< Yohana 13 >
1 Ilikuwa mara tu kabla ya Sikukuu ya Pasaka. Yesu alijua ya kuwa wakati wake wa kuondoka ulimwenguni ili kurudi kwa Baba umewadia. Alikuwa amewapenda watu wake waliokuwa ulimwenguni, naam, aliwapenda hadi kipimo cha mwisho.
逾越节前一天,耶稣知道自己时候已到,将会离开这世界,回到天父那里去。他爱这世上追随他的人,现在他将显示对他们所有的爱。
2 Wakati alipokuwa akila chakula cha jioni na wanafunzi wake, ibilisi alikuwa amekwisha kutia ndani ya moyo wa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni, wazo la kumsaliti Yesu.
吃晚饭的时候,魔鬼已经把出卖耶稣的念头植入西门的儿子——加略人犹大的心里。
3 Yesu akijua ya kwamba Baba ameweka vitu vyote chini ya mamlaka yake na kwamba yeye alitoka kwa Mungu na alikuwa anarudi kwa Mungu,
耶稣知道天父的权力掌控了一切,他知道自己来自上帝,也将回到上帝。
4 hivyo aliondoka chakulani, akavua vazi lake la nje, akajifunga kitambaa kiunoni.
于是他站起身,脱去外衣,在腰上扎了一条毛巾。
5 Kisha akamimina maji kwenye sinia na kuanza kuwanawisha wanafunzi wake miguu na kuikausha kwa kile kitambaa alichokuwa amejifunga kiunoni.
然后倒了一盆水,开始给门徒们洗脚,用腰上的毛巾擦干。
6 Alipomfikia Simoni Petro, Petro akamwambia, “Bwana, je, wewe utaninawisha mimi miguu?”
轮到彼得时,他问到:“主啊,你要给我洗脚吗?”
7 Yesu akamjibu, “Hivi sasa hutambui lile ninalofanya, lakini baadaye utaelewa.”
耶稣回答:“你现在并不知道我在为你做什么,但总有一天会明白。”
8 Petro akamwambia, “La, wewe hutaninawisha miguu kamwe.” Yesu akamjibu, “Kama nisipokunawisha, wewe huna sehemu nami.” (aiōn )
彼得说:“不!不要洗我的脚!”耶稣回答:“如果我不为你洗脚,你和我就没有任何关系了。” (aiōn )
9 Ndipo Simoni Petro akajibu, “Usininawishe miguu peke yake, Bwana, bali pamoja na mikono na kichwa pia!”
彼得说:“主啊,那就不要只是洗我的脚,连我的手和头也都洗吧!”
10 Yesu akamjibu, “Mtu aliyekwisha kuoga anahitaji kunawa miguu tu, kwani mwili wake wote ni safi. Ninyi ni safi, ingawa si kila mmoja wenu.”
耶稣回答:“洗过澡的人只要洗脚就能获得全身的洁净。你们是洁净的,但并非人人如此。”
11 Kwa kuwa yeye alijua ni nani ambaye angemsaliti, ndiyo sababu akasema si kila mmoja aliyekuwa safi.
因为耶稣知道谁出卖了他,所以他说“但并非人人如此。”
12 Alipomaliza kuwanawisha miguu yao, alivaa tena mavazi yake, akarudi alikokuwa ameketi, akawauliza, “Je, mmeelewa nililowafanyia?
耶稣洗完了门徒们的脚,穿上外衣回到座位上坐下,对他们说:“你们理解我为你们所做的一切吗?
13 Ninyi mnaniita mimi ‘Mwalimu’ na ‘Bwana,’ hii ni sawa, maana ndivyo nilivyo.
你们称呼我‘老师’和‘主’,这样称呼没错,我本来就是。
14 Kwa hiyo, ikiwa mimi niliye Bwana wenu na Mwalimu wenu nimewanawisha ninyi miguu, pia hamna budi kunawishana miguu ninyi kwa ninyi.
如果作为主和你们的老师,仍然为你们洗脚,你们也应当为彼此洗脚。
15 Mimi nimewawekea kielelezo kwamba imewapasa kutenda kama vile nilivyowatendea ninyi.
我为你们做出榜样,希望你们也能做我所做的事情。
16 Amin, amin nawaambia, mtumishi si mkuu kuliko bwana wake, wala aliyetumwa si mkuu kuliko yule aliyemtuma.
实话实说,仆人不能高于主人,奉命行事之人不能高过派遣他之人。
17 Sasa kwa kuwa mmejua mambo haya, heri yenu ninyi kama mkiyatenda.
既然你们已经理解了这些事,付诸行动就会有福报。
18 “Sisemi hivi kuhusu ninyi nyote. Ninawajua wale niliowachagua. Lakini ni ili Andiko lipate kutimia, kwamba, ‘Yeye aliyekula chakula changu, ameinua kisigino chake dhidi yangu.’
但我并不是说你们所有人,我知道自己选择的那些人,但是经文中说:‘与我一起用餐的人会背叛我’,这句话将会应验。
19 “Ninawaambia mambo haya kabla hayajatukia, ili yatakapotukia mpate kuamini ya kuwa Mimi ndiye.
