< Yohana 17 >
1 Baada ya Yesu kusema haya, alitazama kuelekea mbinguni akawaombea na kusema: “Baba, saa imewadia. Umtukuze Mwanao, ili Mwanao apate kukutukuza wewe.
Jesus spoke these words, and lifted up his eyes to heaven, and said: Father, the hour has come: glorify thy Son, that thy Son may also glorify thee;
2 Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa. (aiōnios )
as thou hast given him authority over all flesh, that he may give eternal life to all that thou hast given him. (aiōnios )
3 Nao uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe uliye Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios )
And this is life eternal, to know thee, the only true God, and Jesus Christ whom thou has sent. (aiōnios )
4 Nimekutukuza wewe duniani kwa kuitimiza ile kazi uliyonipa niifanye.
I have glorified thee on the earth; I have finished the work which thou gavest me to do.
5 Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ulimwengu haujakuwepo.
And now, Father, glorify me with thyself, with the glory which I had with thee before the world was.
6 “Nimelidhihirisha jina lako kwa wale ulionipa kutoka ulimwengu. Walikuwa wako, nawe ukanipa mimi, nao wamelitii neno lako.
I have made known thy name to the men that thou gavest me out of the world. Thine they were, and thou gavest them, to me, and they have kept thy word.
7 Sasa wamejua ya kuwa vyote ulivyonipa vimetoka kwako,
Now they know that all things that thou hast given me are from thee;
8 kwa kuwa maneno yale ulionipa nimewapa wao, nao wameyapokea na kujua kwamba kweli nimetoka kwako, nao wameamini kuwa wewe ulinituma.
for the words which thou gavest me I have given them; and they have received them, and they know surely that I came forth from thee, and they believe that thou didst send me.
9 Ninawaombea wao. Mimi siuombei ulimwengu, bali nawaombea wale ulionipa kwa sababu wao ni wako.
I pray for them; I pray not for the world, but for them whom thou hast given me; for they are thine.
10 Wote walio wangu ni wako na walio wako ni wangu, nami nimetukuzwa ndani yao.
And all mine are thine, and thine are mine, and I am glorified in them.
11 Mimi sasa simo tena ulimwenguni, lakini wao bado wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa uweza wa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
And I am no longer in the world; but these are in the world, and I come to thee. Holy Father, keep in thy name those whom thou hast given me, that they may be one, as we are one.
12 Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda, wakawa salama kwa lile jina ulilonipa. Hakuna hata mmoja aliyepotea, isipokuwa yule aliyekusudiwa upotevu, ili Maandiko yapate kutimia.
While I was with them in the world, I kept them in thy name. Those whom thou gavest me, I have kept; and none of them is lost but the son of perdition, that the scripture may be fulfilled.
13 “Lakini sasa naja kwako, nami ninasema mambo haya wakati bado nikiwa ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu kamili ndani yao.
And now I come to thee; and these things I speak in the world, that they may have my joy fulfilled in themselves.
14 Nimewapa neno lako, nao ulimwengu umewachukia kwa kuwa wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa ulimwengu huu.
I have given them thy word; and the world has hated them, because they are not of the world, even as I am not of the world.
15 Siombi kwamba uwaondoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya yule mwovu.
I do not pray thee to take them out of the world, but to keep them from the Evil One.
16 Wao si wa ulimwengu huu, kama vile mimi nisivyo wa ulimwengu.
They are not of the world, as I am not of the world.
17 Uwatakase kwa ile kweli, neno lako ndilo kweli.
Sanctify them through thy truth; thy word is truth.
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami nawatuma vivyo hivyo.
As thou hast sent me into the world, so I send them into the world;
19 Kwa ajili yao najiweka wakfu ili wao nao wapate kutakaswa katika ile kweli.
and for them I sanctify myself, that they also may be sanctified through the truth.
20 “Siwaombei hawa peke yao, bali nawaombea na wale wote watakaoniamini kupitia neno lao
I pray, not for these only, but for those also who shall believe on me through their word;
21 ili wawe na umoja kama vile wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi nilivyo ndani yako, wao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini ya kuwa wewe ndiye uliyenituma mimi.
that they all may be one, as thou, Father, art in me, and I in thee, that they may be one in us: that the world may believe that thou hast sent me.
22 Utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
And the glory which thou gavest me, I have given them, that they may be one, as we are one;
23 Mimi ndani yako na wewe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja na ulimwengu upate kujua ya kuwa umenituma, nami nimewapenda wao kama unavyonipenda mimi.
I in them, and thou in me, that they may be made perfect in one, that the world may know that thou hast sent me, and hast loved them, as thou hast loved me.
24 “Baba, shauku yangu ni kwamba, wale ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili waweze kuuona utukufu wangu, yaani, utukufu ule ulionipa kwa kuwa ulinipenda hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
Father, I wish that they also, whom thou hast given me, may be with me where I am, that they may behold my glory, which thou hast given me; for thou didst love me before the foundation of the world.
25 “Baba Mwenye Haki, ingawa ulimwengu haukujui, mimi ninakujua, nao wanajua ya kuwa umenituma.
Righteous Father, though the world has not known thee, yet I have known thee, and these have known that thou hast sent me.
26 Nimefanya jina lako lijulikane kwao nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili kwamba upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”
And I have made known to them thy name, and will continue to make it known, that the love with which thou hast loved me may be in them, and I in them.