< Yohana 12 >
1 Siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alikwenda Bethania mahali ambako Lazaro aliyekuwa amefufuliwa na Yesu alikuwa anaishi.
Six jours avant la Pâque, Jésus vint à Béthanie, où était Lazare, le mort qu’il avait ressuscité.
2 Wakaandaa karamu kwa heshima ya Yesu. Martha akawahudumia wakati Lazaro alikuwa miongoni mwa waliokaa mezani pamoja na Yesu.
Là, on lui fit un souper, et Marthe servait. Or, Lazare était de ceux qui se trouvaient à table avec lui.
3 Kisha Maria akachukua chupa ya painti moja yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa, akayamimina miguuni mwa Yesu na kuifuta kwa nywele zake. Nyumba nzima ikajaa harufu nzuri ya manukato.
Marie, ayant pris une livre d’un parfum de nard pur très précieux, en oignit les pieds de Jésus, et les essuya avec ses cheveux; et la maison fut remplie de l’odeur du parfum.
4 Ndipo Yuda Iskariote mwana wa Simoni, mmoja wa wale wanafunzi ambaye ndiye angemsaliti Yesu, akasema,
Alors un de ses disciples, Judas Iscariote, celui qui devait le trahir, dit:
5 “Kwa nini manukato haya hayakuuzwa kwa dinari 300 na fedha hizo wakapewa maskini?”
« Pourquoi n’a-t-on pas vendu ce parfum trois cents deniers, pour les donner aux pauvres? »
6 Yuda alisema hivi si kwa kuwa aliwajali maskini, bali kwa kuwa alikuwa mwizi, kwani ndiye alikuwa akitunza mfuko wa fedha akawa anaiba kile kilichowekwa humo.
Il dit cela, non qu’il se souciât des pauvres, mais parce qu’il était voleur, et qu’ayant la bourse, il dérobait ce qu’on y mettait.
7 Yesu akasema, “Mwacheni. Aliyanunua manukato hayo ili ayaweke kwa ajili ya siku ya maziko yangu.
Jésus lui dit donc: « Laisse-la; elle a gardé ce parfum pour le jour de ma sépulture.
8 Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.”
Car vous aurez toujours des pauvres avec vous; mais moi, vous ne m’aurez pas toujours! »
9 Umati mkubwa wa Wayahudi walipojua kwamba Yesu alikuwa huko Bethania, walikuja si tu kwa ajili ya Yesu, lakini pia kumwona Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua.
Un grand nombre de Juifs surent que Jésus était à Béthanie, et ils vinrent, non seulement à cause de Jésus, mais aussi pour voir Lazare qu’il avait ressuscité des morts.
10 Kwa hiyo viongozi wa makuhani wakafanya mpango wa kumuua Lazaro pia,
Mais les Princes des prêtres délibérèrent de faire mourir aussi Lazare,
11 kwa kuwa kutokana na habari za kufufuliwa kwake Wayahudi wengi walikuwa wanamwendea Yesu na kumwamini.
parce que beaucoup de Juifs se retiraient à cause de lui, et croyaient en Jésus.
12 Siku iliyofuata umati mkubwa uliokuwa umekuja kwenye Sikukuu walisikia kwamba Yesu angekuja Yerusalemu.
Le lendemain, une multitude de gens qui étaient venus pour la fête, ayant appris que Jésus se rendait à Jérusalem,
13 Basi wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki, huku wakipaza sauti wakisema, “Hosana!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amebarikiwa Mfalme wa Israeli!”
prirent des rameaux de palmiers, et allèrent au-devant de lui, en criant: « Hosanna! Béni soit celui qui vient au nom du Seigneur, le Roi d’Israël! »
14 Yesu akamkuta mwana-punda akampanda, kama ilivyoandikwa,
Jésus, ayant trouvé un ânon, monta dessus, selon ce qui est écrit:
15 “Usiogope, Ewe binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda!”
« Ne crains point, fille de Sion, voici ton Roi qui vient, assis sur le petit d’une ânesse. »
16 Wanafunzi wake Yesu mwanzoni hawakuelewa mambo haya, lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka kuwa mambo haya yalikuwa yameandikwa kwa ajili yake na alitendewa yeye.
— Ses disciples ne comprirent pas d’abord ces choses; mais lorsque Jésus fut glorifié, ils se souvinrent qu’elles avaient été écrites de lui, et qu’il les avait accomplies en ce qui le regarde. —
17 Wale waliokuwepo wakati Yesu alipomwita Lazaro kutoka kaburini na kumfufua kutoka kwa wafu, waliendelea kushuhudia.
La foule donc qui était avec lui lorsqu’il appela Lazare du tombeau et le ressuscita des morts lui rendait témoignage;
18 Ni kwa sababu pia walikuwa wamesikia kwamba alikuwa ametenda muujiza huu ndiyo maana umati wa watu ukaenda kumlaki.
et c’est aussi parce qu’elle avait appris qu’il avait fait ce miracle, que la multitude s’était portée à sa rencontre.
