< Yohana 17 >

1 Baada ya Yesu kusema haya, alitazama kuelekea mbinguni akawaombea na kusema: “Baba, saa imewadia. Umtukuze Mwanao, ili Mwanao apate kukutukuza wewe.
Това като изговори Исус, дигна очите си към небето, и рече: Отче настана часът; прослави Сина Си, за да Те прослави и Сина Ти,
2 Kwa kuwa umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili ili awape uzima wa milele wale uliompa. (aiōnios g166)
според както си Му дал власт над всяка твар да даде вечен живот на всички, които си Му дал. (aiōnios g166)
3 Nao uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe uliye Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu Kristo uliyemtuma. (aiōnios g166)
А това е вечен живот, да познаят Тебе, единия истинен Бог, и Исуса Христа, Когото си изпратил. (aiōnios g166)
4 Nimekutukuza wewe duniani kwa kuitimiza ile kazi uliyonipa niifanye.
Аз те прославих на земята, като свърших делото, което Ти Ми даде да върша.
5 Hivyo sasa, Baba, unitukuze mbele zako kwa ule utukufu niliokuwa nao pamoja na wewe kabla ulimwengu haujakuwepo.
И сега прослави Ме, Отче, у Себе Си със славата, която имах у Тебе преди създанието на света.
6 “Nimelidhihirisha jina lako kwa wale ulionipa kutoka ulimwengu. Walikuwa wako, nawe ukanipa mimi, nao wamelitii neno lako.
Изявих името Ти на човеците, които Ми даде от света. Те бяха Твои, и Ти ги даде на Мене, и те упазиха Твоето слово.
7 Sasa wamejua ya kuwa vyote ulivyonipa vimetoka kwako,
Сега знаят, че всичко, което си Ми дал е от Тебе;
8 kwa kuwa maneno yale ulionipa nimewapa wao, nao wameyapokea na kujua kwamba kweli nimetoka kwako, nao wameamini kuwa wewe ulinituma.
защото думите, които Ми даде Ти, Аз ги предадох на тях, и те ги приеха; и наистина знаят че, от Тебе излязох, и вярват, че Ти си Ме пратил.
9 Ninawaombea wao. Mimi siuombei ulimwengu, bali nawaombea wale ulionipa kwa sababu wao ni wako.
Аз за тях се моля; не се моля за света, а за тия, които си Ми дал, защото са Твои.
10 Wote walio wangu ni wako na walio wako ni wangu, nami nimetukuzwa ndani yao.
И всичко Мое е Твое, Твоето Мое, и Аз се прославям в тях.
11 Mimi sasa simo tena ulimwenguni, lakini wao bado wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba Mtakatifu, uwalinde kwa uweza wa jina lako ulilonipa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
Не съм вече на света, а тия са на света, и Аз ида при Тебе, Отче свети, опази в името Си тия, които си Ми дал, за да бъдат едно, както сме и Ние.
12 Nilipokuwa pamoja nao, niliwalinda, wakawa salama kwa lile jina ulilonipa. Hakuna hata mmoja aliyepotea, isipokuwa yule aliyekusudiwa upotevu, ili Maandiko yapate kutimia.
Докато бях с тях, Аз пазех в Твоето име тия, които Ми даде; упазих ги, и нито един от тях не погина, освен сина на погибелта, за да се изпълни писанието.
13 “Lakini sasa naja kwako, nami ninasema mambo haya wakati bado nikiwa ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu kamili ndani yao.
А сега ида при тебе; но догдето съм още на света казвам това, за да имат Моята радост пълна в себе си.
14 Nimewapa neno lako, nao ulimwengu umewachukia kwa kuwa wao si wa ulimwengu kama mimi nisivyo wa ulimwengu huu.
Аз им предадох Твоето слово; и светът ги намрази, защото те не са от света, както и Аз не съм от него.
15 Siombi kwamba uwaondoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya yule mwovu.
Не се моля да ги вземеш от света, но да ги пазиш от лукавия.
16 Wao si wa ulimwengu huu, kama vile mimi nisivyo wa ulimwengu.
Те не са от света както и Аз не съм от света.
17 Uwatakase kwa ile kweli, neno lako ndilo kweli.
Освети ги чрез истината; Твоето слово е истина.
18 Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami nawatuma vivyo hivyo.
Както Ти прати Мене в света, така и Аз пратих тях в света;
19 Kwa ajili yao najiweka wakfu ili wao nao wapate kutakaswa katika ile kweli.
и заради тях Аз освещавам Себе Си, за да бъдат и те осветени чрез истината.
20 “Siwaombei hawa peke yao, bali nawaombea na wale wote watakaoniamini kupitia neno lao
И не само за тях се моля, но и за ония, които биха повярвали в Мене чрез тяхното учение,
21 ili wawe na umoja kama vile wewe Baba ulivyo ndani yangu na mimi nilivyo ndani yako, wao nao wawe ndani yetu, ili ulimwengu upate kuamini ya kuwa wewe ndiye uliyenituma mimi.
да бъдат всички едно; както Ти Отче, си в Мене и Аз в Тебе, тъй и те да бъдат в Нас, за да повярва светът, че Ти си Ме пратил.
22 Utukufu ule ulionipa nimewapa wao, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo wamoja.
И славата, която Ти Ми даде, Аз я дадох на тях; за да бъдат едно, както и Ние сме едно;
23 Mimi ndani yako na wewe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja na ulimwengu upate kujua ya kuwa umenituma, nami nimewapenda wao kama unavyonipenda mimi.
Аз в тях, и Ти в Мене, за да бъдат съвършени в единство; за да познае светът, че Ти си Ме пратил, и си възлюбил тях както си възлюбил и Мене.
24 “Baba, shauku yangu ni kwamba, wale ulionipa wawe pamoja nami pale nilipo, ili waweze kuuona utukufu wangu, yaani, utukufu ule ulionipa kwa kuwa ulinipenda hata kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu.
Отче, желая гдето съм Аз, да бъдат с Мене и тия, които FOOTNOTE ( Гръцки: Каквото. ) си Ми дал, за да гледат Моята слава, която си Ми дал; защото си Ме възлюбил преди създанието на света.
25 “Baba Mwenye Haki, ingawa ulimwengu haukujui, mimi ninakujua, nao wanajua ya kuwa umenituma.
Отче праведни, светът не Те е познал, но Аз Те познах; и тия познаха, че Ти си Ме пратил.
26 Nimefanya jina lako lijulikane kwao nami nitaendelea kufanya lijulikane, ili kwamba upendo ule unaonipenda mimi uwe ndani yao na mimi mwenyewe nipate kuwa ndani yao.”
И явих им Твоето име, и ще явя, та любовта, с която си Ме възлюбил, да бъде в тях и Аз в тях.

< Yohana 17 >