< Yohana 13 >

1 Ilikuwa mara tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua ya kuwa wakati wake wa kuondoka ulimwenguni ili kurudi kwa Baba umewadia. Alikuwa amewapenda watu wake waliokuwa ulimwenguni, naam, aliwapenda hadi kipimo cha mwisho.
Un priekš Lieldienas svētkiem Jēzus zinādams, ka Viņa laiks bija nācis, no šīs pasaules iet pie Tā Tēva, tā kā Viņš mīlējis tos savējos, kas bija pasaulē, tā Viņš tos mīlēja līdz galam.
2 Wakati alipokuwa akila chakula cha jioni na wanafunzi wake, ibilisi alikuwa amekwisha kutia ndani ya moyo wa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni, wazo la kumsaliti Yesu.
Un vakariņu ēdot, (kad jau velns Jūdasam Iskariotam, Sīmaņa dēlam, sirdī bija iedevis, Viņu nodot),
3 Yesu akijua ya kwamba Baba ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake na kwamba yeye alitoka kwa Mungu na alikuwa anarudi kwa Mungu,
Jēzus, zinādams, ka Tas Tēvs Viņam visas lietas bija devis rokās, un ka Viņš nācis no Dieva un aizies pie Dieva,
4 hivyo aliondoka chakulani, akavua vazi lake la nje, akajifunga kitambaa kiunoni.
Cēlās no vakariņa, novilka savus svārkus un priekšautu ņēmis ar to apsējās.
5 Kisha akamimina maji kwenye sinia na kuanza kuwanawisha wanafunzi wake miguu na kuikausha kwa kile kitambaa alichokuwa amejifunga kiunoni.
Pēc Viņš ūdeni lej traukā un iesāka tiem mācekļiem kājas mazgāt un tās žāvēt ar to priekšautu, ar ko Viņš bija apsējies.
6 Alipomfikia Simoni Petro, Petro akamwambia, “Bwana, je, wewe utaninawisha mimi miguu?”
Tad Viņš nāk pie Sīmaņa Pētera. Tas uz Viņu saka: “Kungs, vai Tu man kājas mazgāsi?”
7 Yesu akamjibu, “Hivi sasa hutambui lile ninalofanya, lakini baadaye utaelewa.”
Jēzus atbildēja un uz to sacīja: “Ko Es daru, to tu tagad nezini, bet pēc tu to sapratīsi.”
8 Petro akamwambia, “La, wewe hutaninawisha miguu kamwe.” Yesu akamjibu, “Kama nisipokunawisha, wewe huna sehemu nami.” (aiōn g165)
Tad Pēteris uz Viņu saka: “Nemūžam Tev nebūs manas kājas mazgāt.” Jēzus tam atbildēja: “Ja Es tevi nemazgāšu, tad tev nebūs daļas ar Mani.” (aiōn g165)
9 Ndipo Simoni Petro akajibu, “Usininawishe miguu peke yake, Bwana, bali pamoja na mikono na kichwa pia!”
Sīmanis Pēteris uz Viņu saka: “Kungs, nevien manas kājas, bet arī rokas un galvu!”
10 Yesu akamjibu, “Mtu aliyekwisha kuoga anahitaji kunawa miguu tu, kwani mwili wake wote ni safi. Ninyi ni safi, ingawa si kila mmoja wenu.”
Jēzus uz to saka: “Kas ir mazgāts, tam nevajag kā vien kājas mazgāt, bet viņš ir viscaur šķīsts. Jūs arī esat šķīsti, bet ne visi.”
11 Kwa kuwa yeye alijua ni nani ambaye angemsaliti, ndiyo sababu akasema si kila mmoja aliyekuwa safi.
Jo Viņš Savu nodevēju gan zināja; tāpēc Viņš sacīja: “Jūs neesat visi šķīsti.”
12 Alipomaliza kuwanawisha miguu yao, alivaa tena mavazi yake, akarudi alikokuwa ameketi, akawauliza, “Je, mmeelewa nililowafanyia?
