< Yohana 12 >
1 Siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alikwenda Bethania mahali ambako Lazaro aliyekuwa amefufuliwa na Yesu alikuwa anaishi.
Six jours avant la Pâque, Jésus se rendit à Béthanie, où était Lazare, qui était mort, et qu'il avait ressuscité des morts.
2 Wakaandaa karamu kwa heshima ya Yesu. Martha akawahudumia wakati Lazaro alikuwa miongoni mwa waliokaa mezani pamoja na Yesu.
Là, on lui fit un souper. Marthe servait, mais Lazare était du nombre de ceux qui étaient à table avec lui.
3 Kisha Maria akachukua chupa ya painti moja yenye manukato ya nardo safi ya thamani kubwa, akayamimina miguuni mwa Yesu na kuifuta kwa nywele zake. Nyumba nzima ikajaa harufu nzuri ya manukato.
Marie prit une livre d'onguent de nard pur, très précieux, et elle oignit les pieds de Jésus; elle lui essuya les pieds avec ses cheveux. La maison fut remplie de l'odeur du parfum.
4 Ndipo Yuda Iskariote mwana wa Simoni, mmoja wa wale wanafunzi ambaye ndiye angemsaliti Yesu, akasema,
Alors Judas Iscariote, fils de Simon, l'un de ses disciples, qui allait le trahir, dit:
5 “Kwa nini manukato haya hayakuuzwa kwa dinari 300 na fedha hizo wakapewa maskini?”
« Pourquoi ce parfum n'a-t-il pas été vendu trois cents deniers et donné aux pauvres? »
6 Yuda alisema hivi si kwa kuwa aliwajali maskini, bali kwa kuwa alikuwa mwizi, kwani ndiye alikuwa akitunza mfuko wa fedha akawa anaiba kile kilichowekwa humo.
Il disait cela, non qu'il se souciât des pauvres, mais parce qu'il était voleur et qu'ayant la tirelire, il avait l'habitude de voler ce qu'on y mettait.
7 Yesu akasema, “Mwacheni. Aliyanunua manukato hayo ili ayaweke kwa ajili ya siku ya maziko yangu.
Mais Jésus dit: « Laisse-la tranquille. Elle a gardé cela pour le jour de ma sépulture.
8 Maskini mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa nami siku zote.”
Car vous avez toujours les pauvres avec vous, mais vous ne m'avez pas toujours, moi. »
9 Umati mkubwa wa Wayahudi walipojua kwamba Yesu alikuwa huko Bethania, walikuja si tu kwa ajili ya Yesu, lakini pia kumwona Lazaro ambaye Yesu alikuwa amemfufua.
Une grande foule de Juifs apprit donc qu'il était là, et ils vinrent, non seulement à cause de Jésus, mais aussi pour voir Lazare, qu'il avait ressuscité des morts.
10 Kwa hiyo viongozi wa makuhani wakafanya mpango wa kumuua Lazaro pia,
Mais les principaux sacrificateurs complotèrent de faire mourir aussi Lazare,
11 kwa kuwa kutokana na habari za kufufuliwa kwake Wayahudi wengi walikuwa wanamwendea Yesu na kumwamini.
parce que, à cause de lui, beaucoup de Juifs s'en allèrent et crurent en Jésus.
12 Siku iliyofuata umati mkubwa uliokuwa umekuja kwenye Sikukuu walisikia kwamba Yesu angekuja Yerusalemu.
Le lendemain, une grande foule était venue à la fête. Lorsqu'ils apprirent que Jésus venait à Jérusalem,
13 Basi wakachukua matawi ya mitende, wakatoka kwenda kumlaki, huku wakipaza sauti wakisema, “Hosana!” “Amebarikiwa yeye ajaye kwa Jina la Bwana!” “Amebarikiwa Mfalme wa Israeli!”
ils prirent les branches des palmiers, sortirent à sa rencontre et s'écrièrent: « Hosanna! Béni soit celui qui vient au nom du Seigneur, le roi d'Israël! »
14 Yesu akamkuta mwana-punda akampanda, kama ilivyoandikwa,
Jésus, ayant trouvé un jeune âne, s'assit dessus. Selon qu'il est écrit:
15 “Usiogope, Ewe binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda!”
« Ne crains pas, fille de Sion. Voici que ton Roi vient, assis sur un ânon. »
16 Wanafunzi wake Yesu mwanzoni hawakuelewa mambo haya, lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka kuwa mambo haya yalikuwa yameandikwa kwa ajili yake na alitendewa yeye.
Ses disciples ne comprirent pas d'abord ces choses; mais, lorsque Jésus fut glorifié, ils se souvinrent que ces choses étaient écrites de lui, et qu'ils les avaient faites pour lui.
