Akawauliza tena, “Mnamtafuta nani?” Nao wakamjibu, “Yesu wa Nazareti.”
tato yIshuH punarapi pR^iShThavAn kaM gaveShayatha? tataste pratyavadan nAsaratIyaM yIshuM|
8 Yesu akawaambia, “Nimekwisha kuwaambia kuwa, mimi ndiye; kwa hiyo kama mnanitafuta mimi, waacheni hawa watu waende zao.”
tadA yIshuH pratyuditavAn ahameva sa imAM kathAmachakatham; yadi mAmanvichChatha tarhImAn gantuM mA vArayata|
9 Hii ilikuwa ili litimie lile neno alilosema, “Sikumpoteza hata mmoja miongoni mwa wale ulionipa.”
itthaM bhUte mahyaM yAllokAn adadAsteShAm ekamapi nAhArayam imAM yAM kathAM sa svayamakathayat sA kathA saphalA jAtA|
10 Simoni Petro, aliyekuwa na upanga, akaufuta na kumkata sikio la kuume mtumishi wa kuhani mkuu. Jina la mtumishi huyo aliitwa Malko.
tadA shimonpitarasya nikaTe kha NgalsthiteH sa taM niShkoShaM kR^itvA mahAyAjakasya mAlkhanAmAnaM dAsam Ahatya tasya dakShiNakarNaM ChinnavAn|
11 Yesu akamwambia Petro, “Rudisha upanga wako kwenye ala yake. Je, hainipasi kukinywea kikombe alichonipa Baba?”
tato yIshuH pitaram avadat, kha NgaM koShe sthApaya mama pitA mahyaM pAtuM yaM kaMsam adadAt tenAhaM kiM na pAsyAmi?
12 Hivyo wale askari, wakiwa pamoja na majemadari wao na maafisa wa Wayahudi, wakamkamata Yesu na kumfunga.
tadA sainyagaNaH senApati ryihUdIyAnAM padAtayashcha yIshuM ghR^itvA baddhvA hAnannAmnaH kiyaphAH shvashurasya samIpaM prathamam anayan|
13 Kwanza wakampeleka kwa Anasi, mkwewe Kayafa, aliyekuwa kuhani mkuu mwaka ule.
sa kiyaphAstasmin vatsare mahAyAjatvapade niyuktaH
14 Kayafa ndiye alikuwa amewashauri Wayahudi kwamba imempasa mtu mmoja kufa kwa ajili ya watu.
san sAdhAraNalokAnAM ma NgalArtham ekajanasya maraNamuchitam iti yihUdIyaiH sArddham amantrayat|
15 Simoni Petro pamoja na mwanafunzi mwingine walikuwa wakimfuata Yesu. Huyu mwanafunzi mwingine alikuwa anafahamika kwa kuhani mkuu, hivyo aliingia ndani ya ukumbi pamoja na Yesu.
tadA shimonpitaro. anyaikashiShyashcha yIshoH pashchAd agachChatAM tasyAnyashiShyasya mahAyAjakena parichitatvAt sa yIshunA saha mahAyAjakasyATTAlikAM prAvishat|
16 Lakini Petro alisimama nje karibu na lango, ndipo yule mwanafunzi mwingine, aliyejulikana na kuhani mkuu, akazungumza na msichana aliyekuwa analinda lango, akamruhusu Petro aingie ndani.
kintu pitaro bahirdvArasya samIpe. atiShThad ataeva mahAyAjakena parichitaH sa shiShyaH punarbahirgatvA dauvAyikAyai kathayitvA pitaram abhyantaram Anayat|
17 Yule msichana akamuuliza Petro, “Je, wewe pia si mmoja wa wanafunzi wa mtu huyu?” Petro akajibu, “Sio mimi.”
tadA sa dvArarakShikA pitaram avadat tvaM kiM na tasya mAnavasya shiShyaH? tataH sovadad ahaM na bhavAmi|
18 Wale watumishi na askari walikuwa wamesimama wakiota moto wa makaa kwa sababu palikuwa na baridi, Petro naye alikuwa amesimama pamoja nao akiota moto.