Kad Tas nu viņu kājas bija mazgājis, tad Viņš ņēma savus svārkus un atkal nosēdās un uz tiem sacīja: “Vai jūs zināt, ko Es jums esmu darījis?
13 Ninyi mnaniita mimi ‘Mwalimu’ na ‘Bwana,’ hii ni sawa, maana ndivyo nilivyo.
Jūs Mani saucat par Mācītāju un par Kungu, un tas pareizi runāts, jo Es tas esmu.
14 Kwa hiyo, ikiwa mimi niliye Bwana wenu na Mwalimu wenu nimewanawisha ninyi miguu, pia hamna budi kunawishana miguu ninyi kwa ninyi.
Ja tad Es, jūsu Kungs un Mācītājs, jūsu kājas esmu mazgājis, tad arī jums būs cits citam kājas mazgāt.
15 Mimi nimewawekea kielelezo kwamba imewapasa kutenda kama vile nilivyowatendea ninyi.
Jo Es jums priekšzīmi esmu devis, lai jūs darāt, kā Es jums esmu darījis.
16 Amin, amin nawaambia, mtumishi si mkuu kuliko bwana wake, wala aliyetumwa si mkuu kuliko yule aliyemtuma.
Patiesi, patiesi, Es jums saku: kalps nav lielāks par savu kungu, nedz, kas sūtīts, lielāks par to, kas viņu sūtījis.
17 Sasa kwa kuwa mmejua mambo haya, heri yenu ninyi kama mkiyatenda.
Ja jūs tā zināt, svētīgi jūs esat, kad jūs to darāt.
18 “Sisemi hivi kuhusu ninyi nyote. Ninawajua wale niliowachagua. Lakini ni ili Andiko lipate kutimia, kwamba, ‘Yeye aliyekula chakula changu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.’
Es nerunāju par jums visiem; Es zinu, kurus Es esmu izredzējis; bet lai tas raksts piepildās: kas ar Mani maizi ēd, tas Mani min ar kājām.
19 “Ninawaambia mambo haya kabla hayajatukia, ili yatakapotukia mpate kuamini ya kuwa Mimi ndiye.
Tagad Es jums to saku, pirms tas notiek, lai, kad tas notiek, jūs ticat, ka Es Tas esmu.
20 Amin, amin nawaambia, yeyote anayempokea yule niliyemtuma anipokea mimi, naye anipokeaye mimi ampokea yeye aliyenituma mimi.”
Patiesi, patiesi, Es jums saku: kas uzņem, ja Es kādu sūtīšu, tas Mani uzņem; un kas Mani uzņem, tas uzņem To, kas Mani sūtījis.”
21 Baada ya kusema haya, Yesu alifadhaika sana moyoni, akasema, “Amin, amin nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
To sacījis, Jēzus garā aizgrābts liecināja un sacīja: “Patiesi, Es jums saku, viens no jums Mani nodos.”
22 Wanafunzi wake wakatazamana bila kujua kuwa alikuwa anamsema nani.
Tad tie mācekļi cits uz citu skatījās, nezinādami, par kuru Tas runā.
23 Mmoja wa wanafunzi wake ambaye Yesu alimpenda sana, alikuwa ameegama kifuani mwa Yesu.
Un viens no viņa mācekļiem sēdēja pie Jēzus krūtīm, to Jēzus mīlēja.
24 Simoni Petro akampungia mkono yule mwanafunzi, akamwambia, “Muulize anamaanisha nani.”
Tad Sīmanis Pēteris šim met ar acīm, lai vaicā, kurš tas esot, par ko Viņš runā?
25 Yule mwanafunzi akamwegemea Yesu, akamuuliza, “Bwana, tuambie, ni nani?”
Un tas pielocīdamies pie Jēzus krūtīm uz Viņu saka: “Kungs, kurš tas ir?”
26 Yesu akajibu, “Ni yule nitakayempa hiki kipande cha mkate baada ya kukichovya kwenye bakuli.” Hivyo baada ya kukichovya kile kipande cha mkate, akampa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni.