19 Hivyo Mafarisayo walipoona hayo wakaambiana, “Mnaona, hamwezi kufanya lolote. Angalieni, ulimwengu wote unamfuata yeye!”
Les Pharisiens se dirent donc entre eux: « Vous voyez bien que vous ne gagnez rien; voilà que tout le monde court après lui. »
20 Basi palikuwa Wayunani fulani miongoni mwa wale waliokuwa wamekwenda kuabudu wakati wa Sikukuu.
Or, il y avait quelques Gentils parmi ceux qui étaient montés pour adorer, lors de la fête.
21 Hawa wakamjia Filipo, ambaye alikuwa mwenyeji wa Bethsaida huko Galilaya, wakiwa na ombi. Wakamwambia, “Tungependa kumwona Yesu.”
Ils s’approchèrent de Philippe, qui était de Bethsaïde en Galilée, et lui firent cette demande: « Seigneur, nous voudrions bien voir Jésus. »
22 Filipo akaenda akamweleza Andrea, nao wote wawili wakamwambia Yesu.
Philippe alla le dire à André, puis André et Philippe allèrent le dire à Jésus.
23 Yesu akawajibu, “Saa imewadia ya Mwana wa Adamu kutukuzwa.
Jésus leur répondit: « L’heure est venue où le Fils de l’homme doit être glorifié.
24 Amin, amin nawaambia, mbegu ya ngano isipoanguka ardhini na kufa, hubakia kama mbegu peke yake. Lakini ikifa huzaa mbegu nyingi.
En vérité, en vérité, je vous le dis, si le grain de blé tombé en terre ne meurt pas, il demeure seul; mais s’il meurt, il porte beaucoup de fruit.
25 Mtu yeyote anayependa maisha yake atayapoteza, naye ayachukiaye maisha yake katika ulimwengu huu atayaokoa hata kwa uzima wa milele. (aiōnios )
Celui qui aime sa vie, la perdra; et celui qui hait sa vie en ce monde, la conservera pour la vie éternelle. (aiōnios )
26 Mtu yeyote akinitumikia lazima anifuate, nami mahali nilipo ndipo mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu akinitumikia, Baba yangu atamheshimu.
Si quelqu’un veut être mon serviteur, qu’il me suive, et là où je suis, là aussi sera mon serviteur. Si quelqu’un me sert, mon Père l’honorera.
27 “Sasa roho yangu imefadhaika sana. Niseme nini? ‘Baba, niokoe katika saa hii.’ Lakini ni kwa kusudi hili nimeufikia wakati huu.
Maintenant mon âme est troublée; et que dirai-je?… Père, délivrez-moi de cette heure… Mais c’est pour cela que je suis arrivé à cette heure.
28 Baba, litukuze jina lako.” Ndipo ikaja sauti kutoka mbinguni, “Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.”
Père, glorifiez votre nom. » Et une voix vint du ciel: « Je l’ai glorifié et je le glorifierai encore. »
29 Ule umati wa watu uliokuwa mahali pale uliisikia nao ukasema, “Hiyo ni sauti ya radi,” wengine wakasema, “Malaika ameongea naye.”
La foule qui était là et qui avait entendu, disait: « C’est le tonnerre »; d’autres disaient: « Un ange lui a parlé. »
30 Yesu akawaambia, “Sauti hii imesikika kwa faida yenu, wala si kwa faida yangu.
Jésus dit: « Ce n’est pas pour moi que cette voix s’est fait entendre, mais pour vous.
31 Sasa ni saa ya hukumu kwa ajili ya ulimwengu huu, sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje.
C’est maintenant le jugement de ce monde; c’est maintenant que le Prince de ce monde va être jeté dehors.
32 Lakini mimi, nikiinuliwa kutoka nchi, nitawavuta watu wote waje kwangu.”
Et moi, quand j’aurai été élevé de la terre, j’attirerai tous les hommes à moi. »
33 Yesu aliyasema haya akionyesha ni kifo gani atakachokufa.
Ce qu’il disait, pour marquer de quelle mort il devait mourir.
34 Ule umati wa watu ukapiga kelele ukasema, “Tumesikia kutoka Sheria kwamba ‘Kristo adumu milele,’ wewe wawezaje kusema, ‘Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu’? Huyu ‘Mwana wa Adamu’ ni nani?” (aiōn )
La foule lui répondit: « Nous avons appris par la Loi que le Christ demeure éternellement: comment donc dites-vous: il faut que le Fils de l’homme soit élevé? Qui est ce Fils de l’homme? » (aiōn )
35 Ndipo Yesu akawaambia, “Bado kitambo kidogo nuru ingalipo pamoja nanyi. Enendeni maadamu mna nuru, msije mkakumbwa na giza. Mtu anayetembea gizani hajui anakokwenda.
