< Yohana 13 >

1 Ilikuwa mara tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua ya kuwa wakati wake wa kuondoka ulimwenguni ili kurudi kwa Baba umewadia. Alikuwa amewapenda watu wake waliokuwa ulimwenguni, naam, aliwapenda hadi kipimo cha mwisho.
Or, avant la fête de la Pâque, Jésus, sachant que son heure était venue de quitter ce monde pour le Père, ayant aimé les siens qui étaient dans le monde, les aima jusqu'à la fin.
2 Wakati alipokuwa akila chakula cha jioni na wanafunzi wake, ibilisi alikuwa amekwisha kutia ndani ya moyo wa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni, wazo la kumsaliti Yesu.
Pendant le repas, le diable ayant déjà mis dans le cœur de Judas Iscariote, fils de Simon, le désir de le trahir,
3 Yesu akijua ya kwamba Baba ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake na kwamba yeye alitoka kwa Mungu na alikuwa anarudi kwa Mungu,
Jésus, sachant que le Père avait remis toutes choses entre ses mains, qu'il venait de Dieu et qu'il allait à Dieu,
4 hivyo aliondoka chakulani, akavua vazi lake la nje, akajifunga kitambaa kiunoni.
se leva du repas et mit de côté ses vêtements de dessus. Il prit une serviette et s'en enveloppa la taille.
5 Kisha akamimina maji kwenye sinia na kuanza kuwanawisha wanafunzi wake miguu na kuikausha kwa kile kitambaa alichokuwa amejifunga kiunoni.
Puis il versa de l'eau dans la cuvette, se mit à laver les pieds des disciples et à les essuyer avec la serviette dont il était enveloppé.
6 Alipomfikia Simoni Petro, Petro akamwambia, “Bwana, je, wewe utaninawisha mimi miguu?”
Puis il s'approcha de Simon Pierre. Il lui dit: « Seigneur, est-ce toi qui me laves les pieds? »
7 Yesu akamjibu, “Hivi sasa hutambui lile ninalofanya, lakini baadaye utaelewa.”
Jésus lui répondit: « Tu ne sais pas ce que je fais maintenant, mais tu comprendras plus tard. »
8 Petro akamwambia, “La, wewe hutaninawisha miguu kamwe.” Yesu akamjibu, “Kama nisipokunawisha, wewe huna sehemu nami.” (aiōn g165)
Pierre lui dit: « Tu ne me laveras jamais les pieds! » Jésus lui répondit: « Si je ne te lave pas, tu n'as rien à faire avec moi. » (aiōn g165)
9 Ndipo Simoni Petro akajibu, “Usininawishe miguu peke yake, Bwana, bali pamoja na mikono na kichwa pia!”
Simon-Pierre lui dit: « Seigneur, non seulement mes pieds, mais aussi mes mains et ma tête! »
10 Yesu akamjibu, “Mtu aliyekwisha kuoga anahitaji kunawa miguu tu, kwani mwili wake wote ni safi. Ninyi ni safi, ingawa si kila mmoja wenu.”
Jésus lui dit: « Quelqu'un qui s'est baigné n'a besoin que de se laver les pieds, mais il est complètement pur. Vous êtes purs, mais pas tous. »
11 Kwa kuwa yeye alijua ni nani ambaye angemsaliti, ndiyo sababu akasema si kila mmoja aliyekuwa safi.
Car il connaissait celui qui allait le trahir; c'est pourquoi il dit: « Vous n'êtes pas tous purs. »
12 Alipomaliza kuwanawisha miguu yao, alivaa tena mavazi yake, akarudi alikokuwa ameketi, akawauliza, “Je, mmeelewa nililowafanyia?
Après leur avoir lavé les pieds, remis son vêtement de dessus et s'être assis, il leur dit: « Savez-vous ce que je vous ai fait?
13 Ninyi mnaniita mimi ‘Mwalimu’ na ‘Bwana,’ hii ni sawa, maana ndivyo nilivyo.
Vous m'appelez: « Maître » et « Seigneur ». Vous le dites bien, car je suis ainsi.
14 Kwa hiyo, ikiwa mimi niliye Bwana wenu na Mwalimu wenu nimewanawisha ninyi miguu, pia hamna budi kunawishana miguu ninyi kwa ninyi.
Si donc moi, le Seigneur et le Maître, je vous ai lavé les pieds, vous devez aussi vous laver les pieds les uns aux autres.
15 Mimi nimewawekea kielelezo kwamba imewapasa kutenda kama vile nilivyowatendea ninyi.
Car je vous ai donné un exemple, afin que vous fassiez aussi comme je vous ai fait.
16 Amin, amin nawaambia, mtumishi si mkuu kuliko bwana wake, wala aliyetumwa si mkuu kuliko yule aliyemtuma.
Je vous le dis en vérité, le serviteur n'est pas plus grand que son maître, et l'envoyé n'est pas plus grand que celui qui l'a envoyé.
17 Sasa kwa kuwa mmejua mambo haya, heri yenu ninyi kama mkiyatenda.
Si vous savez ces choses, vous êtes bénis si vous les mettez en pratique.
18 “Sisemi hivi kuhusu ninyi nyote. Ninawajua wale niliowachagua. Lakini ni ili Andiko lipate kutimia, kwamba, ‘Yeye aliyekula chakula changu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.’
Je ne parle pas de vous tous. Je sais qui j'ai choisi, mais c'est pour que s'accomplisse cette parole de l'Écriture: « Celui qui mange le pain avec moi a levé le talon contre moi ».
19 “Ninawaambia mambo haya kabla hayajatukia, ili yatakapotukia mpate kuamini ya kuwa Mimi ndiye.
