< Yohana 16 >
1 “Nimewaambia mambo haya yote ili msije mkaiacha imani.
Je vous ai dit ces choses, afin que vous ne soyez point scandalisés.
2 Watawatenga na masinagogi. Naam, saa yaja ambayo mtu yeyote atakayewaua atadhani kwa kufanya hivyo anamtumikia Mungu.
Ils vous chasseront des Synagogues; même le temps vient que quiconque vous fera mourir, croira servir Dieu.
3 Nao watawatenda haya kwa sababu hawamjui Baba wala mimi.
Et ils vous feront ces choses, parce qu'ils n'ont point connu le Père, ni moi.
4 Lakini nimewaambia ninyi mambo haya, ili saa hiyo ikiwadia mpate kukumbuka ya kuwa nilikuwa nimewaambia. Sikuwaambia mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
Mais je vous ai dit ces choses, afin que quand l'heure sera venue, il vous souvienne que je vous les ai dites; et je ne vous ai point dit ces choses dès le commencement, parce que j'étais avec vous.
5 “Sasa mimi ninakwenda kwake yeye aliyenituma, lakini hakuna hata aniulizaye, ‘Unakwenda wapi?’
Mais maintenant je m'en vais à celui qui m'a envoyé, et aucun de vous ne me demande: où vas-tu?
6 Kwa sababu nimewaambia mambo haya, mioyo yenu imejawa na huzuni.
Mais parce que je vous ai dit ces choses, la tristesse a rempli votre cœur.
7 Lakini nawaambia kweli, yafaa mimi niondoke, kwa kuwa nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu, lakini nikienda nitamtuma kwenu.
Toutefois je vous dis la vérité, il vous est avantageux que je m'en aille, car si je ne m'en vais, le Consolateur ne viendra point à vous; mais si je m'en vais, je vous l'enverrai.
8 Naye atakapokuja, atauthibitishia ulimwengu kuhusu dhambi, haki na hukumu.
Et quand il sera venu, il convaincra le monde de péché, de justice, et de jugement.
9 Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi,
De péché, parce qu'ils ne croient point en moi.
10 kwa habari ya haki, kwa sababu ninakwenda kwa Baba, nanyi hamtaniona tena,
De justice, parce que je m'en vais à mon Père, et que vous ne me verrez plus.
11 kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.
De jugement, parce que le Prince de ce monde est [déjà] jugé.
12 “Bado ninayo mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili sasa.
J'ai à vous dire encore plusieurs choses, mais elles sont encore au-dessus de votre portée.
13 Atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza awatie katika kweli yote. Yeye hatanena kwa ajili yake mwenyewe, bali atanena yale yote atakayosikia, naye atawaonyesha mambo yajayo.
Mais quand celui-là, [savoir] l'Esprit de vérité, sera venu, il vous conduira en toute vérité; car il ne parlera point de soi-même, mais il dira tout ce qu'il aura ouï, et il vous annoncera les choses à venir.
14 Atanitukuza mimi, kwa maana atayachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.
Celui-là me glorifiera; car il prendra du mien, et il vous l'annoncera.
15 Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu. Ndiyo maana nimesema Roho atachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.
Tout ce que mon Père a, est mien; c'est pourquoi j'ai dit, qu'il prendra du mien, et qu'il vous l'annoncera.
16 “Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona.”
Dans peu de temps, vous ne me verrez point; et après un peu de temps, vous me verrez: car je m'en vais à mon Père.
17 Baadhi ya wanafunzi wakaulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’? Naye ana maana gani asemapo, ‘Kwa sababu ninakwenda kwa Baba’?”
Et quelques-uns de ses Disciples dirent entre eux: qu'est-ce qu'il nous dit: dans peu de temps, vous ne me verrez point; et un peu de temps après vous me verrez, car je m'en vais à mon Père?
18 Wakaendelea kuulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Kitambo kidogo’? Hatuelewi hilo analosema.”
Ils disaient donc: que signifient ces mots: un peu de temps? nous ne comprenons pas ce qu'il dit.
19 Yesu akatambua kuwa walitaka kumuuliza juu ya hilo, hivyo akawaambia, “Je, mnaulizana nina maana gani niliposema, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’?
Et Jésus connaissant qu'ils le voulaient interroger, leur dit: vous demandez entre vous touchant ce que j'ai dit: dans peu de temps, vous ne me verrez plus, et un peu de temps après vous me verrez.