17 Wale waliokuwepo wakati Yesu alipomwita Lazaro kutoka kaburini na kumfufua kutoka kwa wafu, waliendelea kushuhudia.
La foule qui était avec lui, lorsqu'il appela Lazare hors du sépulcre et le ressuscita des morts, rendait donc témoignage à ce sujet.
18 Ni kwa sababu pia walikuwa wamesikia kwamba alikuwa ametenda muujiza huu ndiyo maana umati wa watu ukaenda kumlaki.
C'est pourquoi aussi la foule alla au-devant de lui, parce qu'elle avait appris qu'il avait fait ce miracle.
19 Hivyo Mafarisayo walipoona hayo wakaambiana, “Mnaona, hamwezi kufanya lolote. Angalieni, ulimwengu wote unamfuata yeye!”
Les pharisiens se dirent alors entre eux: « Voyez comme vous ne faites rien. Voici que le monde est allé après lui. »
20 Basi palikuwa Wayunani fulani miongoni mwa wale waliokuwa wamekwenda kuabudu wakati wa Sikukuu.
Or, il y avait quelques Grecs parmi ceux qui montaient se prosterner à la fête.
21 Hawa wakamjia Filipo, ambaye alikuwa mwenyeji wa Bethsaida huko Galilaya, wakiwa na ombi. Wakamwambia, “Tungependa kumwona Yesu.”
Ils vinrent donc trouver Philippe, qui était de Bethsaïda en Galilée, et lui demandèrent: « Seigneur, nous voulons voir Jésus. »
22 Filipo akaenda akamweleza Andrea, nao wote wawili wakamwambia Yesu.
Philippe vint le dire à André; et André vint à son tour avec Philippe, et ils le dirent à Jésus.
23 Yesu akawajibu, “Saa imewadia ya Mwana wa Adamu kutukuzwa.
Jésus leur répondit: « Le temps est venu où le Fils de l'homme sera glorifié.
24 Amin, amin nawaambia, mbegu ya ngano isipoanguka ardhini na kufa, hubakia kama mbegu peke yake. Lakini ikifa huzaa mbegu nyingi.
Je vous le dis en vérité, si le grain de blé ne tombe en terre et ne meurt, il reste seul. Mais s'il meurt, il porte beaucoup de fruit.
25 Mtu yeyote anayependa maisha yake atayapoteza, naye ayachukiaye maisha yake katika ulimwengu huu atayaokoa hata kwa uzima wa milele. (aiōnios )
Celui qui aime sa vie la perdra. Celui qui hait sa vie dans ce monde la gardera pour la vie éternelle. (aiōnios )
26 Mtu yeyote akinitumikia lazima anifuate, nami mahali nilipo ndipo mtumishi wangu atakapokuwa. Mtu akinitumikia, Baba yangu atamheshimu.
Si quelqu'un me sert, qu'il me suive. Là où je suis, là aussi sera mon serviteur. Si quelqu'un me sert, le Père l'honorera.
27 “Sasa roho yangu imefadhaika sana. Niseme nini? ‘Baba, niokoe katika saa hii.’ Lakini ni kwa kusudi hili nimeufikia wakati huu.
« Maintenant mon âme est troublée. Que dirai-je? « Père, sauve-moi de ce temps »? Mais c'est pour cette cause que je suis arrivé à ce moment.
28 Baba, litukuze jina lako.” Ndipo ikaja sauti kutoka mbinguni, “Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.”
Père, glorifie ton nom! » Alors une voix sortit du ciel, disant: « Je l'ai glorifié et je le glorifierai encore. »
29 Ule umati wa watu uliokuwa mahali pale uliisikia nao ukasema, “Hiyo ni sauti ya radi,” wengine wakasema, “Malaika ameongea naye.”
C'est pourquoi la foule qui se tenait là et qui l'entendait disait que c'était un tonnerre. D'autres disaient: « Un ange lui a parlé. »
30 Yesu akawaambia, “Sauti hii imesikika kwa faida yenu, wala si kwa faida yangu.
Jésus répondit: « Cette voix n'est pas venue à cause de moi, mais à cause de vous.
31 Sasa ni saa ya hukumu kwa ajili ya ulimwengu huu, sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje.
Maintenant, c'est le jugement de ce monde. Maintenant, le prince de ce monde sera chassé.
32 Lakini mimi, nikiinuliwa kutoka nchi, nitawavuta watu wote waje kwangu.”
Et moi, si je suis élevé de la terre, j'attirerai à moi tous les peuples. »
33 Yesu aliyasema haya akionyesha ni kifo gani atakachokufa.
Mais il disait cela en indiquant par quel genre de mort il devait mourir.
