< Yohana 13 >

1 Ilikuwa mara tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua ya kuwa wakati wake wa kuondoka ulimwenguni ili kurudi kwa Baba umewadia. Alikuwa amewapenda watu wake waliokuwa ulimwenguni, naam, aliwapenda hadi kipimo cha mwisho.
Jesus having perceived, before the feast of the passover, that his time to remove out of this world to his Father, was come; and having loved his own, who were in the world, he loved them to the last.
2 Wakati alipokuwa akila chakula cha jioni na wanafunzi wake, ibilisi alikuwa amekwisha kutia ndani ya moyo wa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni, wazo la kumsaliti Yesu.
Now while they were at the supper, (the devil having already put it into the heart of Judas Iscariot, Simon's son, to betray him, )
3 Yesu akijua ya kwamba Baba ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake na kwamba yeye alitoka kwa Mungu na alikuwa anarudi kwa Mungu,
Jesus, though he knew that the Father had subjected everything to him, and that he came from God, and was returning to God;
4 hivyo aliondoka chakulani, akavua vazi lake la nje, akajifunga kitambaa kiunoni.
arose from supper, and laying aside his mantle, girt himself about with a towel.
5 Kisha akamimina maji kwenye sinia na kuanza kuwanawisha wanafunzi wake miguu na kuikausha kwa kile kitambaa alichokuwa amejifunga kiunoni.
Then he poured water into a basin, and began to wash the feet of his disciples, and to wipe them with the towel with which he was girded.
6 Alipomfikia Simoni Petro, Petro akamwambia, “Bwana, je, wewe utaninawisha mimi miguu?”
When he came to Simon Peter, Peter said to him, Master, would you wash my feet?
7 Yesu akamjibu, “Hivi sasa hutambui lile ninalofanya, lakini baadaye utaelewa.”
Jesus answered, At present you do not comprehend what I am doing; but you shall know hereafter.
8 Petro akamwambia, “La, wewe hutaninawisha miguu kamwe.” Yesu akamjibu, “Kama nisipokunawisha, wewe huna sehemu nami.” (aiōn g165)
Peter replied, You shall never wash my feet. Jesus answered, Unless I wash you, you can have no part with me. (aiōn g165)
9 Ndipo Simoni Petro akajibu, “Usininawishe miguu peke yake, Bwana, bali pamoja na mikono na kichwa pia!”
Simon Peter said to him, Master, not my feet only; but also my hands and my head.
10 Yesu akamjibu, “Mtu aliyekwisha kuoga anahitaji kunawa miguu tu, kwani mwili wake wote ni safi. Ninyi ni safi, ingawa si kila mmoja wenu.”
Jesus replied, He who has been bathing, needs only to wash his feet; the rest of his body being clean.
11 Kwa kuwa yeye alijua ni nani ambaye angemsaliti, ndiyo sababu akasema si kila mmoja aliyekuwa safi.
You are clean, but not all. For he knew who would betray him; therefore he said, You are not all clean.
12 Alipomaliza kuwanawisha miguu yao, alivaa tena mavazi yake, akarudi alikokuwa ameketi, akawauliza, “Je, mmeelewa nililowafanyia?
After he had washed their feet, he put on his mantle, and replacing himself at table, said to them, Do you understand what I have been doing to you?
13 Ninyi mnaniita mimi ‘Mwalimu’ na ‘Bwana,’ hii ni sawa, maana ndivyo nilivyo.
You call me the Teacher and the Master; and you say right; for so I am.
14 Kwa hiyo, ikiwa mimi niliye Bwana wenu na Mwalimu wenu nimewanawisha ninyi miguu, pia hamna budi kunawishana miguu ninyi kwa ninyi.
If I, then, the Master and the Teacher, have washed your feet; you also ought to wash one another's feet.
15 Mimi nimewawekea kielelezo kwamba imewapasa kutenda kama vile nilivyowatendea ninyi.
For I have given you an example, that you should do as I have done to you.
16 Amin, amin nawaambia, mtumishi si mkuu kuliko bwana wake, wala aliyetumwa si mkuu kuliko yule aliyemtuma.
Most assuredly, I say to you, the servant is not greater than his master, nor is the apostle greater than he who sends him.
17 Sasa kwa kuwa mmejua mambo haya, heri yenu ninyi kama mkiyatenda.
Happy are you, who know these things, provided you practice them.
18 “Sisemi hivi kuhusu ninyi nyote. Ninawajua wale niliowachagua. Lakini ni ili Andiko lipate kutimia, kwamba, ‘Yeye aliyekula chakula changu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.’
I speak not of you all. I know whom I have chosen: but the scripture must be fulfilled, "He that eats at my table, has lifted up his heel against me."
