< Yohana 17 >
1 Baada ya Yesu kusema haya, alitazama kuelekea mbinguni akawaombea na kusema: “Baba, saa imewadia. Umtukuze Mwanao, ili Mwanao apate kukutukuza wewe.
Acuna ngthu a pyen law käna Jesuh khana mang lü, “Ka Pa aw, akcün pha law päng ve. Capa naw a ning mhlünmtai law vaia, na Capa mhlünmtaia.
2 Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa. (aiōnios )
Acukba khyange naküta khana khyaibahnak a na pet am, na peta khyang naküt üng angsäia xünnak a jah pet khawh vaia. (aiōnios )
3 Nao uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe uliye Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios )
“Angsäia xünnak hin ta, nang Pamhnam kcang däk ja na tüi law Jesuh Khritaw ksingnak cen ni. (aiōnios )
4 Nimekutukuza wewe duniani kwa kuitimiza ile kazi uliyonipa niifanye.
“Ka pawh vaia khut na na pet mcän lü, khawmdek khana ka ning mhlünmtai pängki.
5 Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ulimwengu haujakuwepo.
“Aw ka Pa aw, khawmdek am a ngtüi ham üng nang am atänga hlüngtainak ka yah cen atuh pi na hmai maa na pe bea.
6 “Nimelidhihirisha jina lako kwa wale ulionipa kutoka ulimwengu. Walikuwa wako, nawe ukanipa mimi, nao wamelitii neno lako.
“Khawmdek üngka jah xü lü na na jah petea veia na ngming ka jah mtheh päng ni. Amimi na jah kaa kyase, kei üng na na jah pet päng ni. Amimi naw na ngthukhyü pi läklamkie.
7 Sasa wamejua ya kuwa vyote ulivyonipa vimetoka kwako,
“Na na jah pet naküt cun nang üngka naw lawki ti ksing päng ve u.
8 kwa kuwa maneno yale ulionipa nimewapa wao, nao wameyapokea na kujua kwamba kweli nimetoka kwako, nao wameamini kuwa wewe ulinituma.
“Na na jah peta ngthue pi ka jah pet; acun dokhamei u lü nang üngka naw ka lawki ti angsinga ksing ve u. Nang naw na na tüi law ti pi jumkie.
9 Ninawaombea wao. Mimi siuombei ulimwengu, bali nawaombea wale ulionipa kwa sababu wao ni wako.
“Ami phäha ktaiyü veng. Khawmdeka phäha am ktaiyü nawng. Nang naw na na jah pete na kaa ami kyaa phäha, hinea phäha ni ka ktaiyü ve.
10 Wote walio wangu ni wako na walio wako ni wangu, nami nimetukuzwa ndani yao.
“Ka kaa naküt cun na ka ni, na ka naküt cun pi ka kaa kyaki. Keia hlüngtainak cun acune üngkhyüh ngdang ve.
11 Mimi sasa simo tena ulimwenguni, lakini wao bado wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa uweza wa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
“Acunüng, na veia ka law khaia kyase, kei khawmdek khana am ve ti nawng. Hine hin khawmdeka khana ve hüt khaie. Ngcingcaihkia ka Pa aw, nini pumata ni kyaa mäiha, amimi pi pumata ami kya thei vaia, na na peta na ngming jomah am jah kcungvawnga.
12 Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda, wakawa salama kwa lile jina ulilonipa. Hakuna hata mmoja aliyepotea, isipokuwa yule aliyekusudiwa upotevu, ili Maandiko yapate kutimia.
“Ami hlawnga ka vea küt üng, na na peta na ngming jomah am ka jah kcungvawng khawiki. Cangcim a küm lawnak vaia, khyükia capa mata thea, u pi am khyük khaia ka jah kcungvawng ni.
13 “Lakini sasa naja kwako, nami ninasema mambo haya wakati bado nikiwa ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu kamili ndani yao.
