< Yohana 17 >

1 Baada ya Yesu kusema haya, alitazama kuelekea mbinguni akawaombea na kusema: “Baba, saa imewadia. Umtukuze Mwanao, ili Mwanao apate kukutukuza wewe.
To powiedziawszy, Jezus podniósł swoje oczy ku niebu i rzekł: Ojcze, nadeszła godzina. Uwielbij swego Syna, aby też twój Syn uwielbił ciebie;
2 Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa. (aiōnios g166)
Jak mu dałeś władzę nad wszelkim ciałem, aby dał życie wieczne tym wszystkim, których mu dałeś. (aiōnios g166)
3 Nao uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe uliye Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios g166)
A to jest życie wieczne, aby poznali ciebie, jedynego prawdziwego Boga i tego, którego posłałeś, Jezusa Chrystusa. (aiōnios g166)
4 Nimekutukuza wewe duniani kwa kuitimiza ile kazi uliyonipa niifanye.
Ja uwielbiłem ciebie na ziemi i dokończyłem dzieła, które mi dałeś do wykonania.
5 Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ulimwengu haujakuwepo.
A teraz ty, Ojcze, uwielbij mnie u siebie tą chwałą, którą miałem u ciebie, zanim powstał świat.
6 “Nimelidhihirisha jina lako kwa wale ulionipa kutoka ulimwengu. Walikuwa wako, nawe ukanipa mimi, nao wamelitii neno lako.
Objawiłem twoje imię ludziom, których mi dałeś ze świata. Twoimi byli i dałeś mi ich, a oni zachowali twoje słowa.
7 Sasa wamejua ya kuwa vyote ulivyonipa vimetoka kwako,
A teraz poznali, że wszystko, co mi dałeś, pochodzi od ciebie.
8 kwa kuwa maneno yale ulionipa nimewapa wao, nao wameyapokea na kujua kwamba kweli nimetoka kwako, nao wameamini kuwa wewe ulinituma.
Dałem im bowiem słowa, które mi dałeś, a oni [je] przyjęli i prawdziwie poznali, że wyszedłem od ciebie, i uwierzyli, że ty mnie posłałeś.
9 Ninawaombea wao. Mimi siuombei ulimwengu, bali nawaombea wale ulionipa kwa sababu wao ni wako.
Ja proszę za nimi. Nie proszę za światem, ale za tymi, których mi dałeś, bo są twoi.
10 Wote walio wangu ni wako na walio wako ni wangu, nami nimetukuzwa ndani yao.
I wszystko moje jest twoje, a twoje jest moje i jestem uwielbiony w nich.
11 Mimi sasa simo tena ulimwenguni, lakini wao bado wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa uweza wa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
A nie jestem już na świecie, ale oni są na świecie, a ja idę do ciebie. Ojcze święty, zachowaj w twoim imieniu tych, których mi dałeś, aby byli jedno jak i my.
12 Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda, wakawa salama kwa lile jina ulilonipa. Hakuna hata mmoja aliyepotea, isipokuwa yule aliyekusudiwa upotevu, ili Maandiko yapate kutimia.
Gdy byłem z nimi na świecie, ja zachowywałem ich w twoim imieniu. Strzegłem [tych], których mi dałeś, i żaden z nich nie zginął prócz syna zatracenia, żeby się wypełniło Pismo.
13 “Lakini sasa naja kwako, nami ninasema mambo haya wakati bado nikiwa ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu kamili ndani yao.
Ale teraz idę do ciebie i mówię to na świecie, aby mieli w sobie moją radość w pełni.
14 Nimewapa neno lako, nao ulimwengu umewachukia kwa kuwa wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa ulimwengu huu.
Ja dałem im twoje słowo, a świat ich znienawidził, bo nie są ze świata, jak [i] ja nie jestem ze świata.
15 Siombi kwamba uwaondoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya yule mwovu.
Nie proszę, abyś zabrał ich ze świata, ale abyś zachował ich od złego.
16 Wao si wa ulimwengu huu, kama vile mimi nisivyo wa ulimwengu.
Nie są ze świata, jak [i] ja nie jestem ze świata.
17 Uwatakase kwa ile kweli, neno lako ndilo kweli.
Uświęć ich w twojej prawdzie. Twoje słowo jest prawdą.
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami nawatuma vivyo hivyo.
Jak ty posłałeś mnie na świat, [tak] i ja posłałem ich na świat.
19 Kwa ajili yao najiweka wakfu ili wao nao wapate kutakaswa katika ile kweli.
A ja za nich uświęcam samego siebie, aby i oni byli uświęceni w prawdzie.
20 “Siwaombei hawa peke yao, bali nawaombea na wale wote watakaoniamini kupitia neno lao
A nie tylko za nimi proszę, lecz i za tymi, którzy przez ich słowo uwierzą we mnie;
21 ili wawe na umoja kama vile wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi nilivyo ndani yako, wao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini ya kuwa wewe ndiye uliyenituma mimi.
Aby wszyscy byli jedno, jak ty, Ojcze, we mnie, a ja w tobie, aby i oni byli w nas jedno, aby świat uwierzył, że ty mnie posłałeś.
22 Utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
I dałem im tę chwałę, którą mi dałeś, aby byli jedno, jak my jesteśmy jedno.
23 Mimi ndani yako na wewe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja na ulimwengu upate kujua ya kuwa umenituma, nami nimewapenda wao kama unavyonipenda mimi.
Ja w nich, a ty we mnie, aby byli doskonali w jedno, żeby świat poznał, że ty mnie posłałeś i że umiłowałeś ich, jak [i] mnie umiłowałeś.
24 “Baba, shauku yangu ni kwamba, wale ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili waweze kuuona utukufu wangu, yaani, utukufu ule ulionipa kwa kuwa ulinipenda hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
Ojcze, chcę, aby ci, których mi dałeś, byli ze mną tam, gdzie ja jestem, aby oglądali moją chwałę, którą mi dałeś, ponieważ umiłowałeś mnie przed założeniem świata.
25 “Baba Mwenye Haki, ingawa ulimwengu haukujui, mimi ninakujua, nao wanajua ya kuwa umenituma.
Ojcze sprawiedliwy, świat ciebie nie poznał, ale ja cię poznałem i oni poznali, że ty mnie posłałeś.
26 Nimefanya jina lako lijulikane kwao nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili kwamba upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”
Objawiłem im twoje imię i [jeszcze] objawię, aby miłość, którą mnie umiłowałeś, była w nich i ja w nich.

< Yohana 17 >