19 “Ninawaambia mambo haya kabla hayajatukia, ili yatakapotukia mpate kuamini ya kuwa Mimi ndiye.
I tell you this now, before it happen; that when it happens, you may believe that I am the Messiah.
20 Amin, amin nawaambia, yeyote anayempokea yule niliyemtuma anipokea mimi, naye anipokeaye mimi ampokea yeye aliyenituma mimi.”
Most assuredly, I say to you, he that receives whomsoever I send, receives me; and he that receives me, receives him who sent me.
21 Baada ya kusema haya, Yesu alifadhaika sana moyoni, akasema, “Amin, amin nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
After uttering these words, Jesus was troubled in spirit, and declared, saying, Most assuredly, I say to you, one of you will betray me.
22 Wanafunzi wake wakatazamana bila kujua kuwa alikuwa anamsema nani.
Then the disciples looked one upon another, doubting of whom he spoke.
23 Mmoja wa wanafunzi wake ambaye Yesu alimpenda sana, alikuwa ameegama kifuani mwa Yesu.
Now one of his disciples, one whom Jesus loved, was lying close to his breast:
24 Simoni Petro akampungia mkono yule mwanafunzi, akamwambia, “Muulize anamaanisha nani.”
Simon Peter, therefore, made a sign to him, to inquire whom he meant.
25 Yule mwanafunzi akamwegemea Yesu, akamuuliza, “Bwana, tuambie, ni nani?”
He, then, reclining on Jesus' bosom, said to him, Master, who is it?
26 Yesu akajibu, “Ni yule nitakayempa hiki kipande cha mkate baada ya kukichovya kwenye bakuli.” Hivyo baada ya kukichovya kile kipande cha mkate, akampa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni.
Jesus answered, It is he to whom I shall give this morsel, after I have dipped it. And having dipped the morsel, he gave it to Judas Iscariot, the son of Simon.
27 Mara tu baada ya kukipokea kile kipande cha mkate, Shetani akamwingia. Yesu akamwambia Yuda, “Lile unalotaka kulitenda litende haraka.”
After receiving the morsel, Satan entered into him. And Jesus said to him, What you do, do quickly.
28 Hakuna hata mmoja wa wale waliokuwa wameketi naye mezani aliyeelewa kwa nini Yesu alimwambia hivyo.
But none at the table knew, why he gave this order.
29 Kwa kuwa Yuda alikuwa mtunza fedha, wengine walifikiri Yesu alikuwa amemwambia akanunue vitu vilivyohitajika kwa ajili ya Sikukuu, au kuwapa maskini chochote.
Some imagined, because Judas had the purse, that Jesus had signified to him to buy necessaries for the festival; or, to give something to the poor.
30 Mara tu baada ya kupokea ule mkate, Yuda akatoka nje. Wakati huo ulikuwa ni usiku.
When Judas had taken the morsel, he immediately went out: and it was night.
31 Baada ya Yuda kutoka nje, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Adamu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
When he was gone, Jesus said, the Son of Man is now glorified, and God is glorified by him.
32 Ikiwa Mungu ametukuzwa ndani ya Mwana, Mungu atamtukuza Mwana ndani yake mwenyewe naye atamtukuza mara.
If God is glorified by him, God also will glorify him by himself, and that without delay.
33 “Watoto wangu, mimi bado niko pamoja nanyi kwa kitambo kidogo. Mtanitafuta, na kama vile nilivyowaambia Wayahudi, vivyo hivyo sasa nawaambia na ninyi. Niendako, ninyi hamwezi kuja.
My children, I have now but a little time to be with you. You will seek me, and what I said to the Jews, Whither I go, you can not come; I say at present to you.
34 “Amri mpya nawapa: Mpendane kama mimi nilivyowapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi mpendane.
A new commandment I give you, that you love one another; that as I have loved you, you also love one another.
35 Kama mkipendana ninyi kwa ninyi, kwa njia hii, watu wote watajua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu.”
By this shall all men know, that you are my disciples, if you have love one to another.
36 Simoni Petro akamuuliza, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akamjibu, “Ninakokwenda huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”
Simon Peter said to him, Master, whither are you going? Jesus answered, Whither I am going, you can not follow me now; but afterward you shall follow me.
37 Petro akamuuliza tena, “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Mimi niko tayari kuutoa uhai wangu kwa ajili yako.”
Peter replied, Master, why can not I follow you presently? I will lay down my life for your sake!
38 Yesu akamjibu, “Je, ni kweli uko tayari kuutoa uhai wako kwa ajili yangu? Amin, amin nakuambia, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
Jesus answered him, Will you lay down your life for my sake? Most assuredly, I say to you, the cock shall not crow, till you have disowned me thrice.

< Yohana 13 >