< Yohana 13 >

1 Ilikuwa mara tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua ya kuwa wakati wake wa kuondoka ulimwenguni ili kurudi kwa Baba umewadia. Alikuwa amewapenda watu wake waliokuwa ulimwenguni, naam, aliwapenda hadi kipimo cha mwisho.
Now before the feast of the passover, Jesus knew that his hour had come that he must go out of this world to his Father; and having loved his own that were in the world, he loved them to the end.
2 Wakati alipokuwa akila chakula cha jioni na wanafunzi wake, ibilisi alikuwa amekwisha kutia ndani ya moyo wa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni, wazo la kumsaliti Yesu.
And supper being over, the devil having already put it into the heart of Judas Iscariot, the son of Simon, to deliver him up,
3 Yesu akijua ya kwamba Baba ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake na kwamba yeye alitoka kwa Mungu na alikuwa anarudi kwa Mungu,
Jesus, knowing that the Father had delivered all things into his hands, and that he had come from God, and was going to God,
4 hivyo aliondoka chakulani, akavua vazi lake la nje, akajifunga kitambaa kiunoni.
arose from supper, and laid aside his garments, and taking a towel, he girded himself.
5 Kisha akamimina maji kwenye sinia na kuanza kuwanawisha wanafunzi wake miguu na kuikausha kwa kile kitambaa alichokuwa amejifunga kiunoni.
Then he poured water into a basin, and began to wash his disciples feet, and to wipe them with the towel with which he was girded.
6 Alipomfikia Simoni Petro, Petro akamwambia, “Bwana, je, wewe utaninawisha mimi miguu?”
Then he came to Simon Peter; and Peter said to him: Lord, dost thou wash my feet?
7 Yesu akamjibu, “Hivi sasa hutambui lile ninalofanya, lakini baadaye utaelewa.”
Jesus answered and said to him: What I am doing you know not now, but you will know hereafter.
8 Petro akamwambia, “La, wewe hutaninawisha miguu kamwe.” Yesu akamjibu, “Kama nisipokunawisha, wewe huna sehemu nami.” (aiōn g165)
Peter said to him: Thou shalt never wash my feet. Jesus answered him: Unless I wash you, you have no part with me. (aiōn g165)
9 Ndipo Simoni Petro akajibu, “Usininawishe miguu peke yake, Bwana, bali pamoja na mikono na kichwa pia!”
Simon Peter said to him: Lord, not my feet only, but my hands and my head.
10 Yesu akamjibu, “Mtu aliyekwisha kuoga anahitaji kunawa miguu tu, kwani mwili wake wote ni safi. Ninyi ni safi, ingawa si kila mmoja wenu.”
Jesus said to him: He that has bathed needs nothing else save to wash his feet, but is wholly clean. And you are clean, but not all.
11 Kwa kuwa yeye alijua ni nani ambaye angemsaliti, ndiyo sababu akasema si kila mmoja aliyekuwa safi.
For he knew who would deliver him up; for this reason he said, You are not all clean.
12 Alipomaliza kuwanawisha miguu yao, alivaa tena mavazi yake, akarudi alikokuwa ameketi, akawauliza, “Je, mmeelewa nililowafanyia?
Therefore, when he had washed their feet, and had taken his garments, he reclined at table again, and said to them: Do you understand what I have done for you?
13 Ninyi mnaniita mimi ‘Mwalimu’ na ‘Bwana,’ hii ni sawa, maana ndivyo nilivyo.
You call me Teacher and Lord; and you say well, for so I am.
14 Kwa hiyo, ikiwa mimi niliye Bwana wenu na Mwalimu wenu nimewanawisha ninyi miguu, pia hamna budi kunawishana miguu ninyi kwa ninyi.
If, then, I, your Lord and your Teacher, have washed your feet, you also ought to wash one another’s feet.
15 Mimi nimewawekea kielelezo kwamba imewapasa kutenda kama vile nilivyowatendea ninyi.
For I have given you an example, that you also may do as I have done for you.
16 Amin, amin nawaambia, mtumishi si mkuu kuliko bwana wake, wala aliyetumwa si mkuu kuliko yule aliyemtuma.
Verily, verily I say to you, the servant is not greater than his master, nor is he that is sent greater than he that sent him.
17 Sasa kwa kuwa mmejua mambo haya, heri yenu ninyi kama mkiyatenda.
If you know these things, blessed are you, if you do them.
18 “Sisemi hivi kuhusu ninyi nyote. Ninawajua wale niliowachagua. Lakini ni ili Andiko lipate kutimia, kwamba, ‘Yeye aliyekula chakula changu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.’
I speak not of you all. I know whom I have chosen: but that the scripture may be fulfilled, He that eats bread with me has lifted up his heel against me.
