< Yohana 12 >

1 Siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alikwenda Bethania mahali ambako Lazaro aliyekuwa amefufuliwa na Yesu alikuwa anaishi.
Jésus donc six jours avant Pâque vint à Béthanie, où était Lazare qui avait été mort, et qu'il avait ressuscité des morts.
2 Wakaandaa karamu kwa heshima ya Yesu. Martha akawahudumia wakati Lazaro alikuwa miongoni mwa waliokaa mezani pamoja na Yesu.
Et on lui fit là un souper, et Marthe servait et Lazare était un de ceux qui étaient à table avec lui.
3 Kisha Maria akachukua chupa ya painti moja yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa, akayamimina miguuni mwa Yesu na kuifuta kwa nywele zake. Nyumba nzima ikajaa harufu nzuri ya manukato.
Alors Marie ayant pris une livre de nard pur de grand prix, en oignit les pieds de Jésus, et les essuya avec ses cheveux; et la maison fut remplie de l'odeur du parfum.
4 Ndipo Yuda Iskariote mwana wa Simoni, mmoja wa wale wanafunzi ambaye ndiye angemsaliti Yesu, akasema,
Alors Judas Iscariot, fils de Simon, l'un de ses Disciples, celui à qui il devait arriver de le trahir, dit:
5 “Kwa nini manukato haya hayakuuzwa kwa dinari 300 na fedha hizo wakapewa maskini?”
Pourquoi ce parfum n'a-t-il pas été vendu trois cents deniers, et [cet argent] donné aux pauvres?
6 Yuda alisema hivi si kwa kuwa aliwajali maskini, bali kwa kuwa alikuwa mwizi, kwani ndiye alikuwa akitunza mfuko wa fedha akawa anaiba kile kilichowekwa humo.
Or il dit cela, non point qu'il se souciât des pauvres, mais parce qu'il était larron, et qu'il avait la bourse, et portait ce qu'on y mettait.
7 Yesu akasema, “Mwacheni. Aliyanunua manukato hayo ili ayaweke kwa ajili ya siku ya maziko yangu.
Mais Jésus lui dit: laisse-la [faire]; elle l'a gardé pour le jour [de l'appareil] de ma sépulture.
8 Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.”
Car vous aurez toujours des pauvres avec vous; mais vous ne m'aurez pas toujours.
9 Umati mkubwa wa Wayahudi walipojua kwamba Yesu alikuwa huko Bethania, walikuja si tu kwa ajili ya Yesu, lakini pia kumwona Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua.
Et de grandes troupes des Juifs ayant su qu'il était là, y vinrent, non seulement à cause de Jésus, mais aussi pour voir Lazare, qu'il avait ressuscité des morts.
10 Kwa hiyo viongozi wa makuhani wakafanya mpango wa kumuua Lazaro pia,
Sur quoi les principaux Sacrificateurs résolurent de faire mourir aussi Lazare.
11 kwa kuwa kutokana na habari za kufufuliwa kwake Wayahudi wengi walikuwa wanamwendea Yesu na kumwamini.
Car plusieurs des Juifs se retiraient d'avec eux à cause de lui, et croyaient en Jésus.
12 Siku iliyofuata umati mkubwa uliokuwa umekuja kwenye Sikukuu walisikia kwamba Yesu angekuja Yerusalemu.
Le lendemain une grande quantité de peuple qui était venu à la Fête, ayant ouï dire que Jésus venait à Jérusalem,
13 Basi wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki, huku wakipaza sauti wakisema, “Hosana!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amebarikiwa Mfalme wa Israeli!”
Prirent des rameaux de palmes, et sortirent au-devant de lui, et ils criaient: Hosanna! béni soit le Roi d'Israël qui vient au Nom du Seigneur!
14 Yesu akamkuta mwana-punda akampanda, kama ilivyoandikwa,
Et Jésus ayant recouvré un ânon, s'assit dessus, suivant ce qui est écrit:
15 “Usiogope, Ewe binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda!”
Ne crains point, fille de Sion; voici, ton Roi vient, assis sur le poulain d'une ânesse.
16 Wanafunzi wake Yesu mwanzoni hawakuelewa mambo haya, lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka kuwa mambo haya yalikuwa yameandikwa kwa ajili yake na alitendewa yeye.
Or ses Disciples n'entendirent pas d'abord ces choses; mais quand Jésus fut glorifié, ils se souvinrent alors que ces choses étaient écrites de lui, et qu'ils avaient fait ces choses à son égard.
17 Wale waliokuwepo wakati Yesu alipomwita Lazaro kutoka kaburini na kumfufua kutoka kwa wafu, waliendelea kushuhudia.
Et la troupe qui était avec lui, rendait témoignage qu'il avait appelé Lazare hors du sépulcre, et qu'il l'avait ressuscité des morts.
