< Yohana 17 >
1 Baada ya Yesu kusema haya, alitazama kuelekea mbinguni akawaombea na kusema: “Baba, saa imewadia. Umtukuze Mwanao, ili Mwanao apate kukutukuza wewe.
Ayant ainsi parlé, Jésus leva les yeux au ciel et dit: « Père, l’heure est venue, glorifies ton Fils, afin que ton Fils te glorifie,
2 Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa. (aiōnios )
puisque tu lui as donné autorité sur toute chair, afin qu’à tous ceux que tu lui as donnés, il donne la vie éternelle. (aiōnios )
3 Nao uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe uliye Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios )
Or, la vie éternelle, c’est qu’ils te connaissent, toi, le seul vrai Dieu, et celui que tu as envoyé, Jésus-Christ. (aiōnios )
4 Nimekutukuza wewe duniani kwa kuitimiza ile kazi uliyonipa niifanye.
Je t’ai glorifié sur la terre, j’ai achevé l’œuvre que tu m’as donnée à faire.
5 Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ulimwengu haujakuwepo.
Et maintenant à toi, Père, glorifies-moi auprès de toi, de la gloire que j’avais auprès de toi, avant que le monde fût.
6 “Nimelidhihirisha jina lako kwa wale ulionipa kutoka ulimwengu. Walikuwa wako, nawe ukanipa mimi, nao wamelitii neno lako.
J’ai manifesté ton nom aux hommes que tu m’as donnés du milieu du monde. Ils étaient à toi, et tu me les as donnés: et ils ont gardé ta parole.
7 Sasa wamejua ya kuwa vyote ulivyonipa vimetoka kwako,
Ils savent à présent que tout ce que tu m’as donné vient de toi;
8 kwa kuwa maneno yale ulionipa nimewapa wao, nao wameyapokea na kujua kwamba kweli nimetoka kwako, nao wameamini kuwa wewe ulinituma.
car les paroles que tu m’as données, je les leur ai données; et ils les ont reçues, et ils ont vraiment reconnu que je suis sorti de toi, et ils ont cru que c’est toi qui m’avez envoyé.
9 Ninawaombea wao. Mimi siuombei ulimwengu, bali nawaombea wale ulionipa kwa sababu wao ni wako.
C’est pour eux que je prie. Je ne prie pas pour le monde, mais pour ceux que tu m’as donnés; parce qu’ils sont à toi:
10 Wote walio wangu ni wako na walio wako ni wangu, nami nimetukuzwa ndani yao.
car tout ce qui est à moi est à toi, et tout ce qui est à toi est à moi, et que je suis glorifié en eux.
11 Mimi sasa simo tena ulimwenguni, lakini wao bado wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa uweza wa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
Je ne suis plus dans le monde; pour eux, ils sont dans le monde, et moi, je vais à toi. Père saint, garde dans ton nom ceux que tu m’as donnés, afin qu’ils ne fassent qu’un, comme nous.
12 Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda, wakawa salama kwa lile jina ulilonipa. Hakuna hata mmoja aliyepotea, isipokuwa yule aliyekusudiwa upotevu, ili Maandiko yapate kutimia.
Lorsque j’étais avec eux, je les conservais dans ton nom. J’ai gardé ceux que tu m’a donnés, et pas un d’eux ne s’est perdu, hormis le fils de perdition, afin que l’Ecriture fût accomplie.
13 “Lakini sasa naja kwako, nami ninasema mambo haya wakati bado nikiwa ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu kamili ndani yao.
Maintenant je vais à toi, et je fais cette prière, pendant que je suis dans le monde, afin qu’ils aient en eux la plénitude de ma joie.
14 Nimewapa neno lako, nao ulimwengu umewachukia kwa kuwa wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa ulimwengu huu.
Je leur ai donné ta parole, et le monde les a haïs, parce qu’ils ne sont pas du monde, comme moi-même je ne suis pas du monde.
15 Siombi kwamba uwaondoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya yule mwovu.
Je ne te demande pas de les ôter du monde, mais de les garder du mal.
16 Wao si wa ulimwengu huu, kama vile mimi nisivyo wa ulimwengu.
Ils ne sont pas du monde, comme moi-même je ne suis pas du monde.
17 Uwatakase kwa ile kweli, neno lako ndilo kweli.
Sanctifie-les dans la vérité: ta parole est la vérité.
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami nawatuma vivyo hivyo.
Comme tu m’as envoyé dans le monde, je les ai aussi envoyés dans le monde.
19 Kwa ajili yao najiweka wakfu ili wao nao wapate kutakaswa katika ile kweli.
Et je me sanctifie moi-même pour eux, afin qu’eux aussi soient sanctifiés en vérité.
20 “Siwaombei hawa peke yao, bali nawaombea na wale wote watakaoniamini kupitia neno lao
Je ne prie pas pour eux seulement, mais aussi pour ceux qui, par leur prédication, croiront en moi,
21 ili wawe na umoja kama vile wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi nilivyo ndani yako, wao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini ya kuwa wewe ndiye uliyenituma mimi.
pour que tous ils soient un, comme toi, mon Père, tu es en moi, et moi en toi, — pour que, eux aussi, ils soient [un] en nous, afin que le monde croie que tu m’as envoyé.
22 Utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
Et je leur ai donné la gloire que tu m’a donnée, afin qu’ils soient un comme nous sommes un,
23 Mimi ndani yako na wewe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja na ulimwengu upate kujua ya kuwa umenituma, nami nimewapenda wao kama unavyonipenda mimi.
moi en eux, et toi en moi, afin qu’ils soient parfaitement un, et que le monde connaisse que tu m’as envoyé, et que tu les as aimés comme tu m’as aimé.
24 “Baba, shauku yangu ni kwamba, wale ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili waweze kuuona utukufu wangu, yaani, utukufu ule ulionipa kwa kuwa ulinipenda hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
Père, ceux que tu m’as donnés, je veux que là où je suis, ils y soient avec moi, afin qu’ils voient la gloire que tu m’as donnée, parce que tu m’as aimé avant la création du monde.
25 “Baba Mwenye Haki, ingawa ulimwengu haukujui, mimi ninakujua, nao wanajua ya kuwa umenituma.
Père juste, le monde ne t’a pas connu; mais moi, je t’ai connu, et ceux-ci ont connu que c’est toi qui m’avez envoyé.
26 Nimefanya jina lako lijulikane kwao nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili kwamba upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”
Et je leur ai fait connaître ton nom, et je le leur ferai connaître, afin que l’amour dont tu m’as aimé soit en eux, et que je sois moi aussi en eux. »