< Yohana 17 >
1 Baada ya Yesu kusema haya, alitazama kuelekea mbinguni akawaombea na kusema: “Baba, saa imewadia. Umtukuze Mwanao, ili Mwanao apate kukutukuza wewe.
Jesus said these things, and then, lifting up his eyes toward heaven, he said: “Father, the hour has arrived: glorify your Son, so that your Son may glorify you,
2 Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa. (aiōnios )
just as you have given authority over all flesh to him, so that he may give eternal life to all those whom you have given to him. (aiōnios )
3 Nao uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe uliye Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios )
And this is eternal life: that they may know you, the only true God, and Jesus Christ, whom you have sent. (aiōnios )
4 Nimekutukuza wewe duniani kwa kuitimiza ile kazi uliyonipa niifanye.
I have glorified you on earth. I have completed the work that you gave me to accomplish.
5 Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ulimwengu haujakuwepo.
And now Father, glorify me within yourself, with the glory that I had with you before the world ever was.
6 “Nimelidhihirisha jina lako kwa wale ulionipa kutoka ulimwengu. Walikuwa wako, nawe ukanipa mimi, nao wamelitii neno lako.
I have manifested your name to the men whom you have given to me from the world. They were yours, and you gave them to me. And they have kept your word.
7 Sasa wamejua ya kuwa vyote ulivyonipa vimetoka kwako,
Now they realize that all the things that you have given me are from you.
8 kwa kuwa maneno yale ulionipa nimewapa wao, nao wameyapokea na kujua kwamba kweli nimetoka kwako, nao wameamini kuwa wewe ulinituma.
For I have given them the words that you gave to me. And they have accepted these words, and they have truly understood that I went forth from you, and they have believed that you sent me.
9 Ninawaombea wao. Mimi siuombei ulimwengu, bali nawaombea wale ulionipa kwa sababu wao ni wako.
I pray for them. I do not pray for the world, but for those whom you have given to me. For they are yours.
10 Wote walio wangu ni wako na walio wako ni wangu, nami nimetukuzwa ndani yao.
And all that is mine is yours, and all that is yours is mine, and I am glorified in this.
11 Mimi sasa simo tena ulimwenguni, lakini wao bado wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa uweza wa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
And though I am not in the world, these are in the world, and I am coming to you. Father most holy, preserve them in your name, those whom you have given to me, so that they may be one, even as we are one.
12 Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda, wakawa salama kwa lile jina ulilonipa. Hakuna hata mmoja aliyepotea, isipokuwa yule aliyekusudiwa upotevu, ili Maandiko yapate kutimia.
While I was with them, I preserved them in your name. I have guarded those whom you have given to me, and not one of them is lost, except the son of perdition, so that the Scripture may be fulfilled.
13 “Lakini sasa naja kwako, nami ninasema mambo haya wakati bado nikiwa ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu kamili ndani yao.
And now I am coming to you. But I am speaking these things in the world, so that they may have the fullness of my joy within themselves.
14 Nimewapa neno lako, nao ulimwengu umewachukia kwa kuwa wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa ulimwengu huu.
I have given them your word, and the world has hated them. For they are not of the world, just as I, too, am not of the world.
15 Siombi kwamba uwaondoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya yule mwovu.
I am not praying that you would take them out of the world, but that you would preserve them from evil.
16 Wao si wa ulimwengu huu, kama vile mimi nisivyo wa ulimwengu.
They are not of the world, just as I also am not of the world.
17 Uwatakase kwa ile kweli, neno lako ndilo kweli.
Sanctify them in truth. Your word is truth.
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami nawatuma vivyo hivyo.
Just as you have sent me into the world, I also have sent them into the world.
19 Kwa ajili yao najiweka wakfu ili wao nao wapate kutakaswa katika ile kweli.
And it is for them that I sanctify myself, so that they, too, may be sanctified in truth.
20 “Siwaombei hawa peke yao, bali nawaombea na wale wote watakaoniamini kupitia neno lao
But I am not praying for them only, but also for those who through their word shall believe in me.
21 ili wawe na umoja kama vile wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi nilivyo ndani yako, wao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini ya kuwa wewe ndiye uliyenituma mimi.
So may they all be one. Just as you, Father, are in me, and I am in you, so also may they be one in us: so that the world may believe that you have sent me.
22 Utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
And the glory that you have given to me, I have given to them, so that they may be one, just as we also are one.
23 Mimi ndani yako na wewe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja na ulimwengu upate kujua ya kuwa umenituma, nami nimewapenda wao kama unavyonipenda mimi.
I am in them, and you are in me. So may they be perfected as one. And may the world know that you have sent me and that you have loved them, just as you have also loved me.
24 “Baba, shauku yangu ni kwamba, wale ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili waweze kuuona utukufu wangu, yaani, utukufu ule ulionipa kwa kuwa ulinipenda hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
Father, I will that where I am, those whom you have given to me may also be with me, so that they may see my glory which you have given to me. For you loved me before the founding of the world.
25 “Baba Mwenye Haki, ingawa ulimwengu haukujui, mimi ninakujua, nao wanajua ya kuwa umenituma.
Father most just, the world has not known you. But I have known you. And these have known that you sent me.
26 Nimefanya jina lako lijulikane kwao nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili kwamba upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”
And I have made known your name to them, and I will make it known, so that the love in which you have loved me may be in them, and so that I may be in them.”