34 Ule umati wa watu ukapiga kelele ukasema, “Tumesikia kutoka Sheria kwamba ‘Kristo adumu milele,’ wewe wawezaje kusema, ‘Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa juu’? Huyu ‘Mwana wa Adamu’ ni nani?” (aiōn )
La foule lui répondit: « Nous avons appris par la loi que le Christ demeure éternellement. Comment dis-tu: « Il faut que le Fils de l'homme soit élevé »? Qui est ce Fils de l'homme? » (aiōn )
35 Ndipo Yesu akawaambia, “Bado kitambo kidogo nuru ingalipo pamoja nanyi. Enendeni maadamu mna nuru, msije mkakumbwa na giza. Mtu anayetembea gizani hajui anakokwenda.
Jésus leur dit donc: « La lumière est encore pour un peu de temps avec vous. Marchez pendant que vous avez la lumière, afin que les ténèbres ne vous surprennent pas. Celui qui marche dans les ténèbres ne sait pas où il va.
36 Wekeni tumaini lenu katika nuru hiyo ili mpate kuwa wana wa nuru.” Baada ya kusema haya, Yesu aliondoka, akajificha wasimwone.
Pendant que vous avez la lumière, croyez en la lumière, afin de devenir des enfants de lumière. » Jésus dit ces choses, puis il s'en alla et se cacha d'eux.
37 Hata baada ya Yesu kufanya miujiza hii yote mbele yao, bado hawakumwamini.
Mais, bien qu'il eût fait devant eux tant de miracles, ils ne crurent pas en lui,
38 Hili lilikuwa ili kutimiza lile neno la nabii Isaya lililosema: “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?”
afin que s'accomplît la parole qu'Ésaïe, le prophète, avait prononcée: « Seigneur, qui a cru à notre rapport? A qui le bras du Seigneur a-t-il été révélé? »
39 Kwa hivyo hawakuamini, kwa sababu Isaya anasema mahali pengine:
C'est pour cela qu'ils ne pouvaient pas croire, car Ésaïe a encore dit:
40 “Amewafanya vipofu, na kuifanya mioyo yao kuwa migumu, ili wasiweze kuona kwa macho yao, wala kuelewa kwa mioyo yao, wasije wakageuka nami nikawaponya.”
« Il a aveuglé leurs yeux et il a endurci leur cœur, de peur qu'ils ne voient avec leurs yeux, et perçoivent avec leur cœur, et tournerait, et je les guérirais. »
41 Isaya alisema haya alipoona utukufu wa Yesu na kunena habari zake.
Ésaïe a dit ces choses en voyant sa gloire, et il a parlé de lui.
42 Lakini wengi miongoni mwa viongozi wa Wayahudi walimwamini, lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakukiri waziwazi kwa maana waliogopa kufukuzwa katika masinagogi.
Cependant, beaucoup de chefs croyaient en lui; mais, à cause des pharisiens, ils ne le confessaient pas, afin de ne pas être exclus de la synagogue,
43 Wao walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zitokazo kwa Mungu.
car ils aimaient mieux les louanges des hommes que celles de Dieu.
44 Yesu akapaza sauti akasema, “Yeyote aniaminiye, haniamini mimi peke yangu, bali yeye aliyenituma.
Jésus s'écria: « Celui qui croit en moi ne croit pas en moi, mais en celui qui m'a envoyé.
45 Yeyote anionaye mimi, amemwona yeye aliyenituma.
Celui qui me voit voit celui qui m'a envoyé.
46 Mimi nimekuja kama nuru ulimwenguni, ili kwamba kila mtu aniaminiye asibaki gizani.
Je suis venu comme une lumière dans le monde, afin que quiconque croit en moi ne demeure pas dans les ténèbres.
47 “Mimi simhukumu mtu yeyote anayesikia maneno yangu na asiyatii, kwa maana sikuja kuuhukumu ulimwengu, bali kuuokoa.
Si quelqu'un écoute mes paroles et ne croit pas, je ne le juge pas. Car je suis venu non pas pour juger le monde, mais pour sauver le monde.
48 Yuko amhukumuye yeye anikataaye mimi na kutokuyapokea maneno yangu, yaani, yale maneno niliyosema yenyewe yatamhukumu siku ya mwisho.
Celui qui me rejette, et qui ne reçoit pas mes paroles, a quelqu'un qui le juge. La parole que j'ai prononcée le jugera au dernier jour.
49 Kwa maana sisemi kwa ajili yangu mwenyewe, bali Baba aliyenituma aliniamuru ni nini cha kusema na jinsi ya kukisema.
Car je n'ai pas parlé de moi-même, mais le Père qui m'a envoyé m'a donné un commandement, celui de savoir ce que je dois dire et ce que je dois dire.
50 Nami ninajua amri zake huongoza hadi kwenye uzima wa milele. Hivyo lolote nisemalo, ndilo lile Baba aliloniambia niseme.” (aiōnios )
Je sais que son commandement est la vie éternelle. Les choses donc que je dis, je les dis comme le Père me les a dites. » (aiōnios )