我在事情还没有发生之前告诉你们,因为当它发生的时候,你们就会相信我是谁。
20 Amin, amin nawaambia, yeyote anayempokea yule niliyemtuma anipokea mimi, naye anipokeaye mimi ampokea yeye aliyenituma mimi.”
告诉你们实话,迎接我所派遣的人,就是迎接我,迎接我,就是迎接派我来此之人。”
21 Baada ya kusema haya, Yesu alifadhaika sana moyoni, akasema, “Amin, amin nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.”
耶稣说完这番话,深感难过,于是大声说:“告诉你们实话,你们中间有一个人要出卖我。”
22 Wanafunzi wake wakatazamana bila kujua kuwa alikuwa anamsema nani.
门徒们看着彼此,不知道他所指是谁。
23 Mmoja wa wanafunzi wake ambaye Yesu alimpenda sana, alikuwa ameegama kifuani mwa Yesu.
耶稣所爱的那名门徒坐在他身边,侧身靠近耶稣。
24 Simoni Petro akampungia mkono yule mwanafunzi, akamwambia, “Muulize anamaanisha nani.”
彼得向他示意,让他询问耶稣这个叛徒到底是谁。
25 Yule mwanafunzi akamwegemea Yesu, akamuuliza, “Bwana, tuambie, ni nani?”
于是那个门徒倾斜身体贴近耶稣,问到:“主啊,是谁呢?”
26 Yesu akajibu, “Ni yule nitakayempa hiki kipande cha mkate baada ya kukichovya kwenye bakuli.” Hivyo baada ya kukichovya kile kipande cha mkate, akampa Yuda Iskariote, mwana wa Simoni.
耶稣回答:“我蘸一小块饼,把它给谁就是那个人了。”
27 Mara tu baada ya kukipokea kile kipande cha mkate, Shetani akamwingia. Yesu akamwambia Yuda, “Lile unalotaka kulitenda litende haraka.”
于是他蘸了一小块饼,递给加略人西门的儿子犹大。犹大接过饼以后,撒旦就进入他的身体。耶稣对他说:“你想做什么,快去做吧。”
28 Hakuna hata mmoja wa wale waliokuwa wameketi naye mezani aliyeelewa kwa nini Yesu alimwambia hivyo.
在座众人都不知道耶稣为什么这样对犹大说话。
29 Kwa kuwa Yuda alikuwa mtunza fedha, wengine walifikiri Yesu alikuwa amemwambia akanunue vitu vilivyohitajika kwa ajili ya Sikukuu, au kuwapa maskini chochote.
由于犹大负责管钱,所以有人以为耶稣是叫他去购买逾越节所需用品,或是拿点东西去接济穷人。
30 Mara tu baada ya kupokea ule mkate, Yuda akatoka nje. Wakati huo ulikuwa ni usiku.
犹大吃了饼后立刻就离开,走进了一片黑夜。
31 Baada ya Yuda kutoka nje, Yesu akasema, “Sasa Mwana wa Adamu ametukuzwa, naye Mungu ametukuzwa ndani yake.
他离开后,耶稣就说:“现在人子已获得荣耀,上帝也通过人子获得荣耀,
32 Ikiwa Mungu ametukuzwa ndani ya Mwana, Mungu atamtukuza Mwana ndani yake mwenyewe naye atamtukuza mara.
上帝如果通过人子获得荣耀,也将会让人子获得荣耀,并且会立刻这么做。
33 “Watoto wangu, mimi bado niko pamoja nanyi kwa kitambo kidogo. Mtanitafuta, na kama vile nilivyowaambia Wayahudi, vivyo hivyo sasa nawaambia na ninyi. Niendako, ninyi hamwezi kuja.
我的孩子们,我与你们在一起的时候不多了。你们会寻找我,但我要把对犹太人所说的告诉你们:‘我去的地方,你们不能去。’
34 “Amri mpya nawapa: Mpendane kama mimi nilivyowapenda ninyi, vivyo hivyo nanyi mpendane.
我现在要给你们一个新命令:要爱彼此,要像我爱你们的方式爱彼此。
35 Kama mkipendana ninyi kwa ninyi, kwa njia hii, watu wote watajua kuwa ninyi ni wanafunzi wangu.”
如果你们爱彼此,你就是向所有人证明,你们是我的门徒。”
36 Simoni Petro akamuuliza, “Bwana, unakwenda wapi?” Yesu akamjibu, “Ninakokwenda huwezi kunifuata sasa, lakini utanifuata baadaye.”
彼得对耶稣说:“主啊,你要去哪里?”耶稣回答:“我去的地方,你现在无法跟随,但今后会跟上我。”
37 Petro akamuuliza tena, “Bwana, kwa nini siwezi kukufuata sasa? Mimi niko tayari kuutoa uhai wangu kwa ajili yako.”
彼得说:“主啊,为什么我现在不能跟随你?为了你,要我放弃生命也可以!”
38 Yesu akamjibu, “Je, ni kweli uko tayari kuutoa uhai wako kwa ajili yangu? Amin, amin nakuambia, kabla jogoo hajawika, utanikana mara tatu.”
耶稣说:“你愿意为我放弃生命吗?告诉你实话,鸡叫之前,你一定会有三次不认我。”