“Acunsepi, tukbäih na veia ka law khaia kyase, hine naw keia jenak ami mlung k’uma kümkawikia ami yahei vaia phäh, kei naw hina ngthu khawmdek khana ka ve ham üng ka pyen ni.
14 Nimewapa neno lako, nao ulimwengu umewachukia kwa kuwa wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa ulimwengu huu.
“Na ngthu ka jah peki; acunüng, kei khawmdek üng am ka sängeia mäiha, amimi pi khawmdek üng am sängei u se, khawmdek naw jah hnengki.
15 Siombi kwamba uwaondoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya yule mwovu.
“Ahin he khawmdek khan üngka naw na jah lak be vaia ka täsamki am ni. Khawyaipaa kut üngkhyüh na jah yungkaih vaia na veia ka täsamki.
16 Wao si wa ulimwengu huu, kama vile mimi nisivyo wa ulimwengu.
“Kei khawmdek üng am ka sängeia mäiha, amimi pi khawmdek üng am sängei u.
17 Uwatakase kwa ile kweli, neno lako ndilo kweli.
“Amimi, ngthungtak am jah ngcimcaihsaka, na ngthu cun ngthungtaka pi kyaki.
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami nawatuma vivyo hivyo.
“Nang naw kei khawmdeka na na tüiha mäiha, kei naw pi amimi ka jah tüihki.
19 Kwa ajili yao najiweka wakfu ili wao nao wapate kutakaswa katika ile kweli.
“Amimi akcanga na veia ami ng’apei law vaia phäh, kei ami phäha kamät na veia ka ng’apeiki.
20 “Siwaombei hawa peke yao, bali nawaombea na wale wote watakaoniamini kupitia neno lao
“Hinea phäh däka ka ktaiyüki am ni, hinea ngthu pyena phäh kei na jum law khaiea phäha pi ka ktaiyüki.
21 ili wawe na umoja kama vile wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi nilivyo ndani yako, wao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini ya kuwa wewe ndiye uliyenituma mimi.
“Ami yümmat law vaia ka ktaiyüki. Pa aw, nang kei üng ve lü kei nang üng ka vea mäiha, amimi pi nini üng ve law u se. Amimi ami yümmat üng va, khawmdek khyange naw na na tüi law ti cun jum law khaie.
22 Utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
“Nang ja kei pumsa mata ni thawna mäiha amimi pi pumsa mata ami thawn thei vaia; hlüngtainak na na pet cen ka jah peki.
23 Mimi ndani yako na wewe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja na ulimwengu upate kujua ya kuwa umenituma, nami nimewapenda wao kama unavyonipenda mimi.
“Kei amimi üng ve lü, nang kei üng veki se, amimi ami yümmat law vaia phäh. Acunüng va, na na tüih law ja na na mhläkphyanaka mäiha, na jah mhläkphyanaki ti cun khawmdek khyange naw ksing law khaie.
24 “Baba, shauku yangu ni kwamba, wale ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili waweze kuuona utukufu wangu, yaani, utukufu ule ulionipa kwa kuwa ulinipenda hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
“Ka Pa aw, khawmdek am a ngtüi ham üng na mhläkphya na lü na na peta hlüngtainak cen, ka venaka ve u lü keia hlüngtainak ami hmu thei vaia hlüei veng.
25 “Baba Mwenye Haki, ingawa ulimwengu haukujui, mimi ninakujua, nao wanajua ya kuwa umenituma.
“Ngsungpyunkia Pa aw, khawmdek naw am ni ksing. Kei naw ta ni ksing veng; hine naw pi na na tüi law ti ksingki he.
26 Nimefanya jina lako lijulikane kwao nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili kwamba upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”
“Ka hama na taka mhläkphyanak cen amimi üng ve se, kei pi amimi üng ka ve vaia, ami veia na ngming ka jah ksingsaki, ka jah ksingsak ham lä khai” ti lü ktaiyüki.