Désormais, je vous le dis avant que cela n'arrive, afin que, lorsque cela arrivera, vous croyiez que c'est moi.
20 Amin, amin nawaambia, yeyote anayempokea yule niliyemtuma anipokea mimi, naye anipokeaye mimi ampokea yeye aliyenituma mimi.”
Je vous le dis en toute certitude: celui qui reçoit celui que j'envoie, me reçoit; et celui qui me reçoit, reçoit celui qui m'a envoyé. »
21 Baada ya kusema haya, Yesu alifadhaika sana moyoni, akasema, “Amin, amin nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
Après avoir dit cela, Jésus fut troublé en esprit, et il déclara: « Je vous le dis en toute certitude, l'un de vous me livrera. »
22 Wanafunzi wake wakatazamana bila kujua kuwa alikuwa anamsema nani.
Les disciples se regardaient les uns les autres, perplexes quant à la personne dont il parlait.
23 Mmoja wa wanafunzi wake ambaye Yesu alimpenda sana, alikuwa ameegama kifuani mwa Yesu.
Un de ses disciples, que Jésus aimait, était à table, appuyé contre la poitrine de Jésus.
24 Simoni Petro akampungia mkono yule mwanafunzi, akamwambia, “Muulize anamaanisha nani.”
Simon-Pierre lui fit donc signe de venir, et lui dit: « Dis-nous qui est celui dont il parle. »
25 Yule mwanafunzi akamwegemea Yesu, akamuuliza, “Bwana, tuambie, ni nani?”
Lui, s'appuyant, comme il l'était, sur la poitrine de Jésus, lui demanda: « Seigneur, qui est-ce? »
26 Yesu akajibu, “Ni yule nitakayempa hiki kipande cha mkate baada ya kukichovya kwenye bakuli.” Hivyo baada ya kukichovya kile kipande cha mkate, akampa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni.
Jésus répondit donc: « C'est celui à qui je donnerai ce morceau de pain quand je l'aurai trempé. » Ayant donc trempé le morceau de pain, il le donna à Judas, fils de Simon Iscariot.
27 Mara tu baada ya kukipokea kile kipande cha mkate, Shetani akamwingia. Yesu akamwambia Yuda, “Lile unalotaka kulitenda litende haraka.”
Après le morceau de pain, Satan entra en lui. Alors Jésus lui dit: « Ce que tu fais, fais-le vite. »
28 Hakuna hata mmoja wa wale waliokuwa wameketi naye mezani aliyeelewa kwa nini Yesu alimwambia hivyo.
Or, personne à table ne savait pourquoi il lui disait cela.
29 Kwa kuwa Yuda alikuwa mtunza fedha, wengine walifikiri Yesu alikuwa amemwambia akanunue vitu vilivyohitajika kwa ajili ya Sikukuu, au kuwapa maskini chochote.
Car quelques-uns pensaient, parce que Judas avait la tirelire, que Jésus lui avait dit: « Achète ce dont nous avons besoin pour la fête », ou qu'il devait donner quelque chose aux pauvres.
30 Mara tu baada ya kupokea ule mkate, Yuda akatoka nje. Wakati huo ulikuwa ni usiku.
Ayant donc reçu ce morceau, il sortit aussitôt. C'était la nuit.
31 Baada ya Yuda kutoka nje, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Adamu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
Lorsqu'il fut sorti, Jésus dit: Maintenant, le Fils de l'homme a été glorifié, et Dieu a été glorifié en lui.
32 Ikiwa Mungu ametukuzwa ndani ya Mwana, Mungu atamtukuza Mwana ndani yake mwenyewe naye atamtukuza mara.
Si Dieu a été glorifié en lui, Dieu le glorifiera aussi en lui-même, et il le glorifiera aussitôt.
33 “Watoto wangu, mimi bado niko pamoja nanyi kwa kitambo kidogo. Mtanitafuta, na kama vile nilivyowaambia Wayahudi, vivyo hivyo sasa nawaambia na ninyi. Niendako, ninyi hamwezi kuja.
Petits enfants, je vais rester encore un peu avec vous. Vous me chercherez, et comme j'ai dit aux Juifs: « Là où je vais, vous ne pouvez pas venir », je vous le dis maintenant.
34 “Amri mpya nawapa: Mpendane kama mimi nilivyowapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi mpendane.
Je vous donne un commandement nouveau: aimez-vous les uns les autres. Comme je vous ai aimés, vous aussi, aimez-vous les uns les autres.
35 Kama mkipendana ninyi kwa ninyi, kwa njia hii, watu wote watajua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu.”
A ceci tous reconnaîtront que vous êtes mes disciples, si vous avez de l'amour les uns pour les autres. »
36 Simoni Petro akamuuliza, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akamjibu, “Ninakokwenda huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”
Simon-Pierre lui dit: « Seigneur, où vas-tu? » Jésus répondit: « Là où je vais, vous ne pouvez pas me suivre maintenant, mais vous me suivrez après. »
37 Petro akamuuliza tena, “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Mimi niko tayari kuutoa uhai wangu kwa ajili yako.”
Pierre lui dit: « Seigneur, pourquoi ne puis-je pas te suivre maintenant? Je donnerai ma vie pour toi. »
38 Yesu akamjibu, “Je, ni kweli uko tayari kuutoa uhai wako kwa ajili yangu? Amin, amin nakuambia, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
Jésus lui répondit: « Veux-tu donner ta vie pour moi? En vérité, je te le dis, le coq ne chantera pas avant que tu ne m'aies renié trois fois.

< Yohana 13 >