Jésus leur dit: « La lumière n’est plus que pour un temps au milieu de vous. Marchez, pendant que vous avez la lumière, de peur que les ténèbres ne vous surprennent: celui qui marche dans les ténèbres ne sait où il va.
36 Wekeni tumaini lenu katika nuru hiyo ili mpate kuwa wana wa nuru.” Baada ya kusema haya, Yesu aliondoka, akajificha wasimwone.
Pendant que vous avez la lumière, croyez en la lumière, afin que vous soyez des enfants de lumière. « Jésus dit ces choses, puis s’en allant il se déroba à leurs yeux.
37 Hata baada ya Yesu kufanya miujiza hii yote mbele yao, bado hawakumwamini.
Quoiqu’il eût fait tant de miracles en leur présence, ils ne croyaient point en lui:
38 Hili lilikuwa ili kutimiza lile neno la nabii Isaya lililosema: “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?”
afin que fût accompli l’oracle du prophète Isaïe, disant: « Seigneur, qui a cru à notre parole? et à qui le bras du Seigneur a-t-il été révélé? »
39 Kwa hivyo hawakuamini, kwa sababu Isaya anasema mahali pengine:
Ils ne pouvaient donc croire, parce qu’Isaïe a dit encore:
40 “Amewafanya vipofu, na kuifanya mioyo yao kuwa migumu, ili wasiweze kuona kwa macho yao, wala kuelewa kwa mioyo yao, wasije wakageuka nami nikawaponya.”
« Il a aveuglé leurs yeux et endurci leur cœur, de peur qu’ils ne voient des yeux, qu’ils ne comprennent du cœur, qu’ils ne se convertissent, et que je ne les guérisse. »
41 Isaya alisema haya alipoona utukufu wa Yesu na kunena habari zake.
Isaïe dit ces choses, lorsqu’il vit la gloire du Seigneur et qu’il parla de lui.
42 Lakini wengi miongoni mwa viongozi wa Wayahudi walimwamini, lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakukiri waziwazi kwa maana waliogopa kufukuzwa katika masinagogi.
Beaucoup, toutefois, même parmi les membres du Sanhédrin, crurent en lui; mais, à cause des Pharisiens, ils ne le confessaient pas, de peur d’être chassés de la synagogue.
43 Wao walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zitokazo kwa Mungu.
Car ils aimèrent la gloire des hommes plus que la gloire de Dieu.
44 Yesu akapaza sauti akasema, “Yeyote aniaminiye, haniamini mimi peke yangu, bali yeye aliyenituma.
Or, Jésus éleva la voix et dit: « Celui qui croit en moi, croit, non pas en moi, mais en celui qui m’a envoyé;
45 Yeyote anionaye mimi, amemwona yeye aliyenituma.
et celui qui me voit, voit celui qui m’a envoyé.
46 Mimi nimekuja kama nuru ulimwenguni, ili kwamba kila mtu aniaminiye asibaki gizani.
Je suis venu dans le monde comme une lumière, afin que celui qui croit en moi, ne demeure pas dans les ténèbres.
47 “Mimi simhukumu mtu yeyote anayesikia maneno yangu na asiyatii, kwa maana sikuja kuuhukumu ulimwengu, bali kuuokoa.
Si quelqu’un entend ma parole, et ne la garde pas, moi je ne le juge point; car je suis venu, non pour juger le monde, mais pour sauver le monde.
48 Yuko amhukumuye yeye anikataaye mimi na kutokuyapokea maneno yangu, yaani, yale maneno niliyosema yenyewe yatamhukumu siku ya mwisho.
Celui qui me méprise et ne reçoit pas ma parole, il a son juge: c’est la parole même que j’ai annoncée; elle le jugera au dernier jour.
49 Kwa maana sisemi kwa ajili yangu mwenyewe, bali Baba aliyenituma aliniamuru ni nini cha kusema na jinsi ya kukisema.
Car je n’ai point parlé de moi-même; mais le Père, qui m’a envoyé, m’a prescrit lui-même ce que je dois dire et ce que je dois enseigner.
50 Nami ninajua amri zake huongoza hadi kwenye uzima wa milele. Hivyo lolote nisemalo, ndilo lile Baba aliloniambia niseme.” (aiōnios )
Et je sais que son commandement est la vie éternelle. Les choses donc que je dis, je les dis comme mon Père me les a enseignées. » (aiōnios )