Jēzus atbild: “Tas ir tas, kam Es to kumosu iemērktu došu;” tad Viņš iemērca to kumosu un dod to Jūdasam, Sīmaņa dēlam, Iskariotam.
27 Mara tu baada ya kukipokea kile kipande cha mkate, Shetani akamwingia. Yesu akamwambia Yuda, “Lile unalotaka kulitenda litende haraka.”
Un pēc tā kumosa tad sātans iegāja iekš tā. Tad Jēzus uz to saka: “Ko tu dari, to dari drīz.”
28 Hakuna hata mmoja wa wale waliokuwa wameketi naye mezani aliyeelewa kwa nini Yesu alimwambia hivyo.
Bet neviens no tiem, kas tur klāt sēdēja, nesaprata, kāpēc Viņš tam to sacīja.
29 Kwa kuwa Yuda alikuwa mtunza fedha, wengine walifikiri Yesu alikuwa amemwambia akanunue vitu vilivyohitajika kwa ajili ya Sikukuu, au kuwapa maskini chochote.
Jo kādiem šķita, tāpēc ka Jūdasam tas maks bija, ka Jēzus uz viņu saka: pērc, ko mums uz svētkiem vajag; vai lai viņš nabagiem ko dotu.
30 Mara tu baada ya kupokea ule mkate, Yuda akatoka nje. Wakati huo ulikuwa ni usiku.
Tad nu, to kumosu ņēmis, viņš izgāja tūdaļ ārā, un nakts bija.
31 Baada ya Yuda kutoka nje, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Adamu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
Kad viņš nu bija izgājis, tad Jēzus saka: “Tagad Tas Cilvēka Dēls ir pagodināts, un Dievs ir pagodināts iekš Viņa.
32 Ikiwa Mungu ametukuzwa ndani ya Mwana, Mungu atamtukuza Mwana ndani yake mwenyewe naye atamtukuza mara.
Ja Dievs ir pagodināts iekš Viņa, tad arī Dievs Viņu pagodinās iekš Sevis paša un Viņu drīz pagodinās.
33 “Watoto wangu, mimi bado niko pamoja nanyi kwa kitambo kidogo. Mtanitafuta, na kama vile nilivyowaambia Wayahudi, vivyo hivyo sasa nawaambia na ninyi. Niendako, ninyi hamwezi kuja.
Bērniņi, Es vēl mazu brīdi esmu pie jums. Jūs Mani meklēsiet, un kā Es tiem Jūdiem esmu sacījis: uz kurieni Es eju, tur jūs nevarat nākt; tā Es jums tagad saku.
34 “Amri mpya nawapa: Mpendane kama mimi nilivyowapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi mpendane.
Jaunu bausli Es jums dodu, ka jūs cits citu mīlējāt, itin kā Es jūs esmu mīlējis, ka arī jūs cits citu mīlējiet.
35 Kama mkipendana ninyi kwa ninyi, kwa njia hii, watu wote watajua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu.”
Pie tam visi nomanīs, ka jūs esat Mani mācekļi, ja jums ir mīlestība savā starpā.”
36 Simoni Petro akamuuliza, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akamjibu, “Ninakokwenda huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”
Sīmanis Pēteris uz Viņu saka: “Kungs, kurp Tu ej?” Jēzus tam atbildēja: “Kur Es eju, tur tu tagad Man nevari nākt pakaļ, bet pēcgalā tu Man nāksi pakaļ.”
37 Petro akamuuliza tena, “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Mimi niko tayari kuutoa uhai wangu kwa ajili yako.”
Pēteris uz Viņu saka: “Kungs, kāpēc es tagad Tev nevaru iet pakaļ? Savu dzīvību es par Tevi nodošu.”
38 Yesu akamjibu, “Je, ni kweli uko tayari kuutoa uhai wako kwa ajili yangu? Amin, amin nakuambia, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
Jēzus tam atbildēja: “Vai tu par Mani savu dzīvību nodosi? Patiesi, patiesi, Es tev saku: gailis nedziedās, pirms tu trīskārt Mani neaizliegsi.

< Yohana 13 >