18 Ni kwa sababu pia walikuwa wamesikia kwamba alikuwa ametenda muujiza huu ndiyo maana umati wa watu ukaenda kumlaki.
C'est pourquoi aussi le peuple alla au-devant de lui; car ils avaient appris qu'il avait fait ce miracle.
19 Hivyo Mafarisayo walipoona hayo wakaambiana, “Mnaona, hamwezi kufanya lolote. Angalieni, ulimwengu wote unamfuata yeye!”
Sur quoi les Pharisiens dirent entre eux: ne voyez-vous pas que vous n'avancez rien? voici, le monde va après lui.
20 Basi palikuwa Wayunani fulani miongoni mwa wale waliokuwa wamekwenda kuabudu wakati wa Sikukuu.
Or il y avait quelques Grecs d'entre ceux qui étaient montés pour adorer [Dieu] pendant la Fête,
21 Hawa wakamjia Filipo, ambaye alikuwa mwenyeji wa Bethsaida huko Galilaya, wakiwa na ombi. Wakamwambia, “Tungependa kumwona Yesu.”
Lesquels vinrent à Philippe, qui était de Bethsaïda de Galilée, et le prièrent, disant: Seigneur! nous désirons de voir Jésus.
22 Filipo akaenda akamweleza Andrea, nao wote wawili wakamwambia Yesu.
Philippe vint, et le dit à André, et André et Philippe le dirent à Jésus.
23 Yesu akawajibu, “Saa imewadia ya Mwana wa Adamu kutukuzwa.
Et Jésus leur répondit, disant: l'heure est venue que le Fils de l'homme doit être glorifié.
24 Amin, amin nawaambia, mbegu ya ngano isipoanguka ardhini na kufa, hubakia kama mbegu peke yake. Lakini ikifa huzaa mbegu nyingi.
En vérité, en vérité je vous dis: si le grain de froment tombant dans la terre ne meurt point, il demeure seul; mais s'il meurt, il porte beaucoup de fruit.
25 Mtu yeyote anayependa maisha yake atayapoteza, naye ayachukiaye maisha yake katika ulimwengu huu atayaokoa hata kwa uzima wa milele. (aiōnios g166)
Celui qui aime sa vie, la perdra; et celui qui hait sa vie en ce monde, la conservera jusque dans la vie éternelle. (aiōnios g166)
26 Mtu yeyote akinitumikia lazima anifuate, nami mahali nilipo ndipo mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu akinitumikia, Baba yangu atamheshimu.
Si quelqu'un me sert, qu'il me suive; et où je serai, là aussi sera celui qui me sert; et si quelqu'un me sert, mon Père l'honorera.
27 “Sasa roho yangu imefadhaika sana. Niseme nini? ‘Baba, niokoe katika saa hii.’ Lakini ni kwa kusudi hili nimeufikia wakati huu.
Maintenant mon âme est agitée; et que dirai-je? ô Père! délivre-moi de cette heure; mais c'est pour cela que je suis venu à cette heure.
28 Baba, litukuze jina lako.” Ndipo ikaja sauti kutoka mbinguni, “Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.”
Père glorifie ton Nom: Alors une voix vint du ciel, [disant]: et je l'ai glorifié, et je le glorifierai encore.
29 Ule umati wa watu uliokuwa mahali pale uliisikia nao ukasema, “Hiyo ni sauti ya radi,” wengine wakasema, “Malaika ameongea naye.”
Et la troupe qui était là, et qui avait ouï [cette voix], disait que c'était un tonnerre qui avait été fait; les autres disaient: un Ange lui a parlé.
30 Yesu akawaambia, “Sauti hii imesikika kwa faida yenu, wala si kwa faida yangu.
Jésus prit la parole, et dit: cette voix n'est point venue pour moi, mais pour vous.
31 Sasa ni saa ya hukumu kwa ajili ya ulimwengu huu, sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje.
Maintenant est venu le jugement de ce monde; maintenant le Prince de ce monde sera jeté dehors.
32 Lakini mimi, nikiinuliwa kutoka nchi, nitawavuta watu wote waje kwangu.”
Et moi, quand je serai élevé de la terre, je tirerai tous les hommes à moi.
33 Yesu aliyasema haya akionyesha ni kifo gani atakachokufa.
Or il disait cela signifiant de quelle mort il devait mourir.
34 Ule umati wa watu ukapiga kelele ukasema, “Tumesikia kutoka Sheria kwamba ‘Kristo adumu milele,’ wewe wawezaje kusema, ‘Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu’? Huyu ‘Mwana wa Adamu’ ni nani?” (aiōn g165)
Les troupes lui répondirent: nous avons appris par la Loi, que le Christ demeure éternellement, comment donc dis-tu qu'il faut que le Fils de l'homme soit élevé? Qui est ce Fils de l'homme? (aiōn g165)
35 Ndipo Yesu akawaambia, “Bado kitambo kidogo nuru ingalipo pamoja nanyi. Enendeni maadamu mna nuru, msije mkakumbwa na giza. Mtu anayetembea gizani hajui anakokwenda.
