< Yohana 17 >

1 Baada ya Yesu kusema haya, alitazama kuelekea mbinguni akawaombea na kusema: “Baba, saa imewadia. Umtukuze Mwanao, ili Mwanao apate kukutukuza wewe.
Jesus spoke these words; and lifting up His eyes to heaven, said, Father, the hour has come; glorify thy Son, in order that the Son may glorify thee:
2 Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa. (aiōnios g166)
as thou didst give Him authority over all flesh, in order that whatsoever thou hast given unto Him, He may give unto them eternal life. (aiōnios g166)
3 Nao uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe uliye Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios g166)
But this is eternal life, that they know thee the only true God, and Jesus Christ whom thou didst send. (aiōnios g166)
4 Nimekutukuza wewe duniani kwa kuitimiza ile kazi uliyonipa niifanye.
I glorified thee upon the earth, having finished the work that thou hast given to me that I may do it.
5 Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ulimwengu haujakuwepo.
And now, Father, glorify thou me with thyself with the glory which I had with thee before the world was.
6 “Nimelidhihirisha jina lako kwa wale ulionipa kutoka ulimwengu. Walikuwa wako, nawe ukanipa mimi, nao wamelitii neno lako.
I have manifested thy name, to the men whom thou didst give me out of the world. They were thine, and thou didst give them to me; and they have kept thy word:
7 Sasa wamejua ya kuwa vyote ulivyonipa vimetoka kwako,
now they know that all things so many as thou hast given to me are with thee:
8 kwa kuwa maneno yale ulionipa nimewapa wao, nao wameyapokea na kujua kwamba kweli nimetoka kwako, nao wameamini kuwa wewe ulinituma.
because the words which thou didst give me I have given unto them; and they received them, and they know truly that I came out from thee, and they believed that thou didst send me.
9 Ninawaombea wao. Mimi siuombei ulimwengu, bali nawaombea wale ulionipa kwa sababu wao ni wako.
I pray for these: I pray not for the world; but for those whom thou hast given me, because they are thine:
10 Wote walio wangu ni wako na walio wako ni wangu, nami nimetukuzwa ndani yao.
and all mine are thine, and thine are mine: and I have been glorified in them.
11 Mimi sasa simo tena ulimwenguni, lakini wao bado wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa uweza wa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
And I am no longer in the world, and they are in the world, and I come to thee. Holy Father, keep them through my name whom thou hast given unto me, in order that they may be one, as we are.
12 Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda, wakawa salama kwa lile jina ulilonipa. Hakuna hata mmoja aliyepotea, isipokuwa yule aliyekusudiwa upotevu, ili Maandiko yapate kutimia.
When I was with them, I was keeping them in thy name whom thou hast given unto me. And I guarded them, and no one of them perished, except the son of perdition; that the Scripture may be fulfilled.
13 “Lakini sasa naja kwako, nami ninasema mambo haya wakati bado nikiwa ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu kamili ndani yao.
And now I come to thee; and speak these things in the world, that they may have my joy complete in themselves.
14 Nimewapa neno lako, nao ulimwengu umewachukia kwa kuwa wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa ulimwengu huu.
I have given unto them thy word; and the world hated them, because they are not of the world, as I am not of the world.
15 Siombi kwamba uwaondoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya yule mwovu.
I do not pray that you may take them out of the world, but that you may keep them from the evil one.
16 Wao si wa ulimwengu huu, kama vile mimi nisivyo wa ulimwengu.
They are not of the world, as I am not of the world.
17 Uwatakase kwa ile kweli, neno lako ndilo kweli.
Sanctify them through the truth: thy word is truth.
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami nawatuma vivyo hivyo.
As thou didst send me into the world, I also sent them into the world:
19 Kwa ajili yao najiweka wakfu ili wao nao wapate kutakaswa katika ile kweli.
and I sanctify myself in their behalf, in order that they may also be sanctified through the truth.
20 “Siwaombei hawa peke yao, bali nawaombea na wale wote watakaoniamini kupitia neno lao
And I not only pray for these, but also for those believing on me through their word;
21 ili wawe na umoja kama vile wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi nilivyo ndani yako, wao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini ya kuwa wewe ndiye uliyenituma mimi.
that they may all be one, as thou, Father, art in me, and I in thee, that they also may be in us; that the world may believe that thou didst send me.
22 Utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
And I have given unto them the glory which thou hast given unto me; in order that they may be one, as we are one;
23 Mimi ndani yako na wewe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja na ulimwengu upate kujua ya kuwa umenituma, nami nimewapenda wao kama unavyonipenda mimi.
I in them, and thou in me, in order that they may be perfected into one; in order that the world may know that thou didst send me, and didst love them, as thou didst love me.
24 “Baba, shauku yangu ni kwamba, wale ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili waweze kuuona utukufu wangu, yaani, utukufu ule ulionipa kwa kuwa ulinipenda hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
Father, that which thou hast given unto me, I wish that they may also be with me, where I am, in order that they may behold my glory, which thou hast given unto me: because thou didst love me before the foundation of the world.
25 “Baba Mwenye Haki, ingawa ulimwengu haukujui, mimi ninakujua, nao wanajua ya kuwa umenituma.
Righteous Father, indeed the world does not know thee, but I know thee, and they know that thou didst send me;
26 Nimefanya jina lako lijulikane kwao nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili kwamba upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”
I made known thy name to them, and will make it known; in order that the love with which thou didst love me may be in them, and I in them.

< Yohana 17 >