19 “Ninawaambia mambo haya kabla hayajatukia, ili yatakapotukia mpate kuamini ya kuwa Mimi ndiye.
I tell you this now, before it comes to pass, that when it comes to pass, you may believe that I am he.
20 Amin, amin nawaambia, yeyote anayempokea yule niliyemtuma anipokea mimi, naye anipokeaye mimi ampokea yeye aliyenituma mimi.”
Verily, verily I say to you, he that receives him that I shall send, receives me; and he that receives me, receives him that sent me.
21 Baada ya kusema haya, Yesu alifadhaika sana moyoni, akasema, “Amin, amin nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
When Jesus had spoken these things, he was troubled in spirit, and testified and said: Verily, verily I say to you, that one of you will deliver me up.
22 Wanafunzi wake wakatazamana bila kujua kuwa alikuwa anamsema nani.
Then the disciples looked at one another, doubting of whom he spoke.
23 Mmoja wa wanafunzi wake ambaye Yesu alimpenda sana, alikuwa ameegama kifuani mwa Yesu.
There was reclining on the bosom of Jesus, one of his disciples, whom Jesus loved.
24 Simoni Petro akampungia mkono yule mwanafunzi, akamwambia, “Muulize anamaanisha nani.”
Then Simon Peter beckoned to this one, that he should inquire who it was of whom he spoke.
25 Yule mwanafunzi akamwegemea Yesu, akamuuliza, “Bwana, tuambie, ni nani?”
And he that was reclining on Jesus breast, said to him: Lord, who is it?
26 Yesu akajibu, “Ni yule nitakayempa hiki kipande cha mkate baada ya kukichovya kwenye bakuli.” Hivyo baada ya kukichovya kile kipande cha mkate, akampa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni.
Jesus answered: It is he to whom I shall give this morsel after I have dipped it. And when he had dipped the morsel, he gave it to Judas Iscariot, the son of Simon.
27 Mara tu baada ya kukipokea kile kipande cha mkate, Shetani akamwingia. Yesu akamwambia Yuda, “Lile unalotaka kulitenda litende haraka.”
And after the morsel was given, then Satan entered into him. Then Jesus said to him: What you do, do quickly.
28 Hakuna hata mmoja wa wale waliokuwa wameketi naye mezani aliyeelewa kwa nini Yesu alimwambia hivyo.
But none of those who reclined at table with him knew for what purpose he said this to him.
29 Kwa kuwa Yuda alikuwa mtunza fedha, wengine walifikiri Yesu alikuwa amemwambia akanunue vitu vilivyohitajika kwa ajili ya Sikukuu, au kuwapa maskini chochote.
For some thought, because Judas had the purse, that Jesus had said to him: Buy what we need for the feast; or, that he should give something to the poor.
30 Mara tu baada ya kupokea ule mkate, Yuda akatoka nje. Wakati huo ulikuwa ni usiku.
Then, on receiving the morsel, he immediately went out; and it was night.
31 Baada ya Yuda kutoka nje, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Adamu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
When he had gone out, Jesus said: Now is the Son of man glorified, and God is glorified in him.
32 Ikiwa Mungu ametukuzwa ndani ya Mwana, Mungu atamtukuza Mwana ndani yake mwenyewe naye atamtukuza mara.
If God is glorified in him, God will also glorify him in himself, and will immediately glorify him.
33 “Watoto wangu, mimi bado niko pamoja nanyi kwa kitambo kidogo. Mtanitafuta, na kama vile nilivyowaambia Wayahudi, vivyo hivyo sasa nawaambia na ninyi. Niendako, ninyi hamwezi kuja.
Little children, yet a little while I am with you. You will seek me, and, as I said to the Jews, whither I go, you can not come, so now I say to you.
34 “Amri mpya nawapa: Mpendane kama mimi nilivyowapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi mpendane.
A new commandment I give to you, That you love one another; as I have loved you, that you also love one another.
35 Kama mkipendana ninyi kwa ninyi, kwa njia hii, watu wote watajua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu.”
By this shall all men know that you are my disciples, if you have love one for another.
36 Simoni Petro akamuuliza, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akamjibu, “Ninakokwenda huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”
Simon Peter said to him: Lord, whither goest thou? Jesus answered him: Whither I go, you can not follow me now; but you shall follow me hereafter.
37 Petro akamuuliza tena, “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Mimi niko tayari kuutoa uhai wangu kwa ajili yako.”
Peter said to him: Lord, why can I not follow thee now? I will lay down my life for thee.
38 Yesu akamjibu, “Je, ni kweli uko tayari kuutoa uhai wako kwa ajili yangu? Amin, amin nakuambia, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
Jesus answered him: Will you lay down your life for me? Verily, verily I say to you, the cock will not crow till you have denied me three times.

< Yohana 13 >