< Yohana 16 >
1 “Nimewaambia mambo haya yote ili msije mkaiacha imani.
I've told you this so you won't give up your trust in me.
2 Watawatenga na masinagogi. Naam, saa yaja ambayo mtu yeyote atakayewaua atadhani kwa kufanya hivyo anamtumikia Mungu.
They will expel you from the synagogues—in fact the time is coming when those who kill you will think they are doing God a service.
3 Nao watawatenda haya kwa sababu hawamjui Baba wala mimi.
They'll do this because they have never known the Father or me. I've told you this so that when these things happen, you'll remember what I told you.
4 Lakini nimewaambia ninyi mambo haya, ili saa hiyo ikiwadia mpate kukumbuka ya kuwa nilikuwa nimewaambia. Sikuwaambia mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
I didn't need to tell you this right at the beginning because I was going to be with you.
5 “Sasa mimi ninakwenda kwake yeye aliyenituma, lakini hakuna hata aniulizaye, ‘Unakwenda wapi?’
But now I'm going to the one who sent me, and yet not one of you is asking me, ‘Where are you going?’
6 Kwa sababu nimewaambia mambo haya, mioyo yenu imejawa na huzuni.
Of course, now that I've told you, you're full of grief.
7 Lakini nawaambia kweli, yafaa mimi niondoke, kwa kuwa nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu, lakini nikienda nitamtuma kwenu.
But I'm telling you the truth: it's better for you that I go away, for if I don't the Comforter won't come to you. If I go away, I will send him to you.
8 Naye atakapokuja, atauthibitishia ulimwengu kuhusu dhambi, haki na hukumu.
When he comes, he will convince those in the world that they have wrong ideas regarding sin, about what is right, and about judgment:
9 Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi,
Sin, for they don't trust in me.
10 kwa habari ya haki, kwa sababu ninakwenda kwa Baba, nanyi hamtaniona tena,
What is right, for I'm going to the Father and you won't see me any longer.
11 kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.
Judgment, for the ruler of this world has been condemned.
12 “Bado ninayo mambo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili sasa.
There's much more I want to explain to you, but you couldn't stand it now.
13 Atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza awatie katika kweli yote. Yeye hatanena kwa ajili yake mwenyewe, bali atanena yale yote atakayosikia, naye atawaonyesha mambo yajayo.
However, when the Spirit of truth comes, he will teach you the whole truth. He doesn't speak for himself, but he only says what he hears, and he will tell you what's going to happen.
14 Atanitukuza mimi, kwa maana atayachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.
He brings me glory for he teaches you whatever he receives from me.
15 Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu. Ndiyo maana nimesema Roho atachukua yaliyo yangu na kuwajulisha ninyi.
All that belongs to the Father is mine. This is why I said that the Spirit teaches you whatever he receives from me.
16 “Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona.”
In a little while you won't see me anymore, but then a little while after that you will see me.”
17 Baadhi ya wanafunzi wakaulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’? Naye ana maana gani asemapo, ‘Kwa sababu ninakwenda kwa Baba’?”
Some of his disciples said to one another, “What does he mean, ‘In a little while you won't see me, but a little while after that you will see me’? and ‘For I'm going to the Father’?”
18 Wakaendelea kuulizana, “Ana maana gani asemapo, ‘Kitambo kidogo’? Hatuelewi hilo analosema.”
They were asking, “What does he mean by ‘in a little while’? We don't know what he's talking about.”
19 Yesu akatambua kuwa walitaka kumuuliza juu ya hilo, hivyo akawaambia, “Je, mnaulizana nina maana gani niliposema, ‘Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona’?
Jesus realized that they wanted to ask him about this. So he asked them, “Are you wondering about my comment, ‘In a little while you won't see me, but a little while after that you will see me’?
20 Amin, amin nawaambia, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi. Ninyi mtahuzunika, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
I tell you the truth, you will weep and mourn, but the world will rejoice. You will grieve, but your grief will turn into joy.
21 Mwanamke anapokuwa na utungu wa kuzaa huwa na maumivu kwa sababu saa yake imewadia. Lakini mtoto akiisha kuzaliwa, yule mwanamke husahau maumivu hayo kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtoto ulimwenguni.
A woman in labor suffers pain because her time has come, but once the baby is born, she forgets the agony because of the joy that a child has been brought into the world.
22 Hivyo ninyi mna maumivu sasa, lakini nitawaona tena, nayo mioyo yenu itafurahi na furaha yenu hakuna awaondoleaye.
Yes, you're grieving now, but I will see you again; and you will rejoice, and no one can take away your joy.
23 Katika siku hiyo hamtaniuliza neno lolote. Amin, amin nawaambia, kama mkimwomba Baba jambo lolote kwa jina langu, yeye atawapa.
When that time comes you won't need to ask me for anything. I tell you the truth, the Father will give you whatever you ask in my name.
24 Mpaka sasa hamjaomba jambo lolote kwa Jina langu. Ombeni nanyi mtapewa, ili furaha yenu ipate kuwa kamili.
Until now you haven't asked for anything in my name, so ask and you shall receive, and your happiness will be complete.
25 “Nimewaambia mambo haya kwa mafumbo. Saa yaja ambapo sitazungumza nanyi tena kwa mafumbo bali nitawaeleza waziwazi kuhusu Baba.
I've been talking to you using picture language. But soon I won't use such picture language any more when I speak to you. Instead I'll explain the Father to you very plainly.
26 Siku hiyo mtaomba kwa Jina langu. Wala sitawaambia kwamba nitamwomba Baba kwa ajili yenu,
At that time you will ask in my name. I'm not saying to you that I will plead with the Father on your behalf,
27 kwa maana Baba mwenyewe anawapenda, kwa sababu mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu.
for the Father himself loves you—because you love me and believe that I came from God.
28 Nilitoka kwa Baba na kuja ulimwenguni, sasa naondoka ulimwenguni na kurudi kwa Baba.”
I left the Father and came into the world; now I leave the world and return to my Father.”
29 Ndipo wanafunzi wake wakasema, “Sasa unazungumza waziwazi, wala si kwa mafumbo.
Then the disciples said, “Now you're talking very plainly and not using picture language.
30 Sasa tumejua kwamba wewe unajua mambo yote, wala hakuna haja ya mtu kukuuliza maswali. Kwa jambo hili tunaamini kwamba ulitoka kwa Mungu.”
Now we're certain that you know everything, and that in order to know what questions people are thinking you don't need to ask them. This convinces us that you came from God.”
31 Yesu akawajibu, “Je, sasa mnaamini?
“Are you really convinced now?” Jesus asked.
32 Saa inakuja, naam, imekwisha kuwadia, mtakapotawanyika kila mmoja kwenda nyumbani kwake na kuniacha peke yangu. Lakini mimi siko peke yangu kwa sababu Baba yu pamoja nami.
“The time is coming—in fact it's just about to happen—when you will be scattered, each of you to your own homes, leaving me all alone. But I'm not really alone, for the Father is with me.
33 Nimewaambia mambo haya, ili mpate kuwa na amani mkiwa ndani yangu. Ulimwenguni mtapata dhiki. Lakini jipeni moyo, kwa maana mimi nimeushinda ulimwengu.”
I've told you all this so that you may have peace because you are one with me. You will suffer in this world, but be brave—I have defeated the world!”