< Yohana 17 >
1 Baada ya Yesu kusema haya, alitazama kuelekea mbinguni akawaombea na kusema: “Baba, saa imewadia. Umtukuze Mwanao, ili Mwanao apate kukutukuza wewe.
When he had thus spoken, Jesus raised his eyes to heaven and said. "Father, the hour is come. Glorify the Son, that thy Son may glorify thee;
2 Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa. (aiōnios )
"since thou hast given him authority over all mankind, to give eternal life to all whom thou hast given him. (aiōnios )
3 Nao uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe uliye Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios )
"And this is eternal life, to know thee, the only true God, and Jesus Christ whom thou hast sent. (aiōnios )
4 Nimekutukuza wewe duniani kwa kuitimiza ile kazi uliyonipa niifanye.
"I have glorified thee on the earth; I have finished the work which thou gavest me to do.
5 Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ulimwengu haujakuwepo.
"And now, O Father, glorify thou me with own self, with the glory I had with thee before the world began.
6 “Nimelidhihirisha jina lako kwa wale ulionipa kutoka ulimwengu. Walikuwa wako, nawe ukanipa mimi, nao wamelitii neno lako.
"I have made known thy name to the men whom thou gavest me out of the world. Thine they were, and thou gavest them to me, and they have kept thy word.
7 Sasa wamejua ya kuwa vyote ulivyonipa vimetoka kwako,
"They know now that whatever thou hast given me was from thee;
8 kwa kuwa maneno yale ulionipa nimewapa wao, nao wameyapokea na kujua kwamba kweli nimetoka kwako, nao wameamini kuwa wewe ulinituma.
"for I have given them the words which thou gavest me; and they have received them, and they have believed that thou didst send me.
9 Ninawaombea wao. Mimi siuombei ulimwengu, bali nawaombea wale ulionipa kwa sababu wao ni wako.
"I am praying for them; I am not praying for the world, but for those whom thou hast given me; for they are thine,
10 Wote walio wangu ni wako na walio wako ni wangu, nami nimetukuzwa ndani yao.
"and all thine are mine, and mine are thine; and I am glorified in them.
11 Mimi sasa simo tena ulimwenguni, lakini wao bado wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa uweza wa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
12 Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda, wakawa salama kwa lile jina ulilonipa. Hakuna hata mmoja aliyepotea, isipokuwa yule aliyekusudiwa upotevu, ili Maandiko yapate kutimia.
13 “Lakini sasa naja kwako, nami ninasema mambo haya wakati bado nikiwa ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu kamili ndani yao.
14 Nimewapa neno lako, nao ulimwengu umewachukia kwa kuwa wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa ulimwengu huu.
15 Siombi kwamba uwaondoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya yule mwovu.
16 Wao si wa ulimwengu huu, kama vile mimi nisivyo wa ulimwengu.
17 Uwatakase kwa ile kweli, neno lako ndilo kweli.
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami nawatuma vivyo hivyo.
"As thou hast sent me into the world, even so I also have sent them into the world.
19 Kwa ajili yao najiweka wakfu ili wao nao wapate kutakaswa katika ile kweli.
"And for their sakes I dedicate myself, that they also may be thoroughly dedicated in the truth.
20 “Siwaombei hawa peke yao, bali nawaombea na wale wote watakaoniamini kupitia neno lao
"Nor do I pray for them alone, but for those also who believe in me through their word,
21 ili wawe na umoja kama vile wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi nilivyo ndani yako, wao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini ya kuwa wewe ndiye uliyenituma mimi.
"that they may all be one, even as thou, Father, art in me and I in thee; that they also may be in us; in order that the world may believe that thou hast sent me.
22 Utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
"And the glory which thou gavest me I have given them; that they may be one even as we are one,
23 Mimi ndani yako na wewe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja na ulimwengu upate kujua ya kuwa umenituma, nami nimewapenda wao kama unavyonipenda mimi.
"I in them and thou in me; that they may be made perfectly one, so that the world may recognize that thou didst send me, and hast loved them as thou hast loved me.
24 “Baba, shauku yangu ni kwamba, wale ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili waweze kuuona utukufu wangu, yaani, utukufu ule ulionipa kwa kuwa ulinipenda hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
"Father, it is my will that wherever I am these also, thy gift to me, may be with me, that they may see the glory, my glory which thou hast given me, because thou didst love me before the foundations of the world.
25 “Baba Mwenye Haki, ingawa ulimwengu haukujui, mimi ninakujua, nao wanajua ya kuwa umenituma.
"O righteous Father, though the world knew thee not, I have known thee, and these have known that though didst send me.
26 Nimefanya jina lako lijulikane kwao nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili kwamba upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”
"And I have declared - and will declare - thy name unto them, that the love with which thou hast loved me may be in them, and that I may be in them."