tataH paraM yatsthAne dAsAH padAtayashcha shItahetora NgArai rvahniM prajvAlya tApaM sevitavantastatsthAne pitarastiShThan taiH saha vahnitApaM sevitum Arabhata|
19 Wakati huo kuhani mkuu akawa anamuuliza Yesu kuhusu wanafunzi wake na mafundisho yake.
tadA shiShyeShUpadeshe cha mahAyAjakena yIshuH pR^iShTaH
20 Yesu akamjibu, “Nimekuwa nikizungumza waziwazi mbele ya watu wote. Siku zote nimefundisha katika masinagogi na Hekaluni, mahali ambapo Wayahudi wote hukusanyika. Sikusema jambo lolote kwa siri.
san pratyuktavAn sarvvalokAnAM samakShaM kathAmakathayaM guptaM kAmapi kathAM na kathayitvA yat sthAnaM yihUdIyAH satataM gachChanti tatra bhajanagehe mandire chAshikShayaM|
21 Mbona unaniuliza mimi maswali? Waulize wale walionisikia yale niliyowaambia. Wao wanajua niliyosema.”
mattaH kutaH pR^ichChasi? ye janA madupadesham ashR^iNvan tAneva pR^ichCha yadyad avadaM te tat jAninta|
22 Alipomaliza kusema hayo, mmoja wa askari aliyekuwa amesimama karibu naye, akampiga Yesu kofi usoni, kisha akasema, “Je, hivyo ndivyo unavyomjibu kuhani mkuu?”
tadetthaM pratyuditatvAt nikaTasthapadAti ryIshuM chapeTenAhatya vyAharat mahAyAjakam evaM prativadasi?
23 Yesu akamjibu akasema, “Kama nimesema jambo baya, shuhudia huo ubaya niliousema. Lakini kama nimesema yaliyo kweli, mbona umenipiga?”
tato yIshuH pratigaditavAn yadyayathArtham achakathaM tarhi tasyAyathArthasya pramANaM dehi, kintu yadi yathArthaM tarhi kuto heto rmAm atADayaH?
24 Ndipo Anasi akampeleka Yesu kwa kuhani mkuu Kayafa, akiwa bado amefungwa.
pUrvvaM hAnan sabandhanaM taM kiyaphAmahAyAjakasya samIpaM praiShayat|
25 Wakati huo Simoni Petro alikuwa amesimama akiota moto. Baadhi ya wale waliokuwepo wakamuuliza, “Je, wewe si mmoja wa wanafunzi wake?” Petro akakana, akasema, “Sio mimi.”
shimonpitarastiShThan vahnitApaM sevate, etasmin samaye kiyantastam apR^ichChan tvaM kim etasya janasya shiShyo na? tataH sopahnutyAbravId ahaM na bhavAmi|
26 Mmoja wa watumishi wa kuhani mkuu, ndugu yake yule mtu ambaye Petro alikuwa amemkata sikio, akamuuliza, “Je, mimi sikukuona kule bustanini ukiwa na Yesu?”
tadA mahAyAjakasya yasya dAsasya pitaraH karNamachChinat tasya kuTumbaH pratyuditavAn udyAne tena saha tiShThantaM tvAM kiM nApashyaM?
27 Kwa mara nyingine tena Petro akakana, naye jogoo akawika wakati huo huo.
kintu pitaraH punarapahnutya kathitavAn; tadAnIM kukkuTo. araut|
28 Ndipo Wayahudi wakamchukua Yesu kutoka kwa Kayafa na kumpeleka kwenye jumba la kifalme la mtawala wa Kirumi. Wakati huo ilikuwa ni alfajiri, ili kuepuka kuwa najisi kwa taratibu za ibada, Wayahudi hawakuingia ndani kwa sababu ya sheria za Kiyahudi. Wangehesabiwa kuwa najisi kama wangeingia nyumbani mwa mtu asiye Myahudi na wasingeruhusiwa kushiriki katika Sikukuu ya Pasaka.
tadanantaraM pratyUShe te kiyaphAgR^ihAd adhipate rgR^ihaM yIshum anayan kintu yasmin ashuchitve jAte tai rnistArotsave na bhoktavyaM, tasya bhayAd yihUdIyAstadgR^ihaM nAvishan|
29 Hivyo Pilato akatoka nje walikokuwa akawauliza, “Mmeleta mashtaka gani kumhusu mtu huyu?”
aparaM pIlAto bahirAgatya tAn pR^iShThavAn etasya manuShyasya kaM doShaM vadatha?
