< Yohana 17 >

1 Baada ya Yesu kusema haya, alitazama kuelekea mbinguni akawaombea na kusema: “Baba, saa imewadia. Umtukuze Mwanao, ili Mwanao apate kukutukuza wewe.
בסיימו לדבר נשא ישוע את עיניו השמימה ואמר:”אבי, הגיעה השעה; פאר את בנך כדי שבנך יפאר אותך.
2 Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa. (aiōnios g166)
הרי נתת לו סמכות וכוח על כל בני־האדם, כדי שיעניק חיי עולם לכל מי שנתת לו. (aiōnios g166)
3 Nao uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe uliye Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios g166)
חיי עולם פירושם להכיר אותך, אלוהי האמת לבדו, ואת ישוע המשיח אשר שלחת. (aiōnios g166)
4 Nimekutukuza wewe duniani kwa kuitimiza ile kazi uliyonipa niifanye.
סיימתי את המשימה שהטלת עלי, וכך פארתי אותך על־פני הארץ.
5 Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ulimwengu haujakuwepo.
עתה, אבי, פאר אותי בכבוד שהיה לי איתך עוד לפני בריאת העולם.
6 “Nimelidhihirisha jina lako kwa wale ulionipa kutoka ulimwengu. Walikuwa wako, nawe ukanipa mimi, nao wamelitii neno lako.
”סיפרתי על אודותיך לכל האנשים שנתת לי בעולם. למעשה הם היו שלך תמיד; אתה נתת לי אותם והם שמעו בקולך.
7 Sasa wamejua ya kuwa vyote ulivyonipa vimetoka kwako,
עתה הם יודעים שכל מה שנתת לי ממך הוא,
8 kwa kuwa maneno yale ulionipa nimewapa wao, nao wameyapokea na kujua kwamba kweli nimetoka kwako, nao wameamini kuwa wewe ulinituma.
כי מסרתי להם את המצוות שמסרת לי. הם קיבלו אותן, והם יודעים בבטחון שבאתי לעולם מעמך ושאתה שלחת אותי.
9 Ninawaombea wao. Mimi siuombei ulimwengu, bali nawaombea wale ulionipa kwa sababu wao ni wako.
”איני מתפלל בעד העולם כולו, אלא בעד אלה שנתת לי, כי הם שייכים לך.
10 Wote walio wangu ni wako na walio wako ni wangu, nami nimetukuzwa ndani yao.
אלה שהם שלי הם שלך, ושלך הם שלי, ולכן הם תפארתי.
11 Mimi sasa simo tena ulimwenguni, lakini wao bado wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa uweza wa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
כעת אני עוזב את העולם ומשאיר אותם כאן. אבי הקדוש, אני בא אליך ומבקש ממך: שמור על כל אלה שנתת לי, כדי שיתאחדו ויהיו לאחד – כמונו.
12 Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda, wakawa salama kwa lile jina ulilonipa. Hakuna hata mmoja aliyepotea, isipokuwa yule aliyekusudiwa upotevu, ili Maandiko yapate kutimia.
בהיותי כאן בעולם שמרתי על אלה שנתת לי אך אחד מהם לא אבד, מלבד בן־הגיהינום שבו נתקיימה הנבואה שבכתבי־הקודש.
13 “Lakini sasa naja kwako, nami ninasema mambo haya wakati bado nikiwa ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu kamili ndani yao.
”עכשיו אני בא אליך. סיפרתי להם דברים רבים בהיותי עמם, כדי שיימלאו בשמחתי,
14 Nimewapa neno lako, nao ulimwengu umewachukia kwa kuwa wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa ulimwengu huu.
ומסרתי להם את מצוותיך. העולם שונא אותם, כי אינם שייכים לו, כשם שאני איני שייך לעולם.
15 Siombi kwamba uwaondoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya yule mwovu.
אני לא מבקש ממך להוציא אותם מהעולם, אלא לשמרם מהרע.
16 Wao si wa ulimwengu huu, kama vile mimi nisivyo wa ulimwengu.
הם אינם שייכים לעולם הזה, כשם שאני איני שייך לעולם הזה.
17 Uwatakase kwa ile kweli, neno lako ndilo kweli.
למד אותם את דבר האמת, כדי שיהיו קדושים וטהורים.
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami nawatuma vivyo hivyo.
כשם ששלחת אותי אל העולם כך גם אני שולח אותם אל העולם.
19 Kwa ajili yao najiweka wakfu ili wao nao wapate kutakaswa katika ile kweli.
אני מוסר את עצמי למענם, כדי שיגדלו באמת ובקדושה.
20 “Siwaombei hawa peke yao, bali nawaombea na wale wote watakaoniamini kupitia neno lao
”אינני מתפלל רק בעד אלה כאן, אלא גם בעד אלה שיאמינו בי בעתיד, לאחר שישמעו את עדויות המאמינים.
21 ili wawe na umoja kama vile wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi nilivyo ndani yako, wao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini ya kuwa wewe ndiye uliyenituma mimi.
אני מתפלל שהם יהיו מאוחדים כמונו; שהם יהיו בנו כשם שאתה בי ואני בך, כדי שהעולם יאמין שאתה שלחת אותי.
22 Utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
”נתתי להם את הכבוד שנתת לי, כדי שיהיו מאוחדים כשם שאנחנו מאוחדים –
23 Mimi ndani yako na wewe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja na ulimwengu upate kujua ya kuwa umenituma, nami nimewapenda wao kama unavyonipenda mimi.
אני בהם ואתה בי, כדי שאחדותם תהיה שלמה, וכדי שהעולם ידע שאתה שלחתני ושאתה אוהב אותם כמו שאתה אוהב אותי.
24 “Baba, shauku yangu ni kwamba, wale ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili waweze kuuona utukufu wangu, yaani, utukufu ule ulionipa kwa kuwa ulinipenda hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
אבי, אני רוצה שאלה אשר נתת לי יהיו במקום שבו אהיה, כדי שיוכלו לראות את התפארת והכבוד שהענקת לי על שום שאהבת אותי עוד לפני בריאת העולם.
25 “Baba Mwenye Haki, ingawa ulimwengu haukujui, mimi ninakujua, nao wanajua ya kuwa umenituma.
”הו, אבי הצדיק, העולם אינו מכיר אותך, אבל אני מכיר אותך, והתלמידים שנתת לי יודעים שאתה שלחתני.
26 Nimefanya jina lako lijulikane kwao nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili kwamba upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”
אני הודעתי להם את שמך, ואוסיף להודיע, כדי שהם יאהבו אותי כשם שאתה אוהב אותי וכדי שגם אני אהיה בהם.“

< Yohana 17 >