< Yohana 17 >
1 Baada ya Yesu kusema haya, alitazama kuelekea mbinguni akawaombea na kusema: “Baba, saa imewadia. Umtukuze Mwanao, ili Mwanao apate kukutukuza wewe.
Jésus dit ces choses, puis, levant les yeux au ciel, il dit: « Père, le moment est venu. Glorifie ton Fils, afin que ton Fils aussi te glorifie.
2 Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa. (aiōnios )
De même que tu lui as donné autorité sur toute chair, de même il donnera la vie éternelle à tous ceux que tu lui as donnés. (aiōnios )
3 Nao uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe uliye Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios )
La vie éternelle, c'est qu'ils te connaissent, toi, le seul vrai Dieu, et celui que tu as envoyé, Jésus-Christ. (aiōnios )
4 Nimekutukuza wewe duniani kwa kuitimiza ile kazi uliyonipa niifanye.
Je t'ai glorifié sur la terre. J'ai accompli l'œuvre que tu m'as donnée à faire.
5 Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ulimwengu haujakuwepo.
Maintenant, Père, glorifie-moi auprès de toi-même de la gloire que j'avais auprès de toi avant que le monde n'existe.
6 “Nimelidhihirisha jina lako kwa wale ulionipa kutoka ulimwengu. Walikuwa wako, nawe ukanipa mimi, nao wamelitii neno lako.
« J'ai révélé ton nom au peuple que tu m'as donné hors du monde. Ils étaient à toi, et tu me les as donnés. Ils ont gardé ta parole.
7 Sasa wamejua ya kuwa vyote ulivyonipa vimetoka kwako,
Ils savent maintenant que tout ce que tu m'as donné vient de toi,
8 kwa kuwa maneno yale ulionipa nimewapa wao, nao wameyapokea na kujua kwamba kweli nimetoka kwako, nao wameamini kuwa wewe ulinituma.
car les paroles que tu m'as données, je les leur ai données; ils les ont reçues, et ils ont su avec certitude que je venais de toi. Ils ont cru que tu m'avais envoyé.
9 Ninawaombea wao. Mimi siuombei ulimwengu, bali nawaombea wale ulionipa kwa sababu wao ni wako.
Je prie pour eux. Je ne prie pas pour le monde, mais pour ceux que tu m'as donnés, car ils sont à toi.
10 Wote walio wangu ni wako na walio wako ni wangu, nami nimetukuzwa ndani yao.
Tout ce qui est à moi est à toi, et tu es à moi, et je suis glorifié en eux.
11 Mimi sasa simo tena ulimwenguni, lakini wao bado wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa uweza wa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
Je ne suis plus dans le monde, mais eux sont dans le monde, et je viens à toi. Père saint, garde-les par ton nom que tu m'as donné, afin qu'ils soient un, comme nous le sommes.
12 Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda, wakawa salama kwa lile jina ulilonipa. Hakuna hata mmoja aliyepotea, isipokuwa yule aliyekusudiwa upotevu, ili Maandiko yapate kutimia.
Pendant que j'étais avec eux dans le monde, je les ai gardés en ton nom. J'ai gardé ceux que tu m'as donnés. Aucun d'eux n'est perdu, si ce n'est le fils de la destruction, afin que l'Écriture s'accomplisse.
13 “Lakini sasa naja kwako, nami ninasema mambo haya wakati bado nikiwa ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu kamili ndani yao.
Mais maintenant, je viens à toi, et je dis ces choses dans le monde, afin qu'ils aient ma joie parfaite en eux-mêmes.
14 Nimewapa neno lako, nao ulimwengu umewachukia kwa kuwa wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa ulimwengu huu.
Je leur ai donné votre parole. Le monde les a haïs parce qu'ils ne sont pas du monde, comme moi je ne suis pas du monde.
15 Siombi kwamba uwaondoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya yule mwovu.
Je ne te prie pas de les retirer du monde, mais de les préserver du malin.
16 Wao si wa ulimwengu huu, kama vile mimi nisivyo wa ulimwengu.
Ils ne sont pas du monde, comme moi je ne suis pas du monde.
17 Uwatakase kwa ile kweli, neno lako ndilo kweli.
Sanctifie-les dans ta vérité. Ta parole est vérité.
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami nawatuma vivyo hivyo.
De même que tu m'as envoyé dans le monde, de même je les ai envoyés dans le monde.
19 Kwa ajili yao najiweka wakfu ili wao nao wapate kutakaswa katika ile kweli.
C'est pour eux que je me sanctifie, afin qu'eux aussi soient sanctifiés dans la vérité.
20 “Siwaombei hawa peke yao, bali nawaombea na wale wote watakaoniamini kupitia neno lao
Ce n'est pas pour eux seulement que je prie, mais aussi pour ceux qui croiront en moi par leur parole,
21 ili wawe na umoja kama vile wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi nilivyo ndani yako, wao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini ya kuwa wewe ndiye uliyenituma mimi.
afin que tous soient un, comme toi, Père, tu es en moi, et moi en toi, afin qu'eux aussi soient un en nous, pour que le monde croie que tu m'as envoyé.
22 Utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
La gloire que tu m'as donnée, je la leur ai donnée, afin qu'ils soient un, comme nous sommes un,
23 Mimi ndani yako na wewe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja na ulimwengu upate kujua ya kuwa umenituma, nami nimewapenda wao kama unavyonipenda mimi.
moi en eux, et toi en moi, pour qu'ils deviennent un, afin que le monde sache que tu m'as envoyé et que tu les as aimés comme tu m'as aimé.
24 “Baba, shauku yangu ni kwamba, wale ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili waweze kuuona utukufu wangu, yaani, utukufu ule ulionipa kwa kuwa ulinipenda hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
Père, je désire que ceux que tu m'as donnés soient aussi avec moi là où je suis, afin qu'ils voient la gloire que tu m'as donnée, car tu m'as aimé avant la fondation du monde.
25 “Baba Mwenye Haki, ingawa ulimwengu haukujui, mimi ninakujua, nao wanajua ya kuwa umenituma.
Père juste, le monde ne t'a pas connu, mais moi je t'ai connu, et eux ont su que tu m'avais envoyé.
26 Nimefanya jina lako lijulikane kwao nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili kwamba upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”
Je leur ai fait connaître ton nom, et je le ferai connaître, afin que l'amour dont tu m'as aimé soit en eux, et que je sois en eux. »