30 Wao wakamjibu, “Kama huyu mtu hakuwa mhalifu tusingemleta kwako.”
tadA te petyavadan duShkarmmakAriNi na sati bhavataH samIpe nainaM samArpayiShyAmaH|
31 Pilato akawaambia, “Basi mchukueni ninyi mkamhukumu kwa kufuata sheria zenu.” Wayahudi wakamjibu, “Sisi haturuhusiwi kutoa hukumu ya kifo kwa mtu yeyote.”
tataH pIlAto. avadad yUyamenaM gR^ihItvA sveShAM vyavasthayA vichArayata| tadA yihUdIyAH pratyavadan kasyApi manuShyasya prANadaNDaM karttuM nAsmAkam adhikAro. asti|
32 Walisema hivyo ili yale maneno aliyosema Yesu kuhusu kifo atakachokufa yapate kutimia.
evaM sati yIshuH svasya mR^ityau yAM kathAM kathitavAn sA saphalAbhavat|
33 Kwa hiyo Pilato akaingia ndani ya jumba la kifalme, akamwita Yesu, akamuuliza, “Wewe ndiye mfalme wa Wayahudi?”
tadanantaraM pIlAtaH punarapi tad rAjagR^ihaM gatvA yIshumAhUya pR^iShTavAn tvaM kiM yihUdIyAnAM rAjA?
34 Yesu akamjibu, “Je, unauliza swali hili kutokana na mawazo yako mwenyewe, au uliambiwa na watu kunihusu mimi?”
yIshuH pratyavadat tvam etAM kathAM svataH kathayasi kimanyaH kashchin mayi kathitavAn?
35 Pilato akamjibu, “Mimi si Myahudi, ama sivyo? Taifa lako mwenyewe na viongozi wa makuhani wamekukabidhi kwangu. Umefanya kosa gani?”
pIlAto. avadad ahaM kiM yihUdIyaH? tava svadeshIyA visheShataH pradhAnayAjakA mama nikaTe tvAM samArpayana, tvaM kiM kR^itavAn?
36 Yesu akajibu, “Ufalme wangu si wa ulimwengu huu. Ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, wafuasi wangu wangenipigania ili nisitiwe mikononi mwa Wayahudi. Lakini kama ilivyo, ufalme wangu hautoki hapa ulimwenguni.”
yIshuH pratyavadat mama rAjyam etajjagatsambandhIyaM na bhavati yadi mama rAjyaM jagatsambandhIyam abhaviShyat tarhi yihUdIyAnAM hasteShu yathA samarpito nAbhavaM tadarthaM mama sevakA ayotsyan kintu mama rAjyam aihikaM na|
37 Pilato akamuuliza, “Kwa hiyo wewe ni mfalme?” Yesu akajibu, “Wewe wasema kwamba mimi ni mfalme. Kwa kusudi hili nilizaliwa, na kwa ajili ya hili nilikuja ulimwenguni, ili niishuhudie kweli. Mtu yeyote aliye wa kweli husikia sauti yangu.”
tadA pIlAtaH kathitavAn, tarhi tvaM rAjA bhavasi? yIshuH pratyuktavAn tvaM satyaM kathayasi, rAjAhaM bhavAmi; satyatAyAM sAkShyaM dAtuM janiM gR^ihItvA jagatyasmin avatIrNavAn, tasmAt satyadharmmapakShapAtino mama kathAM shR^iNvanti|
38 Pilato akamuuliza Yesu, “Kweli ni nini?” Baada ya kusema haya Pilato akaenda nje tena akawaambia wale viongozi wa Wayahudi waliomshtaki Yesu, “Sioni kosa lolote alilotenda mtu huyu.
tadA satyaM kiM? etAM kathAM paShTvA pIlAtaH punarapi bahirgatvA yihUdIyAn abhAShata, ahaM tasya kamapyaparAdhaM na prApnomi|
39 Lakini ninyi mna desturi yenu kwamba wakati wa Pasaka nimwachie huru mfungwa mmoja mnayemtaka. Je, mnataka niwafungulie huyu ‘Mfalme wa Wayahudi’?”
nistArotsavasamaye yuShmAbhirabhiruchita eko jano mayA mochayitavya eShA yuShmAkaM rItirasti, ataeva yuShmAkaM nikaTe yihUdIyAnAM rAjAnaM kiM mochayAmi, yuShmAkam ichChA kA?
40 Wao wakapiga kelele wakisema, “Si huyu mtu, bali tufungulie Baraba!” Yule Baraba alikuwa mnyangʼanyi.
tadA te sarvve ruvanto vyAharan enaM mAnuShaM nahi barabbAM mochaya| kintu sa barabbA dasyurAsIt|