20 Amin, amin nawaambia, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi. Ninyi mtahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
En vérité, en vérité je vous dis, que vous pleurerez et vous vous lamenterez, et le monde se réjouira; vous serez, dis-je, attristés; mais votre tristesse sera changée en joie.
21 Mwanamke anapokuwa na utungu wa kuzaa huwa na maumivu kwa sababu saa yake imewadia. Lakini mtoto akiisha kuzaliwa, yule mwanamke husahau maumivu hayo kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtoto ulimwenguni.
Quand une femme accouche, elle sent des douleurs, parce que son terme est venu, mais après qu'elle a fait un petit enfant, il ne lui souvient plus de ses douleurs, à cause de la joie qu'elle a de ce qu'elle a mis un homme au monde.
22 Hivyo ninyi mna maumivu sasa, lakini nitawaona tena, nayo mioyo yenu itafurahi na furaha yenu hakuna awaondoleaye.
Vous avez donc aussi maintenant de la tristesse; mais je vous reverrai encore, et votre cœur se réjouira, et personne ne vous ôtera votre joie.
23 Katika siku hiyo hamtaniuliza neno lolote. Amin, amin nawaambia, kama mkimwomba Baba jambo lolote kwa jina langu, yeye atawapa.
Et en ce jour-là vous ne m'interrogerez de rien. En vérité, en vérité je vous dis, que toutes les choses que vous demanderez au Père en mon Nom, il vous les donnera.
24 Mpaka sasa hamjaomba jambo lolote kwa Jina langu. Ombeni nanyi mtapewa, ili furaha yenu ipate kuwa kamili.
Jusqu'à présent vous n'avez rien demandé en mon Nom; demandez, et vous recevrez, afin que votre joie soit parfaite.
25 “Nimewaambia mambo haya kwa mafumbo. Saa yaja ambapo sitazungumza nanyi tena kwa mafumbo bali nitawaeleza waziwazi kuhusu Baba.
Je vous ai dit ces choses par des similitudes, mais l'heure vient que je ne vous parlerai plus par des paraboles; mais je vous parlerai ouvertement de [mon] Père.
26 Siku hiyo mtaomba kwa Jina langu. Wala sitawaambia kwamba nitamwomba Baba kwa ajili yenu,
En ce jour-là vous demanderez [des grâces] en mon Nom, et je ne vous dis pas que je prierai le Père pour vous;
27 kwa maana Baba mwenyewe anawapenda, kwa sababu mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu.
Car le Père lui-même vous aime, parce que vous m'avez aimé, et que vous avez cru, que je suis issu de Dieu.
28 Nilitoka kwa Baba na kuja ulimwenguni, sasa naondoka ulimwenguni na kurudi kwa Baba.”
Je suis issu du Père, et je suis venu au monde; [et] encore, je laisse le monde, et je m'en vais au Père.
29 Ndipo wanafunzi wake wakasema, “Sasa unazungumza waziwazi, wala si kwa mafumbo.
Ses Disciples lui dirent: voici, maintenant tu parles ouvertement, et tu n'uses plus de paraboles.
30 Sasa tumejua kwamba wewe unajua mambo yote, wala hakuna haja ya mtu kukuuliza maswali. Kwa jambo hili tunaamini kwamba ulitoka kwa Mungu.”
Maintenant nous connaissons que tu sais toutes choses, et que tu n'as pas besoin que personne t'interroge; à cause de cela nous croyons que tu es issu de Dieu.
31 Yesu akawajibu, “Je, sasa mnaamini?
Jésus leur répondit: croyez vous maintenant?
32 Saa inakuja, naam, imekwisha kuwadia, mtakapotawanyika kila mmoja kwenda nyumbani kwake na kuniacha peke yangu. Lakini mimi siko peke yangu kwa sababu Baba yu pamoja nami.
Voici, l'heure vient, et elle est déjà venue, que vous serez dispersés chacun de son côté, et vous me laisserez seul; mais je ne suis point seul, car le Père est avec moi.
33 Nimewaambia mambo haya, ili mpate kuwa na amani mkiwa ndani yangu. Ulimwenguni mtapata dhiki. Lakini jipeni moyo, kwa maana mimi nimeushinda ulimwengu.”
Je vous ai dit ces choses afin que vous ayez la paix en moi; vous aurez de l'angoisse au monde, mais ayez bon courage, j'ai vaincu le monde.