Alors Jésus leur dit: la lumière est encore avec vous pour un peu de temps: marchez pendant que vous avez la lumière, de peur que les ténèbres ne vous surprennent; car celui qui marche dans les ténèbres, ne sait où il va.
36 Wekeni tumaini lenu katika nuru hiyo ili mpate kuwa wana wa nuru.” Baada ya kusema haya, Yesu aliondoka, akajificha wasimwone.
Pendant que vous avez la lumière croyez en la lumière, afin que vous soyez enfants de lumière. Jésus dit ces choses, puis il s'en alla, et se cacha de devant eux.
37 Hata baada ya Yesu kufanya miujiza hii yote mbele yao, bado hawakumwamini.
Et quoiqu'il eût fait tant de miracles devant eux, ils ne crurent point en lui.
38 Hili lilikuwa ili kutimiza lile neno la nabii Isaya lililosema: “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?”
De sorte que cette parole qui a été dite par Esaïe le Prophète, fut accomplie: Seigneur, qui a cru à notre parole, et à qui a été révélé le bras du Seigneur?
39 Kwa hivyo hawakuamini, kwa sababu Isaya anasema mahali pengine:
C'est pourquoi ils ne pouvaient croire, à cause qu'Esaïe dit encore:
40 “Amewafanya vipofu, na kuifanya mioyo yao kuwa migumu, ili wasiweze kuona kwa macho yao, wala kuelewa kwa mioyo yao, wasije wakageuka nami nikawaponya.”
Il a aveuglé leurs yeux, et il a endurci leur cœur, afin qu'ils ne voient point de leurs yeux, et qu'ils n'entendent du cœur, et qu'ils ne soient convertis, et que je ne les guérisse.
41 Isaya alisema haya alipoona utukufu wa Yesu na kunena habari zake.
Esaïe dit ces choses quand il vit sa gloire, et qu'il parla de lui.
42 Lakini wengi miongoni mwa viongozi wa Wayahudi walimwamini, lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakukiri waziwazi kwa maana waliogopa kufukuzwa katika masinagogi.
Cependant plusieurs des principaux mêmes crurent en lui; mais ils ne le confessaient point à cause des Pharisiens, de peur d'être chassés hors de la Synagogue.
43 Wao walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zitokazo kwa Mungu.
Car ils ont mieux aimé la gloire des hommes, que la gloire de Dieu.
44 Yesu akapaza sauti akasema, “Yeyote aniaminiye, haniamini mimi peke yangu, bali yeye aliyenituma.
Or Jésus s'écria, et dit: celui qui croit en moi, ne croit point [seulement] en moi, mais en celui qui m'a envoyé.
45 Yeyote anionaye mimi, amemwona yeye aliyenituma.
Et celui qui me contemple, contemple celui qui m'a envoyé.
46 Mimi nimekuja kama nuru ulimwenguni, ili kwamba kila mtu aniaminiye asibaki gizani.
Je suis venu au monde pour [en] être la lumière, afin que quiconque croit en moi ne demeure point dans les ténèbres.
47 “Mimi simhukumu mtu yeyote anayesikia maneno yangu na asiyatii, kwa maana sikuja kuuhukumu ulimwengu, bali kuuokoa.
Et si quelqu'un entend mes paroles, et ne les croit point, je ne le juge point; car je ne suis point venu pour juger le monde, mais pour sauver le monde.
48 Yuko amhukumuye yeye anikataaye mimi na kutokuyapokea maneno yangu, yaani, yale maneno niliyosema yenyewe yatamhukumu siku ya mwisho.
Celui qui me rejette, et ne reçoit point mes paroles, il a qui le juge: la parole que j'ai annoncée, sera celle qui le jugera au dernier jour.
49 Kwa maana sisemi kwa ajili yangu mwenyewe, bali Baba aliyenituma aliniamuru ni nini cha kusema na jinsi ya kukisema.
Car je n'ai point parlé de moi-même, mais le Père qui m'a envoyé, m'a prescrit ce que j'ai à dire et de quoi je dois parler.
50 Nami ninajua amri zake huongoza hadi kwenye uzima wa milele. Hivyo lolote nisemalo, ndilo lile Baba aliloniambia niseme.” (aiōnios g166)
Et je sais que son commandement est la vie éternelle; les choses donc que je dis, je les dis comme mon Père me les a dites. (aiōnios g166)

< Yohana 12 >